Trafiki ni mradi wa mapato Serikalini na wakubwa fulani

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,333
24,227
Comrade Kinana amepasua jipu.

Hili lilikuwa halisemwi na viongozi wengi maana Polisi ni chombo nyeti cha Ulinzi na Usalama.

Lakini vitendo vya Askari wetu wa Traffic vimekithiri kwa fines zinazoingizia serikali mapato na vile vile hela ya pembeni wanayopata askari.

Ni jambo la kawaida sasa ukisafiri kwa mfano kila mahali pa speed limit 50km/hr, basi yupo askari wa kupiga fine.

Mimi binafsi nimesafiri nchi ya Zimbabwe na niliingia vijijini kama kilometa 400 na mwenyeji wangu. Hatukuwahi kuona Traffic barabarani, bali askari wa check points ambao wanakuuliza kama mko salama na unaendelea na safari yako.

Comrade Kinana ambacho hakuenda mbali ni kwamba, hao askari wanotoza fine za serikali na za kwao binafsi iko hivi:

- Malori yanatozwa shs 1-2000/= kumalizana. Kama hapo njiani yanapita malori 200 kwa siku hapo ni 400,000

- Magari madogo ni 5-10,000/= kumalizana na kama yatapita magari 400 basi kwa siku askari anaweza kupata si chini ya milioni 1-2.

- Mkicheki vizuri askari anayekusimamisha haji na Defender bali gari lake binafsi analilificha vichakani-si mbali na anapo kamua mapato.

Kuna hisia kuwa mapato hayo kwa siku, wakubwa Traffic hata wakubwa zaidi wanapelekewa mgao ili vijana walindwe kikazi.

Vilevile kuna tetesi ya kiongozi wa ngazi za juu Polisi kuwa na ukwasi wa kutisha, ambapo hizi "fine" za barabarani zikiwa moja ya vyanzo vya ukwasi.

Hapo nyuma tulisitushwa na kauli ya kuruhusu hii rushwa, wakati Magufuli akiwa Rais, alisema ati hii ni hela ya kiwi!

Nampongeza Comrade Kinana kwa kulisemea hili tatizo la Traffic.

Ni wakati muafaka sasa, kwa serikali kujitathmini na jeshi lake la Polisi kitengo cha Traffic kukomesha kero ya wazi ya rushwa na usumbufu mkubwa barabarani.
 
Katika hili, Mzee Kinana anatakiwa kuungwa mkono kwa 100%. Hawa jamaa watafutiwe majukumu mengine. Ifikie wakati nao wajifunze kuishi kwa kutegemea mshahara kama kada nyingine, badala ya rushwa kandamizi.

Yaani wamewafanya wamiliki wa magari kama ng'ombe wao wa maziwa! Jambo hili halikubaliki hata kidogo.
 
Comrade Kinana amepasua jipu.
Hili lilikuwa halisemwi na viongozi wengi maana Polisi ni chombo nyeti cha Ulinzi na Usalama.

Lakini vitendo vya Askari wetu wa Traffic vimekithiri kwa fines zinazoingizia serikali mapato na vile vile hela ya pembeni wanayopata askari.

Ni jambo la kawaida sasa ukisafiri kwa mfano kila mahali pa speed limit 50km/hr, basi yupo askari wa kupiga fine.

Mimi binafsi nimesafiri nchi ya Zimbabwe na niliingia vijijini kama kilometa 400 na mwenyeji wangu. Hatukuwahi kuona Traffic barabarani, bali askari wa check points ambao wanakuuliza kama mko salama na unaendelea na safari yako.

Comrade Kinana ambacho hakuenda mbali ni kwamba, hao askari wanotoza fine za serikali na za kwai binafsi :

- Malori yanatozwa shs 1-2000/= kumalizana. Kama hapo njiani yanapita malori 200 kwa siku hapo ni 400,000

- Magari madogo ni 5-10,000/= kumalizana na kama yatapita magari 400 basi kwa siku askari anaweza kupata si chini ya milioni 1-2.

- Mkicheki vizuri askari anayekusimamisha haji na Defender bali gari lake binafsi analilificha vichakani-si mbali na anapo kamua mapato.

Kuna hisia kuwa mapato hayo kwa siku, wakubwa Traffic hata wakubwa zaidi wanapelekewa mgao ili vijana walindwe kikazi.

