Tujadili: Pre-ndoa... Plan B aka 'BIMA'

Tujadili: Pre-ndoa... Plan B aka 'BIMA'

Dah!Dunia hii ina mambo sana

Sababu kubwa ya kuwa na plan B hasa ni kutojiamini,kama hujiamini ni vigumu sana kumuamini mwenzako

Sababu nyingine ni kuporomoka kwa maadili,watu siku hizi wanaishi bila utu na ubinadamu

Labda ndo maendeleo!
 
Aisee
so uchumba umepoteza maana yake halisi au watu wanatumia gear ya uchumba kupata chance ya kumgegeda mtu???

so sad kusema NDIYO!
lakini NDIO ukweli uliopo!
yani hizi engagemet ring tu hizi mbn zinagawiwa sana!af na hiv siku hizi ndo wanaitaga wenyewe suprise!hata baba hajui wala kaka,watu wanavalishana pete!wapo wanaomaanisha kweli lakini wasio na stara na miili yao wanazimtumia sana hzi kuuumiza wenzao!
zamani mabinti wakitolewa mahari wanakuwa na uoga?siku hizi wanabaki kukwambia ah da snowhite kwani unafikir na mwenywe ni wa kumuamini banaaa,hebu niache mi nikajirushe zangu!
ah unabaki na ghaaa!ndo mumo mumo ndoa zinatokea humo,unategemea nini,
unafikir ni umri ?hapana ni basi tu watu tumeamua kujitoa fahamu siku hiz!
 
Kaunga unasema Plan B...lolz.....naiona kama ni mada ngeni japo ni challenging!..Kama ulivosema kwa zamani nadhani ilikuwa ngumu kidogo as compared na sasa...Nadhani ni kawaida kwenye maisha kuwa na 'back up' in case ukitokea wakati wa emergence ukapoteza kitu flani basi kiulaaiiini unachukua akiba yako....Lakini kwenye mahusiano nadhani ni ngumu kidogo kuiweka kwenye uhalisia hasa kwa watoto wa kiume..Japo nahisi kwa watoto wa kike inaweza kuwepo (manake wanafuatwa)....Katika zama za sasa ambapo mwolewaji/muoaji ndio wanakuwa 'centre' of everything kwenye ndoa nahisi 'backups' zinaweza kuwepo unlike zamani ambapo 'wazazi' ndo walikuwa 'play makers' kwenye 'uoaji/uolewaji wa watoto wao...

Nadhani kimsingi hakuna Tatizo kuwa na Plan B...as long as mtu akishakuwa committed na mwingine hadi ndoa basi ataachana na backups zote. UZURI wake ni kuwa inasaidia sana hasa kipindi hiki ambamo WASANII wamekuwa wengi... Ndoa zimekuwa kama 'a certain stage of life' ambayo unalazimika tu kuipitia but is not something that is driven by love between the two...Na kwa sababu siioni kama ni tatizo siwezi shauri sana mbinu za kuachana nayo..................

Waoh interesting and honest observation sasa, should we put Do and Dont Do guides zitakazo wainform watu wanaokuwa na plan B. Say ....uwe na simu mbili, moja ya mchuchu na nyingine ya plan B? au unaonaje? Maana watu wanachemka kila siku (kuna bandiko mchumba kaenda kwa mdada chuoni hakumkuta na kaambiwa hayupo since jana (kaenda kwa plan B possibly).
 
Nakumbuka sana mafundisho ya dini nikiwa secondary kuhusu Urafiki, Uchumba na Ndoa; tuliambiwa (na kweli ina make sense) kuwa ni vizuri kuwa na marafiki wengi, lakini mchumba ni mmoja na kipindi cha uchumba maana yake unakuwa umefungwa (huwezi kuruhusu mchumba mwingine in case umemkubali wa kwanza); hiki ni kipindi cha kuchunguzana tabia kabla ya kujifunga moja kwa moja kwenye ndoa.

Lakini kwa sasa idadi kubwa ya watu (hasa wadada) walioko kwenye uchumba wana kuwa na bima au plan B au mpango wa kando. Hali hii ikija kugundulika mara nyingi hupelekea muhusika kukosa yote hata kama alikuwa anapenda kuolewa.

Sasa wana jamvi naomba tujadili kuhusu:-
  • ulazima au umuhimu wa plan B
  • Kiini cha tatizo hasa ni nini?
  • Nini kifanyike ili hii hali isiendelee?

cc lara 1, amu, Paloma, Nicas Mtei, Eiyer, Evelyn Salt na walioko kwenye ndoa watuambie waliolewa/oa na plan A au B gfsonwin, @fp, snowhite, Dark City, Mtambuzi, Wiyelele Kaizer hata wale walio kwenye complicated situation kama The Boss, KIKUNGU SnowBall Kongosho et el karibuni.


