SIMULIZI: THE LOST BOYS (29)
MTUNZI: FRANK MASAI
MAWASILIANO: 0752353039
WALIJUA kuwa Hans anapenda sana kumpeleka Eve sehemu zenye maji,hivyo kuna barabara ambayo walipita,walijua wazi kuwa hawa wanaelekea sehemu fulani. Hisia hizo,zikasafirishwa na kuwafikia Sunday na Ban.
Nao wakina Sunday,wakajipanga kwa ajili ya mashambulizi hayo kwa kukusanya vitu muhimu na kwenda sehemu hiyo.
Hisia zao zilikuwa ni kweli.Baada ya dakika kadhaa za bodaboda na taksi kuwa barabarani,hatimaye waliingia mahala ambapo palikuwa ni kusudio lao.
Watu walikuwa wengi sana katika sehemu ile ambao ulikuwa ni ufukwe wa Mikadi.Ufukwe ambao hauna kawaida ya kujaza sana watu kama ule wa Coco.
Hans alkuwa ni mwenye tabasamu kila mara pale alipokuwa akimuangalia Eve jinsi alivyokuwa kapendeza.
“Leo umependeza sana.”Hans alimwaga sifa kwa kimwana yule ambaye alichanua tabasamu pana usoni pake.Hiyo ni baada ya kupata sehemu moja yenye kivuli na kukaa.
“Nawe umependeza sana. Hans ila na maongezi na wewe,tofauti na yale ya siku zote.”Eve alitoa sifa na kufunguka kilichomkutanisha na Hans kwa wakati ule.
“Niambie tu!.”Hans alijibu bila kusitasita.
“Embu nisubiri kwanza nikachukue pale koni.”Eve alinyanyuka na akiwa na mavazi yake ya ufukweni na kwenda sehemu moja ambayo kunauzwa koni.
Huku nyuma Hans akabaki peke yake akipunga upepo na ndio muda huo huo Sunday aliutumia kufanya yake.
Sunday alienda pale alipo Hans na kisha kwa utaalamu mkubwa alijidai kajikwaa na kumdondokea Hans kwenye mapaja.
Kitendo kile kilimshitua Hans lakini hali ilimrudi na kuwa nzuri pale alipogundua ni Sunday. Alimsalimia kwa furaha na Sunday naye akaitikia salamu ile huku akimuomba msamaha kwa kilichotokea.
Baada ya salamu hiyo na msamaha,Sunday alititia eneo lile kwa furaha kubwa kwa kuamini mchezo alioucheza umetimia bila shaka.
Ukweli ni kwamba,wakati Sunday anamdondokea Hans,alikuwa kashika sindano ndogo zile za kubania karatasi. Sindano ile ndio alikuwa kaipaka dawa aliyokusudi.
Kitendo cha kumdondokea,kilimpa upenyo Sunday kumchoma kidogo Hans bila ya yeye kuhisi maumivu makali kama yale ya kumdondokea.
Baada ya kufanikiwa kumchoma na kisindano kile,aimuomba msamaha na kuondoka mahala pale akimuacha Hans hana hili wala lile.
Dakika tatu mbele,Eve alirudi na makopo mawili ya koni.Moja akampatia Hans na linguine akabaki nalo yeye,kisha taratibu wakaanza kujiburudisha.
“Mimi nachotaka kujua ni kama unahusika na mambo yaliyowatokea Fred na Junior.Maana wote wanalalamika kuwa ni wewe ndiye umefanya,sasa niambie ukweli wote ikibidi niwaite wote ili mpatane maana mtu kama Junior aliapa atakuua.”Eve alianzisha maongezi hayo baada ya kubugia vijiko kadhaa vya koni aliyonunua.
“Kwa hiyo na wewe unaamini.”Hans aliuliza.
“Naweza kuamini.Lakini najua huwezi kufanya vile kama hujachokozwa.”Eve aliweka wazi hisia zake.
“Okey.Kiukweli kabisa,Fred ni mimi ndiye nimefanya lakini Junior sifahamu aliyefanya.”Hans alijibu na kusikiliza Eve atatoa maamuzi gani.
“Sasa kwa nini ulimfanyia vile Fred?.”Eve alitupa kete nyingine ya swali.
