The lost boys

Season I

Hans 1 vs Ban 0

Ila wanafurahisha sana... mambo yao, makundi yote ni safi sana...

Mwanamke ukimtumia kwenye dili lolote liwe haramu au halali linafanikiwa tu...


Cc: mahondaw
 
Season II

Acha kubisa kuhusu mwanamke...

Wagumu waliingiziwa maboya na wanawake... ( wakina Ban)

Naona pia The lost boys (wakina Hans) nao wanataka kuangukia huko huko...



Cc: mahondaw
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (12)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

ILIPOISHIA......

Tuache haya ya kichwani.Nakupeleka kifuani.
Haya yote nakuelezea ili upate picha halisi na kujijibu mwenyewe kwa nini hawa jamaa watatu ambao wasichana kwao ni sumu,wagande na kudata huku kila mmoja akiapa kwa wakati wake kuwa watafanya kila njia ili wampate.

Alikuwa na kifua saa sita.Kama hujui kifua saa sita ni nini.Basi kaa ukijua kuanzia leo kuwa alikuwa anachuchu kiduchu ambazo zinawaacha watu wenye hela zao wakibakiwa na uchu wa kutaka hata kuziona zikiwa wazi.

Zilikuwa hazina kero wala kupigwa jeki kama zile za Nicki Minaj.Hizi hata zisipovishwa sidiria zilionekana wazi zimesimama dede.Lakini alipenda kuzipa sidiria ili asiwaumize maboya boya wa chuo kile.
Nashindwa kumwelezea uzuri wa miguu yake.Ila naweza kusema ni miguu ambayo ilifamfanya aonekane mrefu kiasi na asiyekuwa na tatizo au kusababisha watu wamcheke mtu aliyesimama naye kwa kuonekana mfupi kuliko yeye. Eve alikuwa hana maurefu hayo ya Hashim Thabit wala maurefu ya Twiga.Na zaidi hakuwa mfupi kama kifaru wala ufupi wa kuigizia vichekesho.

SASA ENDELEA......

Mimi namjua Eve,kwani hata akitembea alikuwa si wa kujiaibisha kwa kutembea kama kundi la nyumbu au pundamilia linapita.Alikuwa hana vishindo vya wanyama hao wala kutimua mavumbi hata kama anatembea kwenye vumbi hilo.

Nje ya hayo maumbile yake.Eve alikuwa anaweza kujipanga kimavazi aisee.Hakuwa wa kuvaa makachumbali,yaani hakuwa wakuvaa nguo zenye rangi nyingi.

Si mwajua kachumbali navyokuwa na rangi nyingi? Utakuta kitunguu kina rangi yake,nyanya rangi yake,pilipili rangi yake,karoti kama zipo zitakuwa na rangi zake,pilipili hoho ukiamua kuweka inakuwa na ukijani wa kukolea kuliko pilipili ile ya kuwasha.Wengine wanaweka kageji kwenye kachumbali hiyo ambayo nayo ina-rangi yake.

Sasa kuna watu wanavaa kachumbali bwana.Lakini kwa Eve,ilikuwa tofauti sana.Kama akiamua kuvaa rangi tofauti,basi alizipangilia.Kama nyeusi alijua inaendana na rangi za kung’aa kama njano,pinki na nyeupe ambayo hiyo nyeupe inaendana na rangi yoyote.

Hakuwa mtu wa kuvaa rangi ya kijani kwa nyeusi kama baadhi ya wanawake wengine wa pale chuo.Ukivaa hivyo utakuwa kama jalala,yaani utaonekana mchafu.Rangi zilizofifia zinaenda na rangi za kung’aa bwana.Na ndivyo Eve alivyokuwa akijipanga katika mavazi yake.Acheni wakina Junior wadate aisee.Mtoto alikuwa anaweza haswaa.

Uzuri huo wa Eve ndio ulimfanya hata Ban adate na kuingia mwenyewe laini.Na uzuri huohuo ndio unawaingiza mtegoni wale jamaa walikuwa wanajiita Ant-Girls.Ni hatari na balaa juu yake hasa pale ilipogundulika wale wote walikuwa wanamtaka msichana mmoja,ambaye ndiye waziri mkuu wa chuo kile kwa wakati ule
HUYO NDIYE EVE JOHANESS.
**********
Ilipita wiki tangu wakina Hans wakutane na Eve.Kila mmoja alikuwa anakutana na Eve kwa muda wake na kuna muda walikuwa wanakutana naye kwa pamoja na kuongea naye mambo mbalimbali yanayotokea pale chuoni na duniani.

Eve alitokea kuwaelewa sana wale jamaa kutokana na ucheshi na mambo yao.Kila mmoja alikuwa akitumia kipaji chake kufikisha hisia zake kwa mwanadada yule mlimbwende.
Aliyejua kutunga tenzi,alifanya hivyo na aliyejua kuitumia biblia kwa kugeuza mistari ya kitabu kile na kuwa mistari ya kufikisha hisia zake,naye alifanya hivyo.

Huku mwanasayansi naye akichanganya maneno na falsafa za wanasayansi na kuwa mistari ya mapenzi inayovuta hisia za kila mwanamke atakayesikia yale maneno.
Hiyo ndiyo sababu kubwa ya Eve kupenda kukaa na wale jamaa kwani kila muda alikuwa anapata maneno matamu kupitiliza.

Licha ya hayo yote kutokea,hakuna aliyewahi kumtamkia moja kwa moja kuwa wanampenda mwanamke yule.Wote walikuwa wazee wa mistari tu!.Lakini hakuna aliyewahi sema au kumwambia Eve kuwa anahitaji kuwa mpenzi wake.

Hilo ndilo lilikuwa tatizo la hawa jamaa japo wenyewe wakikutana peke yao,wanaambizana kuwa wameshampiga saundi mtoto yule na wanasubiri majibu tu!.

Mambo yalizidi kunoga pale wale wagumu waliporudi chuoni.Walikuwa wamebadilika sana kitabia,na kila mtu aliwapenda kwa nidhamu waliyoionesha baada ya kurudi.Sasa wakawa mstari wa mbele kushirikiana na wenzao huku rafiki zao wakubwa wakiwa ni walewale wakina Hans.

Hali ile ya wakina Junior kutambiana kila wanapokutana,ikazua kiriba cha roho.Kwa nini huyu hivi na mimi hivi?.

Kiriba hicho cha roho kikaanza kutengeneza wivu taratibu na matokeo ya wivu huwa ni chuki baina ya watu.Na ndicho kilichofuata baada ya wivu ule.

Kila mmoja akatafuta njia maalumu ya kumpindua mwenzake.Huyo Mtakatifu Fred naye aliamua kwenda na wale wahuni nyama kwa nyama.Kama wao waliamua kumfanyia uhuni,basi na yeye aliamua kuwa kama wao.Si mwajua kuwa ukitaka kumuua Shetani ni lazima na wewe ujivike ushetani.Basi ndivyo ilivyotokea kwa Fred.

Msaada mkubwa walioona utawasaidia ulikuwa ni kwenda kwa wagumu na kusema matatizo yao huku wakitoa kiasi cha fedha kwa ajili ya kazi hiyo kufanyika.

Hakuna aliyejua kuwa mwenzake anawatumia wagumu kumwaribia na nafasi kama hiyo ndiyo wagumu waliona kama nafasi ya kulipa kisasi chao japo kisasi hicho walikuwa hawataki kilete majanga kama kile cha mara ya kwanza.Hichi kilikuwa kisasi cha akili ambacho kilikuwa kina lengo la kuwakusanyia hela zao tu.

Naam,wagumu walipewa shavu la kufa mtu kwa ajili ya kuharibu mikakati ya mmoja wa kundi la akina Hans. Ban na wenzake walikuwa ni watu wa kuagiza tu! Tuletee ichi ili kazi ikamilike haraka,au fanya hivi na toa ichi halafu usubiri matokeo.Hiyo ndiyo ikawa kazi ya wagumu.

Kwa upande wa Suarez yeye aliamua kukaa pembeni na kuwashangaa jamaa zake kwa nini wamechanganyikiwa kiasi kile kwa muda mfupi tu!.Alikaa pembeni kwani hata alipowashauri walikuwa wagumu kuelewa na wagumu kufikiri kwa mtendo yao
Wote kwa muda tofauti ,walimpa Suarez mikakati yao. Pale alipojaribu kuwarekebisha,walimwijia juu na kumuona kama anawazingua tu!Hivyo wakaacha kabisa kumpa taarifa jamaa huyu na taarifa zikawa zinapelekwa kwa wagumu.

Suarez akawa mtu wa kutabasamu na kuwaona hawa jamaa kama marimbukeni tu!.Ipo siku watadamka na watajijua kuwa walikuwa wanabugi sana.Hivyo aliwaacha na kubaki muangalia filamu ile ya bure kabisa,yenye wingi wa vituko na vichekesho visivyokwama.

Eve yeye alikuwa hana taarifa zozote kutokana na ule mkanganyiko baina ya wale rafiki zake wapya.Yeye alichojua ni kwamba ana marafiki wenye maneno matamu yanayoweza kusababisha chakula kikajila.Hakujua kama wenzake tayari wanacheza ligi kuu na kombe likiwa ni yeye.

Na kizuri zaidi kundi lile lilikuwa pamoja kama zamani.Yaani ni kama walikuwa hawajawekeana bifu,wote walionekana wana furaha sana pale wanapokutana. Hakuna aliyejua roho ya mwenzake zaidi roho yake na MUNGU pekee.

Hawa watu watatu,namaanisha Hans,Junior na Fred.Walijipanga sana kimaneno kwa ajili ya Eve.Na mengi waliyaongea yalikuwa ni maneno matamu ambayo kiukweli hata wasichana wengine wangeyasikia au wao ndio wangekuwa wanaambiwa,sidhani kama wangekataa kuwa japo na mmoja wa wavulana hao watatu.
Ngoja nikupe maongezi ya kila mmoja wao akikutana na Eve.

JUNIOR NA EVE.

Mara nyingi Junii au alipenda sana kumpeleka Eve chuo cha kule mlimani.Na walipenda sana kukalia mawe yale ya mlimani.
Huku wakipata upepo na vinywaji mbalimbali walivyotoa supa-maketi ya Mlimani City.Junior alikuwa anam-mbeleza kwa gitaa Eve huku akitoa maneno yake ya kisanii kumwelekea mrembo yule ambaye siku zote alimuona Junii kama mtu mchangamfu na mwenye wingi wa maneno.

“Wajua nini My Beautiful”.Junior alianza kumuongelesha Eve baada kumpigia gitaa kwa muda.

“Nambie tu My Junior”.Eve naye alimwambia huku akisogea karibu kabisa kwa Junior kwani tayari alishajua maneno matamu yanaanza kumwagika kutoka kinywani kwa kachaa yule mjanja mjanja lakini bonge la boya kwa kimwana Eve.

“Nataka ufahamu kuwa fahari ya moyo wa binadamu ni kuona furaha kwa mwenzake ikikamilika bila bugudha.Kama mimi hapa sasa hivi,najisikia sana fahari kuwa na wewe na ninadhani nawe wajisikia the same way”.Junior alimuanza taratibu Eve kama hataki vile.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (13)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

ILIPOISHIA......

JUNIOR NA EVE.

Mara nyingi Junii au alipenda sana kumpeleka Eve chuo cha kule mlimani.Na walipenda sana kukalia mawe yale ya mlimani.
Huku wakipata upepo na vinywaji mbalimbali walivyotoa supa-maketi ya Mlimani City.Junior alikuwa anam-mbeleza kwa gitaa Eve huku akitoa maneno yake ya kisanii kumwelekea mrembo yule ambaye siku zote alimuona Junii kama mtu mchangamfu na mwenye wingi wa maneno.

“Wajua nini My Beautiful”.Junior alianza kumuongelesha Eve baada kumpigia gitaa kwa muda.

“Nambie tu My Junior”.Eve naye alimwambia huku akisogea karibu kabisa kwa Junior kwani tayari alishajua maneno matamu yanaanza kumwagika kutoka kinywani kwa kachaa yule mjanja mjanja lakini bonge la boya kwa kimwana Eve.

“Nataka ufahamu kuwa fahari ya moyo wa binadamu ni kuona furaha kwa mwenzake ikikamilika bila bugudha.Kama mimi hapa sasa hivi,najisikia sana fahari kuwa na wewe na ninadhani nawe wajisikia the same way”.Junior alimuanza taratibu Eve kama hataki vile.

SASA ENDELEA....

Eve aliyekuwa kapambwa na tabasamu huku asielewe siku ile ni nini Junii ataongea,alizidi kujipenyeza kwa Junii na kumgusa kwa makusudi na kifua chake kwenye eneo la ubavu wa kijana yule msanii.

“Endelea sasa msanii wangu.Mi najisikia fahari sana niwapo na wewe Junii.Unanifanya nisahau mengi.Embu endelea kunipa fahari hiyo My Junior”.Junior kusikia hivyo na kile kifua kilivyokuwa karibu yake,wacha kabisa.Jamaa likawa bwege kama si fala kabisa.

“Daah!Beautiful unanifanya nione dunia kama imeegemea upande wangu na vitu vyote vizuri katika maisha haya vimeterezea upande huohuo ambao mimi nipo mimi.Muda wote wanifanya nijisikie raha na amani niwapo na wewe.

Sauti yako nyembamba kama nota namba moja katika gitaa,ndiyo hasa inayonifanya nijisikie nipo hewani pale napoisikia sauti yako mwanana ya kumtoa samaki magamba bila kisu.

Nashindwa kukwambia huu kiasi gani mwenye mvuto.Ila kama MUNGU akiniuliza huu mzuri kiasi gani,naweza nikamjibu kwa kumwambia kuwa kakuumba kwa udongo wa kipekee ambao hakuna binadamu mwingine aliyewahi kuumbiwa udongo huo”.Junior alikuwa anafunguka maneno ambayo hadi leo hatujui aliyatoa wapi.

“Mmmh!My Junior,ya kweli hayo jamani?”.Eve ilibidi aulize.Lakini uliza yake ilikuwa ina jambo ndani yake.Kauliza ili Junii aendelee au kauliza ili kujua kama maneno ya Junii ni ya kweli,au kauliza ili aonekane kama kachangia kitu.Mimi na wewe hatujui,ila moja ni jibu lake.

“Sasa nikudanganye nini My Beautiful One.Embu angalia machoni pangu”.Junior alimuomba Eve atazame macho yake.Na Eve naye akatazama huku katoa lile tabasamu lake la kumtoa samaki magamba.

“Najua bado hujajua ni kwa nini umeangalia macho haya.Ila naomba kukuuliza.

Ndani ya macho haya umeona nini?”.Junii alimuuliza Eve swali ambalo laweza kukufanya ujue kama mwanamke huyo anaelewa maana ya mapenzi uliyonayo kwake au haelewi.
Inawezekana Eve alijua ni nini ajibu,lakini kwa kuwa alikuwa hataki kuonekana kama anaelewa,akajibu kinyume na mimi nayeandika nilivyodhani.

“Naona mboni My Junior”.Eve alimjibu huku bado tabasamu likitamba kwa mbwembwe usoni pake.

“My Beautiful One.Sidhani kama ndani ya macho yangu waweza kuona kitu kama hicho.Sawa kuna mboni,ila pia ukiangalia vizuri utajiona na wewe.

Nataka uelewe kuwa macho ni zaidi ya kioo.Macho ni zaidi ya kujieleza uonacho.Macho yangu ukiyaangalia,nadhani wajua wazi kuwa yanaeleza ni kiasi gani Junior mimi nashindwa kufumba macho pale napoona sura yako au napoikumbuka.Niamini My Beauty,wewe ni zaidi ya mboni uionayo wakati unaangalia macho yangu.
Siwezi kusema ya moyoni yaliyojificha lakini kama unataka kujua ya moyoni,ni lazima ujue haya ya machoni uyaonayo.

Moyo ni zaidi ya jinsi uujuavyo katika sanaa hii ya Maulana”.Hapo Junior aliposema sanaa ya Maulana,alionesha tendo kwa mikono yake kwa kutengeneza duara angani.Akimaanisha sanaa ya Maulana ni Dunia.Akaendelea.

“Moyo waweza kubeba kila kitu ambacho binadamu hawezi kukibeba kwa mikono yake.Na hata mikono hiyo ikibeba,itaambulia kudondosha au kukipoteza.Lakini moyo ukiamua kubeba,umebeba tu! Ni wewe mwenyewe kuamua kupoteza au kukitupa kitu ulichokibeba.

Kwa mfano siri za watu.Ni moyo pekee waweza kubeba hiyo kitu.Hakuna awezaye kuifanya siri hiyo ipate kopi yake kana kwamba umeihifadhi labda kwenye karatasi au CD.

Ndivyo ilivyo katika mapenzi.Kwanza ni moyo ndo una-disaidi kuwa huyu ndiye na huyu siye.Huyu aingie na huyu aisiingie.

Baada ya hapo ndio unapeleka kwenye ubongo na kumwambia ubongo aweke kumbukumbu juu ya moyo ulichoamua.Vinginevyo bila moyo kungekuwa hakuna mapenzi au upendo wowote kwa mwanadamu”.Junior alikuwa anabwabwaja maneno ambayo kiasi fulani yalikuwa kama yanamfungua Eve.Na kwa mwonekano yalikuwa yanamuingia vilivyo Eve.

“Mmmh!My Junior.Lakini upendo si wajengwa kwa hisia kwanza ndio unapelekwa moyoni?”.Eve ilibidi afanye kama swali lakini kiukweli alikuwa anataka kujua zaidi kupitia kwa Junior.

“Hapana My Beautiful. Hisia ni hali ya nje tu! Lakini moyo ndio kila kitu katika kuthibitisha upendo au mapenzi.

Hisia zaweza kuwa ndio au siyo.Yaani,waweza sema kuwa nampenda pale ulipomwona tu! Hizo ni hisia ndizo zimekutuma useme hivyo.Lakini siku zote moyo ndio unasema kweli kuwa umempenda.

Umewahi kusikia kuwa watu wameachana kwa sababu hawaendani au mke anakuwa nakiburi kwa mme wake na yupo tayari hata kupewa taraka ili aondoke.Umewahi sikia hiyo kitu?”.Junior alimuuliza Eve.

“Hiyo nimesikia sana.Na hata rafiki zangu wamewahi kunihadithia mambo kama hayo kuwatokea”.Eve alijibu huku bado yupo karibu kabisa na Junii ambaye alikuwa anamsikiliza huku anashusha juisi ya embe kwenye koo lake.

“Sasa hao walifuata hisia.Hao hisia ziliwatuma kuwa tunapendana ,na hisia hizo hizo ndizo ziliwaambia kuwa tufunge ndoa.Lakini walipotulia,waligundua kuwa mioyoni mwao hakukuwa na kitu kinachoitwa upendo bali ni hisia ndizo ziliwafanya wadhani wanapendana.

