Gashongoile
JF-Expert Member
- Jun 13, 2013
- 487
- 145
Mi pia nawashangaa sana hao wanaojiita waajiri, na wanaotaka kuambiwa mishahara ya waliowaajiri. Hivi inakuwaje unamwajiri mtumishi halafu unasubiri mtu mwingine akwambie mshahara wake. Kama mnajiita waajiri (ambayo ni kweli kwa namna moja ama nyingine), si mlipaswa kutamka kiasi gani atalipwa huyo mwajiriwa. Kwani hao vilaza mnaowapeleka bungeni si ndio wanaopitisha hiyo mishahara. Kwani wao si wanaipitisha kwa niaba yenu. Basi kwa hoja zenu maana yake wanaopaswa kuujua mshahara wa Rais na pm ni wale tu waliompigia kura maana hao ndio waliomwajiri. Karibuni na mitusi yenu, maana najua mishipa ya Shingo itawasimama na mapovu yatawatoka
Kwa jinsi ulivyojibu hii posst ninauhakika wewe ni wa KIKE maana auelewi haya unachojadili. Mlalia tumbo mkubwa wewe kuna siri gani kujua mshahara wa Raisi?