Tuanzishe Kampeni ya #Kataa Muungano

Tuanzishe Kampeni ya #Kataa Muungano

Sasa nani kakubana?
Ardhi mnamiliki.
Biashara mnafanya.
Na Hambaguliwi.
HESLB mnakopeshwa kwa Kodi za watanganyika.
Na Ajira mnapata huku Tanganyika
Wazanzibari ndo wanafaidika na huu muungano, ukivunjwa, ardhi zote mnanyanganywa, ajira zote mnapokonywa na hamtasomeshwa kwa hela za walipa Kodi wa Tanganyika.
Maana huko Zanzibar, Mtanganyika hawezi miliki ardhi, hawezi Jenga nyumba, biashara kule ni ngumu kufanya kwa Mtanganyika, Kuna ubaguzi wa kidini na wa kikabila kwa Watanganyika .
Sasa Muungano una Faida gani kwa Mtanganyika?
Siyo kirahisi hivyo. Kuna mambo ya haki za binadamu na kina UN wataingilia kati.

Siku muungano ukivunjika inawezekana kukawa na kipindi cha mpito ambapo inawezekana Wazanzibar waliopo bara wakapewa uhuru wa kuchagua, kubaki bara na haki zao zote zikalindwa mfano kupewa uraia wa Tanganyika au kurudi Zanzibar na kinyume chake. Rejea kuvunjika kwa Sudani. Wapo weusi waliamua kubaki Sudan ya Khartoum

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Hoja ya kipumbavu mno.
Sisi shida sio muungano.
Shida ni wewe bwege keyboard worrier
Mkiambiwa muitoe ccm nyoko mnasema hamna mbadala,
Bado kunajisiwa tuu ndicho mlicho bakizwa.

Hoja mezani bandari isiuzwe, base line katiba rasimu warioba, action kuandamana kuitoA ccm
Haya ndo maamuzi ya kiume
Hivi kimantiki, kuna tofauti gani ya kimaoni kati yako wewe na ya mtoa hoja?

Halafu nawashangaeni sana baadhi ya wanaJf, kila utapotaka kujenga hoja lazima u crash kwanza hoja ya mwenzako au uanze na tusi!

Hii ina afya gani katika kujenga maoni jumuishi?
 
Yanafanaikiwa kwa sababu ya Kukosa Elimu,
Ongezea na maandamano ya Mwenge hivi wakuu wa wilaya mikoa ,mawaziri wanafanya kazi gani hadi Mwenge ukazindue miradi mipya,na wenyewe ni wa kuukataa

Tunaitaji Katiba mpya ,ila serikali tatu ni kurudia kulekule hamna nchi ndani ya nchi ,either iwe nchi moja nyingine iwe jimbo ama tuuvunje
Kwani miundo ya Serikali za shirikisho huwaje?

Ninavyofahamu, kila nchi hujulikana kama "State" ndani ya shirikisho na hujifanyia mambo yake kwa ukamilifu ndani ya "United", ikiwa na Bunge lake na Govaner wake.

Kwetu sisi kwa kuwa masikio yashazoea neno "Rais', basi pawepo na Rais wa Tanganyika, Rais wa Zanzbar na Rais wa Muungano kama Katiba rasimu ya Warioba ilivyopendekeza.
 
Wenzetu Watanganyika washalitumbua jipu, sasa ni zamu yetu Wazanzibari kuukamua usaha mpaka tuufikie moyo wake na kuliponya moja kwa moja jeraha.

Ingefaa tuwaulize wenzetu, kama wao wameumia mno kwa kuona uhuru na rasilimali zao zimeingia hatarini kwa mkataba mmoja TU wa bandari, wanadhani wametuumiza kwa kiasi gani sisi wenzao kwa miaka 60 yote hii tangu walipoupora uhuru na mamlaka yetu YOTE na kutudumaza kiustawi kwa kutufungia njia kuu za kiuchumi.

Wanaumia kuona Mzanzibari anakuwa rais wa Tanzania hata kama ni kisheria na kikatiba, wakati wao wamejipa mamlaka ya kimabavu, kwa miaka yote hii ya kutupangia nani atuongoze Wazanzibari na kwa mipaka gani ya mamlaka!