Huwa siamini kuhusu hisia hata mara moja.Hisia zaweza kusema kimbia na moyo waweza kukukataza usikimbie hasa katika hatari.Mara nyingi hisia hana ujasiri,ila moyo bwana,naupa hongera mno.Unaweza kuvumilia.”.Junii alizidi kutema madini na kumwacha Eve hana neno bali tabasamu lisiloisha hamu.

Licha ya tabasamu hilo,Eve hakuthubutu kumuuliza Junii maneno yake yana maana gani.Na si Junii pekee ni hadi Hans na Fred,wote walikuwa wana maneno kama yanaendana,lakini Eve hakuweza kuuliza nia na madhumuni ya maneno hayo.

Alifanya hivyo akijua kwamba wale wavulana wamempenda na wanamuhitaji,lakini walishindwa kumwambia moja kwa moja bali kubaki wakiongea mafumbo kama wamemeza kamusi ya Wahenga.
Pia Eve alishindwa kuuliza kwa sababu alifahamu endapo atauliza tu!.Basi maneno yale yatageuka na kuwa sumu ya kumtongoza,yaani endapo atauliza basi atakuwa kawapa upenyo watu wale wanene wanachoki-feel mioyoni mwao.

Udhaifu wa kutongoza kwa vijana wale watanashati,ukawaponza na kubaki wakiumia na maumivu yao huku kila siku wakibuni misemo mipya ya kuongea.

“My Beautiful.Angalia jua”.Junior aliongea baada ya kumwacha Eve kwa muda akitafakari maneno aliyoyatoa.

“Yaah,My Junior.I see and I think it is gone”.Eve alimjibu Kiingereza Junii.Wakati huo jua ndilo lilikuwa likiwahi machweo yake,yaani ilikuwa ni muda wa saa kumi na mbili na nusu au na dakika zaidi ya thelathini.

“Noo.My Beautiful.Sijamaanisha uangalie ili unipe jibu ya kuwa linaenda kuzama.Nataka nikwambie siri moja ya jua hili ulionalo sasa hivi”.Junii alimrekebisha mawazo Eve.

“Tell me My Junior”.Eve kwa wahka naye akaitika.
“Jua ni kitu cha ajabu sana katika maisha yetu. Kwanza si choyo na halina ubinafsi kwa vitu vinavyofanana nae.Hapa na maana mwezi na nyota.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (14)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

ILIPOISHIA......

“Noo.My Beautiful.Sijamaanisha uangalie ili unipe jibu ya kuwa linaenda kuzama.Nataka nikwambie siri moja ya jua hili ulionalo sasa hivi”.Junii alimrekebisha mawazo Eve.
“Tell me My Junior”.Eve kwa wahka naye akaitika.
“Jua ni kitu cha ajabu sana katika maisha yetu. Kwanza si choyo halina ubinafsi kwa vitu vinavyofanana nae.Hapa na maana mwezi na nyota.

****ENDELEA****

Jua katika muda wake wa kuwaka,unaweza kuuona mwezi na hata nyota.Lakini mwezi na nyota,zina ubinafsi sana.
Vitu hivi katika kuwaka kwake,huwezi kuliona jua hata kidogo.Namaanisha,jua linapozama linaachia kazi ya kuleta nuru mwezi na nyota.Na saa nyingine kukiwa kuna dalili ya mvua hasa mida ya usiku,mwezi na nyota,hujificha ndani ya mawingu na kutuacha sisi binadamu gizani.
Lakini jua,kamwe halifanyi hivyo.Litapambana na dalili ile ya mvua na saa nyingine linajificha ndani ya mawingu lakini baada ya kutufikiria sisi kuwa tupo gizani,hujitokeza na kuendelea kupambana ili tupate mwanga wake.Hiyo ni siri ya jua ambayo mimi nimeigundua”.Junii alimaliza na kumwacha Eve makusudi ili amuulize.
Kama alivyotegemea Eve akaingia line na kuuliza maana ya maneno yale.
“Haha ha haaa.My Beautiful.Kwanza tuanze kushuka huku ili turudi kwetu”.Junii alimwambia Eve,naye Eve hakuwa na kipingamizi zaidi ya kushuka katika mlima ule waliokaa karibu saa moja na nusu wakiongea na kunywa.
Huku wanatembea kurudi mjengoni wanapoishi,Junior aliendelea kutema madini yake.

“Napenda sana binadamu mwenye tabia ya jua kuliko hivi vitu vingine kama mwezi au nyota.Natamani kukwambia kuwa wewe ni kama jua kwa watu”.Eve aliposikia hivyo,alitabasamu na kumsogelea Junii tena na kupitisha mkono wake kwenye mkono wa Junii kisha akamlalia Junii kidogo kwenye bega.

“Kwa nini unasema hivyo my Junior”.Eve alimuuliza Junior huku akijiweka sawa kuzipokea sifa kedekede kutoka kwa msanii yule.
“Popote waliporafiki zako na wewe upo. Kamwe huwaachi wakiwa peke yao. Umekuwa ukiwahakisi mwanga wako kama jua lifanyavyo kwa nyota. Hutaki wakae gizani kama kuna hali hiyo. Nathibitisha haya baada ya kukuona mara nyingi sana upo karibu yetu. Hata iwe saa ngapi,tukikuita waja. Hakuna mwanadamu kama wewe,naweza kusema hivyo.
Umebarikiwa moyo wa jua,moyo ambao hutaki kumwona mwenzako akipata shida wala kuteketea. Kama nikisema wewe ni zaidi yao,sidhani kama nitakuwa nakosea. Hu mzuri kuanzia nje mpaka ndani. Hu mwema kiakili hata matendo. Upo tayari kutoa faraja kwenye mwenye simanzi na upo tayari kufariji kwa kila neno zuri kwa mwenye kuhitaji maneno ya faraja”.Junior alikuwa akibwabwaja maneno mazuri na masafi kwenda kwa kimwana yule,lakini kila alipotaka kutamka hisia zake kutoka moyoni kuwa anampenda Eve,alishindwa na kubaki akiangalia mbele.
Udhaifu huo Eve aliujua hivyo ilikuwa ahueni kwake kwani kama Junior angetamka kuwa anahiotaji kuanzisha mahusiano ya kimapenzi naye,basi mambo aliyoyapaga yasingetimia.
“Mmmh!My Juu,ya kweli hayo”.Eve aliuliza huku bado katoa tabasamu lake mwanana lililopamba hata njia wanayoikanyaga.
“Kwa nini nikudanganye My Beautiful. Umeumbwa kwa ajili ya watu kama sisi wenye kuhitaji faraja. Wewe ungekuwa kiungo katika mwili wa mnyama basi ungekuwa moyo au kichwa. Na kama nikiulizwa una umuhimu gani katika maisha yangu,ningesema wewe ni damu mwilini mwangu. Ukiondoka nakuwa sina uhai,ukisimama nakuwa katika koma na ukimwagika,unaniachia maumivu”.Maneno yalizidi kukandamizwa na Junior.
“Mmmh!Haya bwana.Naona karibu tunafika madarasani. Natamani niendelee kukusikiliza,lakini daah!Yanibidi niende My Junii. Nitakuja kukuona tena kesho,palepale mnapopataga chakula nawenzako”.Eve alikuwa anamwambia Junior baada ya kufika maeneo yalipo madarasa yao.
“Okey, My Beautiful. Uende salama na ukawaangazie wote wenye giza huko uendapo. Wewe ni jua kama nilivyokwambia,usiubane mwanga wako kwa wanaouhitaji”.Junior alimwambia Eve naye Eve kuonesha kama shukrani au ili asimuumize Junior atakapoondoka,au labda kumpa moyo ili Junior ajione mwenye bahati,akambusu shavuni Junior halafu kwa sauti nyembamba na ya kubembeleza,akamnong’eneza sikioni kwa kumwambia kwa heri my Junii.
Safari yao ikaishia hapo huku Junior akibaki kaduwaa asiamini kama ni yeye aliyepewa busu zuri kama lile na mtoto mzuri kama yule.
Alimwangalia Eve jinsi anavyoenda anapoenda naye Eve kama alijua anaangaliwa na Junior,aligeuka na kisha akabusu mkono wake wa kulia na kumfanyia ishara ya kulipuliza busu lile kwenda kwa Junior.
**********
Junior alifika kwa wakina Fred na aliwakuta wote watatu wapo. Wote hawa walikuwa hawana siri juu ya mambo yanayotokea wakikutana na Eve. Japo walikuwa hawafichani,lakini walikuwa wanadanganyana sana. Na ndicho kilitochotokea kwa Junior baada ya kufika mle ndani.
“Tehe! Tehe! Teheeeee. Mtabakia kushika mapembe tu!Maziwa anakamua mtu mwinginee.Tehe! Tehe! Teheee”.Junior alianza mbwembwe zake kwa kucheka kama katuni.
“Naona umeshaanza kujungua mwenyewe. Haya bwana,ila hayo maneno tu! Hata vyombo vya habari siku hizi vinatemeana”.Hans aliongea baada ya Junior kusema maneno yake.
“Sasa kama nyie ni washika mapembe,nisiseme?. Mnakukuruka kushikilia mapembe ng’ombe,na ling’ombe linawarusha-rusha na kuwadoboa tumboni na mapembe yake lakini hata hamkomi. Jingine limeshikilia miguu yake huku chini,linapigwa na kwato za kidevu lakini bado bishi. Utakufa Baba Paroko,hii ligi ya watu wazima.
Wewe Hans kamata mapembe na saidiwa na huyu Suarez.Wewe Baba Paroko,kamata kwato mzee. Mimi nakamua taratibuuu,kama nanawa vile. Najinywea vyangu. Nyie endeleeni kudobolewa na mapembe”.Junior alikuwa anaongea hayo huku anavua viatu vyake na kwenda anapolala.
“Dah!Kwa hiyo na mimi nipo Junior”.Aliuliza Suarez baada ya maneno ya Junior.
“Sasa utakosa wewe. We upo kila usehemu. Ukichoka kupigwa pembe,njoo kwa Baba Paroko umsaidie kupigwa kwato za chembe.Ha ha haaaa”.Junior aliongea kwasharau na kupandisha miguu yake kitandani,kisha akalala kifudifudi.
“Daah! Haya bwana. Ila kama kweli sisi washika mapembe na kwato,sidhani kama kesho kutwa nitaenda kushindwa kukamua maziwa”.Aliongea Hans na kuficha uso wake kwa kitabu.
Maneno hayo yalimshtua Junior na kumfanya akae na kumuuliza Hans.
“Unaenda kukutana naye?”.Junior aliuliza.
“Unauliza jibu tena”.Hans akajibu kwa kifupi wakati huo Fred yeye alikuwa kimya akiwatazama wale jamaa wanachoongea. Siku zote Fred alikuwa mtulivu sana,hakuwa na papala kaika maongezi yake,ila akiongea huwa yanawachoma sana na ndio maana hata Junior aliwachoma kwa maneno yake kwani ndio tabia zao.
“Ha ha haaa,linaenda kula makombo yangu”.Junior alimwambia Hans.
“Yawezekana leo ndo mara yako ya kwanza kukutana Eve wewe. Mwenzako kesho mara ya ………. Eti mara ya ngapi Jogoo wa Jiji”.Hans alijidai kasahau idadi alizokutana nazo na Eve,hivyo akamuuliza Suarez ambaye alikuwa shabiki wa timu ya Liverpool ambao wanajiita majogoo wa jiji.
“Sijui mara ya arobaini hiyo. Daah!Ujue sina uhakika kwa sababu siku nyingine huniambiagi.Ila nahisi itakuwa mara ya arobaini au arobaini na tano hivi”.Alijibu Suarez ili kumuumiza Junior.
“Yaah! Wewe sikukwambiaga mara kumi tu! Kwani sikutaka ujue nimempeleka gesti gani. Kwa hiyo nimekutana na Eve kitu kama mara hamsini hivi mdogo wangu. Unavyosema naenda kula makombo yako,nakushangaa sana. Mi najua hata mate hujawahi kuambulia zaidi ya kuumiza miodole yako kwa kupiga gitaa.
Mgitaa wenyewe unalia kama mgobole wa kuulia tembo au ukipiga sauti nyembamba linalia kama unanoa kisu,hadi unamuumiza meno mtoto mzuri kama yule”.Hans alikuwa anamiga madongo Junior hadi chumba kizima kikawa kimetawala vicheko.
“Eti sijala mate, Thubutuu,wewe unacheza na mimi nini?Leo mtoto nimempa maneno matamu hadi kalegea na kunipa ulimi wake mwenyewe. Mi napiga saundi hata mti wa mbuyu ukizisikia uweza kukatika au kulala hapo hapo. Napiga saundi hadi simba dume linabadilika sauti na kuwa kama ya mtoto wake”.Junior alizidi kujiifia kwa uongo na kuwaacha watu wakitafakari maneno yake kwa kuwa walikuwa hawana uhakika kama ni uongo au kweli.
Uzuri wao walikuwa hawajali kuchangiwa kwa maneno. Leo unaweza kukuta Hans anasemwa na chumba kizima,halafu kesho Junior na siku nyingine ni Fred. Sasa siku ile ilikuwa ni zamu ya Junior na aliyataka mwenyewe
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (15)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

ILIPOISHIA......

“Eti sijala mate, Thubutuu,wewe unacheza na mimi nini?Leo mtoto nimempa maneno matamu hadi kalegea na kunipa ulimi wake mwenyewe. Mi napiga saundi hata mti wa mbuyu ukizisikia uweza kukatika au kulala hapo hapo. Napiga saundi hadi simba dume linabadilika sauti na kuwa kama ya mtoto wake”.Junior alizidi kujiifia kwa uongo na kuwaacha watu wakitafakari maneno yake kwa kuwa walikuwa hawana uhakika kama ni uongo au kweli.
Uzuri wao walikuwa hawajali kuchangiwa kwa maneno. Leo unaweza kukuta Hans anasemwa na chumba kizima,halafu kesho Junior na siku nyingine ni Fred. Sasa siku ile ilikuwa ni zamu ya Junior na aliyataka mwenyewe.

****SASA ENDELEA*****

“Kwenda zako huko.Nilikuwa nakusikiliza kitambo.Tangu umeingia hapa”.Alikuja Fred na kumrukia kwa maneno Junior.
“Tena wewe Baba Paroko kula ngumu,kwa sababu huna sumu.Siku ile kum-kiss manzi ukajiona ndo kidumee. Mwenzako leo nimepewa lile orijino kabisa”.Junior naye akajibu mapigo kwa Fred.
“Acha kutudanganya. Domo lenyewe linanuka hadi huku halafu unasema umekula mate mtoto yule. Sijui umekunywa manini. Usituzuge hapa,huwezi kula mate na maarufu yako ya karanga mdomoni. Eti nilionea maneno matamu,unamaneno gani matamu wewe kama si kulia lia tu!. We si bongo fleva,kazi yako kulia tu!.Nenda huko kaimbe kulia lia magerezani kama ule wimbo wa Tunda. Lakini huna maneno matamu zaidi ya kujisumbua”.Aliongea Fred maneno kumwendea Junior.
“Ha ha haaa.Mzee wa Upako mpe huyo. Kazi kulia kama PNC,wagumu kama Chid Benz tunazidi kunguruma kwa mtoto hadi anasalula viwalo vyake mwenyewe”.Aliongeza Hans lakini Fred naye alimkata.
“Na wewe sepa zako hapa.Huna lolote,yule demu hujala wala nini. Kama umekula niambie umekula lini ili nikuulize swali”.Fred alimwambia Hans.
“Yule wiki iliyopita nilikuwa naye kwenye lodge moja kule Sinza. Hadi nikaoga naye”.Hans alijibu kwa kujiamini wakati huo Junior alishapewa vyake na kutulia,na Suarez yeye alikuwa mtu wa kusikiliza na kucheka kutokana na yale maongezi.
“Eheee,hapo hapo. Sasa mimi nilipiga pale wiki mbili zilizopita na kuna alama nilimwachia kiunoni.Niliandika kwa wino ambao hata ukae mwezi haufutiki. Na nilimwandika wakati kalala,hivyo hajui kama kaandikwa. Niambie,umeona alama hiyo wakati unaoga naye?Na kama umeiona,imeandikwaje. Sema ukweli usidanganye”.Fred alimuuliza Hans ambaye kidogo aligwaya baada ya maneno yale.
Hamna hata mmoja aliyekuwa anamwambia mwenzake ukweli,ilikuwa basi tu! Kutambishiana.
“Jibu.Lione kwanza kichwa lake kama kibuyu cha kuchotea maji kijijini”.Junior alimpa kavu la uso Hans baada ya kumwona kagwaya kujibu.
“Mzee waUpako umetisha. Jamaa kanywea kama mchicha japo mara ya kwanza alikuwa kajaa sufuria”.Suarez alimpa sifa Fred.
“Msijifanye mnajua hapa,kumbe tunaojua tumetulia tuli. Keshokutwa ukienda kukutana naye,mwangalie kiunoni,utakuta nimeandika kwa herufi kubwa jina langu. Hapo ndo utajua kuwa washika mapembe na kwato ni nyie,sisi wazee wa nyonyo tunakamua taratibu maziwa yetu. Mtaniambia nini nyie,mimi fundi. Udambwidambwi mwingi kama Mbwiga Wa Mbwiguke,si fundii.
Mafundi hatuchafuki,sisi wazee wa biliji tu! Sasa wewe kibarua endelea kupigwa kwato na domo lako linalonuka kama kwapa la mwehu”.Akamaliza Fred na hapo kimya kikafuata huku kila mmoja akiwa haamini alichoongea Fred.
Wote walijua ni kweli Fred anaweza kuwa ametembea na Eve hasa kwa sababu alikuwa anajiamini sana katika matendo yake. Lakini haikuwa hivyo,Fred alikuwa ni mtu wa maneno tu kama wao.
“Daah! Mzee wa Upako au Mzee wa Biliji,naona umewanyamazisha wananchi wote. Sasa nadhani watasoma,maana tambo zilikuwa nyingi sana hapa”.Suarez aliongea huku akitabasam baada ya kimya kidogo kupita.
“Hawa wote ni makuku tu! Mchana majanja,usiku yapo hoi kwa kuchoka kwa sababu ya mchana kuchakua chakua majalalani. Kila mbuzi ale kutokana na urefu wa kamba yake.
Kama leo wewe Junior uemtoka naye,hatujakufatilia. Keshokutwa Hans,hamna kumfatilia. Mimi kaniambia Jumapili. Natoka naye usiku kwenda kupata naye msosi hotelini,sitaki usumbufu. Mimi zangu hotelini,wewe Jun wajua wapi unapokutana naye na wewe Hans wajua yako. Hamna kuharibiana,sawa?”. Wote wakajibu sawa na mjadala ukafungwa hapo.
***********

HANS NA EVE.

