Tuandamane Aisee! Ubungo Tanesco Isivunjwe...

Tuandamane Aisee! Ubungo Tanesco Isivunjwe...

Pumba tu badala ya kuandamana kuvunjwa kwa nyumba za watu masikini. Unataka kuandamana jengo la Tanesco
 
Unaandamana upo nchi Gani? Jaribu ndo utajua faida ya kuandamana ni IPI ?
Andamana peke yako itapendeza
 
Nawaletea mada hii ili kujaribu kuishinikiza serikali iangalie upya kuhusu kubomoa jengo lile lenye gharama kubwa mali ya Tanesco pale Ubungo.

Ni kweli laweza kuwa ndani ya hifadhi ya barabara, lakini bado utaalamu waweza kufanyika kama tulivyoona katika tread tofauti humu na flyover ikajengwa bila kubomoa jengo lile lenye thamani ya mabilioni ya fedha. Kusudi ni kuwa hizo bilioni kadhaa za kujenga jengo jipya zipelekwe maeneo mengine kuongeza nguvu za uzalishaji umeme tukielekea kwenye uchumi wa viwanda.

Matokeo haya yanaweza kuipa picha serikali nini cha kufanya. Naamini mshauri mwelekezi kubadili mchoro kwa eneo lile la jengo hawezi kutuchaji hata bilioni moja.
Jibu NDIO, HAPANA au SIJUI
 
Alisema Hashauriki, akiamua ameamua. Kama hashauriki, je kushinikizwa si ndo balaa?

Unataka baba Jesca alambe matapishi yake?
 
Sina hakika sana kama malaika mkuu ni muumini katika kura za wengi wape!

Itakuwa ni ndoto kubadilisha mawazo yake yanayopingwa hata na wasioona!
 
Mkuu ili kutoa mkanganyiko tueleweshe maana ya ndiyo, hapana na sijui.
Kama swali lilivyo, kusema Ndiyo ni kukubali libomolewe, Hapana ni kukataa lisibomolewe na Sijui ni kutokuwa na ufahamu wa jambo hilo
 
Hivi mbona waafrika tunaakili ndogo sana? majengo mangapi tena bora na mazuri kuliko hilo la Tanesco yamebomolewa duniani kupisha miradi ya maendeleo? it means magufuli yeye ni kichaa aamrishe jengo libomolewe bila sababu? au wewe ndio kichaa unaeanzisha poll ya uenda wazimu? tueleze sababu kwanza kwann jengo lisibomolewe ndio tupige kura,
b
 
Sina hakika sana kama malaika mkuu ni muumini katika kura za wengi wape!

Itakuwa ni ndoto kubadilisha mawazo yake yanayopingwa hata na wasioona!
Muhimu ni kuwa hata sisi tusiokuwa na mamlaka tutakuwa tumeonyesha hisia zetu. Kama kuna Waziri mwenye kifua anaweza kulipeleka hili katika Baraza la mawaziri na wakajadili upya (kama waliwahi kujadili awali) na kuona kuwa Tanesco hiyo inahitaji fedha kuweza kujiongezea nguvu kuzalisha umeme kwa ajili ya viwanda nasio kujenga jengo jipya
 
Hivi mbona waafrika tunaakili ndogo sana? majengo mangapi tena bora na mazuri kuliko hilo la Tanesco yamebomolewa duniani kupisha miradi ya maendeleo? it means magufuli yeye ni kichaa aamrishe jengo libomolewe bila sababu? au wewe ndio kichaa unaeanzisha poll ya uenda wazimu? tueleze sababu kwanza kwann jengo lisibomolewe ndio tupige kura,
b
Hakika wewe ni punguani! Unajilinganisha na wengine wenye uwezo? Kabla ya kufanya jambo lazima uangalie uchumi wako ukoje hata kama ni maendeleo. Wewe ukiona Bahresa anavunja nyumba nzuri ili apate parking ya magari yake nawe utavunja yako ujenge banda la kuku eti mbona yule kavunja?
Tumesema barabara yaweza kujengwa tukitumia wataalamu wa michoro wazuri bila kuvunja pale. Jee juhudi za kutafuta na kujifunza kwingine zimefanyika au tumekurupuka kama unavyo kurupuka wewe?
 
Muhimu ni kuwa hata sisi tusiokuwa na mamlaka tutakuwa tumeonyesha hisia zetu. Kama kuna Waziri mwenye kifua anaweza kulipeleka hili katika Baraza la mawaziri na wakajadili upya (kama waliwahi kujadili awali) na kuona kuwa Tanesco hiyo inahitaji fedha kuweza kujiongezea nguvu kuzalisha umeme kwa ajili ya viwanda nasio kujenga jengo jipya
Mkuu tukumbuke pia kwa hulka ya mtukufu wetu, tukiacha hilo.., neno lake pia ndo amri..!