Vilevile kuna tetesi ya kiongozi wa ngazi za juu Polisi kuwa na ukwasi wa kutisha, ambapo hizi "fine" za barabarani zikiwa moja ya vyanzo vya ukwasi.

Hapo nyuma tulisitushwa na kauli ya kuruhusu hii rushwa, wakati Magufuli akiwa Rais, alisema ati hii ni hela ya kiwi!

Nampongeza Comrade Kinana kwa kulisemea hili tatizo la Traffic.

Ni wakati muafaka sasa, kwa serikali kujitathmini na jeshi lake la Polisi kitengo cha Traffic kukomesha kero ya wazi ya rushwa na usumbufu mkubwa barabarani.
Cc.To Elii Mshana &co narudia kumbumbusha kuwa JF wapo Great Thinker pamoja na wale nilio mkumbusha kwenye Uzi wake alipowagusa Jf🤔
 
Kwa nia njema na kauli 'nzuri' yenye kuonyesha neema mzee kasema ila, nasubiri utekelezaji wa haya matamko mazuri mazuri haya.

Bahati mbaya (hata hii comment yangu ni ya kupingwa) baadhi ya nchi zetu za kiafrika tuna viongozi (wapo) wazuri tatizo la maneno yao huwa hayana utekelezaji.

Huwa nasema ni ya kutuvusha sehemu flani.
 
Comrade Kinana amepasua jipu.
Hili lilikuwa halisemwi na viongozi wengi maana Polisi ni chombo nyeti cha Ulinzi na Usalama.

Lakini vitendo vya Askari wetu wa Traffic vimekithiri kwa fines zinazoingizia serikali mapato na vile vile hela ya pembeni wanayopata askari.

Ni jambo la kawaida sasa ukisafiri kwa mfano kila mahali pa speed limit 50km/hr, basi yupo askari wa kupiga fine.

Mimi binafsi nimesafiri nchi ya Zimbabwe na niliingia vijijini kama kilometa 400 na mwenyeji wangu. Hatukuwahi kuona Traffic barabarani, bali askari wa check points ambao wanakuuliza kama mko salama na unaendelea na safari yako.

Comrade Kinana ambacho hakuenda mbali ni kwamba, hao askari wanotoza fine za serikali na za kwai binafsi :

- Malori yanatozwa shs 1-2000/= kumalizana. Kama hapo njiani yanapita malori 200 kwa siku hapo ni 400,000

- Magari madogo ni 5-10,000/= kumalizana na kama yatapita magari 400 basi kwa siku askari anaweza kupata si chini ya milioni 1-2.

- Mkicheki vizuri askari anayekusimamisha haji na Defender bali gari lake binafsi analilificha vichakani-si mbali na anapo kamua mapato.

Kuna hisia kuwa mapato hayo kwa siku, wakubwa Traffic hata wakubwa zaidi wanapelekewa mgao ili vijana walindwe kikazi.

Vilevile kuna tetesi ya kiongozi wa ngazi za juu Polisi kuwa na ukwasi wa kutisha, ambapo hizi "fine" za barabarani zikiwa moja ya vyanzo vya ukwasi.

Hapo nyuma tulisitushwa na kauli ya kuruhusu hii rushwa, wakati Magufuli akiwa Rais, alisema ati hii ni hela ya kiwi!

Nampongeza Comrade Kinana kwa kulisemea hili tatizo la Traffic.

Ni wakati muafaka sasa, kwa serikali kujitathmini na jeshi lake la Polisi kitengo cha Traffic kukomesha kero ya wazi ya rushwa na usumbufu mkubwa barabarani.
Kitimoto, Stimboti wenye nchi yao wamechoka. Mnakwitwa na huku.
 
Katika hili, Mzee Kinana anatakiwa kuungwa mkono kwa 100%. Hawa jamaa watafutiwe majukumu mengine. Ifikie wakati nao wajifunze kuishi kwa kutegemea mshahara kama kada nyingine, badala ya rushwa kandamizi.

