SIMULIZI: THE LOST BOYS (8)
MTUNZI: FRANK MASAI
MAWASILIANO: 0752353039
ILIPOISHIA....
WALE wadada wawili,walipangwa kuwazingua Moi na Sunday na huyu Waziri mkuu,yeye alipangwa kumzingua kubwa la maadui lenyewe,Ban Diho.
Uzuri sasa upo hapa. Japo wadada hawa walipangwa kwa wiki karibu moja na nusu,lakini waliwahi kukutana na Junior,Fred na Hans mara mbili tu!.Huku yule Waziri Mkuu akiwa hajawahi kabisa kukutana na hawa watu zaidi ya Suarez.
Wasichana wale waliunda urafiki na Wagumu kwa siku kama tano. Walikuwa wana uwezo wa kuwashawishi wagumu mpaka wakafanya wanachohitaji. Muda mwingi walikuwa wanawasema sana vibaya wakina Junior kitu kilichofanya wale wagumu kupenda sana kukaa na wale mabinti wawili.
****SASA ENDELEA*****
HUYU dada mwingine ambaye alikuwa na jukumu kubwa kwa Ban,yeye alikuwa haonekani na wale wadada wengine bali yeye alikuwa kaanzisha urafiki wa karibu na Ban. Huyo ndiye yule Waziri Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Hakuna aliyejua nia ya wakina Junior zaidi ya yule Waziri Mkuu ambaye alipewa mkanda mzima uliotokea.Hadithi yote alipewa na Suarez.Hivyo kwa kuwa yeye alikuwa kiongozi,aliona ni heri jambo lile liishe kiuanachuo ila na yeye akiwa shahidi kama kiongozi,na ndio maana alikubali kisasi kilipwe,na kisha wote atawaita na kuwaonya kwa kuwekeana mabifu yasiyo na mpango.
Wale wadada wengine,wao walipewa hela kiasi na wala hawakuhitaji kuuliza kwa nini wamepewa majukumu yale.
**************
Baada ya Ban kupigiwa simu,alitoa tabasamu kubwa kwa kitendo cha dada yule Waziri Mkuu kumuita usiku ule.
Licha ya kuwa Waziri Mkuu,pia dada yule hata angeshiriki u-miss vyuo,angepata tu!. Alikuwa ni mzuri hasa,yaani kwa pale chuo,msichana yeyote alipenda kujifananisha na yule Waziri Mkuu asiye na majigambo wala mapozi kwa mwanachuo au hata mtu baki.
Saa nne za usiku,mrembo yule anampigia simu Ban ili wakaonane. Na yeye Ban bila kufikiria, aliwaaga kwa kuwadanganya rafiki zake kuwa anaenda kukutana na mzazi wake.
Chumba chao kikabaki na Sunday,Moi na Mose. Ambao wawili kati yao,nao pia walipigiwa simu na kila mmoja kwa wakati wake akaondoka kwenda kwa hao wasichana wanachuo ambao kwa muda mfupi walishakaa vichwani mwa Wagumu.
Chumba kikabakiwa na Mose peke yake. Huyu yeye hakupangiwa mwanamke ila kuachwa kwake, ilikuwa ni makusudi.
************
Baada ya Ban kwenda huko alipoitwa,akaanza kubabaishwa na Waziri yule Mkuu kwa lengo la kupoteza muda.
Kwa kuwa mwanaume ni dhaifu sana kwa mwanamke,yaani ni sawa na mfupa kwa fisi,basi Ban naye alilegea akawa bwege kabisa.
Hakujua hayo yote ilikuwa ni fitina za wakina Junior,ndio maana hata pale aliposhikwa mkono na kuvutiwa gizani zaidi,yeye alivutika kama bwege vile. Na hatimaye kazi ya yule dada ikawa inaelekea ukingoni.
Sasa Ban alikuwa uso kwa uso na vijana watatu waliovalia kininja.Kwanza kabisa wale maninja walizuga kama ni vibaka na wanataka kuwapora.Mmoja wapo alimvuta dada mkuu pembeni na Ban alivoona hivyo,alianza kuomba msamaha ili dada yule asifanywe chochote.
Lakini kumbe ilikuwa ni ujanja tu!Mpango ulipangwa, ukapangika. Hatimaye kwa kuwa alijidai nunda basi dada wa watu aliachwa na mzigo wake akabebeshwa yeye.
************
Baada ya kama robo saa ya tukio lile kwa Ban,likatokea tukio kama lilelile kwa Sunday na Moi. Hali iliyofanyika kwa Ban,ndiyo iliyofanyika kwa Moi na Sunday. Nao walitekwa kama kawaida.
Baada ya kutekwa na maninja wale,walivuliwa nguo zote na kubaki kama walivyozaliwa. Wakati huo Ban alikuwa kaachwa mbali kidogo huku naye kavuliwa nguo na kufungwa kamba.
Sunday na Moi,walipovuliwa nguo,wakapelekwa hadi kwa Ban ambaye alikuwa anapigwa na baridi pale alipokuwepo.
Wakawarundika na kuwafunga kamba,kisha wao wakapotea eneo lile na kuelekea vilipo vyumba vya mateka wale.
Huko walikuta mlango umefungwa na kwa kuwa walishajua kuna mtu mmoja kabaki, basi ni lazima wangegonga na kufunguliwa kwa sababu yule wa ndani angejua kuwa wale ni wakina Ban.
Mawazo yalikuwa sawa kabisa. Wakiwa vilevile kininja,waligonga mlango kistaarabu na bila hata kuulizwa ni nani,mlango ukafunguliwa. Hapo wakaingia kama kawaida maninja watatu na kumsukumia Mose ndani kwa nguvu. Naye akayumba yumba hadi akadondokea kitandani.
“Ni nani nyie”.Mose aliuliza kwa sauti ya uoga yenye utetemeshi huku macho yake makubwa na mekundu yakimtoka kama jusi lililobanwa na lango la kanisa.
“Shiiiiiiiiiii. Ukipiga kelele tu! Tunaondoa shingo yako na maini yako tunaenda kulia wali kantini huku mdudu wako tunaupeleka Super Market ya Mlimani City ukauzwe kama sonseji”.Ninja mmoja alimtisha Mose. Huyo alikuwa ni Junior,lakini Mose hakutambua ni nani.
“Poa,lakini nimefanyaje?”Mose aliendelea kuuliza kwa uoga.
“Ngoja utaelewa sasa hivi”.Alijibu ninja mwingine huku akimsogezea uso kwa karibu zaidi. Huyo alikuwa Suarez,wakati huo ninja Hans yeye alishaanza kupekua makabati ya mle ndani.
Kwa msaada mkubwa walioufanya wale maninja watatu,waliweza kuvuruga nguo zao zote za mle kabatini na kuziweka sehemu moja.
“Zetu zilichafuka kichizi. Sasa zenu hazichafuki,zitafanyiwa sayansi hadi zikome”.Ninja mwingine aliyekuwa hajaongea hata mara moja,sasa alifungua mdomo wake, na baada ya hapo akatoa chupa moja kubwa ya maji.
Chupa ile ilikuwa imejaa kimiminika chenye rangi ya njano.Na alipofanikiwa kutoa chupa ile mfukoni,alitoa kichupa kingine kidogo chenye unga mwekundu.
Akachovya kidogo ule unga kwa kutumia kitu kama eye droper. Eye Droper ni kile kichupa kinachotumika kuweka dawa ya macho au ya sikio,ambacho ukitaka kuweka dawa ile,unakiminya,nacho kinatoa tone la dawa.
Baada kuuvuta ule unga kwenye eye droper,akatoa eye droper nyingine yenye maji meupe na kutonesha kwenye ile chupa kubwa ya maji. Hapo maji ya njano yakawa ya blue.
Akachukua ule unga,nao akauweka kwenye maji yale ya blue. Ghafla ulifuka moshi mkubwa sana kutoka kwenye chupa ile.
Ninja yule mwanasayansi,akatabasamu tabasamu la ushindi. Na hapo hapo alichukucha kwa nguvu hadi maji yale yakawa meusi kabisa.
Kitendo bila kuchelewa akaanza kumwagia nguo zilizokuwa mbele yake na zile walizokuwa wamevaa wakina Ban.
Baada ya hapo,alimsukuma pembeni Mose na kuanza kumwaga maji yale kidogo kidogo kwenye magodoro ya mule ndani. Aliporidhika,akamgeukia Mose na kuongea naye.
“Sisi tulikaa kimyaaa,sasa zamu yenu. Sikiliza kwa makini huko nje kitakachokuja kutokea kwa wenzako”.Huyo ni Hans alikuwa anamwambia Mose ambaye tayari alikuwa ameelewa ni wakina nani.
Alikaa kimya huku akiangalia chini kwa hasira zilizojaa uoga.
“Hiyo dawa niliyomwaga hapo,subiri kwa dakika kumi,utaona matokeo yake”.Hans alimaliza,akawakusanya washirika wake na kupotea mle ndani.
***************
Kule kwa wakina Ban,walikuwa wanajitahidi kufungua zile kamba hadi wakafanikiwa.
Kwa kuwa ilikuwa ni usiku sana,waliona ni afadhari hasa pale walipoona kulikuwa hamna watu waliokuwa wanakatiza katiza.
Walijifariji na kushika njia ya kurudi chumbani kwao huku wakiwa vilevile uchi,na pale mbele walikuwa wamepaficha kwa mikono tu!.Umbali wa kutoka pale walipo hadi chumbani kwao,ilikuwa ni kama dakika tano kwa miguu.
Walipofika walikuta kumetulia sana,kitu kilichowapa moyo kuwa hakuna watu muda ule.
Wakachungulia getini kuhakikisha kama ni kweli mawazo yao yalikuwa sawa. Baada ya kuona ni kweli,wakaingia getini wakiwa wanakimbia huku wameinama eti wasionekane.
Lakini wakati wanafanya hivyo,mara mbele yao wakatokea wanachuo wenzao kama mia hivi au mia mbili,tena wanawake wakiwa kwa asilimia kubwa sana.
“Sapraiziiiiii”.Zilisikika sauti za wanawake zikisema na kuwaacha wakina Ban wakiwa wameganda na kutopata cha kufanya kwa wakati ule.
Walibaki wamekodoa macho bila kujua wafanye nini pale walipokuwa wamesimama. Kukimbia hawawezi,kutembea hawawezi wala kunyata kwao ni shida.
Baadhi ya wanachuo walitoa hadi simu zao na kuanza kuwafyatua picha kuonesha kuwa wamefurahia sana ile hali.
****************
Pale wale wadada walipomaliza kazi yao ya kuwapelekea Moi na Sunday kwa wakina Junior,moja kwa moja walirudi vyumbani mwao na kuanza kuwapa taarifa wenzao wa karibu na kuwaomba wajikusanye ili wawakaribishe watu hao kwa kuwafanyia sapraizi.Na kweli walifanikiwa sana kuwakusanya wanawake wenzao.
Kwa upande wa wanaume,ilikuwa ni kazi ya Fred kuwakusanya na kuwapa taarifa za ugeni wa usiku ule,na kila aliyepata habari zile,alimtaarifu mwenzake. Hivyo kundi sasa la kuwasubiri wageni wale waliokuwa uchi,likawa kubwa na lote lilijificha nyuma ya majengo yale wanayokaa wanachuo wengine.