“Wanazingua wale. Ujue siku ile kule Coco eti walinirekodi kwenye kamera wakati najirusha kwenye maji,bsi ikawa utani ni utani.Huyu Fred akawa hadi ananitukana,ndio nikaona bora nilipe.”Hans akatoa sababu ambayo ilimfanya Eve acheke kidogo na kuendelea.
“Ujue ni watoto sana. Sasa hiyo inawasaidia nini?.”Swali lilitupwa lakini lilikuwa halina kitu zaidi ya Hans kunyamaza huku kainamisha kichwa chake.
“We Hans,si nakuuliza?.”Eve alimshtua Hans lakini Hans kichwa kilikuwa vilevile.
“Wewe.”Eve aliita huku anamsukuma.
“Mmmh.”Masikini Hans aliitika huku udenda unamtoka kama vile teja.
“Khaaa! Hivi nyie watu mna matatizo gani? Ona huyu naye leo.”Eve alilalamika peke yake bila mtu yeyote kumfatilia.
“Kichefuchefu.”Hans alisema maneno hayo kwa sauti ya chini kabisa.Sauti ambayo ilimfanya Eve kuuliza tena alichokisema huku anapeleka uso wake karibu namdomo wa Hans ili asikie vizuri.
Kabla hata Hans hajarudia lele neno la kichefuchefu. Eve alitapikiwa usoni na matapishi yaliyotoka mdomoni kwa Hans.
Matapishi yale yalitoka kwa wingi kwani yalijumuisha vyakula vyote alivyokula Hans tangu asubuhi ya siku ile. Yote hayo yaliishia mwilini kwa Eve ambaye alikuwa kaganda kama barafu pale kitendo kile kilipokuwa kinatokea.
Watu ambao walikuwa maeneo yale,walishindwa kuvumilia kucheka na kushangilia kwa kile walichokuwa wanakiona,amahakika Hans alipatikana na aliaibika.
Baada ya kutapika,Hans aliyekuwa kama teja,alidondokea Eve miguuni na kumfanya Eve asiweze kusimama haraka kwa muda ule.
Macho ya Hans yakiwa yaona kwa mbali,ndipo alipomuona na Junior akiwa mmoja wa watu ambao wanamcheka,tena yeye alikuwa anapiga na picha,sijui za ukumbusho au nini.
Baada ya Hans kumuona Junior,aliongea kwa sauti ya chini huku anamuoneshea kidole Junior. Hapo hapo,usingizi mzito ukambeba.
Kazi ikabaki kwa Eve kujipapatua ili ajitoe mwilini mwa Hans ambaye alikuwa kalala usingizi wa hatari.
****
Ni baada ya dakika zisizopungua mbili,ndipo aibu ile ilipomtoka Eve. Matapishi ambayo ametapikiwa na Hans alienda kwenye maji ya ufukwe ule na kujisafisha na Eve alirudi katika hali kiasi fulani. Sasa ikabaki kazi ya kumnyanyua Hans aliyekuwa kajilaza pale kichangani hajitambuni.
Ilikuwa si shuhuri ya kitoto kumnyanyua mtu kama Hans,kwani kila aliyeombwa msaada wa kufanya hivyo,alihofiwa kutapikiwa. Akili kumkichwa zikatakiwa kuchuwa nafasi katika kichwa Eve.
Alichoona cha maana mwanamke yule wa shoka ni kukimbilia nje na kumtafuta dereva taksi mmojawapo na kuja naye hadi pale alipomuacha Hans amelala.
“Haikuwa rahisi wa kitoto kumbeba jamaa yule aliyekuwa kalala fo fo fo,hajitambui wala hajielewi yupo wapi kwa muda ule.
Baada ya kufanikiwa kumpandisha katika taksi,safari iliyofuata ilikuwa ni ya kwenda hospitali.Na moja kwa moja walimpeleka katika hospitali fulani iliyopo pale Msasani na mara moja Hans akaanza kupewa huduma ya kwanza ambayo ilichukua dakika kama kumi na tano.
Dakika kadhaa nyingine,Hans alizinduka mna kuanza kushangaa ilikuwaje mpaka akawa pale. Baada ya kuvuta kumbukumbu,ndipo alipokumbuka yale yote yaliyotokea kwenye ufukwe Mikadi,na hasira zilimpanda zaidi alipokumbuka sura ya Junior ikimchukua picha.
