TRC na Ajali ya Dodoma: Kuna tatizo la kiutendaji

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,316
24,183
Hii ajali ya majuzi, treni kuacha njia baada ya mvua kubwa, limeniacha na maswali ambayo lazima yajibiwe.

Baada ya ajali mbaya ya train na MV Bukoba zilizotokea miaka ya My Mkapa, Awamu ya pili, nilitegemea tutakuwa kumetengenezwa Standard Operatinal Procedures kwa kuendesha hivi vifaa vyetu vya mass transport.

Haingii akilini kuwa reli haikaguliwi KILA KABLA YA SAFARI.

Na haingii akilini kuwa ma Station Master kati ya vituo vikubwa viwili vya karibu hawakuwasiliana.

Na haingii akilini kuwa dereva wa train hakuwa na weather reports, na hali ya mito mbele ya safari yake.

Haingii akilini vile vile kwamba kusafiri kwa reli za TRC is a question of chance, kufika safari yako ni majaaliwa.

Hata yote, TRC inapaswa kuyajibu.

UPANDE WA TRC
÷÷÷÷÷÷÷÷÷÷÷÷÷÷
YAH: TAARIFA YA AJALI YA TRENI B17 NA KICHWA CHA TRENI CHENYE NAMBA 9004

Dar Es Salaam Tarehe 3 Januari 2021

Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Unasikitika Kutangaza tukio la Ajali lilitokea Maeneo ya Kigwe-Bahi umbali wa Kilomita 508 Kutokea Dar Es Alaam na Kilomita 58 Kutokea Dodoma, Treni hiyo ilikuwa inatokea jijini Dar Es Salaam ikielekea Mikoa ya Tabora, Katavi (Mpanda), Kigoma na Mwanza ikiwa na Abiria wapatao 720.

Treni hii iliwasili Dodoma majira ya saa 9:15 alasiri na Kuondoka Dodoma majira ya Saa 11:40 Jioni. Treni hii iliwasili katika kituo cha Kigwe majira ya saa 12:25 Jioni na Kuondoka saa 12:27 Jioni.

Treni hii ilikuwa na Behewa 12 na kati yake Behewa 6 ndizo zilipata ajali Usajili wake ni kama ifuatavyo:
 TCB 3603 ya kwanza kutoka kwenye kichwa cha Treni
 TCB 3612 ya Pili kutoka kwenye kichwa cha Treni
 TCB 3652 ya tatu kutoka kwenye kichwa cha Treni
 TCB 3650 ya Nne kutoka kwenye Kichwa cha Treni
 TCB 3619 ya Tano kutoka kwenye Kichwa cha Treni
 Na ya Mwisho ni yenye Usajili wa Na. RCB 4526.

Mpaka sasa Majeruhi ni 66 na waliopoteza maisha ni watatu (3), akiwemo mtoto mmoja (1) na watu wazima wawili (2).
Majeruhi wamekwisha chukuliwa eneo la Tukio na wanaendelea na matibabu katika
Hospitali za Bahi na hospitali ya Mkoa wa Dodoma.

Uchunguzi wa Chanzo cha ajali unaendelea kufanyika na Shirika litaendelea kutoa Taarifa.

Uongozi wa Shirika la Reli unatoa Pole kwa Abiria wote waliofikwa na ajali, Majeruhi na Ndugu na Jamaa waliopoteza Wapendwa wao.

View attachment 1666115

MAELEZO YA CHANZO CHA AJALI
======================
Kwa mujibu wa mkuu wa kitengo cha uhusiano cha Shirika la Reli Tanzania (TRC), Jamila Mbarouk treni iliyopata ajali juzi ilikuwa na abiria 720, mabehewa ya abiria 10 na ya mizigo mawili, jumla 12.

Alisema treni hiyo iliwasili Dodoma saa 9:15 alasiri na iliondoka saa 11:40 jioni. “Treni iliwasili katika kituo cha Kigwe saa 12:25 na kuondoka saa 12:27,” alisema.

ADVERTISEMENT

Jamila lieleza kuwa baada ya kuondoka kituo cha Kigwe ndipo treni hiyo ilikwenda kupata ajali baada ya injini yake na mabehewa sita ya abiria kuacha njia.

Chanzo cha ajali hiyo kimeelezwa ni mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia juzi na maji yalifurika hata kusomba kokoto juu ya tuta la reli na kuiacha inaning’inia, hivyo injini ya treni iliyumba na kupinduka ikifuatiwa na mabehewa sita.