Kama walivyoahidiana siku tatu zilizopita,ndivyo ilivyokuwa mida fulani ya mchana katika siku ile ya Ijumaa.Eve akiwa na Hans katika fukwe za Coco,walikuwa wametulia kwenye kivuli kimoja cha mwamvuli wa ufukweni na kila mmoja alikuwa katikamavazi ya ufukweni.
Hans akiwa kavaa kaptula moja nyepesi ambayo ilikuwa maalumu kwa maeneo yale,alionekana mwenye tabasamu pana mbele ya mrembo Eve ambaye naye alikuwa kavaa kiblazia kidogo kilichoficha kifua chake lakini kikiacha kitovu nje,na kwa huku chini kajifunga kama mtandio wa ulioanzia maeneo ya tumboni hadi miguuni.
Muda wote Hans alikuwa anatamani ule mtandio wa Eve japo udondoke ili aone kama kweli kuna mwandiko wa Fred kwenye kiuno cha Eve.

Hans akiwa amelala pale kwenye kivuli,alimuona Eve anakuja na vikombe vya plastiki viwili ambavyo ndani yake kulikuwa na koni aina ya Vanilla. Ule mtandio aliokuwa ameuvaa ulikuwa unaangaza na kuonesha nguo yake aliyovaa ndani ambayo ilikuwa ni ya ufukweni zaidi.
Mwangaza ule wa mtandio ambao ulichagizwa zaidi na jua kali ambalo lilikuwa linawaka muda ule,ulimfanya Hans amkodelee Eve macho tangu alipokuwa anatoka kule aliponunulia koni hadi pale alipokuwa Hans.
Eve aliyaona macho yale ya Hans na alijua kachizika kwa yale mapigo.Japo aliona aibu kiasi fulani lakini ilibidi avumilie ili apate anachokitaka kwa Hans,ambacho ni maneno matamu.
Alipofika pale mbele ya Hans,alitabasamu na kumuuliza mbona anamwangalia vile.
“Bado najiuliza MUNGU alichanganya kemikali gani hadi akakutoa kiumbe kama wewe. Sidhani kama MUNGU kakuumba kwa udongo bali kemikali maalumu ambazo ukizichanganya huwezi kupata madhara bali faida ya zao kama wewe,zao lililonifanya nikuite sweet. We ni mtamu Eve”.Hans aliongea huku bado Eve akiwa amesimama mbele yake kwa tabasamu la haja toka usoni pake.
“Mmh! Hans,yanaukweli hayo usemayo?Mbona mi wa kawaida tu! Embu niangalie”.Eve aliongea hayo kama kutaka uhakika kwa Hans na hapo akageuka na kumpa mgongo kidogo Hans na kisha akamgeukia tena.
“Daah! Unajua Eve unaweza kuitoa dunia kwenye mhimili wake na kuifanya ijizungushe kwenye mhimili wako?”.Hans alifanya kama kumtupia swali Eve na kumfanya Eve atabasamu zaidi ya pale na kisha akaenda hadi pale karibu na Hans ambapo palikuwa na kiti kingine cha kulala maalumu kwa ajili ya ufukweni.
“Bwana mimi sielewi hayo Hans,hayo mambo ya dunia kujizungusha si mambo ya Jegrafia?Mimi nilisoma HKL bwana,hata sijui”.Eve aliongea kwa kudeka baada ya kukaa kwenye kile kiti mlalo cha ufukweni.
Hans kusikia hivyo ndio akajiona kama mtu mwenye bahati kuliko hata bahati yenyewe. Akainuka pale alipokuwa kalala na kisha akakaa kumwelekea Eve ambaye naye alikuwa amekaa na vikombe vyake akiwa kavishikilia.
“Leta kwanza nikusaidie hivyo vitu maana naona kama mkono yako itachoka”.Alichukua zile koni na kuziweka pembeni kisha akarudi usoni kwa Eve.
“Sweet Eve,si wajua kuwa dunia inajizunguka kwenye mhimili wake,huku inafuata njia zinazoitwa Obiti na wakati huo huo inakuwa inazunguka jua?Kwani hata hilo la form two hukijui?”.Hans alimuuliza Eve.
“Aaah!Zamani sana hiyo Hans.Ila nakumbuka kidogo”.Alimjibu Eve.
“Basi nisikutese Sweet wangu. Naposema dunia itaacha kujizungusha kwenye muhimili wake na kukuzunguka wewe,namaanisha hata dunia itakufuata wewe unachotaka. Hata ukiiambia zunguka kutoka kati kwenda kulia,itatii au ukiiambia izunguke pembeni kwenda kati napo itatii,hii ni kwa jinsi ulivyokuwa mzuri.
Kama tupo vitani,sina haja ya kubeba mabomu kama Rambo au Shoziniga,wewe ni silaha tosha ya kuwaua maadui. Una madhara matamu na si machungu kama bomu la nyukilia. Naapa mbele ya MUNGU,wewe hujaumbwa na udongo bali kemikali zenye harufu nzuri na utamu uliopitiliza. Hujawekewa asidi kwenye kemikali hizo ulizoumbiwa bali umewekewa asali ambayo siku zote nahisi MUNGU alikuwa ameihifadhi ili aje akuumbie wewe”.Hans akazidi kutema maneno matamu mbele ya mtoto mzuri Eve.
“Wewe HANS wewe. Hivi hujui MUNGU anakuona na kukusikia maneno yote unayoongea?”.Eve alimuuliza Hans huku akimwangalia kwa macho ya yaliyojaa furaha.
“Sidhani kama MUNGU anakataza mimi kukusifa wewe kwa jinsi navyokuhisi moyoni mwangu. MUNGU hakatai hilo,ila cha msingi nisivuke mipaka na kumkufuru”.Hans alimjibu Eve na kumwacha mtoto yule mwenye uzuri wa kuita bila swali.
“Mh!Haya bwana.Basi naomba koni,isije ikayayuka bure maana ikiyayuka inakuwa mbaya”.Eve alikata shauri na Hans akampatia koni na kisha wakaanza kuburudika kwa kiburudisho kile.

Wakati wanaendelea kuburudika,mara kwa mbali ikasikika sauti ya meli ikipiga honi.Hapo Eve akapata swali la kumuuliza Hans.
“Eti Hans,ni kwa nini meli na ukubwa wake haizami kwenye maji lakini shilingi mia na udogo wake inazama?”.Eve alimuuliza swali la Fizikia Hans.
Hans akatabasamu kidogo na kujiweka sawa kwa ajili ya kujibu swali hilo. Japo lilikuwa ni swali la kifizikia,lakini pia Hans alilipeleka mbali zaidi na kuwa la kimapenzi.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (16)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

ILIPOISHIA......

Wakati wanaendelea kuburudika,mara kwa mbali ikasikika sauti ya meli ikipiga honi.Hapo Eve akapata swali la kumuuliza Hans.
“Eti Hans,ni kwa nini meli na ukubwa wake haizami kwenye maji lakini shilingi mia na udogo wake inazama?”.Eve alimuuliza swali la Fizikia Hans.
Hans akatabasamu kidogo na kujiweka sawa kwa ajili ya kujibu swali hilo. Japo lilikuwa ni swali la kifizikia,lakini pia Hans alilipeleka mbali zaidi na kuwa la kimapenzi.

*****ENDELEA*****

“Hilo swali wengi sana wanapenda kuliuliza hasa wale wasiopitia Physics. Ila kwa kuwa umeniuliza,nitakujibu na kukupa mfano hai.
Hapo tunarudi kwenye Law of Floatation,yaani hapo utalezea kuhusu vitu kuelea hasa meli.Law ina state hivi………….(Akaelezea hiyo sheria ya vitu kuelea).
Sasa najibu swali lako kama ifuatavyo”.Eve alikuwa kimya na makini wakati hayo yote Hans anayaelezea.Alionekana wazi mwenye uhitaji wa kufahamu alichouliza.Hans akaendelea.
“Meli kwa huku chini kabisa,ina nafasi kubwa sana ambayo nafasi ile haina tundu hata moja litakalopitisha maji. Yaani ni kama pulizo ile sehemu au dumu ambalo halina kitu na lililofungwa na kifuniko chake. Basi na kule chini ndipo papo hivyo.
Dumu likiwa halina kitu ndani yake,waweza kuelea nalo hata kilomita mia bila kuzama,lakini endapo litaingiza maji basi ujue utazama tu.
Na meli kwa pale chini,imeundwa kwa mtindo huo. Kule chini kuna hewa na ahairuhusiwi maji kuingia. Na nafasi ile ya hewa imepimwa ili kubeba uzito fulani wa mizigo. Kama ukizidisha,ndio unakuta meli inazama.
Shilingi mia au shilingi kumi,hazijatengenezwa na nafasi chini yake bali zenyewe ni mzigo ndo maana zinazama.Umenipata?”Hans alimaliza na kumtupia Eve swali.
“Sina swali aisee,upo juu Hans nimekubali”.Eve alimjibu Hans.
“Nashukuru Sweet. Sasa ngoja nikwambie kitu kuhusu wewe”.Hans aliendeleza tena maongezi.
“Ehee”.Eve akakaa mkao wa kula kwa ajili ya kusikiliza maneno toka kwa Hans.

“MUNGU kakuumba kwa mtindo wa meli,Sweet. Hata ubebe mangapi sidhani kama waweza kuyazamisha. Sweet,najua umebeba mengi sana moyoni mwako,naomba usiyazamishe hata kama yamekuzidi. Elea nayo hadi mwisho wake,naamini MUNGU atakupa zawadi ya kipekee katika maisha yako. Kamwe usijaribu kuyazamisha haya uyaonayo na kuyasikia.

Acha nikusifie Sweet Eve. Uwezo wako wa kubeba haya niongeayo waweza shinda meli zote za jinsia yako. Sikufananishi na ile meli kubwa kama Titanic ila naweza kukufananisha na lile Safina alilotengeneza Nuhu kabla ya MUNGU kuleta Gharika”.Alipofika hapo Eve akarudi nyuma kidogo na akawa kama anamshangaa Hans kwa yale maneno.
“Wewe Hans. Hayo maneno ya Biblia umeyatoa wapi. Na Sayansi na dini ni wapi na wapi?”.Eve akauliza huku bado akimshangaa Hans.
“Ha ha haaa. Sweetie,hujui kuwa nakaa na Mzee Wa Upako? Anatupaka maujuzi mara moja moja. Japo tunajidai hatusikilizi,lakini ndio hivyo,huwa tunachukua maujanja.
Halafu asikudanganye mtu,hakuna mtu ambaye anamuamini MUNGU kama mwana Sayansi.
Ngoja nikupe kidogo kuhusu hawa Wanasayansi hasa wale wa hali ya hewa na wanaopaa na vyombo kwenda nje ya sayari hii ya dunia”.Eve kusikia hivyo alisogea tena karibu na Hans na kumsikiliza.
Eve alikuwa anapenda sana kujifunza mambo mengi kupitia watu tofauti tofauti,hivyo uwepo wa Hans,Fred na Junior,ulimfanya ajifunze mengi sana asiyoyajua. Hans akaendelea.
“Kuna mwanasayansi mmoja,jina nimemsahau,ila yeye alikuwa kajiweka sana kwenye mambo ya Meteolojia,haya mambo yanayohusu hali ya hewa.
Yeye alisema kuwa, kama jua litapungua au kuongezeka uwezo wake wa kuwaka basi dunia inaweza kudondoka. Yaani zile nguvu za ukinzani ambazo ni kama sumaku,na ndizo hizo zinaiweka dunia iendelee kuzunguka katika muhimili wake bila kudondoka,eidha zinaweza kuongezeka nguvu na kuifanya dunia ipoteze mwelekeo au zinaweza kupungua nguvu na kuifanya dunia idondoke. Hiyo yote itatokana na jua kuongezeka na kupungua uwezo wake wa kuwaka.
Kwa maana hiyo,yeye alimaanisha kuwa dunia inategemea sana nguvu za jua katika kujiendesha kwake.Na huyu Mwanasayansi ana Law yake. Ngoja nitakuletea siku moja umjue.

Baada ya kusema hayo,akakaa muda mrefu na hiyo Law yake ikawa inatumika sana.Lakini baadaye lile bara la barafu linaitwa Antakatika,barafu ikaanza kuyeyuka. Vina vya vyanzo vya maji kama bahari na maziwa,vikaanza kupungua. Wachunguzi wakachunguza,wakagundua kuwa miale ya jua imekuwa mikali sana,yaani jua limeongezeka ukali wake.
Walipoenda kuitazama dunia waone kama itakuwa inapoteza mwelekeo,waliikuta ipo vilevile. Mwendo na sehemu ilipo,vilikuwa palepale. Yule mwanasayansi alitikisa kichwa na kusema mwacheni MUNGU awe vilevile MUNGU,hakuna ajuaye uwezo wa MUNGU”.Hans akawa anampa soga Eve ambayo kweli ilimvuta na kumfanya awe kimya.
“Mh! Hans wewe ni kiboko”.Alisifu Eve.
“Na si huyo tu! Wanasayansi wote wanamwamini MUNGU kuliko mtu yeyote. Kuna wale waliotengeneza maroboti. Wameweza vyote,lakini kumpa pumzi wameshindwa,wakasema hiyo ni kazi ya MUNGU. Hivyo japo wanajidai wajanja,lakini bado wanaenda nyumba za ibada na kumuomba MUNGU ili awasaidie”.Hans alizidi kutema madini kwa mtoto mzuri.
Kimya kikapita na kila mmoja akawa anaburudika na kiburudisho chake.Ni Hans ndiye alianzisha tena maongezi mengine.
“Sweetie,wajua kuogelea?”.Hans alimuuliza Eve.
“Mmmh! Mwenzako hata sijui”.Alimjibu Eve.
“Twende nikakufundishe”.Hans aliongea na bila kusubiri jibu alikuwa tayari kanyanyuka na kumnyooshea mkono Eve ili aushike naye anyanyuke.
Eve akabaki bila tendo.Kukataa anashindwa na kukubali anashindwa.Ila kwa kuwa alikuwa katoka na mtu,ilimbidi akubali.
Ni kama Hans alikuwa anasubiri sana kipengele kile ili aone alama ambayo Fred alisema kamchora Eve. Muda huo ukafika aisee.
Eve akatoa ule mtandio baada ya kunyanyuka na akabaki na nguo fulani kwa ajili ya ufukweni ambayo iliacha kiuno chake wazi.
Hapo Hans alicheka sana hadi Eve akauliza una nini.
“Daah!Nimemkumbuka sana Mzee Wa Upako. Jana nilimwambia natoka na wewe tunaenda beach akasema niangalie sana mavazi yangu. Sasa ndio nimekuangalia wewe mavazi yako na mimi,daah! Nimeamua nicheke tu! Hata hatuendani aisee”.Alidanganya Hans ila ukweli alicheka kwa sababu hakuona huo mwandiko ambao Fred alisema kamuandika Eve kiunoni.
“Ha ha haaa,utajiju. Wewe unakuja beach kama unaenda kucheza mpira”.Eve naye alishadadia na hapo akaanza kuelekea palipo na sehemu maalum ya kuogelea huku Hans akiwa pembeni yake.

Eve akatoa ule mtandio baada ya kunyanyuka na akabaki na nguo fulani kwa ajili ya ufukweni ambayo iliacha kiuno chake wazi.
Hapo Hans alicheka sana hadi Eve akauliza una nini.
“Daah!Nimemkumbuka sana Mzee Wa Upako. Jana nilimwambia natoka na wewe tunaenda beach akasema niangalie sana mavazi yangu. Sasa ndio nimekuangalia wewe mavazi yako na mimi,daah! Nimeamua nicheke tu! Hata hatuendani aisee”.Alidanganya Hans ila ukweli alicheka kwa sababu hakuona huo mwandiko ambao Fred alisema kamuandika Eve kiunoni.
“Ha ha haaa,utajiju. Wewe unakuja beach kama unaenda kucheza mpira”.Eve naye alishadadia na hapo akaanza kuelekea palipo na sehemu maalum ya kuogelea huku Hans akiwa pembeni yake.

Walipofika Hans ndiye alikuwa wa kwanza kujitupa majini na kuanza kuogelea huku Eve akiwa nje anaogopa kujitupa majini. Ilibidi Hans atoke na kumfata pale nje maji ya kumuuliza kwa nini ajumuiki naye.
“Mi naogopa bwana Hans”.Eve akamjibu Hans kwa sauti ya puani.
Hans akacheka kidogo na kisha akaanza tena maneno yake aliyobarikiwa na muumba.

“Ujue Eve usiwe kama mtoto mdogo bwana. Haya ni maji tulivu ambayo hayana kakala kama yale ya baharini. Haya ni maalumu hayawezi kupwa wala kujaa. Yale ya baharini kuna muda yanaenda mbali zaidi,na hapo watu ndipo wanapopata nafasi ya kuchezea fukwe za bahari. Lakini baadaye maji yale hurudi na kujaa fukwe yote hii.

Hii kama hujui inatokana na mzunguko wa dunia. Ngoja nikupe mfano hai”.Hans alitoka pale alipo Eve na aliporudi alirudi na chupa ambayo aliweka maji kiasi bila ile chupa kujaa,kisha akaanza kumwonesha anachomaanisha.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (17)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

ILIPOISHIA......

“UJUE Eve usiwe kama mtoto mdogo bwana. Haya ni maji tulivu ambayo hayana kakala kama yale ya baharini. Haya ni maalumu hayawezi kupwa wala kujaa. Yale ya baharini kuna muda yanaenda mbali zaidi,na hapo watu ndipo wanapopata nafasi ya kuchezea fukwe za bahari. Lakini baadaye maji yale hurudi na kujaa fukwe yote hii.

Hii kama hujui inatokana na mzunguko wa dunia. Ngoja nikupe mfano hai”.Hans alitoka pale alipo Eve na aliporudi alirudi na chupa ambayo aliweka maji kiasi bila ile chupa kujaa,kisha akaanza kumwonesha anachomaanisha.

*****ENDELEA*****

“KWA mfano,fanya hapa ndipo sisi tupo”.Akaonesha kule chini ya chupa ambapo chupa ilikuwa imesimamia.
“Si waona kuna maji eeh. Basi dunia inazunguka namna hii”.Akazungusha ile chupa hadi kule chini ambapo alisema ndipo wapo wao kukawa juu.
“Si waona maji yamehama eeh,na ukirudisha tena,maji yanajaa. Basi mfano huu ndio dunia ikifanyacho na ndio maana tunapata kupwa na kujaa kwa bahari.

Na ndivyo binadamu wengi walivyo,wapo wa kupwa na wapo wa kujaa. Kamwe usiyaogope maji bali ogopa walimwengu ambao ndio hawa watu.
Kuna muda huwa hawana madhara na mambo mengi,yaani wanakuwa wana roho nzuri na ya upole wenye wingi wa mambo. Hali hiyo hufanya watu wanajiita wanafunzi au wenye uhitaji wa kujua, waende kujiokotea chochote kupitia watu hawa.