Kitanda cha hospitali alikiona si mahala pake tena. Na kwa kuwa alikuwa hajatundikiwa dripu,aliona ni bora anyanyuke haraka ili aende walipo wakina Junior na kutaka maelezo ya kina ya kwa nini kafanya yale yote.
Alinyanyuka na kuvaa viatu vyake.Kisha alitoka nje na kukutana na Eve akiwa kwenye benchi la kusubiria huduma za pale hospitali.
Alimpita bila hata kuongea naye,kitendo kilichomfanya Eve ashangae na kumuita kwa nguvu. Lakini Hans ni kama hakusikia sauti ile na wala hakuwa na mpango nayo zaidi ya kwenda anapojua yeye.
Eve akaona hayo mengine tena. Alichofanya ni kumkimbilia kisha akamshika began a kumuuliza kulikoni.
“Wewe na wale wajinga kule,mmepanga kuniaibisha. Mmmeniwekea madawa yenu kwenye koni ili nitapike na kulala,si ndio ee.”Hans alimjibu Eve kwa hasira.
“Hee jamani,yamekuwa hayo tena.Mimi naweza kufanya hivyo jamani?.”Eve alikumbwa na taharuki ya ajabu baada ya kusikia laumu zile zilizouvunja moyo wake.
“Ushindwe kufanya hivyo kwani wewe nani?Wewe Malaika?Wewe si binadamu kama mimi tu! Mwenye kinyongo na watu na wenye chuki zilizojikita moyoni mwake. Utashindwa nini kuniwekea madawa? Kuna kitu kinamshinda mwanamke? Kuna kitu kitakushinda wewe kama hunipendi mimi?.”Hans alilopoka maneno mengi na bila hata kusubiri Eve ajitetee,aliuputa mokono wa mrembo yule na kuanza kuondoka.
“Na mwenzako Junior uliyepanga naye mchezo wote,nilimuona akinichukua picha.Sasa atakuhadithia kitakachomkuta.Wajinga nyie.”Msumali wa maneno ulikomelewa na kinywa cha Hans,kisha jamaa yule mguu na njia ukashika nafasi huku akimuacha Eve kakamata kiuno kama anaangalia ngoma ya Kisambaa au Wadigo.Hakika alipatikana,uso ulimshuka kama ngozi ya chini ya shingo ya ng’ombe.
*******
Walijua kuwa Hans anapenda sana kumpeleka Eve sehemu zenye maji,hivyo kuna barabara ambayo walipita,walijua wazi kuwa hawa wanaelekea sehemu fulani. Hisia hizo,zikasafirishwa na kuwafikia Sunday na Ban.
Nao wakina Sunday,wakajipanga kwa ajili ya mashambulizi hayo kwa kukusanya vitu muhimu na kwenda sehemu hiyo.
Hisia zao zilikuwa ni kweli.Baada ya dakika kadhaa za bodaboda na taksi kuwa barabarani,hatimaye waliingia mahala ambapo palikuwa ni kusudio lao.
Watu walikuwa wengi sana katika sehemu ile ambao ulikuwa ni ufukwe wa Mikadi.Ufukwe ambao hauna kawaida ya kujaza sana watu kama ule wa Coco.
Hans alkuwa ni mwenye tabasamu kila mara pale alipokuwa akimuangalia Eve jinsi alivyokuwa kapendeza.
“Leo umependeza sana.”Hans alimwaga sifa kwa kimwana yule ambaye alichanua tabasamu pana usoni pake.Hiyo ni baada ya kupata sehemu moja yenye kivuli na kukaa.
“Nawe umependeza sana. Hans ila na maongezi na wewe,tofauti na yale ya siku zote.”Eve alitoa sifa na kufunguka kilichomkutanisha na Hans kwa wakati ule.
“Niambie tu!.”Hans alijibu bila kusitasita.
“Embu nisubiri kwanza nikachukue pale koni.”Eve alinyanyuka na akiwa na mavazi yake ya ufukweni na kwenda sehemu moja ambayo kunauzwa koni.
Huku nyuma Hans akabaki peke yake akipunga upepo na ndio muda huo huo Sunday aliutumia kufanya yake.
Sunday alienda pale alipo Hans na kisha kwa utaalamu mkubwa alijidai kajikwaa na kumdondokea Hans kwenye mapaja.
