Tibaijuka akataa kupokea shilingi 200 millioni

Tibaijuka akataa kupokea shilingi 200 millioni

Hivi Maprofessor wa Tanzania ni nani aliyewaroga?

Kwanini msijikite kwenye courses mlizosomea badala ya kukimbilia siasani tu?
mkuu siasani wakibaki wenye elimu za hapa na pale...ndo tutakwisha
 
Halafu sijasikia hata CCM wakitoa pole na rambirambi kwa watu wa Kagera
 
90%!ya maprofesa wa Tanzania ni wajinga wajinga sana mfano angalia matendo ya kapuya hata wale wenye phd akina mwakyembe walinunua mabehewa feki huku akimfundisha uzushi phd mwenzake Slaa, wenzao akina kitila, lipumba wamekuwa vioja kwa kweli Uprofesa wa Tz ni kituko

Sio Kweli kwamba maprofesa wa Tanzania ni wajinga,ndio maanake wewe namimi hatujaukwaa uprofesa ,iweje wakufundishe wewe hao hao wewe uwaone wajinga na wewe ujione mwerevu.Au mnataka kupeana vyeo vya uprofesa wa heshima tu bila kuvihenyea.Usione vinaelea vimetafutwa kwa kutumia upstairs mkuu.
 
Uprofesa sasa ni janga kwa taifa!
Haiwezekani mtu ukatae pesa halali hiyo hata kama yeye binafsi haimtoshi mboga anayo, hiyo pesa ingewasaidia waanga wa tetemeko!
 
By Raymond Kaminyoge, Mwananchi

Dar es Salaam. Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anne Tibaijuka amesema amepata tuzo nchini Marekani ikiwa ni kuthamini mchango wake akiwa Umoja wa Mataifa lakini akakataa kuchukua fedha dola 100,000( zaidi ya Sh 200 milioni) ambazo huambatana na tuzo hiyo.

Alisema alikataa kupokea fedha hizo kwa sababu maadili ya nchi yetu hayaruhusu kupokea zawadi kama hiyo.

Alisema lakini aliwaeleza kwamba katika mkoa anakotoka kumetokea tetemeko la ardhi na kuna maafa.

Alisema wao wataamua cha kufanya lakini yeye binafsi amekataa kupokea fedha hizo.

Upuuzi mtupu huu .amekataa kupokea kwa maana angeikabizi hiyo zawadi serikalini kwani maadili ndio yanasema hivyo.na kwa ujanja wake akaikataa na kuilekeza kutolewa kwa waathirika Wa tetemeko bukoba,amekwepa kuipokea na kuikabidhi serikali akihisi ingekwenda kwingineko kutumika.alafu anatutangazia unafiki wake eti nimekataa kwa sababu maadili yanamkataza !!.unafiki mmbaya sana embu atuambie hicho kipengele cha maadili kikokifungu gani.zaidi ya kifungu kinacho ruhusu kupewa zawadi kuipokea na kama inazidi gharama ya elfu 50 ndio sheria uikabidhi serikali.
 
Ana haki akatae hii si hela ya kitunguu tu
Amekataa wapi huyo mnafiki .sana sana ame redirect iende bukoba baadala ya serikali kuu.analeta maujanja ya kizamani alafu anataka natumsifie kwakutudanganya kama watoto
 
Unafiki mwingine wa kiwango cha professor. Hio tuzo kama inaambatana na hio pesa kuna ubaya gani???

Kwa hio hata wanafunzi wanaofaulu vizuri na kupewa Tuzo na pesa au kulipiwa Ada ni kosa ???? Wasichukue zawadi hizi na Ada??
 
Hivi hizi Pesa za shirika LA UN zina tatixo gani si kama Nobel? Alipokea za magumashi(escrow) anakataa hixi safi?
 
Kitendo cha Serikali kutafuta pesa kwa ajili ya kusaidia wahanga wa tetemeko wa mkoa wa Kagera huku jimbo la Buleba likiwa ni sehemu ya mkoa wa Kagera Mbunge wake akiwa ni Profesa Anna Tibaijuka ambaye hivi karibuni ameshinda tuzo ya kimataifa ya maswala ya uongozi na KUKATAA TAKRIBANI T..SH 200 MIL KAMA KIAMBATA CHA TUZO.NI JAMBO LA KUSTAJABISHA KWA KIONGOZI MKUU KAMA HUYU ANAYETOKA KATIKA ENEO LILILOATHIRIKA NA JANGA HILI AMBAPO BADO JUHUDI ZA KUKUSANYA MICHANGO ZINAENDELEA FANYIKA. LAITI KAMA NINGEKUWA NI MWENYEKITI WA CCM NINGEMVUA UANACHAMA KAMA HATUA MUHIMU YA KUELEKEA MVUA UBUNGE WAKE
Anatakiwa afukuzwe kwa kosa la kuilaghai na kuikosesha mapato kwa hila serikali.kwani alichofanya nikuredirect hiyo fedha iende bukoba baadala ya serikalini kwakutoiamini serikali kupokea .kwani sheria ya maadili aikatazi kupokea zawadi ila kwa sharti zawadi ikizidi gharama ya elfu 50 unaipokea na kuikabidhi serikali .mpaka hapo utaona ni jinsi gani sio kiongozi mwadilifu yaani unakuwa kiongozi huku unaitendea hila serikali yako .
 
By Raymond Kaminyoge, Mwananchi

Dar es Salaam. Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anne Tibaijuka amesema amepata tuzo nchini Marekani ikiwa ni kuthamini mchango wake akiwa Umoja wa Mataifa lakini akakataa kuchukua fedha dola 100,000( zaidi ya Sh 200 milioni) ambazo huambatana na tuzo hiyo.

Alisema alikataa kupokea fedha hizo kwa sababu maadili ya nchi yetu hayaruhusu kupokea zawadi kama hiyo.

Alisema lakini aliwaeleza kwamba katika mkoa anakotoka kumetokea tetemeko la ardhi na kuna maafa.

Alisema wao wataamua cha kufanya lakini yeye binafsi amekataa kupokea fedha hizo.

Mama Nakushukuru Kwa Hizo Hela za Vimboga za 200,000,000 Ukilinganisha na Vile Visenti vya 1,600,000,000 vya Escrow, Basi Tungeliziomba na Zile Uzikabithi Kwa ajili ya Kusaidi Kujenga Nyumba zilizoharibiwa na Tetemeko. Na naamini Magu atakufikiria Kukupa Tuzo Nyingine, Jecha anapewa Tuzo Itakuwa Wewe Mama kwani Wewe ni shetani ndio Usipewe!
 
Hizi ni kauli za kihuni kabisa, wapi maadili ya nchi hii yaliposema kiongozi anakatazwa kupokea Tuzo ya wazi kama hiyo inayoambatana na fedha? Huo ni upuuzi unao endelea kuonyeshwa na maprofesa wetu. Kama yeye hana Shida ya Pesa na akazipokea na kupeleka hata jimboni na kuwaambia hii ni zawadi (Tuzo) yangu naomba inunue madawa kwenye zahanati hata wapiga kura wake sii wangemuona wa maana!
Hapo kaonyesha tuu dharau kwa waliokuwa wanansema juu ya zile za Escrow
Mkuu nakuunga mkono huyu mama ana dharau kupita kiasi haiwezekani ukaacha kupokea fedha za tuzo kisa maadili hayaruhusu si afadhali angewaambia badala ya kupewa fedha wampe madawa. Tendo hili linaonyesha jinsi alivyo na dharau kwa wananchi wa jimboni lake ambao wana matatizo mengi. Mbona hela ya rushwa ya escrow alichukua huku akitoa maneno ya ku......nya "Eti hiki tuhela twa mboga" kwani alikuwa hajui sheria inakataza. Pambaaf zake!
 
Kwani Tabora si sehemu ya congo? Mbona kuna wacongomani wengi sana, hata warudi na wanayarwanda pia na kuna maprofesa wawili wajinga wajinga yaani Kapuya na Lipumba.
Wako busy na pesa za watu wakati M/kiti wao tena wenye jimbo kaenda pale akanywa rubisi na amerudi mjini bila hata kutoa mfuko mmoja wa saruji

Wanywa viroba ni shida sana
 
Hao watoa zawadi walikuwa wanamzalilisha professor hawakumbuki Professor milioni mia anatumia kwa mboga au wanajidai hawajui Rwegamalila wa Escrow

By the way Rwegamalila ameshaagiza wakandarisi toka Dubai waje wajenge bukoba iwe kama Dubai wale waliokuwa na nyumba za mbavu za mbwa watapewa gorofa tatu

Hatutaki ujinga wahaya
 
mtoa post huna akili aujui kwanini hajachukua pesa pili hujajua kasema nini kaa kimnya!!!!yeye kawaambia kupokea pesa haifai ila mm ninetoka ulemkoa ulopata maafa nazan ushapata jib tumia akili ya kujiongeza.
Hiyo ni hila ameifanyia serikali kwa kuredirect hiyo pesa iende bukoba kwa kumpatia sifa binafsi ,baadala ya pesa hiyo angeipokea kama zawadi na kwa sheria ya maadili ikizidi gharama ya elfu 50 unaikabidhi serikali.kwa maana ingine alikuwa achukue elfu 50 na akabidhi serikali million 199.950.000/= sana sana huyu kama alitegemea sifa badala yake anatakiwa ashitakiwe kwakuikosesha serikali mapato yake halali.aswa ukizingatia anaelewa fika kuwa alitakiwa apokee na kuikabidhi serikali haki yake.
 
Hiyo ni hila ameifanyia serikali kwa kuredirect hiyo pesa iende bukoba kwa kumpatia sifa binafsi ,baadala ya pesa hiyo angeipokea kama zawadi na kwa sheria ya maadili ikizidi gharama ya elfu 50 unaikabidhi serikali.kwa maana ingine alikuwa achukue elfu 50 na akabidhi serikali million 199.950.000/= sana sana huyu kama alitegemea sifa badala yake anatakiwa ashitakiwe kwakuikosesha serikali mapato yake halali.aswa ukizingatia anaelewa fika kuwa alitakiwa apokee na kuikabidhi serikali haki yake.
Kwani nchi hii vyanzo vya mapato ni 200m tu? keshaikataa imekwisha, kama kafanya sahihi ama kaharibu ni yeye mwenyewe
 
Back
Top Bottom