The chanceslikelihood of running out of rope are VERY high NOWADAYS....Therefore:

..........When you run out of rope; grab onto faith.......... T.B Joshua

"Plan B" is what you will "grab" when you will run out of "rope"!
 
wanaume siku hizi wanasababisha wadada wawe na plan B.....maana unakuta dada kajitoa ilhali mkaka anagegeda tu....akiangalia na umri unasonga anakuwa nao 2/3 atayefika bei tu ndo huyo huyo

Kwa kiasi kukubwa nakubaliana na wewe BADILI TABIA ndio maana wenye plan B wengi ni wadada, l hope watabadili tabia.
 
Last edited by a moderator:
Kwangu, wanaume walio wengi kuwa na Plan B ni kitu cha kawaida, hata baada ya kuoa kuwa na "kidumu" kunasaidia kupunguza pressure. Ukiwa stressed na huyo mmoja, iwapo ndo una huyo tu haaa! Utakufa kwa pressure iwapo akakutendea kosa kubwa! Lakini kama una plan B, naona hata mtu unakuwa stable. Ila kwa wanawake sio vizuri wakawa kama sisi. Historia tangu mwanzo inasema "A man was born a polygamist". Kwa hiyo ipo kwenye damu.
Naona mnatuambukiza hiyo kitu ya historia maana imeanza kuingia kwenye damu zetu pia!
 
Nakumbuka sana mafundisho ya dini nikiwa secondary kuhusu Urafiki, Uchumba na Ndoa; tuliambiwa (na kweli ina make sense) kuwa ni vizuri kuwa na marafiki wengi, lakini mchumba ni mmoja na kipindi cha uchumba maana yake unakuwa umefungwa (huwezi kuruhusu mchumba mwingine in case umemkubali wa kwanza); hiki ni kipindi cha kuchunguzana tabia kabla ya kujifunga moja kwa moja kwenye ndoa.

Hapo tu ndo tunapotofautiana definition ya UCHUMBA.

Mimi nilifundishwa kuwa...
Wakati wa URAFIKI ndiyo wa kuchunguza yote kuhusu tabia ya huyo ambaye ungependa awe mchumba wako.

Wakati wa UCHUMBA ni pale ambapo ninyi wawili mmeshachunguzana mmependana na kuona tabia, interests na dislikes zenu zinafanana na mnaweza kuishi pamoja na kuanzisha familia.

Hapa kuna njia mbili za kuonesha kuzaliwa stage hii ya Uchumba.

1. Ile traditional ambapo unaenda kujitambulisha kwa wazazi wa binti officially kama prospective husband (suitor)

2. Ile ya kuita marafiki zako na kumuuliza mwenzi wako "Will you marry me?" ambayo huhitimishwa kwa kuvalishana pete ya uchumba.

UCHUMBA basi si wakati tena wa kuchunguzana tabia bali ni wakati wa kupanga na kujadili juu ya maisha yenu ya ndoa..kukubaliana juu ya mambo kama finances, watoto, imani n.k.

Wakati huu pia ndio hasa wa kupanga juu ya harusi yenu...

Tulifundishwa kuwa ni heri kuwa na urafiki na binti kwa muda mrefu kuliko uchumba kwani mnapokuwa marafiki (meaning with n strings attached) mnakuwa na uwezo mkubwa wa kufahamiana kiundani bila limitations za 'mchumba wangu akijua niko ivi si ataniacha?'

Pia, Tulifundishwa kuwa uchumba usizidi mwaka mmoja ndipo mfunge ndoa.

NB: Kuna ile feeling ya INSECURITY ambayo inawalazimu wapenzi kukimbilia uchumba ETI kuogopa ataibiwa.

Mfano mzuri ni wa wazazi wangu:
Walisoma A-level shule za jirani (Jangwani na Azania). Walikuwa wote Christian Union moja...baba akiwa mwenyekiti na mama akiwa mweka hazina. Waliimba wote kwaya...THEY WERE JUST FRIENDS THEN.

Wakaenda wote JKT MAKUTOPORA. Walikuwa kombania tofauti lakini walikuwa marafiki bado.

Wakaenda chuo..mama NZUMBE IDM, baba UDSM..walikuwa marafiki bado.

Baada ya Chuo mama akabaki Morogoro baba akawa Dodoma..walikuwa marafiki bado...na walikua na hisia za mapenzi baina ya kila mmoja..ila they took their time kufahamiana tu kwanza bila wasiwasi wa kuibiwa (na mama anasema walikuja wengi..wakaka wenye kazi zao nzuri...vibosi vya Tanarese pale Morogoro, malecturer wa Mzumbe et al) kabla hata hawajasema yale maneno matatu I LOVE YOU.

Baba akamchumbia mama 1982 na 1983 December wakaoana...


I think ndiyo maana mimi mahusiano ya siku hizi yananishinda..ngoja nifanye mchakato wa kuingia utawani..who knows..ninaweza kuwa the next Pope.:A S 39:
 
Hii bana hata bila kuwapa recipes wata-apply tu..manake as nilivosema 'uncertainty' ndizo zinafanya watu wawe so much scared hivyo kutafuta backups....


