Mwanantogakulya
Senior Member
- Mar 18, 2025
- 154
- 153
MKUU wa Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, Dkt. Vincent Anney ameongoza juhudi zilizofanikiwa kuvunja ndoa ya kimila iliyokuwa imefungwa kati ya Mahene Kulwa na mwanafunzi aliyekuwa amechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka huu, baada ya kubainika kuwa aliolewa kwa mahari ya ng'ombe 15.
Tukio hilo lilitokea Julai 19, 2026 katika Kijiji cha Mwamashindike, Kata ya Budekwa, Wilaya ya Maswa. Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 19 alikuwa amechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano katika Shule ya Sekondari Nyalanja, Wilaya ya Meatu, na alitarajiwa kuanza masomo mwezi Julai mwaka huu.
Akizungumza leo Julai 23, 2026, Dkt Anney amesema vyombo vya ulinzi na usalama, hususan Jeshi la Polisi, vilifanikiwa kumkamata Mahene Kulwa pamoja na baba mzazi wa binti huyo, Shilinde Ntegwa, dada yake Felister Kulwa na washenga waliodaiwa kushiriki kufanikisha ndoa hiyo.
Akieleza , Mahene amesema kabla ya kufunga ndoa alimuuliza binti huyo kama alikuwa amemaliza shule, na alijibiwa kuwa hana uhakika wa kuendelea na masomo.
"Nilipokutana naye aliniambia amemaliza shule na hana uhakika kama atafaulu na kuendelea na masomo. Nikawashirikisha wazazi wangu, wakakutana na baba wa binti na wakakubaliana mahari ya ng'ombe 15 ndipo tukafanya harusi ya kimila," amesema.
Ameongeza kuwa siku ya harusi binti huyo alikuwa hajisikii vizuri, hivyo dada yake, Felister Kulwa, alivaa mavazi ya harusi na kukaa nafasi ya bibi harusi ili kuficha utambulisho wa mwanafunzi huyo.
Kwa upande wake, baba wa binti, Shilinde Ntegwa, amekiri kumuozesha mtoto wake kwa madai kuwa hakuwa na nia ya kuendelea na elimu ya Kidato cha Tano.
"Nilimuuliza kuhusu shule, akasema hataki kuendelea na masomo. Lakini kwa sasa ni lazima aende shule," amesema.
Hata hivyo, baada ya kuhojiwa na Dkt Anney mwanafunzi huyo amesema yuko tayari kuendelea na masomo ikiwa atapatiwa nafasi hiyo.
Dkt Anney amesema Serikali itahakikisha mwanafunzi huyo anarudi shuleni ili aendelee kutimiza ndoto zake za elimu.
Aidha, amewataka wazazi wilayani Maswa kuachana na mila na desturi zinazowakatisha wasichana masomo kwa kuwaelimisha kuwa elimu ndiyo msingi wa maendeleo yao na ya taifa.
"Inashangaza kuona walijua ni mwanafunzi, wakaamua kumweka dada yake avae mavazi ya harusi ili watu wasitambue. Nalishukuru Jeshi la Polisi kwa kushiriki operesheni hiyo na kuwakamata wote waliohusika," amesema.
Mwisho.
Tukio hilo lilitokea Julai 19, 2026 katika Kijiji cha Mwamashindike, Kata ya Budekwa, Wilaya ya Maswa. Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 19 alikuwa amechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano katika Shule ya Sekondari Nyalanja, Wilaya ya Meatu, na alitarajiwa kuanza masomo mwezi Julai mwaka huu.
Akizungumza leo Julai 23, 2026, Dkt Anney amesema vyombo vya ulinzi na usalama, hususan Jeshi la Polisi, vilifanikiwa kumkamata Mahene Kulwa pamoja na baba mzazi wa binti huyo, Shilinde Ntegwa, dada yake Felister Kulwa na washenga waliodaiwa kushiriki kufanikisha ndoa hiyo.
Akieleza , Mahene amesema kabla ya kufunga ndoa alimuuliza binti huyo kama alikuwa amemaliza shule, na alijibiwa kuwa hana uhakika wa kuendelea na masomo.
"Nilipokutana naye aliniambia amemaliza shule na hana uhakika kama atafaulu na kuendelea na masomo. Nikawashirikisha wazazi wangu, wakakutana na baba wa binti na wakakubaliana mahari ya ng'ombe 15 ndipo tukafanya harusi ya kimila," amesema.
Ameongeza kuwa siku ya harusi binti huyo alikuwa hajisikii vizuri, hivyo dada yake, Felister Kulwa, alivaa mavazi ya harusi na kukaa nafasi ya bibi harusi ili kuficha utambulisho wa mwanafunzi huyo.
Kwa upande wake, baba wa binti, Shilinde Ntegwa, amekiri kumuozesha mtoto wake kwa madai kuwa hakuwa na nia ya kuendelea na elimu ya Kidato cha Tano.
"Nilimuuliza kuhusu shule, akasema hataki kuendelea na masomo. Lakini kwa sasa ni lazima aende shule," amesema.
Hata hivyo, baada ya kuhojiwa na Dkt Anney mwanafunzi huyo amesema yuko tayari kuendelea na masomo ikiwa atapatiwa nafasi hiyo.
Dkt Anney amesema Serikali itahakikisha mwanafunzi huyo anarudi shuleni ili aendelee kutimiza ndoto zake za elimu.
Aidha, amewataka wazazi wilayani Maswa kuachana na mila na desturi zinazowakatisha wasichana masomo kwa kuwaelimisha kuwa elimu ndiyo msingi wa maendeleo yao na ya taifa.
"Inashangaza kuona walijua ni mwanafunzi, wakaamua kumweka dada yake avae mavazi ya harusi ili watu wasitambue. Nalishukuru Jeshi la Polisi kwa kushiriki operesheni hiyo na kuwakamata wote waliohusika," amesema.
Mwisho.