Lakini kuna hawa wasiopenda kuchezewa sharubu,hawa ndio wazee wa kurudi na kujaa mahasira.Hawa si rahisi kuokota chochote kwao,kwani hawakupi nafasi hiyo hata kidogo. Muda wote wanakuwa wanamiliki eneo lao.

Sidhani kama wewe Swetie upo hivyo. Najua wewe ni kama mimi,siku zote ni watu wa kupwa tu! Tunaruhusu watu waokote chochote pale tunapokupwa. Kamwe usiruhusu kujaa bali jifunze kupitia wao pale wanapokuja kuokota chochote kwako”.

“Mmmh! Wewe Hans hayo yote unayoongea umeyatoa wapi? Mbona kama mwanafalsafa vile. Yaani haya makubwa,na madogo yana nafuu. Haya bwana,ngoja mi niendelee kuokota”.Eve alimwambia Hans baada ya Hans kuweka kikomo katika maongezi yake.

“Mi nilitaka ufahamu kuhusu kupwa na kujaa kwa bahari na ni vipi hali hii inaendana na maisha yetu. Kaa ukifahamu kuwa kila kitu hapa duniani kimeumbwa ili tukitawale sisi. Na kaa ukijua kuwa kila kitu kimeumbwa ili kitufundishe sisi jinsi ya kuishi na jinsi ya kufanya mambo yetu.

Kwa mfano,mchwa. Wale wameumbwa ili watufundishe jinsi ya kufanya kazi. Mti umeumbwa ili sisi tujue kutoa kama ujuavyo wenyewe kutoa kivuli na hewa safi”. Hans aliendelea kumpa maneno mazuri Eve.

“Mmmh! Hans unanidanganya bwana. Na je bata,kuku na mbwa. Hao nao wameumbwa kwa ajili ya sisi kujifunza kupitia wao?.Embu angalia tabia zao. Wanalelewa vizuri na mama yao lakini baadaye wanakuja kuzaa naye tena. Au kama ni mbwa dume,basi kila mbwajike linamtaka,huyo tena wasema kaumbwa ili tujifunze kupitia yeye?”.Eve alimuuliza swali ambalo lilimfanya Hans atabasamu kidogo na kusahau kuwa wameenda pale kuogelea na si kupiga stori.

“Kwani Sweetie,haya maisha umeumbwa kujifunza mazuri pekee?au mazuri na mabaya. Na hivi wajua kuwa mbwa anawakilisha dhambi katika vitabu vya dini? Mbwa alishalaaniwa kwa kupewa dhambi ya urafi. Huyo kuku na bata ndipo watu wanajifunzia tabia za ubakaji na mambo machafu ya kutembea hata na watu saizi ya wazazi wao.

Kila kitu duniani kimeumbwa kitufunze,niamini mimi Swetie. Lakini ndio hivyo,wapo wanaojifunza maovu na wapo tunaojifunza mazuri”.Hans alimwelezea Eve na Eve alibaki bila swali bali kumwangalia Hans bila kummaliza,na mwisho alitikisa kichwa kama kusikitika lakini alikuwa haamini yale aliyoyasikia.

“Vipi Swetie,mbona wasikitika?”.Hans alimuuliza.

“Wewe ni jiniazi Hans”.Alisema ya moyoni.

“Ha ha haaa,twende basi kuogelea kidogo halafu tuondoke si wajua jua linaenda hilo na usafiri wa huku ni majanga tupu”.Hans alitupa kete yake nyingine kumvuta Eve waende kuogelea.

“Lakini nikizama hii kesi ni yako”.Eve alitoa onyo mapema huku akisogea na kukaa kisha akaweka miguu yake kwenye maji yaliyo kwenye “swimming pool” ya pale.

Hans yeye alirudi nyuma kama hatua kumi kisha akaanza kukimbia kwa kasi sana kuelekea ilipo swimming pool ile. Alipofika karibu aliruka juu huku katanguliza mguu mmoja mbele kama anampiga mtu teke la uso. Hakuruka hivyo peke yake bali aliambatanisha na sauti ya kama ya kujikakamua.
“Iyaaaaa”. Baada ya sauti hiyo ilisikika sauti ya kutumbukia kwenye maji na eneo lile lilitapakaa maji kutokana na mtupo wake ule. Ni kama bomu lilitupwa kwenye swimming pool ile.

Eve kama walivyo wanawake wengine walikuwa hoi kwa kucheka na wanaume wengine waliokuwa eneo lile walikuwa wanashndwa kumtafsiri jamaa. Mbele ya mrembo kama Eve,anafanya kituko kama kile.

Hayo yote Hans hakuyafikiria bali alipoibuka toka kule alipokuwa amezama alimfata Eve pale alipo na kuanza kuongea naye huku ameweka mikono yake kwenye mapaja mazuri ya mwanadada yule.

“Njoo basi ndani na wewe”.Hans aliongea kistaarabu kama si yule aliyetoka kufanya kituko muda wa dakika moja uliopita.

“Yaani wewe bwana. Unavyoongea na mambo yako kama si wewe.Embu mwone kwanza”.Eve aliongea huku katabasamu na kumshika kidevu Hans.

“Kwani nimefanya nini Swetie. Embu acha hizo bwana,njoo tuogelee”.Hans aliongea huku akishika kiuno laini cha Eve na kuanza kumvutia ndani ya maji Eve.
Eve naye alikuwa hana kipingamizi bali kuingia ndani maji ila akiwa na uwoga kiasi fulani.

“Ukiogopa ndo unazama”.Hans alitania na kumfanya Eve atake kukimbia lakini Hans alishamkamata vizuri hivyo hakuweza kuondoka.

“Usijali Sweet.Unapokuwa na mimi,usalama unakuwa mkubwa kuliko hata ukiwa na usalama wenyewe. Mimi ndiye Hans The Man,usiogope”.Hans aliongea maneno hayo kwa sauti ya kunong’ona huku kamnyanyua Eve ndani ya maji. Mikono yake mmoja ukipita chini ya mapaja na mwingine nyuma ya mgongo na wakati huo Eve alikuwa kabana mikono yake kwenye shingo ya Hans.

“Ukinizamisha Hans”.Eve aliongea huku akiwa na uoga pale Hans alipokuwa anamshusha majini taratibu.
Alifanikiwa kumshusha na alikuwa kaweka mikono yake nyuma ya mgongo wa Eve na kumwambia aiachie miguu yake isiwe inagusa chini. Eve alifanya hivyo na alionekana kama anaelea. Tabasamu likaupamba uso wa Eve hasa alipojua ladha ya maji yale kwa kuyaoga bila kuzama. Uoga ukamtoka ghafla.

Na Hans naye ni kama alikuwa anamfundisha mtoto baiskeli,taratibu akaanza kumwachia Eve. Naye Eve alikuwa makini akiichezesha miguu yake. Hadi Hans anamaliza kuiachia mikono yake kutoka katika mwili wa Eve,Eve tayari alikuwa kishaweza kuogelea kifudifudi bila kuzama.

Watu walioona tendo lile hawakusita kupiga makofi kwa furaha. Makofi yale yalikuwa kama yanaenda kwa Hans kwa sababu wengi walioyapiga walikuwa wanawake.

Sasa wale matozi waliokuja na wasichana wao,mioyo yao sijui ilikuwaje. Lakini kwa Hans ilkuwa kama hatua moja kwenda mbele. Tatizo likabaki palepale,hawezi kumwambia kama anampenda Eve.

Hilo ni tatizo ambalo limesababishwa na wao wenyewe huko walipotoka. Hawakutaka kuwa na wanawake katika maisha yao,hivyo walikuwa ni waoga na wasiojua ni wapi pa kuanzia kusema nakuhitaji uwe nami katika dunia hii ya mapenzi.
Hans kama ilivyo kwa Junior na Fred,akabaki anaumia kwa maumivu hasa pale sifa za kuwa yeye ni mume mzuri wa Eve zilipokuwa zinatoka kwa watu waliokuwepo pale kwenye swimming pool.

“Hans umeniona?”.Eve alimtoa mawazoni Hans kwa swali hilo na kumfanya Hans apambe uso wake kwa tabasamu la kuchonga.
“Yeah.You did it Swetie”.Hans aliitikia huku akimfata Eve pale alipo na kumshika vizuri kiunoni na kumwomba waondoke kwa kisingizio muda umeenda.

Walitoka ndani ya maji na kuelekea zilipo nguo zao za mtaani. Walizivaa na kuchukua usafiri wa binafsi kuelekea yalipo makazi yao.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (18)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

“Hans umeniona?”.Eve alimtoa mawazoni Hans kwa swali hilo na kumfanya Hans apambe uso wake kwa tabasamu la kuchonga.

“Yeah.You did it Swetie”.Hans aliitikia huku akimfata Eve pale alipo na kumshika vizuri kiunoni na kumwomba waondoke kwa kisingizio muda umeenda.

Walitoka ndani ya maji na kuelekea zilipo nguo zao za mtaani. Walizivaa na kuchukua usafiri wa binafsi kuelekea yalipo makazi yao.

********ENDELEA**********

“Yuhuuuuu”.Hans alifungua mlango wa chumba anachokaa na kuingia huku akitereza kwa mguu mmoja na kutoa sauti hiyo.
Hakuta salamu bali aliingia kwa maneno ya kujigamba kama kawaida yao,.

“Basi mtoto nikamkamata namna hii kwenye kiuno chake laini kama manyoya ya kifaranga cha kuku. Nikamvutia kwangu taratibu,mtoto akavutika na hapo mdomo wangu ukawa unaelekea kwenye kinywa chake na kisha ndimi zetu zikatoka na kuingia kinywani kwa mwenzake. Wajua nini kilitokea?”. Hans aliongea huku akibakiza swali ambalo kila mtu alijua ni wapi alikuwa anaelekea kusema.

“Kwenda zako huko,unamdanganya nani kihivyo?”.Junior ndiye alianza kuongea huku Fred yeye akiwa bize na Biblia yake.

“Hujajibu swali mdogo wangu na tuachie kelele na domo lako linalonuka kama mavunja genge. Hata Swetie aliniambia kuwa unanuka mdomo,kwa hiyo chuna tu!”.Hans alimjibu na kumnyong’onyeza Junior.

“Sasa kama uongo asiseme bwana!! Acha uongo wako”.Fred naye aliingilia. Ni kama Hans alikuwa anamsubiri Fred aongee.

“Kwenda na acha kutuzingua wewe na Biblia yako. Kwanza unamtukana MUNGU kwa kujidai mtu wake wakati liongo balaa”..Hans alimwambia Fred.

“Mimi sijui kusema uongo,sema naendana na mazingira yenyewe. Kama mnajisifu na mimi nisijisifu?”.Fred alijitetea kabla ya Hans hajaendelea na lawama.

“Kwani nini aisee,mbona mnatuweka kwenye mafumbo?”.Suarez aliwauliza Hans na Fred.

“Si huyu anayejidai Baba Paroko sijui Mzee wa Upako. Alisema kamwandika mtoto kiunoni”.Hans aliongea na kukaa kimya na kusikiliza kama Suarez atakuwa anakumbuka maneno yale.
“Eee ndiyo.Jamaa alisema”.Suarez alionesha kumbukumbu zake.
“Basi mtoto hana alama yoyote kiunoni na huyu boya alisema ile alama yaweza kukaa mwezi bila kufutika. Jiongo kichizi,hiloooo”.Hans aliongea huku akimzomea Fred.

“Ha ha haaa. Embu usinikumbushe mwenzako. Hili jamaa mnadhani ni litoto humu? Hata kwa demu linaleta huu utoto.
Leo lilijidai li-Van Damme likajitupa ndani ya mimaji kama linguruwe. Ha ha haaaa”.Fred alijibu mapigo na kumwacha Hans akiwa kama amepata hasira.

“Kwa hiyo mwanangu tunafatana eeh. Si tuliagana hakuna kuingiliana katika ishu hizi? Mmeamua kunifatilia si ndio Wa Upako”.Hans alionesha wazi kaumia kwa kitendo kile.

“Hapa tumezidi kudanganyana ndio maana tumeamua kushuhudia kama hayo msemayo ni kweli. Ha ha haaaa,jamaa likajidai li-Chuck Norris. Eti iyaaaaaa,halafu pwaaaaah. Mimaji eneo lote kama gunia la mahindi limedondoshwa toka juu ya ndege na kutua kwenye bwawa,kumbe li-mtu,halafu jitu zima tu! Ha ha haaaa”.Junior naye aliongezea maneno na kumfanya Hans limshuke kama kapigwa na maji ya baridi.
“Sisi hatujakuingilia Hans. Ila na sisi tuliamua tuje kufurahi coco ndio tukakukuta na wewe. Tungekuingilia tungekuja hadi pale,lakini hatukuja bali kukuangalia jinsi ulivyojitupa ndani ya maji kama dubuwasha.Ha ha haaaa”.Fred aliongea na kuzidi kucheka.

“Halafu kuna videmu pembeni vikapiga,jamani huyu kaka vipi? Mbona kama kubwa jinga,ha ha haaaa?”.Junior alizidi kuongeza kumnyong’onyeza Hans na kuendelea kuleta vicheko vya haja mule ndani hata kwa Suarez ambaye alikuwa wala hayupo katika mkumbo huo.

“Halafu pale Eve alifyonza,ulimwona Junii.Hili jamaa si lilijitupa ndani maji halafu likazama,basi demu alijifuta maji na kufyonza. Ha ha haaaa”.Fred alizidisha utani.

“Halafu likaona limemfundisha mtoto kuogelea,kumbe mtoto anajua kuogelea toka zamani kinoma”.Junior alizidi kulembesha yale maongezi huku Hans akiwa haamini yale anayoyasikia.

“Umeona eeh. Mimi si wajua mzee wa mahotelini,siku moja wakati tupo pale Ken, akaniomba twende kuogolea. Mimi nikamwambia siwezi,akasema basi twende nikamuone yeye.
Acha bwana,mtoto anazamia yule,halafu kuna muda anaibuka na kujitupa kama yule Dolphin. Sasa jamaa leo likajidai limemfundisha,ha ha haaaa. Umebumba jamaa yangu”.Fred naye walishamfundisha maneno na ujanja wa mdomoni. Yale mambo ya upole hakuwa nayo kama mwanzo.

Wakati wote Suarez alikuwa anacheka bila kuchangia chochote,ni kama hakuwepo katika yale maongezi,lakini alishindwa asimame upande gani kwa sababu wale wote ni rafiki zake,na wale wote walimkaribisha mara ya kwanza,na yeye ndiye aliyewaleta kwa Eve. Akashindwa hata kutetea bali kubaki kucheka tu!.

“Embu ona hapa mwanangu.Lione hili jamaa”.Junior aliigeuza “laptop” ikaelekea kwa Suarez ambapo ndipo na Hans alikuwepo.
Akacheza ile picha ambayo alihitaji Suarez aione. Hapo alionekana Hans akikimbia kwa kasi ya hatari na kujitupa ndani ya maji.
Suarez alicheka sana kwa sababu ilikuwa ni tendo moja la kuchekesha mno kama ungepata kulishuhudia.

“Kwa hiyo wanangu mkanirekodi pia? Si ndio eeh. Poa bwana. Mmeshinda kwa leo,ila bado hamjashinda hata kidogo”.Hans aliongea kwa kusikitika huku akikaa kitandani kwake.

“Na ukileta uboya tu!.Tunaisambaza hii muvi chuo chote. Tunaandika LITAIRA likiwa na MREMBO,na facebook tunaiweka,na wale marafiki zetu wote wa watsapp,wataipata. Si wajua kilichotokea kwa WAGUMU? Basi kaa ukijua ile ni kazi yangu mimi”.Aliongea Junior kumchimba mkwara Hans ambaye alishapoa kitambo.

Maneno mengi yaliyowatoka wakina Junior yalikuwa hayana ukweli. Eve alikuwa hajui kuogelea kweli,na siku ile Hans ndiye alimfanya aweze kufanya zoezi lile japo si sana.
Ila waliongea yale kama kumtoa Hans mchezoni kwa makusudi kwani maneno yale yangemfanya Hans kuona kama alikuwa anakejeriwa na Eve.

Kimya kikatawala huku kila mmoja akiwa anafanya yake chumbani mule. Ni Fred ndiye aliyeanzisha maongezi tena na safari hii ni baada ya meseji kuingia kwenye simu yake.

“Daah! Kabadilisha siku,eti twende Jumatatu usiku. Hili jamaa litakuwa limemchosha sana. Ila poa,mi zangu za kijentromeni,si kama litaira kujitupa kwenye maji kama litembo”.Maneno hayo yalimfanya Hans amwangalie Fred kwa jicho la ubaya lakini alishindwa cha kufanya zaidi ya kumeza mate na kuongea maneno yaliyodhihirisha kuna kisasi mbele.

“We boya sasa hivi umekuwa mjanja eeh. Sasa ngoja,tutakutana pale katikati. Nitakuonesha mimi ndiye Hans The Crazy”.Aliongea Hans na kuweka earphone zake za simu na kuanza kusikiliza kilichomo mule.
Hakusikia majibu yaliyojibiwa na Fred bali aliona njia sahihi ni kutangaza vita rasmi kati yake na wale rafiki zake.

Uzuri wa Fred alikuwa ni mtu wa kumpeleka Eve maeneo tulivu hasa mida ya usiku. Mahotelini, migahawani,sehemu za maonesho,ndipo Fred alipendelea. Hali hiyo ilimfanya asijulikane wapi ataenda siku hiyo.
************
EVE NA ALFRED.

Ilikuwa ni Jumatatu ya saa mbili za usiku kama saa ya Fred ilivyoonesha pale alipoiangalia wakati yupo katika Hotel moja maarufu jijini Dar es Salaam. Alikuwa kakaa mahali fulani ambapo angeweza kumwona yeyote atakayeingia.

Hakukaa sehemu hiyo labda amwone Eve jinsi atakavyoingia bali alikaa hivyo ili aweze kuwaona na wabaya wake ambao ni Junior na Hans.
Alitangulia kufika kwa sababu alijua umuhimu wa mwanaume kutoka na mwanamke ambaye anamuhitaji. Siku zote aliamini mwanaume rijali ni lazima afike wa kwanza eneo pangwa kati yake na mwanamke anayetoka naye.

Elimu hiyo aliipata kutoka vitabu mbalimbali vinavyotoa sifa za mwanaume rijali au gentleman kama wenzetu wa ng’ambo wanavyolitamka kwa Kiingereza.

Baada ya kutulia kwa saa moja tangu afike pale,alimuona Eve akiingia na mpokezi wa wageni wa Hoteli ile kubwa,alionekana akiongea na Eve na hapo yule mpokezi akamuonesha mahala alipo Fred. Fred naye alipoona alikuwa anaangaliwa yeye,akanyoosha mkono kuonesha kuwa yeye yupo pale.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (19)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

EVE NA ALFRED.

Ilikuwa ni Jumatatu ya saa mbili za usiku kama saa ya Fred ilivyoonesha pale alipoiangalia wakati yupo katika Hotel moja maarufu jijini Dar es Salaam. Alikuwa kakaa mahali fulani ambapo angeweza kumwona yeyote atakayeingia.