Kitendo kile kilimshitua Hans lakini hali ilimrudi na kuwa nzuri pale alipogundua ni Sunday. Alimsalimia kwa furaha na Sunday naye akaitikia salamu ile huku akimuomba msamaha kwa kilichotokea.
Baada ya salamu hiyo na msamaha,Sunday alititia eneo lile kwa furaha kubwa kwa kuamini mchezo alioucheza umetimia bila shaka.
Ukweli ni kwamba,wakati Sunday anamdondokea Hans,alikuwa kashika sindano ndogo zile za kubania karatasi. Sindano ile ndio alikuwa kaipaka dawa aliyokusudi.
Kitendo cha kumdondokea,kilimpa upenyo Sunday kumchoma kidogo Hans bila ya yeye kuhisi maumivu makali kama yale ya kumdondokea.
Baada ya kufanikiwa kumchoma na kisindano kile,aimuomba msamaha na kuondoka mahala pale akimuacha Hans hana hili wala lile.
Dakika tatu mbele,Eve alirudi na makopo mawili ya koni.Moja akampatia Hans na linguine akabaki nalo yeye,kisha taratibu wakaanza kujiburudisha.
“Mimi nachotaka kujua ni kama unahusika na mambo yaliyowatokea Fred na Junior.Maana wote wanalalamika kuwa ni wewe ndiye umefanya,sasa niambie ukweli wote ikibidi niwaite wote ili mpatane maana mtu kama Junior aliapa atakuua.”Eve alianzisha maongezi hayo baada ya kubugia vijiko kadhaa vya koni aliyonunua.
“Kwa hiyo na wewe unaamini.”Hans aliuliza.
“Naweza kuamini.Lakini najua huwezi kufanya vile kama hujachokozwa.”Eve aliweka wazi hisia zake.
“Okey.Kiukweli kabisa,Fred ni mimi ndiye nimefanya lakini Junior sifahamu aliyefanya.”Hans alijibu na kusikiliza Eve atatoa maamuzi gani.
“Sasa kwa nini ulimfanyia vile Fred?.”Eve alitupa kete nyingine ya swali.
“Wanazingua wale. Ujue siku ile kule Coco eti walinirekodi kwenye kamera wakati najirusha kwenye maji,bsi ikawa utani ni utani.Huyu Fred akawa hadi ananitukana,ndio nikaona bora nilipe.”Hans akatoa sababu ambayo ilimfanya Eve acheke kidogo na kuendelea.
“Ujue ni watoto sana. Sasa hiyo inawasaidia nini?.”Swali lilitupwa lakini lilikuwa halina kitu zaidi ya Hans kunyamaza huku kainamisha kichwa chake.
“We Hans,si nakuuliza?.”Eve alimshtua Hans lakini Hans kichwa kilikuwa vilevile.
“Wewe.”Eve aliita huku anamsukuma.
“Mmmh.”Masikini Hans aliitika huku udenda unamtoka kama vile teja.
“Khaaa! Hivi nyie watu mna matatizo gani? Ona huyu naye leo.”Eve alilalamika peke yake bila mtu yeyote kumfatilia.
“Kichefuchefu.”Hans alisema maneno hayo kwa sauti ya chini kabisa.Sauti ambayo ilimfanya Eve kuuliza tena alichokisema huku anapeleka uso wake karibu namdomo wa Hans ili asikie vizuri.
Kabla hata Hans hajarudia lele neno la kichefuchefu. Eve alitapikiwa usoni na matapishi yaliyotoka mdomoni kwa Hans.
Matapishi yale yalitoka kwa wingi kwani yalijumuisha vyakula vyote alivyokula Hans tangu asubuhi ya siku ile. Yote hayo yaliishia mwilini kwa Eve ambaye alikuwa kaganda kama barafu pale kitendo kile kilipokuwa kinatokea.
Watu ambao walikuwa maeneo yale,walishindwa kuvumilia kucheka na kushangilia kwa kile walichokuwa wanakiona,amahakika Hans alipatikana na aliaibika.
Baada ya kutapika,Hans aliyekuwa kama teja,alidondokea Eve miguuni na kumfanya Eve asiweze kusimama haraka kwa muda ule.
Macho ya Hans yakiwa yaona kwa mbali,ndipo alipomuona na Junior akiwa mmoja wa watu ambao wanamcheka,tena yeye alikuwa anapiga na picha,sijui za ukumbusho au nini.
