Tido Mhando atemwa TBC

Tido Mhando atemwa TBC

Kwakweli hakuwa na msimamo..mara aipendelee(kwa muda mrefu) ccm wanachi walipopiga kelele akalegeza kidogo naamini ndio kitu walichochukia hao waliomuajiri,sasa si kwa wananchi wala serikali hana support kokote..bora angechagua moja kuwa baridi au moto na sio vuguvugu..!
 
Pole sana Tido...pale ulikuwa una cheza sana na mafisadiii,,,,,,,pole sana hukujuaa hilo?/
 
ccm ndio wana maaanisha ukitaka fanya serikalini lazima uwe ccm, wapumbavu sana
 
Dah!, wanajamii hivi KWELI TUNAELEKEA WAPI?, kwa hali hii KWELI kuna MSINGI WA NCHI YETU kufika mbali kweli?
 
Kwa kweli Tido Ilikuwa na wakati mgumu sana wakufanya kazi katika taasisi kama hiyo. maana lazima ulikuwa unaingiliwa utendaji wako wa siku hadi siku kutoka kwa chama cha mafisadi. hat hinyo hongera san akwa marekedisho makubwa katika shirika hilo la umma japo ni la mafisadi!
 
Siasa pale inapogeuka kuwa si hasa,

Watawala wanatakiwa kujua kuwa ulimwengu wa sasa sio ule wa kukalia habari, njia za kupata habari ni nyingi na miongoni mwa watunza au watoa habari wana mwamko tofauti, hili hata ndani yao lipo na utaliona kwa watendaji wakuu wao. Lazima sasa watambue kuwa siku hazigandi
 
Ni wakati Chadema iwe na tv na redia kinyume na hivyo kupigana kushinda uchaguzi ujao itakuwa shida kwetu. Uamuzi huu unatakiwa kuchukuliwa sasa maana fedha ya ruzuku na inaweza kabisa kusaidia mtaji huu ama twaweza kuhamasisha wanachama na wapenzi wetu ambao kwa sasa wana imani na sisi na wako tayari kusaidia ili chama chao wakipendacho kifanikishe ajenda ya kuikomboa nchi hii.
 
Nasikia ni kihere here cha kuruhusu mijadala wakati wa kampeni amabyo haikuzaa matunda kwa mwajiri wake CCM.....
 
Sisiemu watakuwa na sababu zao za kumfukuza Tido, sio kwamba kachangia kushindwa kwao. Nakumbuka wakati Kikwete anazindua kampeni zake pale Jangwani, watumishi wa Tido walizima mitambo baada ya Marando kuanza kuirushia madongo sirikali. Hali kadhalika, wakati wa kampeni mikoani, watumishi wa TBC walikuwa wanarusha mara nyingi sana Kampeni za JK kuliko za wapinzani. Sielewi mpaka hapa Tido analaumiwa kwa lipi.
 
Idimi naona tatizo lake ni kunyamazia kipindi cha mchakato majimboni yote mazuri kwa ccm yalizimwa na kipindi kile.
 
Friday, 17 December 2010
BAADA ya kufanya kazi nzuri ya kuboresha matangazo na uendeshaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), serikali imeamua kuachana na mkurugenzi wa chombo hicho, Tido Mhando baada ya mkataba wake kuisha, lakini mtangazaji huyo maarufu ameielezea uamuzi huo kuwa kuwa ni wa utata.

Habari zaidi: Tido Mhando atemwa TBC
 
Tuseme ukweli jamaa ni creative!aliibadilisha tvt kabisa pakawa ni tv yenye mwelekeo wa kutoa habari za kweli!wana jf mnafikiri wana ccm walifurahi kuumbuliwa ktk midahalo ya tbc1?kitendo cha makamba kupiga marufuku wezi wenzake kutoshiriki midahalo ndio ilikua hatima ya tido!vitisho ni sera ya ccm
 
Tido hajafukuzwa ila mkataba wake umekwisha. Hajatolewa TBC bali kamaliza mkataba wake TBC. Labda tujadili kwanini wasimpe tena mkataba mwingine au kwanini wampe tena mkataba mwingine.
 
Inasemekana Tido Mhando katolewa/ kafukuzwa TBC kisa Kussuport CHADEMA kwa njia ya nyuma kipindi cha Uchaguzi. Baadhi ya Viongozi wa Juu wa CCM wanasema Tido Muhando AMECHANGIA Chama chao Kushindwa vibaya kwenye Uchaguzi na pia Tido Mhando amechangia CHADEMA kupata Nguvu ndani ya wananchi.

Kwa mfano wanasema kwa nini Hakusimamisha Kipindi cha MDAHALO Majimboni wakati CCM walishaamua kujitoa kutoshiriki Mdahalo na walishamuamrisha akisimamishe, na yeye ALIKATAA na kusema Hawezi kusimamisha kwani italeta sura mbaya kwa shirika.

Na pia wanamshutumu kwa nini Hakubase 100% upande wa CCM, pia wanamshutumu kuwa alikuwa upande wa Chadema.

Siasa imeingia kumuondoa Tido Mhando.

(Wana jamii Hizi ni shutuma za kweli au ni Hearsays tu?)
acha upotoshaji wewe, huu ndio mimi naita upuuzi na udandiaji teni kwambe

nani kakwambia?
umesoma ile thread nyingine ukaona na wewe uje na yako... pumba kweli

this is not fair the forum nor to Tido and TBC

nashangaa thread kama hii inabaki halafu zile nyeti wanazitoa
 
(Nani ametoa shutuma hizi? au wewe ndiye uliyezitoa. Tupe chanzo cha habari hii pls!)

Source: Ni watu wenye kufuatilia siasa, watu wenye Uchungu wa nchii, watu mtaani na wengine CCM.....Ndio maana nimeuliza ndugu yangu @ Chibidu kuwa hizi ni kweli au ni UZUSHI tu?, kuna Ukweli wowote hapo?
Katika hao watu wote ulio wataja hapo juu na wewe(mpenda shutuma) haupo kweli?
 
Back
Top Bottom