Hakukaa sehemu hiyo labda amwone Eve jinsi atakavyoingia bali alikaa hivyo ili aweze kuwaona na wabaya wake ambao ni Junior na Hans.
Alitangulia kufika kwa sababu alijua umuhimu wa mwanaume kutoka na mwanamke ambaye anamuhitaji. Siku zote aliamini mwanaume rijali ni lazima afike wa kwanza eneo pangwa kati yake na mwanamke anayetoka naye.

Elimu hiyo aliipata kutoka vitabu mbalimbali vinavyotoa sifa za mwanaume rijali au gentleman kama wenzetu wa ng’ambo wanavyolitamka kwa Kiingereza.

Baada ya kutulia kwa saa moja tangu afike pale,alimuona Eve akiingia na mpokezi wa wageni wa Hoteli ile kubwa,alionekana akiongea na Eve na hapo yule mpokezi akamuonesha mahala alipo Fred. Fred naye alipoona alikuwa anaangaliwa yeye,akanyoosha mkono kuonesha kuwa yeye yupo pale.

SASA ENDELEA.....

Kwa mwendo wa madaha uliopambwa na tabasamu la haja usoni pake,mwanadada yule mrembo ambaye alifanya hata wale waliokuwamo katika hoteli ile kugeuka na kumwangalia yeye,alimfata Fred pale alipokuwepo. Naye Fred kabla ya mtoto hajafika,tayari alikuwa kasimama na kwa ajili ya kumpokea.

“Oooh,Malaika wangu. Unaonekana mrembo usiku huu”.Fred aliongea huku akimshika mkono wa Eve na kuubusu.
Fred alicheza kama alivyoelezwa na katika vitabu vingi kuhusu mwanaume rijali. Jambo alilojifunza kutoka katika kusoma kwake huko,ni kutomkumbatia mwanamke ambaye si mwanamke wako bado,bali afanye zoezi dogo tu! La kumshika mkono na kuubusu. Na Fred alifanya hivyo.
“Inaonekana nimekuweka eeh”.Eve aliuliza huku bado katabasamu.
“Si sana na pia ni haki yangu kukaa nikikusubiri wewe Malaika uliyeletwa duniani kwa ajili ya kutangaza injili njema juu ya mioyo yetu”.Fred aliongea huku akijionya kuwa hata kama mwanamke kakuweka muda mrefu,kamwe usiseme umeniweka sana na wala usiseme ndio nafika sasa hivi,bali taja muda wa kati. Yaani ule kati ya umeniweka sana na nimekuja sasa hivi.

Eve akazidi kutabasamu baada ya maneno yale na kama kawaida Fred akazidi kuonesha urijali wake kwa kumvutia kiti kwa nyuma Eve,naye Eve akakaa huku tabasamu likizidi kutanuka kuliko lile la mwanzo alilokuja nalo.

Bila kuchoshana na kama mwanaume yeyote alivyotakiwa kufanya,mhudumu alikuja pale na kuweka vinywaji huku akigawa karatasi maalumu kwa ajili ya kujichagulia chakula. Si kama muhudumu alikosea kuleta vinywaji,bali taarifa hiyo Fred alikuwa tayari kampa mapema tu!.

Eve alishindwa kuvumilia hisia zake za furaha na kujikuta akiuliza swali na tabasamu kuu likiupamba uso wake.

“Ina maana unafanya haya yote kwa ajili yangu Fred?”.Aliuliza Eve baada ya kuona kile kinywaji ndicho anakipendelea na kilikuwa na gharama kubwa sana kwenye ile hoteli.

“Malaika wangu. Siku ya kwanza kukuona nilijiuliza sana kichwani kwangu”.Fred aliongea huku akishika kile kinywaji na kuanza kukifungua kwa vidole vyake.
Ni kimywaji ambacho kipo kwenye chupa ya shampeni,chenyewe kilikuwa hakina kilevi bali hupendwa sana na wanawake japo kilikuwa na gharama kubwa. Fred akawa anakifungua huku anaweka maneno yake.

“Nilijiuliza juu yako. Ni nani huyu atazamaye kama alfajiri,mzuri kama mwezi,safi kama jua wa kutisha kama wenye bendera. Huo ni uzuri wako Malaika wangu,unatisha kwa uzuri wako kama kile kikosi cha bendera viatani. Kile kikirudi nyuma,basi wanajeshi wote hurudi nyuma,kikienda mbele basi jeshi zima huenda mbele’”.Fred aliongea maneno ya kwenye biblia katika kitabu cha wimbo ulio bora.

Sidhani kama Eve alifahamu kwani alikuwa ni mwenye tabasamu juu ya sifa zile. Wakati yote hayo yanaendelea,tayari alikuwa akamaliza kufungua kinywaji kile na kukimimina katika gilasi ambayo ililetwa kwaajili ya Eve.Baada ya kumimina,akaendelea kutema neno.

“Embu jiangalie Malaika wangu. Hatua zako malidadi kama za twiga,mapaja yako a mviringo ni kama johari. Sifa ziende kwa kazi ya mikono ya MUNGU.
Nani atashindwa kuingia gharama juu yako Malaika wangu. Kama nilivyokwambia mwanzo,umeleta taarifa nzuri kuja kwangu,nami nilipozisikia moyo uliruka juu kwa furaha kama yule mama aliyemwona Bikira Maria wakati anamimba ya YESU.

Huu mzuri Malaika wangu,na hustahili kufanyiwa chini ya haya. Kunywa kinywaji ukipendacho na chagua chakula ukionacho wewe waweza kukila na kufurahia huu mtoko wetu”.Fred alimaliza kuongea na kumkaribisha Eve ambaye alishindwa hata kusema neno juu ya maneno yale matamu kwenda kwake.

Akachukua gilasi ile yenye kinywaji na kuitia midomoni mwake na kumimina kiasi kidogo ambacho aliona kitapita vizuri kooni mwake bila kuleta kashi. Wakati huo Fred alikuwa bize akichagua chakula atakachokula.
Hakupenda kumwangalia Eve wakati anakunywa kwa sababu ya imani yake ya kuwa mwanaume rijali,huwa amchunguzi mwanamke anayemtoa out bali humpa uhuru wa kufanya chochote.

“Fred. Wewe unasoma sana vitabu vya dini,si ndio eeh”.Aliuliza Eve swali lililofanya Fred na kisha akajibu kwa kukubali kwa kichwa.

“Sasa kama ni hivyo basi na mimi nataka kukuuliza huko huko”.Aliongea Eve.

“Uliza tu Malaika wangu”.Fred alimpa nafasi Eve.

“Unaamini kuwa kuna mwisho wa dunia? Au unaamini kuwa kuna siku wote tutakufa na kufufuka tena na baadaye kukawa hakuna kifo,kama vitabu vya dini vinavyosema?”.Eve aliuliza swali ambalo kama mfuatiliaji dini huwezi kusema haamini hilo,lakini lilikuwa ni swali la kupima ulijari wa Fred.

Wanaume wengi wangejibu labda kwa kuuliza,hilo nalo swali. Lakini Fred alikuwa mtulivu na kusoma mawazo ya mwadada yule na alipopata akili yake inawaza nini,alifungua kinywa chake na kujibu.

“Naamini hilo Malaika wangu. Naamini ipo siku tutafufuka na kuonana tena. Na nitamshukuru sana MUNGU kama ataniweka na wewe pale tutakapopata ufufuko.

U mwenye bashasha na busara ambazo ni MUNGU pekee ndiye anayejua kwa nini kakupatia. Zawadi yoyote utaipata kama ukimuomba mwanaume. Hata ukisema uletewe kichwa cha Yohane Mbatizaji,utaletewa kutokana na umuhimu wako katika macho ya kila akuonaye.

Sidhani kama una moyo mgumu wa kutoelewa haya uyasikiayo. Ila najua una moyo laini kama sufi ya kondoo wa bwana. Hakuna atakayekataa kufungwa na nila yako,kwani nila yako ni laini na kila mmoja hawezi kukataa kufungwa nayo.

U Malaika uwezaye kuwa mzabibu nasi tukawa matawi yako.Kwa jinsi navyokuangalia machoni kwako,sidhani kama nitakosea kusema kama nikisema unaweza kuingia ndani ya moyo ya mtu na kuvuta kiti cha moyo huo,nawe ukakaa daima ndani yake.

Namaanisha mwanaume yeyote anaweza kukukabidhi moyo wake,akakupenda, akakuthamini na akakupa kila kitu kinachoitwa mapenzi. Niamini Malaika wangu”.Fred aliongea kiasi kwamba hata yule aliyekuja kuchukua menu ya chakula walichoagiza alikuwa katanua mdomo huku aamini yale aliyokuwa anayasikia.

“Vipi kaka,mbona umeganda?”.Fred alimuuliza yule jamaa mhudumu.

“Nimekuja kuchukua menu ya chakula kaka”.Alijibu.

“Poa.Hizi hapa”.Fred alizikusanya menu zote mbili na kumpatia.
Wakati anaondoka baada ya kupewa orodha ile ya chakula ambacho Fred na Eve waliweka tiki kwenye chakula wanachotaka,yule mhudumu aligeuka nyuma na kwa bahati nzuri alikutana na macho ya Fred.
Mhudumu alimwonesha dole gumba ambalo lilipokelewa kwa tabasamu dogo kutoka kwa Fred,na kisha mhudumu alititia ndani kwa ajili ya kuandaa huduma aliyoombwa.

“Yaani wewe unaongea kuliko hata unavyoonekana. Una maneno ambayo yanaweza kumfanya mtu ajiulize mara mia ni wapi umeyapata. Mh! Eti naweza kuwa mzabibu nanyi mkawa matawi,kwani mimi Yesu?Ha ha haaa”.Eve aliongea na kucheka kitu ambacho Fred alikipenda sana hasa baada ya kumuona mwanamke aliyembele yake anacheka kwa sababu yake.

“Wanasema ukicheka unaongeza siku za kuishi. Lakini naamini yule anayekufanya ucheke,anaongeza siku za kuishi mara mia zaidi yako.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (20)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

Wakati anaondoka baada ya kupewa orodha ile ya chakula ambacho Fred na Eve waliweka tiki kwenye chakula wanachotaka,yule mhudumu aligeuka nyuma na kwa bahati nzuri alikutana na macho ya Fred.
Mhudumu alimwonesha dole gumba ambalo lilipokelewa kwa tabasamu dogo kutoka kwa Fred,na kisha mhudumu alititia ndani kwa ajili ya kuandaa huduma aliyoombwa.

“Yaani wewe unaongea kuliko hata unavyoonekana. Una maneno ambayo yanaweza kumfanya mtu ajiulize mara mia ni wapi umeyapata. Mh! Eti naweza kuwa mzabibu nanyi mkawa matawi,kwani mimi Yesu?Ha ha haaa”.Eve aliongea na kucheka kitu ambacho Fred alikipenda sana hasa baada ya kumuona mwanamke aliyembele yake anacheka kwa sababu yake.

“Wanasema ukicheka unaongeza siku za kuishi. Lakini naamini yule anayekufanya ucheke,anaongeza siku za kuishi mara mia zaidi yako.

ENDELEA...

Malaika wangu,usiku huu umeniongezea siku za kuishi katika maisha haya. Huu wa muhimu kwangu kuliko unavyodhani. Nimekufanya uongeze siku,nawe umeniongezea siku zaidi kuliko zile nilizokupa wewe. Nani kama wewe Malaika wangu,endelea kucheka nione meno yako meupe na ya kung’aa kama vazi la Malaika aliyemtokea Bikira Maria.
Endelea kucheka Malaika wangu”.Fred aliongea na kumfanya Eve atikise kicha kushoto na kulia kama anasikitika lakini alikuwa amejawa na tabasamu lililoonesha dhahiri alikuwa haamini anachosikia,au kafurahishwa na yale maneno.

“Yaani wewe. Dah! Basi bwana”.Aliongea Eve na kushindwa kumalizia kauli yake. Wakati huo mhudumu alionekana akija na sinia kubwa lililosheheni chakula walichoagiza.
Mhudumu alifika mahala pale na kisha akaweka chakula mezani.Zoezi lililofata baada ya hapo ni kuwanawisha wageni wale wenye maneno mengi ya kuvutia. Alipomaliza,aliwakaribisha naye akapotea eneo lile akiwaacha wale wawili wakijihudumia vyakula walivyoagiza.

“Unapenda kuku eee”.Fred alimuuliza Eve baada ya kuona Eve anajiwekea kuku kwenye sahani yake.

“Sana. Ni nyama moja baridi isiyo na madhara makubwa kama zilivyonyama za wanyama wengine”Alijibu Eve huku akifunua sahani fulani ambayo ndani yake ilisheheni tambi.

“Na wewe unapenda ugali kwa samaki ee”.Naye Eve alimtupia swali kwa Fred.

“Hiyo ndio sababu ya mimi kuwa imara zaidi ya chuma. Ila wewe yakupasa kula vitu kama hivyo ili ujengeke mwili na kuwa laini. Huu ugali tuachie sisi wafanya kazi ngumu”.Alijibu Fred huku anamega tonge la kwanza la ugali.

“Kwani sisi hatutakiwi kuwa imara?”.Eve alitupa swali lingine lililofanya Fred asile kwanza bali kujibu swali lile.

“Kwa mwanamke kama wewe,hupaswi kuwa imara sana kimwili bali kiakili.Nasema hayo kwa kuwa yule utakayekuwa naye,tayari atakuwa imara kwa ajili yako. Atafanya chochote kwa ajili yako,na hatokuwa tayari kukupoteza. Ni lazima awe imara na ni lazima ale ugali kwa wingi,kama mimi”.Fred aliongea na kunyanyua mkono wake wenye tonge na kuanza kula.
Eve naye alifanya vivyo hivyo lakini yeye alitumia uma na kisu ambacho hakina makali kwa ajili ya kukatia nyama ile ya kuku.
****
Walipomaliza kula,walikaa kidogo na Fred alilipia gharama za vyote vilivyotumika pale. Kilichofuata ni wao kuanza kurudi yalipo makazi yao.

“F mi nataka tutembee kwa miguu hadi chuo”.Aliongea Eve huku akisogea pembeni ya Eve na kuingiza mkono wake katikati ya ubavu na mkono wa Fred,yaani chini ya kwapa la Fred na kisha akabana mkono wake katika mkono wa Fred huku akiongeza deko la maneno yake kwa kulalia bega la kijana yule aliyekuwa kavalia suti ya kijivu iliyomkaa vizuri kama mwanamichezo wa nchi za nje anaenda kuchukua tunzo.

“Usiku huu Malaika wangu.Huogopi?”.Fred alimuuliza Eve wakati huo walishatoka nje ya hoteli ile nzuri ya nyota kuanzia tatu.

“Hivyo hivyo. Nikichoka kutembea ndio nitapanda gari”.Aliongea Eve kwa deko zaidi lililomwacha Fred bila neno bali kumsisimua na kumjaza kichwa.

“Sawa Malaika wangu. Mimi sitaki kukuhudhi. Twende sasa”.Fred alijibu na safari ya kwenda kwao ilianza.

Baada ya mwendo mfupi kidogo huku wakiwa wanapiga soga taratibu. Fred alianzisha tena maongezi yake matamu.

“Malaika wangu. Hivi unaamini kuwa mtu akifa roho yake inabaki kukulinda wewe?Namaanisha kama unandugu au yeyote anayekujali,akifa anakuachia ulinzi hapa duniani,unaamini?”.Fred alimuuliza Eve.

“Mh! Hiyo hapana kwa kweli F”.Eve alijibu na kuendelea kujikunyata kwa Fred ambapo kulimfanya Fred atoe koti lake la suti na kumfunika Eve aliyeonekana anahitaji joto japo mavazi aliyoyavaa yalikuwa hayapitishi baridi sana. Ila kwa kuwa Fred alikuwa anaigiza urijali,ilibidi kuwa hivyo.

“Asante F.Lakini kwani wewe unaamini?”.Alishukuru kwa lile koti,kisha akarudi katika mada.

“Ndio naamini. Embu angalia angani”.Eve akatazama angani wakati huo bado wanatembea njia ambayo ilikuwa na watu kiasi.

“Unaona nini?”.Fred aliuliza.

“Naona nyota na mwezi”.Eve akajibu.

“Wazungu wanasema nyota ni macho ya wale wakupendao,waliokujali wakiwa duniani na wanaopenda kukuona unafanikiwa. Macho haya yanakuangalia vizuri sana. Yaweza kuwa ya mabibi na mababu wa zamani sana. Bado wanataka kukuona ukifanikiwa. Na ndio maana kukiwa hakuna nyota,ni rahisi sana mambo mabaya kukupata”.Fred alijibu lakini hakuishia hapo.
“Hata mimi nikifa,nitakuwa nyota. Nitakulinda kwa kila ovu,nitamsimamisha kila ambaye atataka kukudhuru. Hiyo ni kwa sababu nakujali sana Malaika wangu. Kama ukiniambia nife kwa ajili hiyo,nitakufa ili nikulinde”. Fred alizidi kutiririka maneno ambayo kwa mtu wa kawaida mwanzoni anaweza asiyaamini,ila kwa jinsi yanavyoenda,anakuwa hana budi kuyaamini kwani ni maneno matamu ya kuweza kumfanya yeyote ayasikiaye,kujiona yupo juu kuliko mwanamke mwingine dunia hii.

“Sina usemi hadi hapo”.Eve alikubaliana na maneno yale.

“Tupande basi gari,mi mwenzako nasikia baridi”.Fred alitoa ombi ambalo lilipita bila pingamizi.
Wakaita usafiri binafsi ambao ni tax. Safari ya kwenda yalipo makazi yao,ikachukua nafasi.
*****
Baada ya nusu saa,tayari Eve alifika yalipo makazi yake. Fred alimuomba dereva amsubiri kidogo ili amsindikize mwanadada yule hadi getini.

Kama kawaida ya Eve,ili asipoteze urafiki na wale watu,alimpatia Fred busu moja dogo katika midomo yake na kumfanya Fred atabasamu kwa furaha huku akijiona kama anaelekea kushinda ligi ile.

“Kesho kutwa nitataka nitoke na wewe tena. Naomba hilo F”.Eve aliongea huku akimwangalia Fred machoni.

Unadhani Fred angekataa?Alijibu haraka kwa kukubali,na hapo Eve alimpatia koti lake na kufungua geti la makazi yake,kisha akaingia humo na kufunga geti lile na kumuacha Fred akiwa anatabasamu mwanana. Alishangilia kidogo na kugeuka na kuanza kulielekea gari lililowaleta hadi pale.
******
Dakika nyingine kumi na tano,Fred alikuwa kishafika anapoishi na kama kawaida aliingia kwa fujo huku akitabasamu,lakini yeye hakuwa muongeaji sana kama wakina Junior.
“Vipi kaka?Mbona hautupi matokea huko?”.Suarez Emmanuel alimuuliza Fred baada ya kuona haongei chochote kama wale wenzake.