“Kwa sasa hicho ndio tunachoweza kuwaambia lakini baada ya uchunguzi kamili wa tukio hili tutatoa taarifa kwa wananchi,” alieleza Jamila.

Mwananchi Newspaper
 
Mvua ilinyesha, tuta likachukuliwa na mafuriko, train likaja na kupitia na hatimaye kuporomoka.
Kwahiyo key men au Sub Permanent Way Inspector (SPWI) wa kipande hicho hakutoa taarifa?

Kwasababu nijuavyo mimi japo sipo katika system hiyo Key men au SPWI ndiyo anakuwa subjected na ukaguzi kisha kumpa maelekezo ya njia station master. Sasa dereva anapofika station hupewa line clear na kama kuna hitilafu yoyote hupewa WARNING ORDER.

Dereva kwa upande wangu hapaswi kulaumiwa kabisaaaa
 
Kwahiyo key men au Sub Permanent Way Inspector (SPWI) wa kipande hicho hakutoa taarifa?

Kwasababu nijuavyo mimi japo sipo katika system hiyo Key men au SPWI ndiyo anakuwa subjected na ukaguzi kisha kumpa maelekezo ya njia station master. Sasa dereva anapofika station hupewa line clear na kama kuna hitilafu yoyote hupewa WARNING ORDER.

Dereva kwa upande wangu hapaswi kulaumiwa kabisaaaa
ww ni mtaalamu uko sahihi maswali yako lazima yapate majibu
 
Kwahiyo key men au Sub Permanent Way Inspector (SPWI) wa kipande hicho hakutoa taarifa?

Kwasababu nijuavyo mimi japo sipo katika system hiyo Key men au SPWI ndiyo anakuwa subjected na ukaguzi kisha kumpa maelekezo ya njia station master. Sasa dereva anapofika station hupewa line clear na kama kuna hitilafu yoyote hupewa WARNING ORDER.

Dereva kwa upande wangu hapaswi kulaumiwa kabisaaaa
Hapo nakubaliana kabisa.
Kuna uzembebumefanyika.
 
Hapo nakubaliana kabisa.
Kuna uzembebumefanyika.
Inasikitisha sana ebu tujiulize kitu kutokana na utaratibu wa shirika la reli dereva hapaswi kuendelea na safari pasipo kupewa line clear hivyo mpaka ile treni kwenda kupata capsizement maana yake dereva aliruhusiwa kuendelea na safari.

Kwa ukawaida zaidi endapo kuna sehemu korofi ila njia inapitika dereva hupewa WARNING ORDER kwamba Kilometer flani mpaka fulani unatakiwa kupita kwa mwendo fulani mpaka utakapo maliza hicho kipande.

Hivi endapo pangekaguliwa kwa lile shimo lilivyo mashine ilipo angukia huyo driver angepewa hata line clear kuendelea?
 
Hii ajali ya majuzi, treni kuacha njia baada ya mvua kubwa, limeniacha na maswali ambayo lazima yajibiwe.

Baada ya ajali mbaya ya train na MV Bukoba zilizotokea miaka ya My Mkapa, Awamu ya pili, nilitegemea tutakuwa kumetengenezwa Stand at Operating Procedures kwa kuendesha hivi vifaa vyetu cha mass transport.

Haingii akilini kuwa reli haikaguliwi KILA KABLA YA SAFARI.

Na haingii akilini kuwa ma Station Master kati ya vituo vikubwa viwili vya karibu hawakuwasiliana.

Na haingii akilini kuwa dereva wa train hakuwa na weather reports, na hali ya mito mbele ya safari yake.

Haingii akilini vile vile kwamba kusafiri kwa reli za TRC is a question of chance, kufika safari yako ni majaliwa.

Hata yote, TRC inapaswa kuyajibu.
Watu wanakaa ofisini na kula kiyoyozi.
Ukaguzi nani atawajibika?
 
Mkuu naona unamcchongea Kadogosa
Hii ajali ya majuzi, treni kuacha njia baada ya mvua kubwa, limeniacha na maswali ambayo lazima yajibiwe.

Baada ya ajali mbaya ya train na MV Bukoba zilizotokea miaka ya My Mkapa, Awamu ya pili, nilitegemea tutakuwa kumetengenezwa Stand at Operating Procedures kwa kuendesha hivi vifaa vyetu cha mass transport.

Haingii akilini kuwa reli haikaguliwi KILA KABLA YA SAFARI.

Na haingii akilini kuwa ma Station Master kati ya vituo vikubwa viwili vya karibu hawakuwasiliana.

