Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,252
- 11,652
Ukweli mimi huwa sijui inakuwaje mpaka mtu anakuwa Attractor.
Wanasema beauty is in the eye of beholder (hii naiamini kabisaaaaaaa)......
lakini unaweza kushangaa mtu unajiona wa kawaida tu lakini hali inakuwa mbaya sana......
kuna siku niliwahi kusema hapa nachukia sana kutokewa wengi hawakunielewa kwa nini.
Kikawaida mimi ni mpole sana, na huwa sio muongeaji sana hasa kwa watu ambao siwafahamu.
naweza kusafiri Dar mpaka Moshi kwa basi nikaishia nikamsalimu tu seat mate wangu, labda awe muongeaji sana na anilazimishe sana kuongea naye......
tabasamu ndo kabisaaaaaa, huwa natabasamu tu nikikutana na mtu ambaye namfahamu. zaidi ya hapo huwa sina tabasamu usoni, lol!
kitu cha ajabu, kuna siku nilikaa na baba mmoja kwenye basi, kumsalimu, na kiuhakika sikuwahi kumwona sehemu, lakini aliniambia kitu ambacho kila mara nakikumbuka, na alikuwa sahihi kabisa
Alikwambia nini kwani??
Babu DC!!