“Gentleman huwa haadithii mambo yake”.Fred alijibu kwa kifupi huku anavua viatu vyake karibu na kabati lenye nguo zake.

“Utakuja kuongea tu,boya wewe.Ngoja uone”.Hans aliongea kwa sauti ya chini na iliyojaa kithirani. Halafu akageuka upande mwingine wa kitanda na kuendelea kusoma kitabu alichokuwa anakisoma.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (21)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

DAKIKA nyingine kumi na tano,Fred alikuwa kishafika anapoishi na kama kawaida aliingia kwa fujo huku akitabasamu,lakini yeye hakuwa muongeaji sana kama wakina Junior.

“Vipi kaka?Mbona hautupi matokea huko?”.Suarez Emmanuel alimuuliza Fred baada ya kuona haongei chochote kama wale wenzake.

“Gentleman huwa haadithii mambo yake”.Fred alijibu kwa kifupi huku anavua viatu vyake karibu na kabati lenye nguo zake.

“Utakuja kuongea tu,boya wewe.Ngoja uone”.Hans aliongea kwa sauti ya chini na iliyojaa kithirani. Halafu akageuka upande mwingine wa kitanda na kuendelea kusoma kitabu alichokuwa anakisoma.

*****ENDELEA*****

Ni kama Fred hakuisikia sauti ya Hans,lakini aliisikia sema akaipuuzia kwa kuwa alijua ni utani tu.

“Subiri muone boya litakachokifanya keshokutwa,ha haa”.Fred alijibu mnong’ono wa Hans huku akipanda juu ya kitanda chake wakati huo Junior yeye alikuwa kapitiwa na usingizi muda mrefu.

Asubuhi,marafiki wale walienda darasani lakini Hans alibaki chumbani huku akisingizia anaumwa kidogo,hivyo hawezi kwenda kuhudhuria masomo ya siku ile.

Walipoondoka,Hans alitoa makorokoro yake baadhi na kuanza kuyachanganya. Alitumia saa moja kuchanganya na kujaribu kazi yake aone kama inafanya kazi.

Baada ya kuona mafanikio,alitabasamu kwa mbwembwe na kuitengenisha michanganyo ile ambayo ilikuwa ni unga mweusi na maji fulani ya njano.

Unga aliuweka kwenye kifuko kidogo cha nailoni na yale maji kiasi alifanya hivyo hivyo. Maji na unga ule vikiwa vimetenganishwa,havina madhara ila vikichanganywa pamoja,ndipo vinaweza kusababisha madhara. Hans alivitenganisha na kuvificha katika kabati lake akisubiri siku ya kuvitumia.
*******
Baada ya masomo ya siku nzima. Hatimaye marafiki wale watatu walirudi chumbani kwao na walimkuta Hans akiwa amelala fo fo fo jambo lililofanya aonekane kweli jamaa ni mgonjwa.

Hakuna aliyemsumbua bali kila mmoja alianza kufanya yake huku kichwa cha Fred kikiwa kinawaza zaidi siku ya kesho yake ambapo alitakiwa kwenda kukutana na Eve.

Masaa yakaenda na kupotea,hatimaye ikafika usiku ambapo wote kwa pamoja walitoka kuelekea sehemu wanapouza chakula. Wote walionekana wana furaha,hata Hans aliyekuwa mgonjwa,alikuwa karudi katika hali yake kiasi.

Baada ya kula na kufurahi kwa pamoja,walirudi chumbani kwao huku bado furaha ikiwatawala. Hakuna aliyejua mipango ya mwenzie,ila kila mmoja alikuwa anacheka huku akipanga yake moyoni.

Usiku ukahitimishwa kwa marafiki wale kulala huku kila mmoja akiwa anaota mambo yatakayokwenda kutokea kesho yake,hasa Hans na Fred.
********

Asubuhi ya kesho yake kila mmoja aliamka mwenye tabasamu katika uso wake,matabasamu ambayo yalikuwa yanaonesha walikuwa hawana matata katika siku ile na walikuwa wazima wa afya.

Kila mmoja alianza shughuli zake ndogondogo kabla hawajaenda kujisomea na baadaye kwenda kujipatia kifungua kinywa kabla hawajaingia vipindi vya mchana ambavyo vingewapeleka hadi mida fulani ya chakula cha mchana. Hiyo ndio ilikuwa ni ratiba yao ya kila siku na waliifata vyema.

Baada ya masomo ya siku nzima,ndipo walirudi wanapoishi huku Fred akiwa anamzuka wa kufa mtu na kuona muda kama hauendi,alikuwa anabwabwaja maneno mengi kama simu la mtoto mdogo lile ambalo ukibofya namba moja linaanza kulia hivi,ukibofya namba mbili linalia vile na ukiofya namba tatu na nyingine nyingi,hulia linavyojua lenyewe.
Basi Fred alikuwa hivyo ,kila hadithi alitaka kuwemo hadi wenzake wakawa wanakereka.

“Baba Paroko niaje?Mbona umechangamka kama kachumbari iliyomwagiwa pilipili na ndimu halafu inaliwa na mlevi?.”Aliuliza Suarez.

“Aaah!Sitaki kujichafua kwa kununa kwani leo washika mapembe wanaisoma namba.”Fred aliongea kwa nyodo na kumaliza na cheko moja ya kejeri na majigambo kiasi chake.

“Hapo ndipo ulipokosea. Leo lazima cheko igeuke kilio.”Aliongea Hans kwa sauti ya chini lakini iliyomfikia vema Fred.

“Ha ha haaaa,anadhani na mimi nitakuwa likifaru kujitupa kwenye mimaji hadi iruke ruke pembeni. I am Gentleman”.Aliongea Fred na kuzunguka kidogo kama anacheza muziki.

Wakati hayo yote yanaendelea,walikuwa katika barabara wakorudi maskani waishipo.
“Ha ha haaa,eti likifaru. Jitu likajirusha pwaa. Duuh! Ile sehemu ikawa kama imetupwa bomu la nyukilia.Majitu mingine bwana.”Hapo Junior naye aliongea kumchokoza Hans.

“Leo mtaona historia nyingne tu!. Si watu wanajidai wamejanjaruka wakati tumewajanjarua sisi hadi leo wanavalia suruali chini ya mkanda na wakati walikuja hapa,suruali wanafungia mkanda shingoni. Kudadeki zao.”Aliongea Hans kumpiga dongo Fred.

“Ha ha haaa.Acheni kunichekesha bwana. Suruali inafungiwa shingoni,imekuwa tai hiyo?.”Suarez alisaili kinafki.

“It doesn’t matter. Nachojua nimewapiga gepu wewe na zee la kunuka domo.”Fred alijibu mapigo ya Hans na kuendelea kucheza barabarani kwa furaha.
Walindelea kurumbana hadi wakafika wanapoishi ambapo kila mmoja alijitupa kitandani kwanza ili atoe mchoko kabla ya kuikaribisha jioni.
****
Saa kumi na mbili jioni,Fred alikuwa anajiweka tayari kwa ajili ya kwenda kukutana na kimwana Eve. Mtoto ambaye kabarikiwa kila sifa ya urembo wa sura hadi tabia bila kusahau uzuri wa umbo na miondoko ya madaha. Nani ambaye angesipodata mbele ya kimwana yule matata.

Akiwa tayari kishajiwekea mavazi yake mahala pasafi na salama baada ya kuyanyoosha,Fred alitoka nje kwa ajili ya kwenda kuoga,na wakati huo aliwaacha Junior,Suarez na Hans wakiwa bize na vitabu vyao pale kitandani.

Baada ya dakika tatu za Fred kutoka nje,Hans alinyanyuka toka kitandani kwake na kwenda katika kabati lake. Hakuna aliyejua nini kinaendelea na hakuna aliyemfatilia kwa sababu walijua kaenda kwa nia binafsi.
Alifungua kabati lake na kuchukua vile vifuko viwili vya plastiki,halafu akageuka nyuma kuangalia kama Sua na Junior wanaenda na kipindi.Alipoona wapo bize na mambo yao,akaenda kwenye suruali ya Fred aliyopanga kuvaa siku ile.
Alichofanya ni kuweka vile vinailoni viwili kwenye mfuko wa nyuma wa suruali ile ya Fred.Vinailoni vile ambavyo kimoja kilikuwa na unga na kingine majimaji,ndivyo viliaribu kabisa mtoko wa Fred.

Baada ya kuhakikisha kafanikiwa kufanya zoezi lake bila kushtukiwa,Hans alirudi kitandani kwake na kuendelea kujisomea kitabu alichokuwa kakianza.

Nusu saa baadae,aliingia Fred kwa furaha huku tauro likiwa kiunoni, na shati alilotoka nalo likiwa begani na wakati huo huo mdomo wake ulikuwa unatoa mluzi wa wimbo wa Happy ulioimbwa na Pharrell Williums. Na uzuri alikuwa anaweza kucheza,hilo nalo likawa kivutio kwa rafiki zake.
Lakini ilikuwa kivutio zaidi pale alipokuwa anaendelea kucheza na mara akalitoa tauro kiunoni na kubaki na boxer moja ndogondogo iliyombana vizuri sana.

Basi kwa mbwembwe nyingi akaanza kucheza huku anaimba kiwimbo chake ambacho kilimkaa sana kichwani,tangu asubuhi.

Hata yule aliyekuwa anakisasi naye ilimbidi acheke tu! Maana jamaa alivyokuwa anayarudi na kile kiboxer,waweza sema LMFAO.

Huku anaendelea kutoa burudani ya kucheza,Fred alianza kujipaka manukato mbalimbali katika mwili wake kwa ajili ya siku ile ya faraja kwake.

Baada ya kumaliza hayo,alichukua singlend nyeupe na shati la kijani ya apple alilokuwa kalitundika kwenye kabati lake,akavaa. Alipomaliza,akatinduwa suruali yake ya kijivu,na bila kuichunguza akatinga mwilini mwake na kuichomekea vizuri mwilini.

Akachukua kioo kidogo na kuanza kutana nywele zake kabla hajachukua koti lake la kijivu ambalo alilivaa na kukamilisha suti iliyokuwa imemtoa chicha balaa. Kwa jinsi ilivyokuwa imemkaa,waweza sema huyu kocha tena Morinho au Gadiola.Au msanii mkubwa wa Marekani kama Justin Timberlake au labda Christian Ronaldo akienda kuchukua tunzo ya mchezaji bora wa dunia.Hakika jamaa alipendeza,uongo dhambi.

“Kaka leo umevunja kabati halafu ufunguo umeumeza.”Aliongea Suarez kumsifia Fred.

“Kawaida yangu,unadhani mimi wa makaptula kama tembo mtoto?.”Alijibu Fred huku akitupa dongo dogo kwenda kwa Hans.

“Na leo lazima mtu aje analia hapa.”Aliongea Hans na kugeukia upande mwingine wa kitanda chake.

“Halii mtu. Subirini kuletewa wifi yenu humu.”Fred aliendelea kuleta nyodo zake.

“Basi kaka we nenda kwa maana umeshaanza shombo zako hapa.”Aliongea Junior baada ya maneno kuntu kutoka kwa Fred.

“Naweza nisiondoke na usinifanye kitu.Ila kwa kuwa natakiwa kuondoka ngoja kwa sasa niwaache. But,siwaachi hivihivi.”Fred akatoa simu yake kwenye kipochi kilichokuwa kitandani kwake na kubofya namba kadhaa.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (22)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

Baada ya kumaliza hayo,alichukua singlend nyeupe na shati la kijani ya apple alilokuwa kalitundika kwenye kabati lake,akavaa. Alipomaliza,akatinduwa suruali yake ya kijivu,na bila kuichunguza akatinga mwilini mwake na kuichomekea vizuri mwilini.

Akachukua kioo kidogo na kuanza kutana nywele zake kabla hajachukua koti lake la kijivu ambalo alilivaa na kukamilisha suti iliyokuwa imemtoa chicha balaa. Kwa jinsi ilivyokuwa imemkaa,waweza sema huyu kocha tena Morinho au Gadiola.Au msanii mkubwa wa Marekani kama Justin Timberlake au labda Christian Ronaldo akienda kuchukua tunzo ya mchezaji bora wa dunia.Hakika jamaa alipendeza,uongo dhambi.

“Kaka leo umevunja kabati halafu ufunguo umeumeza.”Aliongea Suarez kumsifia Fred.

“Kawaida yangu,unadhani mimi wa makaptula kama tembo mtoto?.”Alijibu Fred huku akitupa dongo dogo kwenda kwa Hans.

“Na leo lazima mtu aje analia hapa.”Aliongea Hans na kugeukia upande mwingine wa kitanda chake.

“Halii mtu. Subirini kuletewa wifi yenu humu.”Fred aliendelea kuleta nyodo zake.

“Basi kaka we nenda kwa maana umeshaanza shombo zako hapa.”Aliongea Junior baada ya maneno kuntu kutoka kwa Fred.

“Naweza nisiondoke na usinifanye kitu.Ila kwa kuwa natakiwa kuondoka ngoja kwa sasa niwaache. But,siwaachi hivihivi.”Fred akatoa simu yake kwenye kipochi kilichokuwa kitandani kwake na kubofya namba kadhaa.

ENDELEA...

“Nambie Malaika wangu.Furaha ya macho yangu,utamu wa akili yangu na neno takatifu la ulimi wangu.”Fred alibwabwaja baada ya simu kupokelewa.

“Mi mzima Malaika wangu.Upo wapi sasa hivi.”Alisaili Fred baada ya salamu yake kuitikiwa.

“Okey,basi nakuja sasa hivi na teksi kuja kukuchukua,si tayari ushajiandaa ee.”Fred akaendelea.

“Aaah,Malaika wangu,wewe ndiye uwezaye kumfukuza hata shetani mbaya wa kichwa changu. Kwa nini hujali thamani nayokupa ya kutembelea taksi bali kutaka kutembea kwa miguu?.”Aliposema maneno hayo ni kama alimwamsha Hans usingizini kwani alijikuta akitabasamu kwa shangwe.

“Sawa Malaika wangu,najua unataka ufurahie uwepo wangu. Basi tutatembea.”Fred alijibu simu upande wa pili na kukaa kimya kidogo kabla hajamaliza maongezi yake.

“Sawa Malaika wangu.Nitakuja hapo baada ya nusu saa.”Fred akakata simu.

“Sasa nyie wazee wa mapembe,baadae tutaonana. Mi naanza kwenda taratibu,sitaki papara. Natembea kwa miguu hadi kwake na kisha nampeleka mtoto hotel za maana kama kawaida yangu.”Alijisifu Fred na kutoka nje huku Suarez na Junior wakimtakia safari yenye mafanikio.

“Hata usiponi-wish me lucky,lazima nitafanikiwa tu. Tembo mtoto wee.”Alirudisha kichwa chake kwa kuchungulia,ndipo aliongea maneno hayo akayaelekeza kwa Hans.

“Mi sina tatizo na wewe,utarudi tu hapa. Tutaona nani mshindi.”Alijibu Hans kwa sauti ya ujasiri na tulivu.

“Tcio bebee.Subiri wifi yako anakuja.”Aliongea Fred na kufunga mlango wa chumba kile,ikiwa tayari ni saa moja na dakika kadhaa.
*****
Fred mida ya saa moja na dakika zake arobaini na tano,alikuwa nje ya geti la makazi anayoishi Eve Johaness,mwanamke aliyekonga nyoyo za wanachuo karibu wote pale Dar es Salaam.

Ni kweli alitembea kwa miguu ili tu,asiwahi kufika na kumkuta Eve bado hajajiandaa kwani waliahidiana wakutane saa mbili za usiku ule.

Baada ya kufika,alimpa taarifa mrembo wake wa muda kwa kutumia simu yake kuwa tayari yupo nje anamsubiri. Nasema ni mrembo wa muda kwa kuwa Eve alikuwa kama kiti cha basi,leo kakaliwa na huyu,kesho kakaliwa na mwingine.Kwa hiyo huwezi kumuita huyo ni mpenzi wako wa kudumu na mbaya zaidi watu wenyewe walikuwa hata saundi hawajazitema.

“Nimekuweka sana wangu wa ukweli”.Aliongea Eve baada ya kutoka nje na kumkuta Fred akiwa kaegamia mti mmojawapo pale nje.

“Hata YESU alisema atarudi,lakini hadi sasa bado tunamsubiri.Sembuse wewe binadamu mwenzangu uliyeniahidi baada ya dakika kadhaa utakuwa nami? Siwezi kukata tamaa kusubiri kwani kufanya hivyo itabidi kwanza nikate tamaa kumsubiri YESU ndipo nikate tamaa kwako.
Swali lako nalijibu kuwa,hujaniweka hata kidogo. Ni halali yangu kukusubiri hata hadi asubuhi kwani wewe ndiye Malaika wangu. Ulindae moyo wangu na hata kichwa changu chenye wingi wa hamu ya kukuona na kukujulia hali.”Aliongea Fred kiufasaha na kumuacha Eve akiwa katika tabasamu mwanana lililokuwa linazidi kumbanjua Fred mabandu ya magome yaliyo-moyoni mwake na kuuacha moyo huo kuwa mweupe na wenye upendo ulikothiri furaha na amani.

Wakati huo alishamsubiri Eve kwa dakika kama kumi na tano. Na kweli aliwekwa sana tu! Ila kwa kuwa ni mrembo,atafanya nini sasa. Ila angekuwa dume mwenzake,sijui kama angekubali kuwekwa vile.

“Mmmh! Mimi nilidhani nimekuweka bwana maana umekuja mapema na halafu nilikuwa bado hata sijaoga wala kuchagua cha kuvaa,si waona mavazi yangu ya leo?.”Eve alijitetea huku anajiangalia.

“Hayo mavazi ni zaidi ya wewe unavyodhani. Umetoka sana Malaika wangu. Ungekuwa nchi za wenzetu,ungepita kwenye RED KAPETI,ila huku kibongo bongo,utamezewa mate na marijali kuonesha kuwa umependeza.”Fred alimpa sifa dada yule na kumuacha hana neno bali meno yaliyopangana kiustadi mdomoni mwake kutokeza na kumfanya Fred amsifu MAULANA kimoyomoyo kwa kumuumba kiumbe yule ghafi katika peo za macho yake.

Eve japo alikuwa kajikataa kuwa mavazi aliyovaa hayakuwa rasmi,ila kiukweli alikuwa katoka vibaya mun
Gauni lake la refu la silva na lenye ming’aro kadhaa kwenye mikanda iliyopita mabegani pamoja na mmoja mpana kiunoni pake,ulimfanya Eve ang’ae sana usiku ule wa haja kwa watu wale wawili.

Huku chini ali-match na viatu vya rangi ileile ya silva na juu nywele zake alizibana na banio la damu ya mzee,rangi ambayo ilikuwa inaendana na kikoti kidogo alichokiegesha mwilini mwake kabla hajakivaa kabisa pale alipofika kwa Fred.

