ok wakubwa, jirundikieni tu hayo mapesa wakati mafukara vijijini wanaangamia. lakini jueni hata mngekula vipi yote bure tu, ukishindilia sana tumbo sana sana unaishia tu kuvimbiwa, kujamba ushuzi unaonuka na kunya mav. mengi tu basi. na mwisho wa usiku utakufa tu kama atakavyokufa fukara na kuoza tu kama kawaida. ni heri mngewafikiria na mafukara pia, mkagawana nao kidogo na nyie mkala kiasi. mwisho wa siku maisha hayana maana sana kihivyo. Mobutu Seseseko Nguku Wa Zabanga, Sani Abacha, Sadamu Hussein, Ghadafi nk walijirundikia mapesa kibao leo wapo wapi? maisha ya kimaskini ya Mwalimu Mkuu Mzee Nyerere na ya Mzee Madiba yana maana kubwa sana kwa humanity kuliko ya hao majuha yaliyokula hadi kuvimbiwa na kuishia kunya mav mengi tu bure. maisha ni ya kupita tu jaman, tuache ubinafs ulikithiri...hili la mishahara mikubwa ya kuogofya katikati ya malofa wa kutupa inanikumbusha kitabu kimoja cha enzi hizo kiliandikwa....."Tumbo Niachie Nimwekee Mandawa Uji"....lakini wapi, tumbo lilikataa kabisa na mwishowe Mandawa hakuwekewa uji. mnakula, mnavimbiwa kisha mnatapikia kwenye ndala(zilizotoboka) miguuni pa walalahoi..aibu yenu mafisadi!!!!