Na haingii akilini kuwa dereva wa train hakuwa na weather reports, na hali ya mito mbele ya safari yake.

Haingii akilini vile vile kwamba kusafiri kwa reli za TRC is a question of chance, kufika safari yako ni majaliwa.

Hata yote, TRC inapaswa kuyajibu.
 
Hii ajali ya majuzi, treni kuacha njia baada ya mvua kubwa, limeniacha na maswali ambayo lazima yajibiwe.

Baada ya ajali mbaya ya train na MV Bukoba zilizotokea miaka ya My Mkapa, Awamu ya pili, nilitegemea tutakuwa kumetengenezwa Stand at Operating Procedures kwa kuendesha hivi vifaa vyetu cha mass transport.

Haingii akilini kuwa reli haikaguliwi KILA KABLA YA SAFARI.

Na haingii akilini kuwa ma Station Master kati ya vituo vikubwa viwili vya karibu hawakuwasiliana.

Na haingii akilini kuwa dereva wa train hakuwa na weather reports, na hali ya mito mbele ya safari yake.

Haingii akilini vile vile kwamba kusafiri kwa reli za TRC is a question of chance, kufika safari yako ni majaliwa.

Hata yote, TRC inapaswa kuyajibu.
Sure haviingii akilini. ..somewhere kuna uzembe tu..Katika mazingira ya kipindi cha mvua kama hiki kwanini hawafanyi survey au checkup ya njia wakati train inaenda...Viongozi wanajua kabisa mvua huwa zinaletwa tabu kwenye miundombinu ya reli..wataachaje treni ijipeleke kichwakichwa na kwenda kupinduka kweli kabisa ...huu ni uendeshaji wa kizamani wakati ule hakuna mawasiliano ya kutosha na teknolojia ya kizamani...lakini kwa wakati huu au kipindi hiki karne ya 21, kwenye uchumi wa kati hatutegemei ajali kama ile kabisaaa a. ...watu wakisikia watatucheka. Ni aibuu
 
Hii ajali ya majuzi, treni kuacha njia baada ya mvua kubwa, limeniacha na maswali ambayo lazima yajibiwe.

Baada ya ajali mbaya ya train na MV Bukoba zilizotokea miaka ya My Mkapa, Awamu ya pili, nilitegemea tutakuwa kumetengenezwa Stand at Operating Procedures kwa kuendesha hivi vifaa vyetu cha mass transport.

Haingii akilini kuwa reli haikaguliwi KILA KABLA YA SAFARI.

Na haingii akilini kuwa ma Station Master kati ya vituo vikubwa viwili vya karibu hawakuwasiliana.

Na haingii akilini kuwa dereva wa train hakuwa na weather reports, na hali ya mito mbele ya safari yake.

Haingii akilini vile vile kwamba kusafiri kwa reli za TRC is a question of chance, kufika safari yako ni majaliwa.

Hata yote, TRC inapaswa kuyajibu.
Leo tunajitokeza Kuwalaumu hivi TRC kutokana na Ajali iliyotokea ila sijui huwa tunakuwa wapi Kuwapongeza pale wakiwa wanazidhibiti hizi Ajali.
 
Naomba serikali iwawajibishe Station masters wa maeneo treni ilipotoka na ilipokuwa inaenda...huu ni uzembe wa karne ya 19..katika karne ya 21 na standard za uchumi wa kati hatutegemei ajali kama hizi wajameni. ..Ni aibu..wazungu watatucheka na kutudharau wakisikia haya....yes kuna ajali na ajali...lakini ajali kama hii inge we za kuepushika asilimia 100...no doubt
 
Reli ya kati imechakaa mvua kubwa ya dakika 30 inaweza ikabomoa tuta la rail wakat train imetoka kituo fulan kwend kituo fulani....

Rail ya tazara huwez kusikia ovyo mvua imesomba rail japokuw inapita ukanda wenye mvua kubwa na nyingi kwa mwaka..fikiria rail ya kati ingekuwa inapita sehemu Kama bonde la kilombero
 
Reli ya kati imechakaa mvua kubwa ya dakika 30 inaweza ikabomoa tuta la rail wakat train imetoka kituo fulan kwend kituo fulani....

Rail ya tazara huwez kusikia ovyo mvua imesomba rail japokuw inapita ukanda wenye mvua kubwa na nyingi kwa mwaka
Reli ya kati imejengwa mwaka gani na reli ya Tazara mwaka gani
 
Back
Top Bottom