Nilipewa hiyo chumvi ya mawe kama kilo mbili hivi, imetoka kanisani kabisa kuombewa.
Nilikua naishi peke angu kipindi hicho, nilivohamia hiyo Nyumba sikumwaga chumvi wiki kama mbili nalala fresh tu yani shwari, wiki ya tatu nipo napanga panga nikaiona chumvi nikapata wazo la kumwaga, nikaimwaga ndani wala sikunuia kitu niliimwaga tu aseee siku hiyo sikulala, nikianza tu kusinzia naona mtu kasimama kwenye pazia naamka, ilikua ni kufumba fumbua hadi kumi na moja asubuhi, nikaamka nikaenda job. Kesho yake hivo hivo ndoto za mauza uza tu mara naota mdada kavaa white tupu ananisemesha huku kabeba njiwa, na ile Nyumba ilikia na njiwa wengi.
Siku hiyo mchana nmelala, nakumbuka haikua ndoto japo nimelala ila nina fahamu zote ila mwili mzito siwezi hata kufumbua jicho, nikawa nahisi mtu kalala pembeni yangu namsikia kabisa anajigeuza ila ndo siwezi kuamka, nikapapasa nikahisi nimeshika trak suti, kifuani hana nyonyo, nikawaza mbona mwanaume au faza hausi kaja, kushika kichwa duh ana upara hapo ndo nikajua sio yeye make faza hausi ana afro..... Nilikirupuka nywele zinasisimka, natetemeka nikabeba nguo za job nikaenda kwa ndugu, nilirudi mule baada ya miezi mitatu kubeba vitu vyangu.
Nakumbuka mkataba wa nyumba uliandikwa ukihama unarudishiwa kodi sikuomba hata mia, nilivoondoka maza hausi ananipigia anacheka tu unarudi lini shwain zake!!!!
sikumbuki hata chumvi nilikoitupa