Waoh interesting and honest observation sasa, should we put Do and Dont Do guides zitakazo wainform watu wanaokuwa na plan B. Say ....uwe na simu mbili, moja ya mchuchu na nyingine ya plan B? au unaonaje? Maana watu wanachemka kila siku (kuna bandiko mchumba kaenda kwa mdada chuoni hakumkuta na kaambiwa hayupo since jana (kaenda kwa plan B possibly).
 
Dah!Dunia hii ina mambo sana

Sababu kubwa ya kuwa na plan B hasa ni kutojiamini,kama hujiamini ni vigumu sana kumuamini mwenzako

Sababu nyingine ni kuporomoka kwa maadili,watu siku hizi wanaishi bila utu na ubinadamu

Labda ndo maendeleo!

I use to jiamini sana you know; lakini ulikuja kunidiss mwisho wa siku. Huoni our online love case ndio inayofanyika in real life?
 
The chanceslikelihood of running out of rope are VERY high NOWADAYS....Therefore:



"Plan B" is what you will "grab" when you will run out of "rope"!

I honestly like this post! Hata nami mwisho wa siku nikishindwa kufikiria napata tumaini jipya kwenye FAITH
 
Nakumbuka sana mafundisho ya dini nikiwa secondary kuhusu Urafiki, Uchumba na Ndoa; tuliambiwa (na kweli ina make sense) kuwa ni vizuri kuwa na marafiki wengi, lakini mchumba ni mmoja na kipindi cha uchumba maana yake unakuwa umefungwa (huwezi kuruhusu mchumba mwingine in case umemkubali wa kwanza); hiki ni kipindi cha kuchunguzana tabia kabla ya kujifunga moja kwa moja kwenye ndoa. Lakini kwa sasa idadi kubwa ya watu (hasa wadada) walioko kwenye uchumba wana kuwa na bima au plan B au mpango wa kando. Hali hii ikija kugundulika mara nyingi hupelekea muhusika kukosa yote hata kama alikuwa anapenda kuolewa. Sasa wana jamvi naomba tujadili kuhusu:-
  • ulazima au umuhimu wa plan B
  • Kiini cha tatizo hasa ni nini?
  • Nini kifanyike ili hii hali isiendelee?
cc lara 1, amu, Paloma, Nicas Mtei, Eiyer, Evelyn Salt na walioko kwenye ndoa watuambie waliolewa/oa na plan A au B gfsonwin, @fp, snowhite, Dark City, Mtambuzi, Wiyelele Kaizer hata wale walio kwenye complicated situation kama The Boss, KIKUNGU SnowBall Kongosho et el karibuni.
wengi wanachofanya sio kuwa na plan b bali muoaji mostly ndo anakuwa yuko no 2 mdada yupo na mtu wake anaempenda,lakini huyo mtu hana mpango wa kuoa so muoaji anapojitokeza,dada anakubali ndoa huku anakuwa mgumu kumuacha wa kwake so waoaji wengine wanachunguza ndo wanagundua hilo na kusitisha ndoa, ndoa kwenye jamii yetu ni deal sana bado,kuolewa ni bahati wanasema,so kukataa muoaji hata kama hapendwi ni ngumu..
 
Last edited by a moderator:
labda tujiulize kwanini watu wanakuwa na plan B, ni situation inawalazimu au ni tabia tu?
situation inawalazimu,tamaa, hawajijui wanataka nini, kila mmoja anakaa na mwenzie kimachale akihofia kuachwa, mdogo wa friend wangu tumekula wali wake dec, huyu mdogo wetu alikuwa ana boyfriend wake aliekuwa anamtegemea kwenye safari yake ya kuanziasha familia, matokeo yake mrembo alikuja kujua mkaka ana gal mwingine anaetaka kuwekeza kabisa, walilumbana wakatengana, mdada alikuwaga na plan B akaivuta chap kukaba pengo lililoachwa, yule mkaka aliekuwa anategemewa na yeye akamwagwa huko na hiyo plan B yake na yeye akakaba plan C ikaziba pengo,huyu mdogo wetu na huyu boyfriend wake aliekuwa anamtegemea kuanzisha nae familia ndoa zao ilikuwa siku moja na kila mtu na plan B , C zake, life limekuwa ovyoooo sana.
 
Mahusiano yamejaa udanganyifu mwingi vijana wengi wanaumizana tena baada ya kupotezea kipindi adimu cha maisha ya mahusiano yaani 20z kwa wanawake na late 20z na 30z kwa wanaume. Vijana wengi wameingia ktk mahusiano huku wakiwa hawajui hata wanachokitaka kwenye hayo mahusiano. Hili linachangia kwa kiasi kikubwa vijana kuwa na Plan B ili in case A ikafeli anakuwa na B yakuendeleza...

Kwa sasa vijana wa kike na wa kiume wote wana plan A na B na hii ni kutokana na ukweli hapo juu kwamba mahusiano hayapo kama ukweli utakuwa ndiyo silaha ya kuanzisha.
 
Back
Top Bottom