Yaani wamewafanya wamiliki wa magari kama ng'ombe wao wa maziwa! Jambo hili halikubaliki hata kidogo.
Mimi sio Siri nawaita kunguru weupe,kwani kunguru ni mwizi siku zote,ukizubaa amekutia hasara Kwa manufaa yake binafsi na wala SII Kwa manufaa ya taifa🤔
 
Ccp moshi ndiyo linajukumu la kuwazalisha matrafik police,police wa usalama wa Mali na raia,police uhamiamiaji,magereza,
Sasa mjiulize hawa traffic wa sahv wanapitishwa kutoka ccp moshi

Ova
 
Hivi wakuu ukijitahidi gari yako iwe safi,kwa maana spidi ya kawaida,ukiwa umevaa mkanda,bima umelipa na tira inasoma,tairi zipo vizuri na spea yake,nenda kwa usalama umepeleka gari na imekaguliwa na wao vizuri tu.
Taa zote zipo safi,waipa na maji yapo poa,hujazidisha abiria,hujavaa sendo,fire extinguisher ipo vizuri,na unajua kuitumia.
Huhjaovateki sehem isiyoruhusiwa,kwenye zebra umepisha watu wapite,umepaki sehem sahihi,upo kwenye line yako.
Hivi hawa jamaa wanakulaje hela yako?????
 
Hadi leo hii zaidi ya msemaji wa polisi kukiri kupokea ujumbe wa Kinana hamna hatua yeyote ya kumaliza uhuni huu. Bila maandamano ni biashara kama "kawa" trafiki ltd.

Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe. Madereva wa malori walionyesha mfano majuzi hapa.
 
Hivi wakuu ukijitahidi gari yako iwe safi,kwa maana spidi ya kawaida,ukiwa umevaa mkanda,bima umelipa na tira inasoma,tairi zipo vizuri na spea yake,nenda kwa usalama umepeleka gari na imekaguliwa na wao vizuri tu.
Taa zote zipo safi,waipa na maji yapo poa,hujazidisha abiria,hujavaa sendo,fire extinguisher ipo vizuri,na unajua kuitumia.
Huhjaovateki sehem isiyoruhusiwa,kwenye zebra umepisha watu wapite,umepaki sehem sahihi,upo kwenye line yako.
Hivi hawa jamaa wanakulaje hela yako?????
Hii ni nadharia NZURI SANA, but it doesn't apply in real life.

NB: One's mistakes never justify another mistake. Kosa halihalalishi kosa lingine.
 
Hivi wakuu ukijitahidi gari yako iwe safi,kwa maana spidi ya kawaida,ukiwa umevaa mkanda,bima umelipa na tira inasoma,tairi zipo vizuri na spea yake,nenda kwa usalama umepeleka gari na imekaguliwa na wao vizuri tu.
Taa zote zipo safi,waipa na maji yapo poa,hujazidisha abiria,hujavaa sendo,fire extinguisher ipo vizuri,na unajua kuitumia.
Huhjaovateki sehem isiyoruhusiwa,kwenye zebra umepisha watu wapite,umepaki sehem sahihi,upo kwenye line yako.
Hivi hawa jamaa wanakulaje hela yako?????
Atakuambia hela ya kiwi tafadhali.
 
Makamu Mwenyekiti hakufikiri sawa sawa kushauri Trafiki waondolewe barabarani.

Kwa jinsi hawa madereva wetu wanavyovuta bangi na kwa jinsi vyombo vya usafiri vilivyo chakavu , kuna maafa yatatokea muda si mrefu na wa kwanza kulaumu watakuwa wao tena.

Hapa Trafiki waboreshewe maslahi, wapewe training za mara kwa mara,wapewe vitendea kazi bora na waongezwe barabarani.

Madereva nao wafanyiwe vipimo mbali mbali vya afya ikiwemo utimamu wa akili zao maana wanadhamana ya kubeba watu , tuacheni siasa kwenye mambo ya msingi jamani.
 
Comrade Kinana amepasua jipu.

Hili lilikuwa halisemwi na viongozi wengi maana Polisi ni chombo nyeti cha Ulinzi na Usalama.

Lakini vitendo vya Askari wetu wa Traffic vimekithiri kwa fines zinazoingizia serikali mapato na vile vile hela ya pembeni wanayopata askari.

Ni jambo la kawaida sasa ukisafiri kwa mfano kila mahali pa speed limit 50km/hr, basi yupo askari wa kupiga fine.