“Mmmh!Haya bwana,sina cha kusema juu ya hilo.”Eve alikata kinywa cha Fred kwa kukubaliana na maneno yake.

“Sasa nadhani twaweza kwenda Malaika wangu.”Fred aliongea huku akiingiza mkono wa kulia kwenye mkono wa kushoto wa Eve kama wafanyavyo maharusi au waalikwa wawili wa jinsia tofauti wanapoingia kwenye tafrija mojawapo kubwa waliyoitwa.

Ilikuwa ni tayari saa mbili na dakika kadhaa za usiku na ilionesha wazi Eve alikuwa si wa kupanda gari hata pale Fred alipomba wafanye hivyo. Haikujulikana kwa nini,ila Eve alisema anajiona yupo vizuri kifuraha kama watatembea kwa miguu hadi huko wanapoenda.

Dakika thelathini za mwendo wao wa taratibu na wa madaha,tayari walikuwa wameshafika eneo moja la wazi lakini lenye mgahawa mkubwa ambao siku kama ile,kulikuwa kuna watu wengi sana hadi wengine wanakosa sehemu za kukaa.
Kwa kuwa wakina Eve walichelewa kiasi chake,walikuta nafasi nyingine zipo wazi kwa wale wa mwanzo kuondoka.

Walichagua nafasi moja nzuri na yenye mwanga ili waonekane hasa kwa mavazi waliyovaa usiku ule. Yalihitaji sana mwanga ili yavutie zaidi. Lakini kama Fred angelijua kitachomtokea,sidhani kama angechagua kwenda kwenye mgahawa mkubwa kama ule,na kuchagua sehemu yenye mwanga kama pale.
Lakini yote yalibaki kuwa kama ningeli……,basi ningeli….. Yalibaki kuwa majuto tu!
*********
“Unapaonaje hapa Malaika wangu.”Fred alianzisha maongezi baada ya kukaa mahala panapostahili na kumsubiri mhudumu kwa ajili ya kuagiza wanachohitaji.

“Oooh Fred,it is fantastic.”Alijibu Eve huku akiutazama mgahawa ule juu na pembeni kama unauthaminisha.

“Mmh Malaika wangu.Mi mwenyewe najua Kiingereza lakini sipendi sana kukitumia nikiwa na wewe. Napenda tutumie Kiswahili zaidi,kwani tunakuwa huru kuelewana kuliko kutumia vingereza ambavyo havina maana sana katika maongezi yetu.”Alisahihisha Fred baada ya Eve kutumia lugha ya Kiingereza katika maongezi yao.

Ni kweli Fred hakuwahi kutumia lugha nyingine akiwa na Eve,hiyo pia inakuweka vizuri katika mahusiano yako. Si njema sana kuchanganya lugha pale unapokuwa na msichana ambaye unahitaji uwe naye katika mahusiano.

Hali ya kuchanganya lugha uwapo na msichana au mwanamke,inatengeneza maono tofauti katika kichwa cha mtu uliyenaye kwa wakati huo. Na zaidi utaonekana kama unadharau sana hasa pale mtu uliyenaye kumbe shule ilimpiga ngumi katika maisha yake na hajawahi kusomea lugha unayoitumia.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (23)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

“Unapaonaje hapa Malaika wangu.”Fred alianzisha maongezi baada ya kukaa mahala panapostahili na kumsubiri mhudumu kwa ajili ya kuagiza wanachohitaji.

“Oooh Fred,it is fantastic.”Alijibu Eve huku akiutazama mgahawa ule juu na pembeni kama unauthaminisha.

“Mmh Malaika wangu.Mi mwenyewe najua Kiingereza lakini sipendi sana kukitumia nikiwa na wewe. Napenda tutumie Kiswahili zaidi,kwani tunakuwa huru kuelewana kuliko kutumia vingereza ambavyo havina maana sana katika maongezi yetu.”Alisahihisha Fred baada ya Eve kutumia lugha ya Kiingereza katika maongezi yao.

Ni kweli Fred hakuwahi kutumia lugha nyingine akiwa na Eve,hiyo pia inakuweka vizuri katika mahusiano yako. Si njema sana kuchanganya lugha pale unapokuwa na msichana ambaye unahitaji uwe naye katika mahusiano.

Hali ya kuchanganya lugha uwapo na msichana au mwanamke,inatengeneza maono tofauti katika kichwa cha mtu uliyenaye kwa wakati huo. Na zaidi utaonekana kama unadharau sana hasa pale mtu uliyenaye kumbe shule ilimpiga ngumi katika maisha yake na hajawahi kusomea lugha unayoitumia.

SASA ENDELEA...

Kingine utatengeneza ile kauli ya kujifanya unajua sana lugha fulani kuliko lugha ya ulimi wa mama yako. Hisia kama hizo si nzuri kama zikitengenezwa kwenye kichwa cha mwanamke uanayemtaka.

“Mh!Hapo kweli,umeniambia jambo la maana.Mimi kama mwanafunzi wa uandishi wa habari wa nchi hii,sipaswi kutumia lugha kwa kuchanganya changanya hasa pale napoulizwa swali kwa lugha fulani na mimi najibu kwa lugha tofauti niliyoulizwa nayo. Hapo sibishi Fred wangu.”Aliongea Eve huku akiwa anatabasamu lisiloishiwa unyevunyevu unaosababisha kutokauka kwa tabasamu lile.

“Nashukuru Malaika wangu kwa kuelewa hilo.”Alishukuru Fred na wakati huo muhudumu nadhifu wa mgahawa ule alikuwa kaja na kuwapa menu ya chakula wafanye yao.

Baada ya dakika kadhaa,tayari chakula walichokuwa wameagiza kilishakuja mezani kwao.Kitendo bila kupoteza muda,Fred alijivuta kwa mbele ya kiti alichokalia huku kitendo kile kikiwa kama ndio kinamalizia ule mpasuko wa vile vinailoni viwili alivyokuwa kawaviweka Hans mfukoni mwa suruali ya Fred.

Kile kinailoni cha kwanza chenye maji,tayari kilishapasuka muda mchache baada ya Fred kujivuta vuta kwenye kiti chake.Na ule ubaridi wa kimiminika kile Fred aliuhisi sema aliona aibu kuinuka kwa kuwa angeonekana kama kajisaidia haja ndogo.

Sasa wakati anajivuta kwa ajili ya chakula,ndipo kile kinailoni chenye unga nacho kilipopasuka na kusababisha sasa ule unga kuchaganyika na kile kimiminika ambacho kilikuwa bado hakijakauka kabisa kwenye suruali ya Fred. Hapo ndipo balaa lilianzia.

Wakati Fred anaendelea kujilia chakula alichoagiza,mara alianza kuhisi umoto moto kwenye makalio yake. Mara ya kwanza alidhani labda ni kiti au kuna moto karibu yake,lakini alipoangalia kulikuwa hamna hali hiyo na wala kiti alichokalia kilikuwa hakina uwezo wa kupitisha joto alilolihisi.

Alitaka kusimama ili ajikague lakini aliona aibu kutokana na ule umajimaji uliokuwa katika suruali yake.Ikabidi avumilie lakini uvumilivu ule ulikuwa kama unazidi kuchochea hali ya joto kuongezeka pale alipokalia.

Taratibu Fred alianza kuona chakula kichungu na kiti kikawa kama kina upupu kwa jinsi alivyokuwa anasota kwa kwenda mbele huku makalio yake yakiwa msaada mkubwa wa kufanya hayo yote. Lakini kama angejua,angesipoendelea kufanya vile,kwani joto lilizidi maradufu ya pale mwanzo.

Masikini Baba Paroko au Mzee wa Upako,uso ukambadilika ukawa kama kasikia habari mbaya eidha ya msiba au mlipuko wa mabomu kama yale ya Mbagala.

“Vipi Fred wangu,mbona amani hamna?.”Aliuliza Eve baada ya kuona uso wa Fred umekosa amani.
“Hamna Malaika wangu,sema najihisi vibaya kidogo.”Fred aliongea huku akilazimisha tabasamu lakini hali ya makalio yake,alikuwa anaijua yeye.

“Tumbo linauma?.”Eve aliendelea kuuliza maswali kutokana na muonekano aliokuwa nao Fred. Hakika alipaswa kuuliza swali la namna ile kwa maana uso ulikuwa unakunjwa na kukunjuka kama anajisaidia kweli uwani.

“Daah! Eve nakufa.”Fred aliongea kwa sauti ya chini lakini iliyojaa uchungu mkubwa wakati anaitoa.
Mwanamke wa shoka,Eve alijua mambo yameharibika kweli,hadi kaitwa jina lake halisi na mtu ambaye hajawahi kumuita hivyo.Kweli jamaa alizidiwa nusura ya kufa.
Lakini aibu yake ndio ilimponza kwani aliona aibu kunyanyuka licha ya maumivu yaliyikuwa yamamsurubu.

Eve alinyanyuka na kwenda hadi kwa Fred alipokuwa amekaa na kumshika bega huku akijaribu kumnyanyua kichwa alichokuwa kakilaza juu ya meza.
“Fred vipi?.”Eve aliuliza.
“Naungua.”Fred naye alijibu huku akionesha wazi anaemia kwa kuungua.
“Wapi sasa.”Eve naye akawa anasaili kwa makini akifata vitendo vya Fred.
Fred hakuwa na jinsi tena kwani hali ilikuwa mbaya sana kwake. Akamuonesha pale alipokuwa amekalia kuwa ndipo panamuunguza.

Eve kwa haraka alimuomba anyanyuke bila kujua hali ambayo ingetokea baada ya Fred kunyanyuka.

Fred kwa shida na uvumilivu uliomshinda,alianza kunyanyuka taratibu na wakati huo umati mkubwa ulikuwa unaangalia ile filamu japo walikuwa hawaelewi ni nini kinaendelea.

Fred akanyanyuka na kusimama wima. Dah! Kilichoonekana ni zaidi ya wengi walivyodhani.
Ile suruali aliyokuwa kaivaa ilikuwa kama karatasi lililoungua,na hatari zaidi ni pale Eve alipojaribu kuikung’uta kwa nyuma ile suruali.

Ni majivu pekee ndiyo yaliweza kumwagika pale suruali ilivyokung’utwa.Na kibaya zaidi ule mchanganyiko wa Hans uliweza kula nguo ya nje hadi boxer la Fred kwa sehemu kubwa sana na kufanya hata makalio ya Fred kuonekana.

Ilikuwa ni ahueni kwa Fred kwani maumivu ya kuungua yalipungua lakini shughuli ilibaki kwa wale waliokuwa wanashuhudia lile tukio. Wengi wao walicheka sana tena sana.

Fred aliona jambo la msingi ni kufunga koti lake kiunoni ili kuficha ile hali yake. Na baada ya hapo alitoka mahala pale haraka na kwenda mahala kumsubiria Eve ambaye naye chakula kilikuwa kichungu japo alikilipia kwa haraka.

Baada ya kukilipia chakula kile,Eve alitoka kwa kasi kumuwahi Fred ambaye alikuwa hajielewi elewi ni nini kimemtokea kwa muda mfupi ule aliokutana na Eve.
Huku nyuma baada Eve kuondoka,wahudumu wa pale walienda kwenye meza waliyokuwa wamekaa wakina Fred na kutaka kutoa vyombo lakini bila kutegemea Hans na Junior walifika kwenye meza ile na kukataza ule msosi kutolewa.

Hans na Junior walikuwa ni watu ambao hawana aibu kabisa.Hivyo wale wahudumu walipotaka kubisha,wakina Hans walianza maneno ya kejeri yaliyowafanya wale wahudumu wawili kuondoka kwa aibu.

“Yaone kwanza.Kumbe kazi yao kula vyakula wanavyoacha wateja,leo mmenoa.Tunakichukua na kusepa nacho.Hayooo,shutuuu!.”Maneno yalimtoka Hans baada ya wale wahudumu kukubali yaishe na kuanza kuondoka eneo lile.
Hans na Junior walifanya kazi ya haraka sana kwa kuchukua kile chakula na kukimwagia kwenye mifuko misafi na baada ya hapo,walikimbilia bodaboda walizokuja nazo na kupotea eneo lile wakiwaacha baadhi ya wateja hoi kwa vicheko na wengine kukarahika na vile vitendo visivyo na aibu kutoka kwa watu wazima kama wale wakina Hans.
*****
Kwa upande wa Eve na Fred,wenyewe walichukua usafiri binafsi wa taksi na kuwapeleka katika makazi yao.

Ndani ya taksi ile,Fred alikuwa kachanganyikiwa kwa hali iliyomtokea na aliona aibu sana kumuangalia Eve. Hata pale Eve alipofika makazi yake,Fred hakuthubutu kumwangalia usoni bali alimuaga kwa ishara ya mkono tu,bila kusema.
Safari ya kupelekwa makazi yake yalipo,ikaanza na hapo ndipo amani ya moyo ilipomrudia na kuanza kufikiria filamu nzima ya kilichomtokea.
“Hans.”Aliongea Fred baada ya kufikiria kidogo.
“Huyu ni Hans mjinga yule. Yaani Hans kanifanyia hivi kweli?.”Fred aliongea kwa sauti na kumfanya dereva wa taksi aliyopanda kumtazama kwa makini kwa kupitia kioo cha dereva kile cha juu.Maana alidhani mteja wake anaweza kuwa mwehu na kusababisha mambo mengine ndani ya gari.

“Kwa hiyo kanifanyia hivi kunikomoa au kisasi? Yaani huyu Hans kweli ananiabisha mimi? Mimi!!? Kabisa mbele ya umati wa watu, watu zaidi ya mia wameona makalio yangu. Kweli kabisa Hans unaniabisha mbele ya Eve? You will pay for this.”Fred aliongea kwa uchungu lakini yule dereva wala hakuingilia bali kuwa makini tu!Mtu wake asimkabe kama atapandisha ukichaa wake.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (24)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

Ndani ya taksi ile,Fred alikuwa kachanganyikiwa kwa hali iliyomtokea na aliona aibu sana kumuangalia Eve. Hata pale Eve alipofika makazi yake,Fred hakuthubutu kumwangalia usoni bali alimuaga kwa ishara ya mkono tu,bila kusema.
Safari ya kupelekwa makazi yake yalipo,ikaanza na hapo ndipo amani ya moyo ilipomrudia na kuanza kufikiria filamu nzima ya kilichomtokea.
“Hans.”Aliongea Fred baada ya kufikiria kidogo.
“Huyu ni Hans mjinga yule. Yaani Hans kanifanyia hivi kweli?.”Fred aliongea kwa sauti na kumfanya dereva wa taksi aliyopanda kumtazama kwa makini kwa kupitia kioo cha dereva kile cha juu.Maana alidhani mteja wake anaweza kuwa mwehu na kusababisha mambo mengine ndani ya gari.

“Kwa hiyo kanifanyia hivi kunikomoa au kisasi? Yaani huyu Hans kweli ananiabisha mimi? Mimi!!? Kabisa mbele ya umati wa watu, watu zaidi ya mia wameona makalio yangu. Kweli kabisa Hans unaniabisha mbele ya Eve? You will pay for this.”Fred aliongea kwa uchungu lakini yule dereva wala hakuingilia bali kuwa makini tu!Mtu wake asimkabe kama atapandisha ukichaa wake.

SASA ENDELEA...

Baada ya dakika kadhaa,hatimaye taksi ilifika yalipomakazi yake. Fred akashuka na kumlipa yule dereva ujira wake kisha huku akiwa na koti lake kiunoni kama mtoto wa shule ya msingi,alianza kuelekea kilipochumba anachoishi na wenzake.

Alipofika,alifungua mlango na kuwasha taa. Aliwaona rafiki zake wote wakiwa wamelala na wengine kama Hans kukoroma kabisa

Alichofanya Fred ni kuanza kuwaamsha wenzake kwa kuwatingisha na kuwaita kwa kuwapigia kelele.

“Oya nini bwana?Tunakatishana stimu.”Hans aliongea huku akifikicha macho yake baada ya kuamshwa.

“Pumbavu wewe. Wewe wa kunifanyia vile Hans?.”Fred aliongea kwa hasira huku akimuangalia Hans kwa jicho la kummeza mtu.

“Nimefanyaje Baba Paroko?.”Hans aliongea kama kweli hajui kitu.
“Linajifanya halijui boya hili,umeliona linajifanya eti halijui lilichofanya.”Fred alizidi kuongea na safari hii alikuwa anaongea huku anawageukia kwa zamu wakina Junior na Suarez.

“Kwani kafanyaje Mzee wa Upako?Mbona hatukuelewi? Halafu mbona koti umelifunga kiunoni? Au ndio umemvalia kibwebwe mwanaume mwenzako toka huko ulipotoka.”Aliongea Suarez na kumfanya Hans uvumilivu wa kucheka kumshinda.

“Si unaona hili boya linacheka?Linajua lilichofanya.”Fred aliongea kwa jazba na kwa sauti ya juu.
“Kafanyaje kaka?Mbona hufunguki?.”King Junior Nickson naye aliuliza.

Mara Fred akafungua lile koti lake na kulitoa kisha akawageukiwa kwa kuwapa mgongo Hans na Suarez waliokuwa wamelala upande mmoja.

“Hapa umeridhika nini boya wewe?Nakuuliza umeridhika nini.”Ee bwana suruali yake ilikuwa imeungua tokea pale karibu na mkanda hadi huku chini karibu na magoti. Hakika ilikuwa ni kituko cha mwaka au cha siku ile maana hata makalio yake yalikuwa yanaonekana wazi bila kificho. Fred alikuwa kaaibika sana kwa kweli.

“Nakuuliza umefaidika nini hapa?.”Fred alizidi kuuliza huku bado kawapa mgongo Hans na Suarez.
Wakati anafanya hayo yote,Emmanuel Suarez,yeye alikuwa katika taharuki kubwa kutokana na kile alichokuwa anakitazama.
Kinyume na hapo,kwa upande Hassan Jenge,yeye alikuwa kaishiwa nguvu kwa sababu ya kucheka kicheko ambacho kilikuwa kimevutwa kwa muda mrefu na kikakauka kabisa. Ni kama mtoto mdogo pale anapoumia sana,kuna kilio fulani anakivuta hadi kinakauka,pale akiamua kukitoa nje sasa,ni kama filimbi.

Sasa na kwa Hans ilikuwa hivyo,alikivuta kile kicheko kwa ndani na pale alipokitoa nje,ama kweli kilikuwa kicheko cha nguvu.
“Umeona boya hili linacheka.”Fred aligeuka na kuanza kumfata Hans pale alipo kwa hasira. Wakati anafanya hivyo,ndipo pia alipompa fursa Junior na yeye kujionea majanga yaliyokea katika suruali ya rafiki yake.
Naye bila kusita akaangua kicheko cha nguvu.