Tuwathibitishie kwamba iwe iwavyo, sasa tumeshabaini bila chembe ya shaka, kwa yaliyotoka kwenye ndimi zao, kwamba wana chuki kubwa dhidi ya Uarabu na Uislamu na kwamba chuki hizo ndizo zilizochangia pia kutubana tusifurukute ndani ya 'muungano'; na ndio maana kina Lukuvi na Sitta hawakuulizwa chochote na yeyote waliponena waliyoyanena dhidi ya Uarabu na Uislamu, kwa sababu waliwasilisha na kuwakilisha mtazamo rasmi wa Tanganyika kuhusiana na Wazanzibari katika muungano.

Na kwa hapa tulipofika tukubaliane kwamba, kama ni kuuendeleza muungano, basi hakuna mbadala mwingine wa mahusiano yetu ya kisiasa na Watanganyika isipokuwa kufuta kwanza jina Tanzania na kurudi kwenye Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuamua ama kuwa na muungano wa mkataba au wa serikali tatu. Ghairi ya hivyo ni kila nchi kurudi kwenye asili yake ya taifa na nchi kamili

Nyani walioletwa juzi na kina Tippu Tipp tokea Congo wanajiita Wazanzibari na kubana pua. Kama sio Nyerere na Kambona nani angemfukuza Sultani?
 
20230610_014206.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu muungano wa mchongo siku ukivunjika kuja huku na sisi kwenda kule mpaka visa ???vipi kuhusu maduka ,mashamba na nyumba zao walizojenga huku naona wao ndio wataopata hasara maana kwao mbongo hamiliki ardhi zitabinafsishwa au ndio wataamua wawe waBara haha kazi ipo!
 
Scholarships zikitoka kule ukiapply unaulizwa kama wewe mzanzibar kama sio hupati ila zikitoka huku na wao wanaapply kwakua mtanzania huu Muungano wa kidwanzi bora ufe tu kila mtu ale 50 zake
 
Wazanzibari wako tayari hata leo kuvunja muungano, ajabu wanaokataa na wanaoulinda muungano ni wa Tanganyika wenyewe, sasa kwanini?
Ukimsikiza hata lukuvi alipoongea pale kanisani utaelewa kabisa hadi kanisa halitaki kuvunja huu muungano sasa kwanini?
#kataamuunganoniutapeli
 
Wenzetu Watanganyika washalitumbua jipu, sasa ni zamu yetu Wazanzibari kuukamua usaha mpaka tuufikie moyo wake na kuliponya moja kwa moja jeraha.

Ingefaa tuwaulize wenzetu, kama wao wameumia mno kwa kuona uhuru na rasilimali zao zimeingia hatarini kwa mkataba mmoja TU wa bandari, wanadhani wametuumiza kwa kiasi gani sisi wenzao kwa miaka 60 yote hii tangu walipoupora uhuru na mamlaka yetu YOTE na kutudumaza kiustawi kwa kutufungia njia kuu za kiuchumi.

Wanaumia kuona Mzanzibari anakuwa rais wa Tanzania hata kama ni kisheria na kikatiba, wakati wao wamejipa mamlaka ya kimabavu, kwa miaka yote hii ya kutupangia nani atuongoze Wazanzibari na kwa mipaka gani ya mamlaka!

Tuwathibitishie kwamba iwe iwavyo, sasa tumeshabaini bila chembe ya shaka, kwa yaliyotoka kwenye ndimi zao, kwamba wana chuki kubwa dhidi ya Uarabu na Uislamu na kwamba chuki hizo ndizo zilizochangia pia kutubana tusifurukute ndani ya 'muungano'; na ndio maana kina Lukuvi na Sitta hawakuulizwa chochote na yeyote waliponena waliyoyanena dhidi ya Uarabu na Uislamu, kwa sababu waliwasilisha na kuwakilisha mtazamo rasmi wa Tanganyika kuhusiana na Wazanzibari katika muungano.

