Tujifunze Kutoka Libya

Tujifunze Kutoka Libya

Nataka nijibu swali lako kitulivu kabisa, na kama kweli unayo nia ya kuelewa jibu hutajifanya hujui jibu.

Ni hivi: Unaamini au huamini kuwa Samia Suluhu Hassan anajuwa kuwa huo mfumo upo, au hajui?

Kama Samia anajuwa mfumo huo upo, amefanya juhudi zipi za kuurekebisha/kuuondoa ili Tanzania anayoiongoza iwe nchi ya utulivu; na yeye atawale kwa AMANI kabisa? Umemweleza nini huyo Samia kuhusu hili, mkuu Ertugrul? Kwani nawe hutaki Samia atawale nchi hii wakati wananchi wake wote wakiwa na maelewano mazuri, bila ya kugawanyika kimakundi kama kulivyo sasa hivi?

Hivi kweli hujui "maandamano ya fujo na vurugu" yanasababishwa na nani, hujui kweli au unajifanya tu kutojuwa?

Fujo na vurugu vinasababishwa na ukandamizaji; unyimwaji wa haki; bila ya hivyo usingeona fujo na vurugu. WaTanzania ni watu wapole sana; tena wapenda AMANI. Ni nyinyi, mnaopigania huo mfumo na huyo Samia na Kikwete ndio mnaosababisha yote haya.

Kuhusu kuuondoa mfumo kwa njia za fujo na vurugu; hilo hata wewe huna jibu; nijuavyo mimi, bila Samia Suluhu Hassan kuondokana na dhana ya kudhani anaweza kutawala taifa hili kwa nguvu za mitutu ya bunduki; hili hata yeye anacheza kamali tu!

Kwa bahati mbaya sana huu mchezo wake umesababisha waTanzania kupoteza maisha; na inawezekana bado wengine wataendelea kupoteza maisha; na kupoteza muda wa kuliendeleza taifa hili. Lakini na yeye, pamoja na Genge lake lote, hawatatoka salama
Mr. Kalamu

Haya ya kutumia fujo na vurugu kudai haki ambayo mnaitaka sio njia sahihi kwa sasa,madhara yameonekana tayar tena makubwa

Na umekiri tena kwamba huenda kukawa na uwezekano wa watu tena kufa kwa kutimia njia hizo hizo

Je, bado mnataka kuwatumia vijana wasiojielewa na kufuata kila mnacho waambia kuandamana kwa fujo na vurugu ili mfikie lengo lenu hata kama watapoteza uhai wao?

Hapo mnakuwa na tofauti gani na Uongozi wa sasa?
 
Napata sana ukakasi pale unapo ninasibisha na Bakwata na maelekezo ya dini

Nakosa uhalali wa kujadiliana na wewe

Tukuatane kwenye topic nyingine

Asante
Wewe na hawa BAKWATA, si nyote mnahimiza "majadiliano" na "AMANI"" isiyotokana na HAKI, sasa unakataa vipi kuhusishwa na watu unaokubaliana nao mtazamo?
 
Haya ya kutumia fujo na vurugu kudai haki ambayo mnaitaka sio njia sahihi kwa sasa,madhara yameonekana tayar tena makubwa
hivi kwa nini hutaki kuelewa "fujo na vurugu" zinasababishwa na nani.
Kwa nini hutaki kabisa kukubali kutazama hizo vurugu na fujo chanzo chake ni nini?
WaTanzania hawakuamua tu kufanya hizo unazoziita wewe vujo na vurugu; hawa ni watu wapole; wapenda amani miaka yote. Ni nani anayewaroga mara hii wawe watu wa vurugu na fujo bila ya sababu?
Watu tulioshikam
Na umekiri tena kwamba huenda kukawa na uwezekano wa watu tena kufa kwa kutimia njia hizo hizo
sikukiri chochote, ni mambo ambayo Samia na Genge lake mmeamua kuwafanyia waTanzania. Mtawaua hadi hapo watakapokubali matakwa yenu ya kuwatawala kwa nguvu; hili ndilo limetokea Oktoba 29; na litatokea tu kama mtaendelea kuwa na kiburi hicho cha kuwadharau waTanzania
ana miaka yote kama taifa kwa umoja wetu; ni nini tofauti kilichotokea wakati huu?

Kwa kuwa Samia ni mwanamke na muislam,siyo; nawe unakubali upuuzi huo?
 
Je, bado mnataka kuwatumia vijana wasiojielewa na kufuata kila mnacho waambia kuandamana kwa fujo na vurugu ili mfikie lengo lenu hata kama watapoteza uhai wao?
Huu ndio upuuzi nisiokuwa na simile nao kabisa, lugha hiyo hiyo anayotumia Samia, na bado hata huoni aibu kuendelea nayo wakati ukitaka kujibainisha kuwa wewe ni tofauti.

Hawa "vijana wasiojielewa" mmewatoa wapi nyinyi. Hii ni lugha ya wapi hii?
Au hukumbuki pia kuwa Samia alitangaza hao vijana aliowaua walikuwa ni kutoka nje ya nchi, hukusikia akisema hivyo?
Mara, hao "vijana wasiojielewa" wamelipwa pesa ili wakafanye vurugu!

Ni nyinyi tu mnaojuwa ni kipi wanachotaka waTanzania; wengine wote ni wafanya vurugu na fujo? Sasa watu wa namna hii mnataka kuwatawala wa nini; huoni kuwa hamtaweza kuwaua wote na wataendelea kukataa huo upuuzi wenu?
 
Hapo mnakuwa na tofauti gani na Uongozi wa sasa?
Kwa mada zako za sasa, na maandishi mengine uliyoweka humu JF wewe mkuu "ertugrul' huwezi kamwe kujiweka pembeni na uongozi huu unaotaka kujiweka mbali nao hapa.

Nashangaa hata hili hulionei haya kuliweka hivi hapa.
 
Nyie bana huwa mnalishana propaganda za kijinga kisha mnaziamini wenyewe, na sababu huwa mnajadiliana wenye mtazamo mmoja, bila kujua na sisi tuna akili. Ni raslimali zipi ambazo wazungu hawajazifikia hadi sasa hapa nchini, ambazo ndio mnaamini bado wanazitaka?

Mega projects zote wanapewa hao hao, mikopo mikubwa wao ndio wanatukopesha. Labda utaje raslimali wangalau 2 ambazo hazijafikiwa na wazungu, kisha utuonyeshe kuwa hizo ndio wazungu wanazikosa. Kisha mimi nitakuambia sababu zaidi ya tatu halisi zilizoleta machafuko hapa nchini, na hakuna hata moja yenye msukumo wa mzungu.
Akikujibu nitag
 
Huu ndio ujinga ambao tunataka kuutoa kwenye vichwa vyenu

Tayar mmeshafikia tamati kwamba Jenista kauliwa na mfumo,unaweza kudhibitisha hizo taarifa

Mbona vijana mnakuwa wapuuzi hivi

Msiwe wachoyo wa fadhila kwahiyo unataka kusema hakuna maendeleo yaliyofanyika hapa Tanzania?

Au usingelipa bill za umeme na maji ndio ungeona kweli unafaidika na rasilimali za nchi hii

Acheni hizo mambo bwa

Inategemea unafanya harakati gani kwa malengo yapi
Mtu anaonekana mbaya ama mzuri kwa wingi wa aina ya matendo yao.. akiwa na mazuri mengii mabaya machache huyu atakuwa mwema mbele ya macho ya way, akiwa na mabaya mengi mazuri ya kuokoteza atakuwa mbaya.
Kwanini mungu ataweka mizani ya kupima mabaya na mazuri ya mtu?

Haya yetu huwezi kujipiga kifua ukajisifia kuwa tuna maendeleo.
Chora graph ya maendeleo vs maliasili zetu
Maendeleo vs muda toka tupate uhuru.

Ndio utagundua haya kwetu sio maendeleo tumesogea padogo mnooo, hatustahiki haya.

Kama maliasili zetu zinatuthaninisha tuslipie kuna ubaya gani.
Sijakataa kuna vimaendeleo, lakini haya hapa tulipo hatustahiki sisi watanzania.. mwaka wa 60 toka uhuru tuna gesi na matakataka kibao, ika kuna shule za udongo, watoto wanakaa chini darasa moja wanafunzi 100, madawa kipengele, maji safi na salama shida.. mwaka wa 60+
 
Kwa mada zako za sasa, na maandishi mengine uliyoweka humu JF wewe mkuu "ertugrul' huwezi kamwe kujiweka pembeni na uongozi huu unaotaka kujiweka mbali nao hapa.

Nashangaa hata hili hulionei haya kuliweka hivi hapa.
Umekwepa swali kiaina ndugu yangu "Kalamu"
 
Mtu anaonekana mbaya ama mzuri kwa wingi wa aina ya matendo yao.. akiwa na mazuri mengii mabaya machache huyu atakuwa mwema mbele ya macho ya way, akiwa na mabaya mengi mazuri ya kuokoteza atakuwa mbaya.
Kwanini mungu ataweka mizani ya kupima mabaya na mazuri ya mtu?

Haya yetu huwezi kujipiga kifua ukajisifia kuwa tuna maendeleo.
Chora graph ya maendeleo vs maliasili zetu
Maendeleo vs muda toka tupate uhuru.

Ndio utagundua haya kwetu sio maendeleo tumesogea padogo mnooo, hatustahiki haya.

Kama maliasili zetu zinatuthaninisha tuslipie kuna ubaya gani.
Sijakataa kuna vimaendeleo, lakini haya hapa tulipo hatustahiki sisi watanzania.. mwaka wa 60 toka uhuru tuna gesi na matakataka kibao, ika kuna shule za udongo, watoto wanakaa chini darasa moja wanafunzi 100, madawa kipengele, maji safi na salama shida.. mwaka wa 60+
Nakubaliana na wewe ni kweli maendeleo ambayo yapo sasa hayastahili,tungetakiwa tuwe zaidi ya hapo
 
Huu ndio upuuzi nisiokuwa na simile nao kabisa, lugha hiyo hiyo anayotumia Samia, na bado hata huoni aibu kuendelea nayo wakati ukitaka kujibainisha kuwa wewe ni tofauti.

Hawa "vijana wasiojielewa" mmewatoa wapi nyinyi. Hii ni lugha ya wapi hii?
Au hukumbuki pia kuwa Samia alitangaza hao vijana aliowaua walikuwa ni kutoka nje ya nchi, hukusikia akisema hivyo?
Mara, hao "vijana wasiojielewa" wamelipwa pesa ili wakafanye vurugu!

Ni nyinyi tu mnaojuwa ni kipi wanachotaka waTanzania; wengine wote ni wafanya vurugu na fujo? Sasa watu wa namna hii mnataka kuwatawala wa nini; huoni kuwa hamtaweza kuwaua wote na wataendelea kukataa huo upuuzi wenu?
Kwa lugha yoyote ambayo tunaweza kutumia,iwe vijana wasio jielewa,wenye hasira kali,wakurupukaji,haiondoi ukweli kwamba walijazwa upepo na watu ambao hawapo front kwenye maandamano

Hiki ndicho tunachopinga sisi ndugu,tunakataa kuwatumia vijana wa watu kufanikisha agenda za watu wengine
 
hivi kwa nini hutaki kuelewa "fujo na vurugu" zinasababishwa na nani.
Kwa nini hutaki kabisa kukubali kutazama hizo vurugu na fujo chanzo chake ni nini?
WaTanzania hawakuamua tu kufanya hizo unazoziita wewe vujo na vurugu; hawa ni watu wapole; wapenda amani miaka yote. Ni nani anayewaroga mara hii wawe watu wa vurugu na fujo bila ya sababu?
Watu tulioshikam

sikukiri chochote, ni mambo ambayo Samia na Genge lake mmeamua kuwafanyia waTanzania. Mtawaua hadi hapo watakapokubali matakwa yenu ya kuwatawala kwa nguvu; hili ndilo limetokea Oktoba 29; na litatokea tu kama mtaendelea kuwa na kiburi hicho cha kuwadharau waTanzania
ana miaka yote kama taifa kwa umoja wetu; ni nini tofauti kilichotokea wakati huu?

Kwa kuwa Samia ni mwanamke na muislam,siyo; nawe unakubali upuuzi huo?
Mr. Kalamu

Mbona unapenda sana kujificha kwenye hoja uislamu

Umetoa maelezo mazuri sana lkn chini umekuja kuharibu

Uislamu ni shida sana kwako? Tuzungumzie hoja na si dini ya mtu,inakufanya ukose uhalali hata wa hoja unayoileta hapa
 
Kamshauri mama ako. Halafu unatoa wapi ujasiri wa kumfananisha GADAFI na TAKATAKA? Au wewe huwa unaingiziwa gawio la mavuno ya rasilimali za nchi ndani ya akaunti yako? Upumbavu wenu ni mkubwa, ushenzi wenu hauvumiliki! Kama mlifurahi baada ya wananchi kutojitokeza kwa wingi barabarani basi jua ni kitambo kidogo tu mtalia mbwa nyie! Pimbi kabisa unamfananisha yule MAZERI wenu na GADAF?
 
