Timu kususia mechi za Ligi, Bodi ya Ligi (TPLB) wasema hatujapokea barua ya malalamiko kutoka timu yoyote, hata Singida Black Stars

Timu kususia mechi za Ligi, Bodi ya Ligi (TPLB) wasema hatujapokea barua ya malalamiko kutoka timu yoyote, hata Singida Black Stars

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imethibitisha kuwa haijapokea barua yoyote ya malalamiko kutoka kwa klabu yoyote inayoshiriki Ligi Kuu ya NBC wala NBC Championship hadi sasa. Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Habari wa Bodi hiyo, Karim Boimanda, ambaye amesema kuwa hata klabu ya Singida Black Stars, licha ya msemaji wao kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu malalamiko, bado hawajawasilisha barua rasmi kwa TPLB.

"Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) haijapokea barua yoyote kutoka kwa timu yoyote ile ya Ligi Kuu ya NBC wala NBC Championship na hata hao Singida Black Stars licha ya msemaji wao amezungumza na vyombo vya habari ila hatujapokea barua ya malalamiko kutoka kwao."

1748588751643.png
Kauli hiyo inakuja wakati ambapo kumekuwa na mjadala kwenye mitandao ya kijamii kuhusu baadhi ya Vilabu kutaka kususia mechi zilizosalia kwenye Ligi ya NBC kufuatia maamuzi na matukio yanayohusiana na mechi za ligi.
 
Malalamiko ya kususia mechi huwa yanafanywa na simba tu. Hizo timu nyingine zimeshagundua zikipeleka hayo malalamiko kwenye Bodi iliyojaa upendeleo kwa timu moja tu kwenye ligi, zitakuwa zinapoteza tu muda wao. Maana hazitapata haki.
 
Malalamiko ya kususia mechi huwa yanafanywa na simba tu. Hizo timu nyingine zimeshagundua zikipeleka hayo malalamiko kwenye Bodi iliyojaa upendeleo kwa timu moja tu kwenye ligi, zitakuwa zinapoteza tu muda wao. Maana hazitapata haki.
Yanga tukienda CAS watasema hatukupeleke barua TPBL.
 
Ambaye hapeleki timu sheria inachukua mkondo wake, hakuna kubembelezana hapa.
 
Malalamiko ya kususia mechi huwa yanafanywa na simba tu. Hizo timu nyingine zimeshagundua zikipeleka hayo malalamiko kwenye Bodi iliyojaa upendeleo kwa timu moja tu kwenye ligi, zitakuwa zinapoteza tu muda wao. Maana hazitapata haki.
Haya malalamiko yangeanza tangu siku ile Kayoko anafanya yake dhidi ya simba , uto anapewa benati nje ya 18 dhidi ya Ken Gold tungewaelewa . Ila kama yalisubiri kaka yao apumuliwe kisogoni ndipo yaanze basi hayo malalamiko ni ya unafiki mtupu hayana mashiko . Huu ni utoto kama utoto mwingine.
 
Mkuu unahangaika na mautopolo????????????....

"Ujinga si kitu cha kujiuliza kabisa kwa mashabiki wa yanga".
Lini utaacha ujinga wako,hivi unafanya kazi kweli maana kila uzi upo broo fanya kazi ujana ni mfupi sana,mpira umefanya watu wengi kufa masikini
 
Malalamiko ya kususia mechi huwa yanafanywa na simba tu. Hizo timu nyingine zimeshagundua zikipeleka hayo malalamiko kwenye Bodi iliyojaa upendeleo kwa timu moja tu kwenye ligi, zitakuwa zinapoteza tu muda wao. Maana hazitapata haki.
HATUCHEDHI NG'O, sio kususia? Kweli kundu haliona nyaniwe.
 
HATUCHEDHI NG'O, sio kususia? Kweli kundu haliona nyaniwe.
Yanga inataka kwanza mtoe sababu zenye mashiko za kukimbia ile tarehe 8 Machi. Na ndiyo maana ya hiyo kauli mbiu yao.
 
Haya malalamiko yangeanza tangu siku ile Kayoko anafanya yake dhidi ya simba , uto anapewa benati nje ya 18 dhidi ya Ken Gold tungewaelewa . Ila kama yalisubiri kaka yao apumuliwe kisogoni ndipo yaanze basi hayo malalamiko ni ya unafiki mtupu hayana mashiko . Huu ni utoto kama utoto mwingine.
Mapungufu yote ya waamuzi yanatakiwa yakemewe! Na siyo kufanywa kama kichaka cha kuendeleza huo upuuzi.

Binafsi nimekuwa nikimsifia Ahmed Arajiga humu kama mwamuzi bora wa kati nchini! Na hata alipomtoa Ibrahimi Bacca kwa kadi nyekundu mechi ya Yanga dhidi ya Azam! Na Yanga kuishia kupoteza ule mchezo; hakuna shabiki alikuja kumtukana humu jukwaani kwa kuipendelea Azam! Na badala yake baadhi ya mashabiki walimlaumu Bacca kwa kucheza hovyo.
 
Haya malalamiko yangeanza tangu siku ile Kayoko anafanya yake dhidi ya simba , uto anapewa benati nje ya 18 dhidi ya Ken Gold tungewaelewa . Ila kama yalisubiri kaka yao apumuliwe kisogoni ndipo yaanze basi hayo malalamiko ni ya unafiki mtupu hayana mashiko . Huu ni utoto kama utoto mwingine.
Namungo vs simba ( makosa ya kibinadam)
Simba vs mashujaa ( makosa ya kibinadqmu
Simba vs SBS ( Makosa ya kibinadamu)
Ni mengi
 
Wametukwepa kwenye ligi NBC,hawajaridhika,
wanataka watukwepe na CRDB,, ??????,

Jamaa wana roho ya Korosho,
embu twendeni na CRDB watu wapoze machungu ya Dabi
 
Lini utaacha ujinga wako,hivi unafanya kazi kweli maana kila uzi upo broo fanya kazi ujana ni mfupi sana,mpira umefanya watu wengi kufa masikini
Mkuu kwani ameshawahi kukulilia shida au ni wivu wa kinyuma mwiko unakusumbua, nchi ina wajinga wengi kama sio wivu.
 
Back
Top Bottom