Fred alimfata Hans pale kitandani na kuanza kumsukuma sukuma wakati huo Hans alikuwa anagalagala kitandani hana mbavu.
“Nakwambia wewe boya leo utaniambia nimekukosea nini.”Fred aliongea kwa hasira huku anamvuta Hans aliyekuwa hajiwezi kwa kicheko.
Wakati anafanya hayo ya kuhangaika kumvuta Hans pale kitandani,huku nyuma Junior alikuwa anazidi kuwa hoi kila alipoangalia kile kilichokuwa kinatokea nyuma ya suruali ya Hans. Hakuwa mvumilivu kwa kubana kicheko bali kukiachia kwa nguvu zake zote.

“We boya nakwambia hapa utashuka mwenyewe, boya wewe.”Fred aliendelea kumvuta Hans aliyekuwa kalegea kwa kicheko.

Hali hiyo ya Fred kumvuta Hans iliendelea kwa muda wa dakika zisizopungua mbili na zilikwama pale Fred alipochana fulana iliyokatwa mikono,mali ya Hans.

“Baba Paroko umenichania Tisheti langu kwa sababu ya ujinga wako,si ndio eeh.”Hans aliongea huku kakunja uso kuonesha kachukizwa na kile kitendo.

“Nakwambia we boya leo nakuchania hadi boxer lako. Utanieleza nimekufanya nini.”Fred aliendelea kumvuta Hans pale kitandani bila kujali kama kishaifanyia unyambirisi fulana ya Hans.

“Kwani Fred ilikuwaje kaka hadi ikatokea hayo yote? Mbona unamvuta tu jamaa kama alikuwa kwenye mambo yenu?.”Suarez alimuuliza Fred baada ya kuona zogo linazidi kuwa kubwa.

“Labda unisaidie kuuliza wewe kaka maana hadi nachaniwa shati hapa bila kosa.”Hans alijibu huku akijeweka mbali na Fred kwa kujisukumia ukutani kabisa mwa kitanda chake.

“Unajua nini Sua (Shua),huyu jamaa kaniwekea makemiko kwenye mifuko ya suruali yangu. Sasa nimefika pale tulipopanga kufika,tukakaa kwenye viti,mara nikaanza kuungua………”Fred hakumalizia Suarez anayehadithiwa akamkata ulimi.

“Ulifika mlipopanga,ilikuwa wapi? Mbona unaongea mafumbo? Kama ni kwenye moto ndipo mlipofikia,sasa kwa nini usiungue?.”Suarez aliongea na kumfanya Hans aanze kucheka tena.

“Wewe Sua vipi? Gentleman ahadithii mambo yake.Au umesahau?.”Junior aliongea huku akiwa naye anacheka balaa.

“Umeona ee Junior. Gentleman ahadithii ishu zake hata kidogo,ha ha haaaa. Unaleta mambo ya kwenye video hapa.”Hans aliongea huku akiwa anazidi kujisogeza mbali na Fred aliyekuwa kajaa gesi ya hasira nusura ya kupasuka.

“Ha ha haaaaa, Think Like A lady…..”Junior aliongea na kumuoneshea kidole Hans amalizie ile sentensi.

“Act Like A Man…. Ha ha ha haaa,jamaa alikuwa anajidai Dremer.”Hans naye alimalizia sentensi ile huku akimfananisha Fred na Dremer,jamaa mmojawapo aliyeigiza filamu ya Think like a lady,Act like a man. Filamu ambayo Fred alikuwa anaingalia sana na kuigiza vitendo vya mule kwa Eve.

“Embu acheni washikaji. Mwanangu Fred endelea ili tujue kama ni kweli au si kweli,ikibidi Eve aitwe na aambiwe hii ishu.”Suarez aliongea akimwambia Fred aliyekuwa kasimama katikati ya chumba kama anawanga.

“Mwanangu nilienda na mtoto hotelini……”Kabla hajamaliza Junior akadakia tena.

“Hotelini wapi? Pale mgahawani bwana.”Junior akaropoka.

“Kumbe na wewe boya unahusika,Junii na wewe unahusika kweli kwenye hili? Aisee kweli mlikamia”.Fred aliongea kwa uchungu hadi Suarez ilim-bidi ainuke na kushuka kule juu anapolala na kumkalisha kwenye kiti kimojawapo wanachosomea mule ndani.

“Sisi tulienda kununua msosi ndio tukaona picha zima,wala mimi sijui kilichokuwa kinaendelea. Eti Sua hatujakuaga kuwa tunaenda ule mgahawa kuchukua chakula?.”Junior alijitetea.

“Waliniaga mwanangu,na wala mi mwenyewe sijui kama ulikuwa umeenda kule.”Suarez alimpunguza munkari Fred ulioanza kujaa juu ya Junior.

“Aaag,kwanza mmeongea kuhusu chakula,mimi nimeshikwa na njaa ghafla.”Hans alinyanyuka na kufuata kabati lake ambapo alilifungua na kuibuka na sinia moja kubwa kiasi.Akaliweka juu ya meza ya kusomea iliyokaribu kabisa na alipokaa Fred.

Baada ya zoezi hilo dogo la kuweka sinia juu ya meza,akapekua tena kwenye kabati lake na kuchomoa mfuko mweusi uliokuwa umenona kwa nje kutokana na chakula cha ndani kuwa na mafuta sana.
Akafungua mfuko ule na kumwagia kilichomo kwenye sinia lilipomezani.

Ghafla hali ya chumba kile ilibadilika na kupambwa na harufu nzuri ya chakula kile kilichowekwa kwenye sinia.
Lakini hali pia ilim-badilika Fred na kuwa ya taharuki zaidi. Midomo ilim-baki wazi na macho yakiwa yamekodelea kile chakula hali ambayo baadaye ilizidi kubadilika kwa midomo kutaka kuongea lakini ilishindwa na kubaki vidole kuoneshea kile chakura kilicho-mezani,ungemuona ungesema huyu jamaa ni bubu.
Hali hiyo haikumfanya Hans kujichukulia paja na kuanza kulitafuna kwa uchu. Hapo hapo na Junior aliinuka toka kwenye kitanda chake cha chini na kwenda kujichukulia kilichopo kwenye sinia lile la Hans.

“Nimekitolea jasho hiki.Kupambana na wale wahudumu hadi kukipata wadhani jambo dogo lile.”Junior aliongea huku akishika mgongo wa kuku na kuanza ku-usosomola.

“Fred vipi kaka,mboa hivyo?.”Suarez alimuuliza Fred baada ya kumuona hana la kuongea bali kushikwa na kigugumizi.

“Chakula chetu,mimi na Eve.”Fred aliongea huku machozi kama yanataka kumtoka.

“Sasa nyie mliacha chakula chote hiki,nyie vipi?Na bahati yenu vinywaji hamkununua.”Hans hakuwa nyuma kuongea japo alikuwa anabugia tambi kwenye kinywa chake.

Fred hakuvumilia hali ile. Yaani kuaibika, ka-aibika, chakula kimelipiwa bila kuliwa. Halafu mbaya zaidi wanao-kila ndio hao waliomuaibisha. Haikuwezekana kukubalika kwenye kichwa cha Fred.
 
SIMULIZI: THE LOST BOYS (25)

MTUNZI: FRANK MASAI

MAWASILIANO: 0752353039

****ILIPOISHIA*****

Hali hiyo haikumfanya Hans kujichukulia paja na kuanza kulitafuna kwa uchu. Hapo hapo na Junior aliinuka toka kwenye kitanda chake cha chini na kwenda kujichukulia kilichopo kwenye sinia lile la Hans.

“Nimekitolea jasho hiki.Kupambana na wale wahudumu hadi kukipata wadhani jambo dogo lile.”Junior aliongea huku akishika mgongo wa kuku na kuanza ku-usosomola.

“Fred vipi kaka,mboa hivyo?.”Suarez alimuuliza Fred baada ya kumuona hana la kuongea bali kushikwa na kigugumizi.

“Chakula chetu,mimi na Eve.”Fred aliongea huku machozi kama yanataka kumtoka.

“Sasa nyie mliacha chakula chote hiki,nyie vipi?Na bahati yenu vinywaji hamkununua.”Hans hakuwa nyuma kuongea japo alikuwa anabugia tambi kwenye kinywa chake.

Fred hakuvumilia hali ile. Yaani kuaibika, ka-aibika, chakula kimelipiwa bila kuliwa. Halafu mbaya zaidi wanao-kila ndio hao waliomuaibisha. Haikuwezekana kukubalika kwenye kichwa cha Fred.

SASA ENDELEA...

Hali hiyo ya kutovumilia,ilimfanya Fred akwapue lile sinia kwenye vidole vilivyokuwa vinaendela kufakamia ule msosi wa ghari,aliougharamia mpenzi wake kwaajili yake.

“Pumbavu zenu,sasa ole wake boya asogee.”Fred aliongea huku anaelekea pembeni na sinia lile la chakula kwa lengo la kukila peke yake.

“Mwanangu na sisi tumeweka chakula chetu humo,kwani chenu kilikuwa kingi hivyo.”Junior aliongea huku akimfata Fred kule ukutani alipoenda.

“Nitakumwagia hizi tambi,kuku na haya makachumbali usoni na hutonifanya kitu,nisogelee sasa.”Baba Paroko aligeuka gaidi kwelikweli.
Junior ilibidi harudi nyuma hasa alipofikiria muwasho wa ile kachumbali mdomoni,sasa anaambiwa atamwagiwa usoni.

Fred akawa m-babe mule ndani. Akachukua paja moja la kuku na kumrushia Suarez,naye Suarez akalidaka na kulitia mdomoni kwake.
Fred akageukia ukutani na wakati huohuo akawapa wakina Hans mgongo na kuwafanya waone ile suruali ilivyokuwa imeharibika.Kicheko kikaanza kwa kasi ya ajabu lakini Fred hakujali zaidi ya kuendelea kula huku akicheza taratibu na kukata kiuno kwa mbali. Hasira zikamuisha kihivyo maana angeendelea kuwa na hasira hizo,ingekuwa hasara kwake. Cha msingi aliona bora asahau,lakini si kwamba alisahau kabisa.
*****
Kesho yake waliamka wenye furaha kama jana yake usiku kulikuwa hakujatokea kitu. Walikuwa ni watu wenye amani kupitiliza huku ikionekana wazi hakuna kisasi baina yao.

Lakini ajuaye moyo wa mwanadamu una nini,ni yeye mwenyewe binadamu pamoja na MUNGU wake.
Moyo wa Fred ulikuwa haujafurahia kabisa kile kitendo alichofanyiwa na Hans. Pia alikuwa kampatia sana hasira Junior kwa kuwa mshirika wa Hans. Hayo yote aliyaweka moyoni na kuyapangia mkakati kabambe wa kuyalipa.

Bila wale jamaa zake kujua yaliyo-moyoni mwake.Fred alionesha mwenye amani na furaha kila wakati huku akiwa mstari wa mbele kukumbushia kilichomtokea jana.
****
Siku nne mbele toka siku ya tukio la Fred,ilikuwa ni zamu ya Junior kukutana na Eve. Fred alifahamu hilo,hivyo akaanza kutafuta njia za kulipa kisasi kwa alichofanyiwa na wale rafiki zake.

Aliangaika sana na mwisho wake aliona ni bora aende kwa wagumu kuomba msaada kwani Junior alionekana ni mtu makini sana kwenye mambo yake.

Haikuwa rahisi kwa Junior kuacha nguo zake hovyo,wala kabati lake. Kifupi alizidisha umakini hasa kila alipofikiria tukio lililomtokea Fred. Sasa Alfred aliamua kuomba msaada kwa Wagumu,walewale aliowahi kuwaabisha walipofika chuoni kwa mara ya kwanza. Ndio walewale wakina Moi Shabala,Kamanda wao Ban Diho na Sunday Magembe.

“Kwa hiyo mkuu unatakaje sasa.”Kamanda wa Wagumu,Ban Diho alimuuliza Fred baada ya Fred kutoa mkasa mzima ulimkuta.

“Nataka boya naye aibike mbele ya mtoto kama mimi nilivyoaibika.”Fred aliongea kwa hamasa juu ya nia yake

“Basi usijali. Cha msingi taarifa umetupa,sisi tutapiga kazi kama kawaida ila yapasa uache kitu hapa,hatupigi kazi bila mshiko,si wajua sisi makamanda.”Ban aliongea kwa makini huku akimwangalia usoni Fred aliyewafuata chumbani kwao.

“Hilo usijali,nyie niambieni kiasi mnachotaka.”Fred alizidi kujiingiza kwenye dhamira yake ya kisasi.
Kwa kuwa wale jamaa walikuwa na kisasi na lile kundi la akina Hans,waliamua kuutumia mwanya huo kulipa walichowahi kufanyiwa.

“Hapo utaacha elfu hamsini mwanangu.”Ban alimjibu Fred na kumuacha kinywa wazi.

“Kaka mbona kitu kidogo sana lakini umekaza hivyo. Au unaenda kuua? Sitaki mauaji,nataka aibike tu!.”Fred alishindwa kuzuia hisia zake juu ya ile bei aliyotajiwa na Ban.

“Hafi mtu hapa jembe langu. Tunataka kukufanyia kazi ya uhakika. We mwenyewe si wacheki makamanda tupo wangapi? Huyo dogo ataaibika mpaka mwenyewe utakuja na kutuongeza elfu hamsini nyingine. Ila kwa sasa,sisi tunataka hiyo fifte halafu kazi nzima tutaifanya wenyewe hadi iishe.”Ban alizidi kumvuta Fred ili amuingize kitanzini kwa ile hela aliyomtajia kama gharama.

“Fanyeni elfu thelathini basi,hiyo hamsini mimi sina.”Fred alibembeleza jambo kana kwamba anachotaka kufanya ni sheria iliyoruhusiwa na tume yakutunga sheria hapa nchini.

“Kama utataka kwa bei hiyo,itabidi na wewe uwemo kwenye mchakato huo. Sisi tutakutafutia kila kitendea kazi,halafu utakamilisha kazi hiyo we mwenyewe.Unasemaje.”Ban alikuwa mkavu na mwenye msisitizo wakati anaongea hayo.

“Mazee,mimi yamenishinda na ndio maana nimekuj kwenu. Nisaidieni bwana.”Fred alizidi kubembeleza huku shingo yake kaiweka upande kuwasilisha bembelezo lile.

“Sikiliza kamanda Fred,sisi tutakupigia kazi ya maana ambayo hutatambulika kama ni wewe bali yule Hans. Na kama Junior atamshuku yule,ni lazima atataka kulipa kisasi. Sasa wewe ndiye utatuletea mteja huyo. Na yeye tutampa bei kama yako,na kama yawezekana tutaipandisha juu iwe kama elfu sabini au laki moja. Wewe ndio utakuwa unamsukuma ili alipe kiasi hicho,tena ikibidi mkopeshe kiasi kilichozidi.

Akitulipa,sisi tunakata elfu hamsini yetu,kile kilichozidi tunakupa wewe kama shukrani ya kutuletea mteja. Hapo vipi kamanda.”Safari hii aliongea Moi Shabala kibiashara zaidi.

“Hapo haina noma. Basi nipeni nusu saa kwanza nikafanye mambo benki.”Fred aliomba ruhusa na kutoka chumbani kwa akina Ban akiwa ameridhika na maamuzi yake juu ya kulipa kisasi kwa Junior.
*****
Alienda benki na kufanya muhamala wa fedha kwa kiasi cha shilingi elfu sabini. Elfu ishirini aliweka pembeni na elfu hamsini akaiweka mahala kwingine. Hapo tayari akawa amekamilisha kazi iliyompeleka benki na akawa tayari kwa ajili ya kuingia vitani,vita ya kijinga kabisa kuwahi kutokea katika maisha ya mwanadamu wa leo.

Baada ya dakika zisizopungua arobaini,Fred alikuwa chumbai kwa akina Ban akifanya makabidhiano ya fedha zile alizoenda kuzichomoa benki.

“Mzigo ndio huo hapa wazee. Nataka kazi ifanyike bila mimi kujulikana, na pia nataka siku ya tukio na mimi mnitaarifu ili niwepo eneo hilo nione kitakachotokea.”Fred alikuwa anatoa kiasi cha fedha huku anaongea hayo.

“Hamna shaka hata kidogo. Deal done.”Ban alikamilisha maongezi huku akikabidhi noti tano nyekundu,fedha halali kwa malipo nchini Tanzania kwa Sunday Magembe aliyekuwa katoa tabasamu la pongezi kwa kamanda wao,Ban.

“Basi fresh. Mambo yote ni kesho. Dogo ndio anaenda kukutana manzi. Fanyeni yenu kama kawa.”Fred aliweka hitimisho juu ya maongezi yale na kutoka nje chumba kile akiwa na uhakika wa kazi yake kufanyika bila zengwe wala kokoro.
Ama hakika alipania kufanya kisasi,kitendo cha kutoa kiasi kile cha fedha kwa ajili ya kumuaibisha mwenzako,ni kitendo cha kijasiri sana kupata kutokea kwenye dunia ya sasa,dunia iliyojaa vituko kila kona ya pembe zake. Yote yanabaki kuwa siri yake,hakuna aliyepaswa kujua kama analipa kisasi zaidi ya wale aliyowapa kazi ile.
*****
Huku nyuma baada ya Fred kuondoka,Ban alipanga jeshi lake kwa ajili yakutimiza kazi waliyokuwa wamekabidhiwa na Fred,kazi ya kuhakikisha Junior anaaibika mbele ya umati wa watu.

“Umeona maboya hayo? Sasa ni muda wa wao kuaibika,walidhani tumesahau ya siku zile? Sasa hapa ni kuwafanya waaibike bila sisi kugundulika. Yaani tunacheza chezo huku tunawapakazia wao. Tunakula hela,na bado tunawaabisha. Huo ndio mpango.”Aliongea kamanda mkuu wa chumba kile,Ban Diho.

“Hapo kamanda umecheza kama Pele. Naikumbuka sana ile siku tuliyotembea uchi. Mi kidogo nihame na chuo,ila nikajikaza kiume tu.”Moi Shabala naye aliongezea chachandu juu ya maongezi yale.

“Na hapo lazima ziwamwagike haswaa,si walijidai manunda. Sasa wamekutana na manunda square.”Ban aliongea kwa chuki iliyokuwa wazi kabisa.

“Ndio maana yake. Watajua wenyewe wakipigana,wakikatana mapanga,wakitishiana bastola na hata wakichinjana. Cha msingi sisi tupange jinsi ya kumwaibisha huyo dogo ili akome.”Mdomo wa Sunday nao haukuwa nyuma kudhibitisha kuwa yupo ndani ya wenzake na hawezi kuwatosa.

“Hapa watasanda tu!.Sisi ndio maji,ukishindwa kwa kutunawa,utatugida tu.”Ban alimaliza tambo zilizokuwa zinaendelea chumbani mule na sasa alikuwa kajiweka wima kwa jili ya kuanza kazi ya kuupanga mkakati uliokuwa umewatinga mbele yao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom