The Radar Scandal: Investigation & Progress

Labour wamepinga motion na kushinda. At least ujumbe umefika. Inasikitisha
kwamba tunatetewa na Conservative.

Maneno ya JK naona yanamfunga kweli kweli.
 
Nimeikosa lakini nitaipata wanaporudia, nilikuwa nafuatilia kashfa ya Kagame ile missile waliyotumia kuangusha ndege ilitoka Urusi ambao waliwauzia Uganda. kagame amekubali International investigation. Huyu jamaa na rafiki yake M7 jasho litawatoka saa.

Hiyo motion leo ni siku mbaya kwa sababu police wamemkamata tena rafiki mkubwa wa Blair (Lord Levy) anayekifadhili chama cha Labour kwa hiyo isingekuwa vizuri kwa wao kushindwa tena under party lines.
 
Si mchezo!
Bravo Mwanakijiji!
Hizi ni habari njema kwa wanaJF na watanzania wote kwa ujumla!
Mwendo mdundo, hakuna kulala!
 
jamani nashukuru, mmenifanya nienda na kutafuta majadiliano yote ya Bunge hilo leo.

Mjadala kuhusu ununuzi wa rada ulikuwa mkali katika Bunge la Uingereza hapo jana, baada ya wabunge kadhaa kutaka serikali ya Uingereza kufuatilia kwa ukaribu na kukubali kuwajibika kwa kashfa hii na kuhakikisha kuwa mauzo kama haya hayatatokea tena. Kama nilivyosema awali na imethibitishwa kwenye Bunge la Uingereza jana rada hii ni sehemu tu kwani sehemu ya pili ilizimwa kimya kimya. Unaweza kujisomea mjadala huu uliochukua masaa karibu mawili hapa na utaona mmoja wa Wabunge Bw. Norman Lamb akinukuu barua yangu kwa niaba ya Watanzania wengine kwa serikali ya Uingereza.

http://www.publications.parliament.uk/pa/cm/cmtoday/cmdebate/11.htm

Kwenda moja kwa moja kwenye kiungo cha Mhe. Norman Lamb akinukuu barua yetu nenda hapa:

http://www.publications.parliament.uk/pa/cm/cmtoday/cmdebate/16.htm

Kujisomea barua yenyewe nenda hapa:

http://www.habaritanzania.com

Ukifuatilia mjadala wa Bunge la Uingereza juu ya suala hili kuna mambo mengine mengi ambayo serikali yetu haijatuambia. Kwa mfano, kwanini serikali ya Tanzania imegoma World Bank kuchapisha ripoti inayohusu ununuzi huu? Kwanini hatuakimbiwa kuwa ununuzi huu ni sehemu tu, na nusu yake bado haijafanyika na ikabidi kuzimwa kimya kimya?
 
I read somewhere that "A thousand mile journey begin with one step". Hongera JF
 


Hebu pause kidogo MJJ, Ina maana zile Rada hatujapata (haipo Tanzania as we speak) bado au mimi naona kizunguzungu..??
 
Hongereni sana wana JF
!!!!!!!!!!!!!!!!!big up.....tusonge mbele. Mbona wanahabari wa bongo wamelala? au wamezibwa midomo?
 
Yebo Yebo.. nilichogundua baada ya kufuatilia mjadala huu wa Bunge la Uingereza kumbe hiyo rada ilikuwa iwe na sehem mbili (is that why it covers only 1/3 of the country?) tuliyonunua ni rada kamili lakini tulitakiwa tununue na sehemu ya pili lakini kutokana na hizi kelele serikali imeamua kula jiwe!!
 
Hongereni sana wana JF
!!!!!!!!!!!!!!!!!big up.....tusonge mbele. Mbona wanahabari wa bongo wamelala? au wamezibwa midomo?


Hao wamezibwa midogo na masikio kabisa...kilicho wazi kwao ni mifuko yao tu.
 