Mimi binafsi nimesafiri nchi ya Zimbabwe na niliingia vijijini kama kilometa 400 na mwenyeji wangu. Hatukuwahi kuona Traffic barabarani, bali askari wa check points ambao wanakuuliza kama mko salama na unaendelea na safari yako.

Comrade Kinana ambacho hakuenda mbali ni kwamba, hao askari wanotoza fine za serikali na za kwai binafsi :

- Malori yanatozwa shs 1-2000/= kumalizana. Kama hapo njiani yanapita malori 200 kwa siku hapo ni 400,000

- Magari madogo ni 5-10,000/= kumalizana na kama yatapita magari 400 basi kwa siku askari anaweza kupata si chini ya milioni 1-2.

- Mkicheki vizuri askari anayekusimamisha haji na Defender bali gari lake binafsi analilificha vichakani-si mbali na anapo kamua mapato.

Kuna hisia kuwa mapato hayo kwa siku, wakubwa Traffic hata wakubwa zaidi wanapelekewa mgao ili vijana walindwe kikazi.

Vilevile kuna tetesi ya kiongozi wa ngazi za juu Polisi kuwa na ukwasi wa kutisha, ambapo hizi "fine" za barabarani zikiwa moja ya vyanzo vya ukwasi.

Hapo nyuma tulisitushwa na kauli ya kuruhusu hii rushwa, wakati Magufuli akiwa Rais, alisema ati hii ni hela ya kiwi!

Nampongeza Comrade Kinana kwa kulisemea hili tatizo la Traffic.

Ni wakati muafaka sasa, kwa serikali kujitathmini na jeshi lake la Polisi kitengo cha Traffic kukomesha kero ya wazi ya rushwa na usumbufu mkubwa barabarani.
Na Maaskari wengi wanataka wawe ma Trafiki,futilia mbaya huo ujinga.
 
Hivi wakuu ukijitahidi gari yako iwe safi,kwa maana spidi ya kawaida,ukiwa umevaa mkanda,bima umelipa na tira inasoma,tairi zipo vizuri na spea yake,nenda kwa usalama umepeleka gari na imekaguliwa na wao vizuri tu.
Taa zote zipo safi,waipa na maji yapo poa,hujazidisha abiria,hujavaa sendo,fire extinguisher ipo vizuri,na unajua kuitumia.
Huhjaovateki sehem isiyoruhusiwa,kwenye zebra umepisha watu wapite,umepaki sehem sahihi,upo kwenye line yako.
Hivi hawa jamaa wanakulaje hela yako?????

Hata ukiwa na gari tokea kiwandani leo na ukayafanya yote hayo uliyoorodhesha ukapita barabara hii:

Tetesi: - Yawezekana hiki ndio kilichopelekea Kinana alalamikie Traffic

Nakazia kwa mtaji huo, safiri njia hiyo hutoboi!

Tatizo kubwa ni kuwa kila askari mmoja ana lake. Wako kama wako na open signed cheque.

Nchi zingine kwa siku katika nchi nzima ukaguzi ni kwenye jambo moja tu kwa gari. Kama ni tairi basi ni tairi tu na husimamishi gari jingine kama tayari umesimamisha moja.

Kwetu mabasi bila 5,000/- ya kuondokea isiyokuwa na risiti stendi mwanzo wa safari. zengwe lake, basi litatoka?

Nchi inanuka rushwa!

Kwa rushwa ilivyotamalaki, PCCB na wengine wa hivyo wana umuhimu gani kuendelea kuwapo?

Habari ndiyo hiyo.
 
Kinachosikitisha zaidi ni chombo kinachoitwa PCCB kilianzishwa kimakosa sana haijui majukumu yake... Inashangaza eti PCCB mpaka waambiwe kachunguzeni pale...upuuzi mtupu.

PCCB wanashindwa kabisa kuchunguza rushwa zinazochukuliwa na Police barabarani pamoja na stendi za magari na kuruhusu magari mabovu kupakia abiria na ndo chanzo Cha ajali nyingi pia.

Gari ni mbovu na inapakia abiria kuliko kawaida then Askari anachungulia mlangoni, anamwita kondakta nje then wanamalizana.
PCCB Bora ivunjwa.
 
Back
Top Bottom