Nyinyi ndio maana kila siku mnalia njaa hapa mjini, wewe unadhani Lundenga ni kichaa? uende kwa Samuel Sitta kufanya nini wakati huyu ndio mgombea Urais wa CCM na akishinda connection za ulaji zinakuwa zilishasukwa siku nyingi!!Sababu ya warembo kumtembelea Lowassa ni nini hasa?
Mama Regina chunga mzigo wako.Teh!teh!
Kweli urais mtamu sana. Edward Lowassa sasa anatumia kila mbinu kuzidi kujijenga. Wakati mwingine anafanya mambo yanamuonyesha kama mtu mwenye uchu wa madaraka hakuna mfano. Mfano nini mantiki ya kutembelewa na mamiss wakati yeye ni mbunge wa kawaida kama hakuna ajenda ya siri nyuma ya pazia? Kweli pesa za mafisadi zinaweza kununua kila kitu hata kama hakina maana! Pichani Lowassa na mkewe wakiwa na mamiss huko Monduli.
Mkuu Umesahau lowassa ni waziri mkuu mstaafu