The Radar Scandal: Investigation & Progress

Chenge anaogopwa? maana kuna wakati alikipa chombo kimoja cha habari mkwara kiasi kwamba hadi leo hawataki kumgusa...
 
Chenge kweli ni mtu hatari sana mikataba mibovu yote anaijua yeye lakini mbona Jk alijua haya yote kabla ya kumurudisha serikalini?. katika matangazo ya TVT kesho yake watu waliongea bila kificho na yote tunayoyaona waliyazungumza lakini chenge na kiburi chake alipeta tu.

Baadhi tulisema wakati Jk anamtangaza kundi la watu tulipoteza mawasiliano gafla lakini mpaka sasa anapeta na inawezekana akasababisha makubwa zaidi ya haya. Nafikiri Chenge ametaaamia mayai akiondoka serikarini tutaona mengi sana.
 


sasa nimelewa
 

JF next mission ni Chenge...

Haogopwi mtu hapa na wala hahongwi mtu, habari za Chenge zitasambaa kwa kila mtanzania mwenye email address na internet access. Habari zake zitasambaa chini kwa chini kwa wanafunzi wote wa vyuo vikuu na baadaye zitakwenda mwenge na mabibo vijiweni kwenye salon. Baadaye zitapata mchapishaji Tanzania na baada ya muda itabidi Chenge atafute pamba za masikio kwani yataziba kwa yowe zitakazomfuata kila atakakokwenda!
 


Pamoja na movu yote ya Lowassa, Chenge alionekana kukerwa sana na kitendo cha kumutoa EL kwenye uwaziri mkuu hata alionekana waziwazi kwenye vyombo vya habari akikataa kuwa EL hakufanya UFiSADi. Unajua ukiwa mwizi huwezi kumuona mwizi mwenzako hivyo huyu Jamaa kama kweli Jk anataka kujenga tanzania yenye maadili hana budi kumwaga. FiSADi mkubwa aliyeataamia mayai.
 

Wewe mwache ahesabu siku,

Nasikia alianza kuhangaika sana alivyoona ile thread ya kwanza rasmi ikianza kuwekwa hapa JF. Ingawa alipuuzia maoni ya watu kwenye radio na magazeti ya nyumbani waliopinga sana kuteuliwa kwake tena kwenye baraza la Kikwete (tena kwenye wizara nyeti) lakini inasemekana kuwa ameanza kujipanga kupambana.

Kuna magazeti yalitaka kuandika habari zake akatoa vitisho na wakanyuti. Chenge yuko on notice... this is just the begining!
 
Kumbe Chenge Kakalia Mengi,mbali na siri lukuki za mikataba yenye mambo,kuna mtu aliyenitumia ka sms ati huyu Bwana ndiye alikalia ishu ya kufukiwa kwa wachimbaji wadogo wadogo kwenye mgodi wa Bulyankulu, akakanusha kwa nguvu zake zote kwamba hilo halikutokea.
Aidha ndiye kinara wa kupinga katiba ya jamhuri ya Muungano isiandikwe upya bali iendelee kusema Tanzania ni nchi ya ujamaa na kujitegemea n.k
 
Baada ya orodha ya mafisadi kutolewa ni nani aliyethubutu kukiri kuwa yeye ni mkurugenzi wa mojawapo ya makampuni yaliyoiba BoT tena huku macho yakiwa meupeeeeee?
 
Hivi kati ya Chenge na Rostam ni nani yawezekana kuwa ndio chanzo kikubwa cha matatizo yetu?
 

Mkuu

Tumejua sasa

Kikwazo kikubwa cha maendleo ya taifa la Tanzania ni Chenge, unajua ukiwa professional na ukatumia Uprofessional wako vibaya unaweza kusababisha balaa kubwa sana.

Huyu jamaa ni Professional na ni FiSADi mkubwa sana. kibaya nilisikia waziri wetu mkuu mpya niliyechumpa baada ya kuchaguliwa kuwa naye anamheshimu sana chenge na ndiye aliyemlea.

naomba waziri mkuu wetu asiwe na urafiki na MAFiSADi, kama amekosa marafiki ajue cheo ni dhamana unaweza kukosa marafiki na marafiki zako wakawa watanzania na nchi yako na ukaishi raha mstarehe.
 
Ingawa hili bomu ni directly la David na Bodi ya Wakurugenzi, lakini cha kujiuliza , kwanini Chenge hakunusa mambo kabla haya-jaharibika, kwa sababu prevention is better than to cure.
Na tatizo jingine kwa nini Chenge alikuwa ana mtetea EL??
 
chenge si lolote si chochote,siku ikifika na yeye ataondoka kama lowasa tu au balali kwa hiyo tusiwe na wasiwasi naye.kubukeni kuwa sauti ya umma ni ya mungu.
 

Tanzania msimwajiri mtu yeyote aliyeenda Havard mwacheni afungue kampuni aiendeshe na kulipa kodi kwa halali . Msimpe cheo hata cha ukarani wote waliokwenda Havard ni wezi............... Angalieni data. Kosa kubwa jingine JK anawaogopa waliokwenda chuo hicho ndio sababu anawapapatikia.
 
[size]hayo ni maswali ambayo Chenge anatakiwa kujibu kama kuna mtu atakuwa na ujasiri wa kumuuliza..[/size]

Hakuna kujibu wala nini afukuzwe tu huu umatonya utaisha lini? Rais aliyepewa madaraka na kushindwa kuyatumia atakuja kujibu maswali.
 

..hili ndilo swali la kujiuliza juu ya hii mikataba.

..imekuwa kama party la fiesta!kila mtu na style yake!
 
Wauze tuu hiyo kampuni ya ATCL kama walivyofanya ya Bia,haina faida yeyote zaidi ya kutia hasara walipa kodi na kutuletea usafiri mbovu na hatari.

washikaji serikali ndo kwanza imeichukua ATC, kama mnakumbuka mkapa alii-privatize kwa makaburu, hawa jamaa walipokuja bongo wakauza zile boieng mbili za ATC ambazo nyerere alinunua mpya kutoka kiwandani seattle USA 1977. halafu wakakodisha zingine mbili kutoka south africa na wakaja na pilots na airhostess wao waliokua wanakaa five star hotels wa kwetu wakakosa kazi, yaani mchezo wenyewe kama wa railway (TRC) wanavyofanya hivi sasa kuchukia mali za trc na kupeleka india hasa hasa vipuri vya engine za treni, sasa nirudi kwenye ATC, hawa makaburu shirika liliwashinda ndipo kikwete akaamua kulichukua tena na walipoondoka waliondoka na zile boieng 737 zao mbili walizokuja nazo, na sisi tukabaki kapa kwa sababu waliziuza za kwetu, hapo kweli akili ipo? yaani walikuja kutia hasara tu ni kama vile net group solutions ya tanesco.tukirudi kwenye hii issue ya sasa mi nafikiri tusiilaumu serikali au chenge wanaohusika ni ATC MANAGEMENT hawa ndo watueleze, chenge lazima achengechenge kwenye hili kwa sababu hii issue imekaa vibaya hata ingekua wewe usingependa kupitisha (sign) issue kama hii, kwa sababu mwishoni hii itaondoka na watu nyie subirini tu.
 
Tatizo la ATC ni ishara ya tatizo linalokabili idara nyingi za serikali; kipaumbele. Mattaka alipoingia ATC kipaumbele chake ni kuleta ndege nyingi (hata kama hana fedha na hana udhamini).. sasa wameingie mikataba ya ndege hizo zote na mambo yatakapoanza kwenda kombo miye sitasema hata neno moja kwani tumeonya toka mwanzo lakini watawala wetu wakapuuza.
 
Pamoja na hayo ya atc, kuna haya mapya na makubwa zaidi ya huyu mhindi kuchukua engine zetu na kuzipeleka india yaani hawa wahindi hawana utani kabisa na tanzania wanataka wawaache wa tz uchi sasa hawa viongozi kama wameshindwa kabisa si watuweke wazi maana wananchi tunaweza kuamua tukamrudishia nchi muingezeza labda tutapona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…