Na kwa hapa tulipofika tukubaliane kwamba, kama ni kuuendeleza muungano, basi hakuna mbadala mwingine wa mahusiano yetu ya kisiasa na Watanganyika isipokuwa kufuta kwanza jina Tanzania na kurudi kwenye Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuamua ama kuwa na muungano wa mkataba au wa serikali tatu. Ghairi ya hivyo ni kila nchi kurudi kwenye asili yake ya taifa na nchi kamili
Uarabu gani unaomhusu Mpemba na Muunguja?
 
Wewe nahisi hauko saw rudi darasani kwanza ,eti pwani wapewe zenji wapewe kwa sababu tunawaogopa au ? Mmechukua bagamoyo mnataka na pwani mzima!
Tushasema tunaukaataa Muungano wa kiboya
Hata ramani hujui kusoma ?
 

Nyani walioletwa juzi na kina Tippu Tipp tokea Congo wanajiita Wazanzibari na kubana pua. Kama sio Nyerere na Kambona nani angemfukuza Sultani?

Huyo tipp topp ulimjua wapi ?? Si historia mnayosomeshwa Lumumba baadaye mkapewa kikoi na kanga , paketi ya sigara na chupa ya soda , na kukimbiza mwenge mchana umulike . Of course bila kuambiwa hivyo hamwezi kutawaliwa na CCM
 
Mama Samia siamini kwa kale kasura kake kama anaweza akawa mpigaji kiasi hicho.
 
Kwani miundo ya Serikali za shirikisho huwaje?

Ninavyofahamu, kila nchi hujulikana kama "State" ndani ya shirikisho na hujifanyia mambo yake kwa ukamilifu ndani ya "United", ikiwa na Bunge lake na Govaner wake.

Kwetu sisi kwa kuwa masikio yashazoea neno "Rais', basi pawepo na Rais wa Tanganyika, Rais wa Zanzbar na Rais wa Muungano kama Katiba rasimu ya Warioba ilivyopendekeza.
Hoja ni kuwa haki sawa,kama tunataka shirikisho la pamoja badi haki za Mtanganyika akiwa zanzibar ziwe sawa na mzanzibar akiwa Tanganyika ,ndoa ya upande mmoja haikubaliki ,haiwezekani ww kila kitu ujenge ukweni,ununue gari ukweni,usomeshe ukweni,na shoo upangiwe mda,misaada yote ya harusi kisiba utoe, ila kwenu hawataki hata kiberiti kiende kea kigezo sisi Ukoo wetu mdogo wao Ukoo mkubwa ,huo ni utapeli,nakazia kwa herufi kubwa
#KATAAMUUNGANO,MUUNGANONIUTAPELI
 
Hata ramani hujui kusoma ?
Hizi ndo hasali za Muungano,yani unaungana na Mtu hata elimu hamna ,umepa kila kitu mwanamke badaye anakwambia mali zote ni zangu tulitafuta wote wakati alikuja na ndala zake hata mfuko wa nguo hana,ona huyu eti pwani apewe Zanzibar, Aisee shekh ulambi hata mchanga yani kwenu hukohuko na ukija huku tunataka visa.
#Kataamuungano,muunganoniutapeli
 
Hizi ndo hasali za Muungano,yani unaungana na Mtu hata elimu hamna ,umepa kila kitu mwanamke badaye anakwambia mali zote ni zangu tulitafuta wote wakati alikuja na ndala zake hata mfuko wa nguo hana,ona huyu eti pwani apewe Zanzibar, Aisee shekh ulambi hata mchanga yani kwenu hukohuko na ukija huku tunataka visa.
#Kataamuungano,muunganoniutapeli
kwani wewe unapeleka nn kule Zanzibar ? hata kiwanja huna ,njaa kali ,unapiga domo tu🤣🤣
 
kwani wewe unapeleka nn kule Zanzibar ? hata kiwanja huna ,njaa kali ,unapiga domo tu🤣🤣
Nipeleke chanini ,acha maswala ya personal attack,sisi kama watanganyika hatuoni manufaa ya Muungano,
Halafu jibu hoja,punguza hisia mkuu .
#Kataamuungano,muunganoniutapeli
 
Back
Top Bottom