Tujadili: Pre-ndoa... Plan B aka 'BIMA'

wakati mwingine ni vizuri kupitwa na wakati babu......
kuna sehemu nimesikia eti kuna dawa ya hospitali inayoweza kufanya mtu awe na feelings nawe.........
na aliyesema ni daktari siyo layman kama mimi
nikaona kweli duniani tunaendelea......
sasa masangoma sijui watatapeli wapi tena?
 

tatizo inakuwaje awe mchumba wakati hata hujamchunguza? Akesha kuwa mchumba hapo umechelewa sana maana ukiachana naye ujue ni kizaazaa kingine na kinakuongezea shinikizo la kumkubali ajaye hata kama unaona ana hitilafu kibao na baadaye hizo hitilafu kuja kukuletea maumivu makali. Peer pressure hujitokeza maana utasikia minong'ono ambayo huwezi kuipuulizia mbali hata siku moja wapambe wakidai huyu naye hakai na mchumba hata siku moja pengine ana mikosi au hana tabia nzuri n.k

Nionavyo katika marafiki ulionao wachunguze na unaposema ni huyu basi awe kweli ni yeye. Mpango wa kando kabla na hata baada ya ndoa ni dalili za ulafi na kutokujiamini na wakati ni ukuta kweli kwani mwishowe huwa ni kilio kwa wahusika kwani kamwe mpango huo hauwezi kukidhi mahitaji yako. tukumbukle hakuna mkamilifu kweye lolote ila kuvumiliana ndiyo chemuchemu ya maelewano na mafanikio kwenye mahusiano.
 

mwizi ni mwizi hakuna uwizi mdogo. Kwahiyo hakuna kisingizio kuwa huyu kala kidogo na huyu ni mlafi ukishachepuka wewe ni mlafi ule tonge moja au umeze mengi wewe ni mlafi tu tena umevimbiwa ila hujui ya kuwa umevimbiwa. Kwani ulafi wako umekupumbaza na kukufanya kuwa mpumbavu na utatafuta vijisababu vya kuhalalisha upumbavu wako lakini haitasaidia utabakia papo hapo hadi za mwizi ni arobaini na ndipo utajuta na kujisemea moyoni hivi nilitoka wapi na huyu?
 

ukiamini huu utapeli basi umekwisha. Kumpenda mtu siyo suala la kimwili ni la kiroho lazima umkubali na hakuna dawa ya hilo ila zipo dawa za kishirikina za kumpumbaza ili akuone tofauti na ulivyo lakini siyo za kumbadilisha misimamo yake dhidi yako na ndiyo maana zinapofubaa basi naye huzinduka na kibanio chake atakachokuweka nacho huwa ni mwendo mdundo hakomi mpaka ahakikishe umelipa siku zote ulimzomkamatia chini nazo na hakuna tiba pale!

Jisomee Mathew 5:26
"Assuredly I say to you, you shall not leave there till you have paid the last penny."
 
duh nimepitwa leo,kama ni maiti imefikishwa makaburini,imeingizwa hadi shimoni,imeanza kufukiwa mie ndo nafika msibani,hata sina cha kuongezea yote yamesemwa.
 
Well ambacho ninakumbuka au kwa uzoefu ni kwamba wengi wameoana-na wachumba ambao sio wale wa mwanzo, au waliotarajiwa, bali na wengine waliojitokeza kwa muda muafaka, mazingira muafaka, na kuwa na maono muafaka. Mara nyingi wachumba 'wa zamani' inabidi kuwaaacha...ustaarabu gani unatumika, ni juu ya mtu mwenyewe lakini wengi wameendelea kuwa marafiki wa familia mpya..na hata kushiriki kwenye sherehe za ndoa za wenzi wao wa zamani.

na labda niseme tu kwamba hapa sio ile mtu unakuwa na plan B intentionally au kama insurance kama ilivo 'siku hizi' hapana....inatokea tu kutokana na mizunguko ya dunia hii na hali halisi ya maisha....kuwa na wachumba wawili at the same time na wote umeahidi kuwaoa/kuolewa nao ni uhuni uliopitiliza....

CC: Dark City retired major general, FP snowhite, Kaunga, SnowBall, cacico, Mtambuzi, AshaDii, gfsonwin, Asprin, Kongosho, BADILI TABIA.

BCC: Nicas Mtei, kwa mafunzo zaidi. sosoliso, saudari, Erickb52.
 
Last edited by a moderator:
duh nimepitwa leo,kama ni maiti imefikishwa makaburini,imeingizwa hadi shimoni,imeanza kufukiwa mie ndo nafika msibani,hata sina cha kuongezea yote yamesemwa.

ulipotea wapi mtoto Asnam?
 
Last edited by a moderator:
inawezekana pia wakawa na ndoa ya amani/raha tele kwani plan B huwa zinatofauti kidunchu sana na plan A, vimeo vinaanzia plan D kuendelea.

Haha ila kweli lakin plan A akikatiaa tu roho lazi,a i undergo vibration
 

Hakuna kitu kama hicho mkubwa mwenzangu, ni utapeli tu kama utapeli mwingine.....

Kama kweli hiyo dawa ipo, basi naomba anipatie mimi.....

Babu DC!!
 

Haha daah kashindikana huyo sasa ebu chukulia alivyo na hadi z halafu kati ya hao alio nao nao wanazo plan mpaka d, hapo ndo tuko wangapi inapo take nafasi.
Lakini utafanyaje plans za ziada muhimu
 
Pengine zombie angekuwa staring ninge hinunua
Na wakaka je? Hawana changamoto hizo?

Mfano elmagnifico tumeshuhudi hapa hapa, kama haikuwa muvi.

Mie nadhani wote tumechachamalishana nywele kwa kweli.
 
Last edited by a moderator:
Aiseeeeeee!
 
The coastal Theory ya Mafiga matatu

Swali, yanaleta uhakika wa ndoa??Au ni vibuzi tu vya kununua unga kilo moja na dagaa?

Theory ya Mafiga matatu sio kwa ajili ya kuleta uhakika wa ndoa, havihusiani kabisa. Mafiga matatu huwa yanakuwepo kabla ya ndoa na pia yanaendelea kuwepo baada ya ndoa(ndani ya ndoa).

Ishu ni kwamba always kunakuwa na wanaume watatu:


Wa kwanza ni yule ambaye anamiliki jumla kiunyumba/kigharama, huyu mara nyingi ndiye anakuwa ndiye mtunzaji mkuu.

Wa pili ni yule ambaye ni chaguo la moyoni la mwanamke, ni yule ambaye mwanamke anampenda tu kwa jinsi alivyo.

Wa tatu ni yule ambaye ni fundi mzuri wa kupiga ile mashine.

Wenyewe(wanawake wenye theory hiyo) wanakwambia ni mara chache kumpata mwanaume mmoja mwenye sifa zote tatu.
 

Pale Msimbazi Center wanafundisha kwa maadili ya dini,(padri au mchungaji) kiafya (daktari) na maadili ya ndoa (wazazi wawili M na F waliodumu kwenye ndoa muda mrefu) kwahiyo angalau unaelimika kila upande huko kwingine sijui mafundisho yao yakoje. uwalu walu wetu tu hatusikii la mkuu wala lamwazini

hii plan B,C,D.... Huko ni kujilipua bora kushika moja likiponyoka unatuliza akili unatafakari unaanza upya
 
Mmmmh!
Plan B si kitu chema hapo utakua unaishi maisha ya mashaka , maanake hata message ikiingia tu wewe moyo unaenda mbio hivi utamwambia Plan A huyo ni nani.
Mimi nafikiri Kuwa upendo wa dhati ulionao juu ya mtu fulani ndio jibu, unapokua na upendo wa kweli hauwezi kuifikiria vinginevyo. Hapa cha msingi ni vema kujitunza kipindi chote cha mahusiano ili mambo yakienda kombo basi unakua hauna doa . Pia kabla ya kukubaliana uchumba ni vizuri mkajuana kwa undani pasipo kutenda dhambi hii inasaidi kufanya maamuzi pasipo shaka.
Unapoolewa au kuoa na plan B mara nyingi sana kunakua na migogoro ktk ndoa, hivyo ni bora vijana muwe waangalifu.
Kumbuka Plan B anaweza yeye akawa amekufanya wewe kua chaguo lake na hawezi kuishi bila wewe , je huoni kuwa utakua umemuumiza mtu hapo na hatakusahau maisha yake yote.
 
Kuweka kwa muhtasari ni kuwa asilimia kubwa ya wanandoa hawajaoa/olewa na wapenzi wao wa kwanza.

CC: Kaunga
 
Last edited by a moderator:

This is why naipenda JF
 
Watu wote hap at per si nikuuchosha mwili

 

hapo kwenye red hapo.. ndo imekuwa fashion siku hizi.. they don't actually say kwamba ni plan B.. ila wanaita multiple choice.. ila kwa wadada wanaotafuta ndoa kwenye multiple choice mara nyingi wanakuwa wao picked up Kaizer.. unajua ni kwanini..? kwa sababu wanafuata taratibu zote za uke tarajiwa kwa kuwa wapole.. wasikivu.. wanyenyekevu.. wenye upendo.. all that in a full package (japo baadae wakishaingia ndani ya ndoa wengine wataonyesha their true colors)..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…