Baada ya Hans kumuona Junior,aliongea kwa sauti ya chini huku anamuoneshea kidole Junior. Hapo hapo,usingizi mzito ukambeba.
Kazi ikabaki kwa Eve kujipapatua ili ajitoe mwilini mwa Hans ambaye alikuwa kalala usingizi wa hatari.
****
Ni baada ya dakika zisizopungua mbili,ndipo aibu ile ilipomtoka Eve. Matapishi ambayo ametapikiwa na Hans alienda kwenye maji ya ufukwe ule na kujisafisha na Eve alirudi katika hali kiasi fulani. Sasa ikabaki kazi ya kumnyanyua Hans aliyekuwa kajilaza pale kichangani hajitambuni.
Ilikuwa si shuhuri ya kitoto kumnyanyua mtu kama Hans,kwani kila aliyeombwa msaada wa kufanya hivyo,alihofiwa kutapikiwa. Akili kumkichwa zikatakiwa kuchuwa nafasi katika kichwa Eve.
Alichoona cha maana mwanamke yule wa shoka ni kukimbilia nje na kumtafuta dereva taksi mmojawapo na kuja naye hadi pale alipomuacha Hans amelala.
“Haikuwa rahisi wa kitoto kumbeba jamaa yule aliyekuwa kalala fo fo fo,hajitambui wala hajielewi yupo wapi kwa muda ule.
Baada ya kufanikiwa kumpandisha katika taksi,safari iliyofuata ilikuwa ni ya kwenda hospitali.Na moja kwa moja walimpeleka katika hospitali fulani iliyopo pale Msasani na mara moja Hans akaanza kupewa huduma ya kwanza ambayo ilichukua dakika kama kumi na tano.
Dakika kadhaa nyingine,Hans alizinduka mna kuanza kushangaa ilikuwaje mpaka akawa pale. Baada ya kuvuta kumbukumbu,ndipo alipokumbuka yale yote yaliyotokea kwenye ufukwe Mikadi,na hasira zilimpanda zaidi alipokumbuka sura ya Junior ikimchukua picha.
Kitanda cha hospitali alikiona si mahala pake tena. Na kwa kuwa alikuwa hajatundikiwa dripu,aliona ni bora anyanyuke haraka ili aende walipo wakina Junior na kutaka maelezo ya kina ya kwa nini kafanya yale yote.
Alinyanyuka na kuvaa viatu vyake.Kisha alitoka nje na kukutana na Eve akiwa kwenye benchi la kusubiria huduma za pale hospitali.
Alimpita bila hata kuongea naye,kitendo kilichomfanya Eve ashangae na kumuita kwa nguvu. Lakini Hans ni kama hakusikia sauti ile na wala hakuwa na mpango nayo zaidi ya kwenda anapojua yeye.
Eve akaona hayo mengine tena. Alichofanya ni kumkimbilia kisha akamshika began a kumuuliza kulikoni.
“Wewe na wale wajinga kule,mmepanga kuniaibisha. Mmmeniwekea madawa yenu kwenye koni ili nitapike na kulala,si ndio ee.”Hans alimjibu Eve kwa hasira.
“Hee jamani,yamekuwa hayo tena.Mimi naweza kufanya hivyo jamani?.”Eve alikumbwa na taharuki ya ajabu baada ya kusikia laumu zile zilizouvunja moyo wake.
“Ushindwe kufanya hivyo kwani wewe nani?Wewe Malaika?Wewe si binadamu kama mimi tu! Mwenye kinyongo na watu na wenye chuki zilizojikita moyoni mwake. Utashindwa nini kuniwekea madawa? Kuna kitu kinamshinda mwanamke? Kuna kitu kitakushinda wewe kama hunipendi mimi?.”Hans alilopoka maneno mengi na bila hata kusubiri Eve ajitetee,aliuputa mokono wa mrembo yule na kuanza kuondoka.
“Na mwenzako Junior uliyepanga naye mchezo wote,nilimuona akinichukua picha.Sasa atakuhadithia kitakachomkuta.Wajinga nyie.”Msumali wa maneno ulikomelewa na kinywa cha Hans,kisha jamaa yule mguu na njia ukashika nafasi huku akimuacha Eve kakamata kiuno kama anaangalia ngoma ya Kisambaa au Wadigo.Hakika alipatikana,uso ulimshuka kama ngozi ya chini ya shingo ya ng’ombe.