Nakubaliana na wewe ni kweli maendeleo ambayo yapo sasa hayastahili,tungetakiwa tuwe zaidi ya hapo
Basi kama unakubali hivyo, ukubali viongozi tulionao ndio hawajatufik8sha huko, nchi imejaa ufisadi, cha kunufaisha nchi nzima kinanufaisha wachache..

Uzalendo umekwisha kabisa..
Sehemu ya serikali kupata bilioni 600, mtu yuko radhi apokee bilioni 100 yeye kisha serikali ipate bilioni 50.

Nchi hii ingekuwa mbali sana kama viongozi wangetanguliza taifa mbele.
 
Basi kama unakubali hivyo, ukubali viongozi tulionao ndio hawajatufik8sha huko, nchi imejaa ufisadi, cha kunufaisha nchi nzima kinanufaisha wachache..

Uzalendo umekwisha kabisa..
Sehemu ya serikali kupata bilioni 600, mtu yuko radhi apokee bilioni 100 yeye kisha serikali ipate bilioni 50.

Nchi hii ingekuwa mbali sana kama viongozi wangetanguliza taifa mbele.
Ni sahihi,kiongozi mmoja ambaye walau alionyesha dira ya kutuvusha toka sehemu moja kwenda nyingine ni Jiwe
 
Ni sahihi,kiongozi mmoja ambaye walau alionyesha dira ya kutuvusha toka sehemu moja kwenda nyingine ni Jiwe
Yes, ye ni atleast, japo kuna namna alikuwa anazingua ila ana uafadhali afadhali kidogo, kuliko huyu..
Tunahitaji viongozi wenye uadilifu A, uzalendo A+, visions A+ tutapiga hatua, ila hawa wa F,F na E moja, hatwendi popote.
 
Nyie mnaandika Ila hamuingii Field kupambana .

Mnafikiri CCM itatoka madarakani kwa maneno matupu ?

Sikia acheni hizi mambo za kuamini kuna MTU atakupambania .

Mnataka vijana warudi barabarani wauliwe tena au Mnataka nini

Nyie watoto wenu mnawalinda Ila mnataka watoto wengine wakaandamane .

Big NO tuta -push agenda hakuna maandamano nyie key body ni watu selfish
 
Nyie mnaandika Ila hamuingii Field kupambana .

Mnafikiri CCM itatoka madarakani kwa maneno matupu ?

Sikia acheni hizi mambo za kuamini kuna MTU atakupambania .

Mnataka vijana warudi barabarani wauliwe tena au Mnataka nini

Nyie watoto wenu mnawalinda Ila mnataka watoto wengine wakaandamane .

Big NO tuta -push agenda hakuna maandamano nyie key body ni watu selfish
Kuitoa ccm mpaka utokee mpasuko mkubwa ndani ya ccm, ambayo utaadhiri hadi majeshi ya dola. Inatakiwa wanasiasa wa upinzani watumie hiyo njia ya kisayansi, sio ukweli au maandamano, make haki hakuna zaidi ya kuishia kufa tu.
 
Mr. Kalamu

Mbona unapenda sana kujificha kwenye hoja uislamu

Umetoa maelezo mazuri sana lkn chini umekuja kuharibu

Uislamu ni shida sana kwako? Tuzungumzie hoja na si dini ya mtu,inakufanya ukose uhalali hata wa hoja unayoileta hapa
Kama unataka kujuwa, jibu langu ni rahisi sana.
"Uislam" kama dini siyo shida kwangu; shida kwangu ni watu wa aina yako mnaopenda kujificha ndani ya uislam huku mkifanya maovu kwa binaadam wengine. Hilo ni shida kubwa sana kwangu.

Sasa basi, kama unapenda kuelewa, nielewe hivyo; vinginevyo endelea kujificha huko kwenye dini huku ukiitumia vibaya; kama inavyotumika CCM wakati huu.
CCM kama chama kimegeuzwa kuwa cha kishetani kabisa; kumbe ni hao viongozi wenye matendo maovu ndio wanaoharibu.

Najuwa vyema maana ya swali lako hilo, na wala siyo mtu wa kwanza kutumia njia hiyo kupenyeza maana unayotaka wewe ionekane kuwa ndiyo shida yangu. Hii ni njia inayotumika kila mara na watu kama wewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom