The Citizen You Can't Be Serious!! Nyie ni Gazeti Makini!!

The Citizen You Can't Be Serious!! Nyie ni Gazeti Makini!!

Kwa nini watanzania tunakuwa wavivu wa kufikiri kiasi hiki? Kama walivyotangulia kusema wengine kama unataka ukweli wa Kakobe si uende kanisani kwake?umeshaambiwa nenda kanisani kwake Jumapili saa nane wakati wa ibada ukaangalie kama yupo au la, kanisa liko wazi kila jumapili nenda kaangalie kwa macho yako kwa nini usiende kutafiti mwenyewe halafu ndio uje kubwa bwaja huku mtandaoni baada ya kudakia habari za mitaani za watu ambao hawajawahi hata kukanyaga pale kanisani wakati liko hapo Mwenge tu?

Asante ndugu yangu kwa kunisaidia kuwaambie maana wengine wanashabikia uongo na uzushi kama mazuzu, yaani we acha tu wanakera kwelikweli.
 
Wewe ESAM nyie so ndo mloleta uzi hapa ukimsifia Kakobe kwamba kafungua Minisrty huko Mareksni...Maajabu haya leo ndo nimesikia eti Kakobe Yupo tangia 2010.....Maajabu haya khaa...

Kha!!! Maajabu gani. Kilichopo Marekani ni ofisi ya Bishop Zachary Kakobe International Ministries waweza kutembelea website yake hapa: https://bishopzacharykakobe.org/en na hiyo ofisi wala hakufungua yeye bali watu wenye uchungu na kazi ya Mungu. Kwa habari zaidi kuhusu hiyo ofisi fuata link hapo juu website ina mawasiliano yote waweza pia kuwasiliana nao kule Revere, Boston - Massachusetts watakueleza mengi kuhusu Bishop Zachary Kakobe International Ministries.
 
Umeisoma kweli stori yenyewe au na wewe ni wale viuongozi vipofu wanaoongoza vipofu (Mathayo 15:13-14)? Binafsi nimeisona stori na nimeridhika Kakobe hayupo nchini na pale wanaweka mikanda. Kuna shida gani na report kama hiyo? Mtundu kisu, the citizen wameact very professional. Soma stori yao utaona ukweli na kama yupo, hawezi kujitokezea kupitia JF. Nakwambia ukweli kwani hayo unayoyasema yapu ndani ya stori kuwa akina Esam na wengine wanaomuamini hawako tayari kusema ingawa ukweli ndio huo.

Unachekesha ndugu Bwaga ya moyoni, yaani umeamini kwa kusoma uzushi huo au uliwahi kuja na kukuta mikanda inasikilizwa? Nilidhani wewe ni mtu makini kumbe ndo wale wale bendera fuata upepo. Nasisitiza hiyo habari hata kama inaonekana balance kwa kiwango chake, bado ni ya UONGO na UZUSHI, kabisa kwani baba yetu wa kiroho Mchungaji Zachary Kakobe tunaye na anaendelea kutulisha neno la Mungu kama kawaida.

Hapo kwenye red, sijui ni professionalism ya namna gani unayoongelea, labda kama ni ya kupika habari hapo sawa. Lakini kusema mwandishi amekuja pasaka akakuta ibada inaendeshwa na Mchungaji Hezron wakati ni uongo wa mchana kweupe. Kama kweli mwandishi alikuja basi inawezekana aliishia nje akamuuliza mtu mgeni lakini hata mgeni angemwambia hajui chochote. Yaani hata sijui nisemeje!!!
 
Usiridhike na kusikia jenga utamaduni wa kutafiti na kujua kitu wewe mwenyewe

Mkuu unaamini Kakobe amepoteza mvuto? Yaani amechuja wenzie walio kuwa chini wamempiga bao akina Lusokelo
 
Mkuu unaamini Kakobe amepoteza mvuto? Yaani amechuja wenzie walio kuwa chini wamempiga bao akina Lusokelo

Mkuu unashangaza kweli mvuto kwa nani, kwa Mungu au wanadamu? Yeye ni mtumwa wa Kristo anatafuta mvuto kwa Bwana wake tu. Na kwa taarifa yako ndo mvuto wake uko juu kuliko wakati mwingine wowote na unazidi kupanda kwa kasi sana
 
mie nashauri waumini wake mkiongozwa na esami muende MCT mkalalamike then ikibidi kakobe akafungue suit ya defamation.
 
mie nashauri waumini wake mkiongozwa na esami muende MCT mkalalamike then ikibidi kakobe akafungue suit ya defamation.

Wala hatutafanya hivyo ila kila mtu aliyejua issue hii ameona aina ya waandishi tulio nao jinsi walivyowababaishaji. Wengine wamemwita mwandishi huyo ni kanjanja wengine uchwara. Nadhani hiyo ni adhabu tosha siku nyingine hawatakurupuka au habari zote watakuwa makini kuhakikisha ziko sahihi kabla ya kuruhusu zichapishwe.

Mtumishi wa Mungu yuko busy na kazi ya Mungu hana muda wa kuvutana na watu wasiojua wanafanya nini.
 
Mkuu unaamini Kakobe amepoteza mvuto? Yaani amechuja wenzie walio kuwa chini wamempiga bao akina Lusokelo

Ndio maana tunasema watanzania ni wepesi kuropoka na wavivu wa kutafakari na kutafiti vitu na hii ndio sifa inayotufanya nchi zingine zipige hatua kimaendeleo kila siku wakati sis tupo pale pale kwa sababu sisi tumekaa kueneza majungu tu, mtumishi wa Mungu ambaye unasema amepoteza mvuto anapata mialiko ya kwenda kuhubiri mahali kama Toronto, Canada atakapohubiri June hii na waimbaji maarufu duniani kama Don moen na krystaal, angalia hapa https://bishopzacharykakobe.org/en/events/upcoming-events

Akisafiri kwenda katika mikutano ya injili anapokelewa kama Rais, Bishop Zachary Kakobe Grand Welcome in Zambia - YouTube ,
Revival in Burundi with Bishop Zachary Kakobe Pt 1/6 - YouTube, Bishop Kakobe statesman-like welcome in various nations - YouTube.

na mpaka wa marais wa nchi wanahudhuria mahubiri yake kama ilivyokuwa Burundi ambako Rais Pierre Nkurunziza alihudhuria katika moja ya mahubiri ya Askofu Kakobe alipofanya ziara ya mikutano ya injili, Revival in Burundi with Bishop Zachary Kakobe Pt 2/6 - YouTube ,Bishop Zachary Kakobe meets Former President of Zambia - YouTube, Bp. Kakobe meets DRC Provincial Governor Moise Katumbi - YouTube

Lakini kubwa zaidi maelfu ya watu wanahuduhuria mikutano hii injili wanasikia neno la Mungu la kuwaongoza kuishi maisha ya usafi na utakatifu mbali na dhambi na maelfu wanaokoka na kuwa mbali na dhambi na kuwa na nafasi ya kwenda mbinguni. achilia wale wanaoponywa na mahangaiko ya kila namna, angalia hapa Gentiles obey the Gospel by deed in Bp. Kakobe Crusades - YouTube , Bishop Kakobe's unprecedented Crusade in Lubumbashi-DRC - YouTube. Bishop Zachary Kakobe's unprecedented Crusade in Zambia - YouTube.

Kama ungekuwa umefanya utafiti kidogo tu wa kuangalia hizi video na kutenga hata jumapili moja ukaenda kanisani Mwenge, usingesema amepoteza mvuto.Kama amepoteza mvuto atakuwa amepoteza mvuto kwako wewe mwenye roho ya mpinga Kristo na wengine kama wewe wasiopenda Jina kuu kuliko majina yote la YESU KRISTO lihubiriwe na Askofu Kakobe na wote wanaopenda kudakia maneno ya mitaani bila kufanya utafiti wowote na kujua ukweli ni upi na uongo ni upi. No research no right to speak.kama una roho wa Mungu, muhubiri yeyote anayehubiri habari njema za injili ili watu waache dhambi ungemuunga mkono badala ya kueneza majungu juu yake.
 
Ndugu Esami,
To make this story short, unaonekana wewe ni mtu wa karibu sana na Mheshimiwa Kakobe, kwanini usimshauri kuwa asikae kimya na aende pale MCL akaonane na Bwana Mkinga au kama Mkinga ni wa level ya chini kwake basi angalua aonane na mabosi wake Mkinga (Machumu na Tido) aseme jamani mimi mbona nipo Dar na wala sipo Marekani kama mnavyosema. Enzi za propaganda ndugu Esami zimekwisha. Siku hizi ni vitendo tu. Na mimi naumia kuona wewe unayejiita a saved person ukijitahidi kuutetea uongo. Sidhani kama unaelewa matokeo yake katika imani yako. Kama hayupo hayupo tu. Jifunze to call a spade a spade hata kama inauma kwasababu ni Baba yako

Unachekesha ndugu Bwaga ya moyoni, yaani umeamini kwa kusoma uzushi huo au uliwahi kuja na kukuta mikanda inasikilizwa? Nilidhani wewe ni mtu makini kumbe ndo wale wale bendera fuata upepo. Nasisitiza hiyo habari hata kama inaonekana balance kwa kiwango chake, bado ni ya UONGO na UZUSHI, kabisa kwani baba yetu wa kiroho Mchungaji Zachary Kakobe tunaye na anaendelea kutulisha neno la Mungu kama kawaida.

Hapo kwenye red, sijui ni professionalism ya namna gani unayoongelea, labda kama ni ya kupika habari hapo sawa. Lakini kusema mwandishi amekuja pasaka akakuta ibada inaendeshwa na Mchungaji Hezron wakati ni uongo wa mchana kweupe. Kama kweli mwandishi alikuja basi inawezekana aliishia nje akamuuliza mtu mgeni lakini hata mgeni angemwambia hajui chochote. Yaani hata sijui nisemeje!!!
 
Naona unajitahidi sana kutetea uongo. Kumbuka kanisa ni mali yake lile (kwa mujibu wa dicuments za usajiri). Sitashangaa baadaye kusikia hata wewe ni mali yake kwani you are a product of his investment. Endelea kupumbazwa. Hata hivyo, nakushukuru kuona mara hii umeachana na neno Baba kwani Baba yetu, kama tulivyoagizwa na Bwana wetu Yesu Kristo, ni mmoja tu na yuko mbinguni.

Bwaga ya moyoni, hukuwa na haja ya kuandika haya yote, niseme moja tu kwamba kilichonisukuma kuanzisha uzi huu ni madai ya mwandishi wa habari hiyo kuwa jumapili ya Pasaka alikuja kanisani akakuta ibada inaongozwa na Mchungaji anayeitwa Hezron, wakati ibada aliongoza Mchungaji Kakobe mwenyewe tangu saa 3 mpaka 11 jioni. Mengine ningemezea lakni sio hili.

Hapo kwenye red labda wewe waambie wanakaribishwa kanisani jumapili kuanzia mida ya saa 7 mchana na kuendelea watamkuta tayari amepanda madhabahuni akifundisha neno la Mungu.

Hapo kwenye blue, mtumishi wa Mungu yuko na shughuli nyingi hana muda huo, yeye yuko mbele za Bwana kuutafuta uso wake saa zote, wenyewe ndo waje kama nilivyosema awali.
 
Naona unajitahidi sana kutetea uongo. Kumbuka kanisa ni mali yake lile (kwa mujibu wa dicuments za usajiri). Sitashangaa baadaye kusikia hata wewe ni mali yake kwani you are a product of his investment. Endelea kupumbazwa. Hata hivyo, nakushukuru kuona mara hii umeachana na neno Baba kwani Baba yetu, kama tulivyoagizwa na Bwana wetu Yesu Kristo, ni mmoja tu na yuko mbinguni.

Mkuu Bwaga ya moyoni, huo ndo ukweli na kama unataka kuuthibitisha nenda jumapili kanisani basi.
 
Ukikanusha habari hizo kuwa za uongo,basi tuwekee ukweli? Wewe ni mchungaji Kakobe? Nahisi kama huko updated; habarai zinasema yuko Congo, Marekani ndiko anakofanyia kazi.


Tunaomba utuletee habari sahihi za aliko, kukanusha habari za The Citzen.

Mbona kaeleweka unataka ushahidi gani Mimi binas habari inanisikitisha sana kwa gazeti kama The Citizen kuandika udaku kama huu
 
Ukikanusha habari hizo kuwa za uongo,basi tuwekee ukweli? Wewe ni mchungaji Kakobe? Nahisi kama huko updated; habarai zinasema yuko Congo, Marekani ndiko anakofanyia kazi.

Tunaomba utuletee habari sahihi za aliko, kukanusha habari za The Citzen.

Unataka ushaidi gani Mimi jumapili ya pasaka nilikuwa kanisani na Askofu kakobe ndiye aliyeongoza ibada Tangu Askofu kakobe atoke Zambia ajawai kukosa ibada pale mwenge. Namshangaa mwandishi kuna umbali gani wa kutoka mwananchi kwenda Mwenge kwa kakobe?
 
Unataka ushaidi gani Mimi jumapili ya pasaka nilikuwa kanisani na Askofu kakobe ndiye aliyeongoza ibada Tangu Askofu kakobe atoke Zambia ajawai kukosa ibada pale mwenge. Namshangaa mwandishi kuna umbali gani wa kutoka mwananchi kwenda Mwenge kwa kakobe?

Kazi yako ni njema
 
ya kakobe mwachie kakobe mwenyewe..

na siyo kumwandika vibaya watanzania ni wavivu wa kufikiri Sasa hapo mwandishi kaa mwenyewe katafuta story kakosa kamua kumwandi baba wa WATU eti kambilia marekani,ni janga kubwa sana kwa nchi kama TANZANIA kuwa na waandishi wa namna hii ni hatari sana kwa nchi,
Ndiyo maana walipewa ole.
 
binafsi nilisoma hard copy version ya the Citizen on sunday na heading ilikuwa "MYSTERY AS KAKOBE VANISHES FROM DAR" Niliisoma habari yote napata shida kuamini kama kilichoandikwa hakina ukweli maana mwandishi inaonekana alitumia muda wake mwingi tu kuandaa ile story. Kuna sehemu anaeleza kuwa amewahoji hadi majirani wa Kakobe nyumbani kwake tena kawataja hao majirani kwa majina! nao wanakiri ni muda mrefu hawajamuona Kakobe na kueleza uwepo wa anonymous hapo nyumbani anayefanya housewarming (sic) na huonekana nyakati za magharibi tu. It's really flabbergasting to hear your version of story ESAM,are the citizen that unprofessional? watakaoenda kanisani jumapili ijayo(nje ya wanaoonekana pro-Kakobe kwenye thread hii) waje hapa kutupa ukweli wa mambo tafadhali
 
Last edited by a moderator:
si nasikia asipokuwepo huwa zinawekwa kanda kanda zake akihubiri huwa haruhusiwi kuhubiri mtu mwingine
Sijawahi kusali kwa Kakobe maelezo niliyotoa ni ya kusikia hivyo siwezi kuthibitisha kama ni ukweli au uongo
Upo hapa dar na wewe unasema umesikia lost one to prove it
@ rodrick
 
Mkuu unashangaza kweli mvuto kwa nani, kwa Mungu au wanadamu? Yeye ni mtumwa wa Kristo anatafuta mvuto kwa Bwana wake tu. Na kwa taarifa yako ndo mvuto wake uko juu kuliko wakati mwingine wowote na unazidi kupanda kwa kasi sana

Masikini Kakobe kawanywesha nn...?Mmekuwa vipofu wala hamuoni, mmekuwa viziwi wala hamsikii..

Hakika maandiko yanasema 'Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa' ......Mungu nusuru watu wako kwani wanaangamia..
 
Back
Top Bottom