Hofu imetawala Tanzania, waandishi wetu wanaogopa kwani wakiandika habari ambazo sirikali hazipendi watafungia, hofu hofu hofu..........

kazi ya ziada inatakiwa ifanywe kuondoa hofu kwa watanzania, ndani ya vyama na serikali kuna mashupavu hawakubalini na ufedhuli ufanyikao, lakini wamejawa hofu, wakipinga wataonekani si wenzao watatengwa au watapigwa fitna.

tufanyejeje kuondokana na hofu?
 

Hii inafuatia mjadala wa jana bungeni.
 
Dawa pekee ni sisi kuwa serious na kutumia akili na nyenzo . We can help and we can fight . Kuna UK , na wengine wengi. Kama Serikali yetu haitasikia hatuwezi kuandamana maana tuko so scattered ila tuta andamana kwa kalamu na ujuzi huu kufikisha ujumbe . Bravo Mzee MKJJ
 
Mwanajiji Hongera sana, JF ni eneo muafaka la mapambano dhidi ya ufisadi. Safi sana. Wana JF, Kanyaga twende mpaka kieleweke!!
 
Jana jioni record ya wasomaji katika mtandao huu ilivunjwa na leo huenda ikapatikana record mpya muda si mrefu.Wezi na wala rushwa anzeni kurudisha mali za wananchi hamuwezi kuendelea kuiba kweupe namna hii.
 
Wabongo Naomba Nichukue Muda Huu Kuongelea Upande Mwengine Wa Shilingi.

Nafikiri Mimi Ni Mmoja Wa Watu Waliopata Nafasi Ya Kuangalia Huo Mjadala. Linalotokea Hapa Baada Ya Kusoma Michango Ya Waliotangulia Inaonyesha Wazi Kwamba Kuna Jjambo Kubwa Ambalo Maya Be Hamkulielewa Au Mmelielewa Na Kwamba Mnajifanya Kama Hamjaelewa.

Kwanza, Suala La Siasa Ya Tanzania Ni La Watanzania Wenyewe Na Raisi Anapochukua Ridhaa Hiyo Basi Ni Kwamba Ufanya Kile Kilichobora Kwa Nchi Yake. Mkapa Amenunua Rada Sio Suala Baya. Suala Linalojadiliwa Na Waingereza Ni Kutaka Kuona Uwazi Wa Deal Lenyewe Lilivyofanyika. Namshukrur Mwana Kijiji Alipoeleza Kwamba Deal Lile Lilitakiwa Kuwa Na Sehemu Mbili. Kwa Hiyo Basi, Maswali Ya Kujiuliza Ni Kwamba Je Ni Vibaya Kwa Kununua Hiyo Rada Kwa Wakati Mmoja?

Suala La Kamisheni Ni Suala Ambalo Halikuzungumzwa. Waingereza Walikuwa Wanalalamika Kwamba Nchi Kama Tanzania Imekuwa Maskini Na Kununua Rada Haikutakiwa.swali Ni Kwamba Usalama Wako Unaweza Jadiliwa Na Mtu Kweli, Hawa Waingereza Ni Wakina Nani Hadi Watuamulie Nini Cha Kufanya Au Tulalaje ?

Suala Jengine Ni Kuhusu Kauli Ya Mh.kikwete Akiwa Waziri Wa Mambo Ya Nje. Nafikiri Mtakubaliana Na Mimi Nitakjapo Sema Kwamba Ile Ni Kauli Ya Commitment Na Ndiyto Maana Hata Yule Mbunge Aliposema Yalke Maneno Alizomewa.

Mimi Nafikiri Tuangalie Kwetu Sisi, Tuachane Na Hizi Siasa Za West Ambazo Zinaweza Kutugombanisha. Tony Blair Knows What He Was Doing, He Is There Kuhahakikisha Kwamba Usalama Duniani Unakaa Sawa, Hawa Conservative Sidhani Kama Wana Nia Hiyo. Naanza Kupata Wasiwasi Na Hii Siasa Yao Kama Kweli Itatusaidiia Sisi Walalahoi Pale Kipawa, Dar Es Salaam Mjini Au Wengine Uita Bongo.

Mungu Ibaliki Tanzania, Mungu Ibaliki Afrika.

Nakaribisha Kukosolewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…