Sasa najiuliza kwa sauti ni lini {sikumbuki} kama alishawahi kutengua maamuzi kwa kushinikizwa, iwe na sisi wanyonge au baraza lake!
Hii ishu nahisi {naamini} ipo beyond politics.
 
Nawaletea mada hii ili kujaribu kuishinikiza serikali iangalie upya kuhusu kubomoa jengo lile lenye gharama kubwa mali ya Tanesco pale Ubungo.

Ni kweli laweza kuwa ndani ya hifadhi ya barabara, lakini bado utaalamu waweza kufanyika kama tulivyoona katika tread tofauti humu na flyover ikajengwa bila kubomoa jengo lile lenye thamani ya mabilioni ya fedha. Kusudi ni kuwa hizo bilioni kadhaa za kujenga jengo jipya zipelekwe maeneo mengine kuongeza nguvu za uzalishaji umeme tukielekea kwenye uchumi wa viwanda.

Matokeo haya yanaweza kuipa picha serikali nini cha kufanya. Naamini mshauri mwelekezi kubadili mchoro kwa eneo lile la jengo hawezi kutuchaji hata bilioni moja.
Jibu NDIO, HAPANA au SIJUI
Akiishakuaamua Sizonje hakuna wa kumpinga!
 
Hilo jengo linanisaidia nn mimi mtu ninaeishi huku huku Kigoma Uvinza ndani ndani huku kusiko kuwa na huduma ya maji waka umeme wala hospital tunaishi kwa kudra za Allah.... Hilo jengo libomolewe tu hakuna namna
 
Akiishakuaamua Sizonje hakuna wa kumpinga!
Lakini atakuja kutoka tuu kama Mkapa alivyotoka na tukamnyang'anya Kiwira aliyo lazimisha ajiuzie kwa bei atakayo yeye. Mtu anayetumia madaraka yake apendavyo ni bora kumuonyesha kupinga hata kama mnajua hatakubali ili wakati ukifika asije sema mbona hamkuniambia kuwa hili halifai?
 
Hilo jengo linanisaidia nn mimi mtu ninaeishi huku huku Kigoma Uvinza ndani ndani huku kusiko kuwa na huduma ya maji waka umeme wala hospital tunaishi kwa kudra za Allah.... Hilo jengo libomolewe tu hakuna namna
Jambazi, hivi unadhani baada ya kubomolewa hilo jengo fedha hizo zaidi ya bilioni 50 zitafikiria kuleta umeme Uvinza au kujenga jengo jipya kwanza?
 
Lakini atakuja kutoka tuu kama Mkapa alivyotoka na tukamnyang'anya Kiwira aliyo lazimisha ajiuzie kwa bei atakayo yeye. Mtu anayetumia madaraka yake apendavyo ni bora kumuonyesha kupinga hata kama mnajua hatakubali ili wakati ukifika asije sema mbona hamkuniambia kuwa hili halifai?
Napenda pia mtukufu atoe pendekezo la kubomoa na ikulu kwa kuwa itajengwa nyingine dodoma na kwamba hii ya sasa ipo karibu sana na chanzo cha maji/bahari hivyo kuwakosesha uhuru samaki na viumbe wengine wa baharini!
 
SIUNGIKUBOMOLEWA. Matumizi mabaya ya kodi. hiyo barabara inaendelea kula kodi zetu. alijenga mkapa double road. Kikwete amejenga mwendo kasi, na sasa inajengwa fly over na yote katika kipindi cha miaka 20 tu. Kuna tatizo la mipango yetu, inakuwa ya muda mfupi mno. Wafikirie jinsi ya kukwepa na design iende bila kugusa jengo.
 
Hivi ni serikali wanataka kubomoa,au ni MTU mmoja tu kaamka kafika hapo bila kujitambua anatoa kauli kwamba BOMOA.hata lile pale BOMOA.tuungane tuweke pingamizi.huko ni kututia hasara sisi waTz,
 
Hilo jengo linanisaidia nn mimi mtu ninaeishi huku huku Kigoma Uvinza ndani ndani huku kusiko kuwa na huduma ya maji waka umeme wala hospital tunaishi kwa kudra za Allah.... Hilo jengo libomolewe tu hakuna namna
Sasa wewe unayeishi huko mapangoni itakusaidia nini hiyo barabara ya juu??
 
Back
Top Bottom