The Citizen You Can't Be Serious!! Nyie ni Gazeti Makini!!

ESAM

JF-Expert Member
Mar 15, 2011
1,164
548
Ndugu wanaJF,

Nimesikitishwa na kushangazwa na habari iliyochapishwa na kupewa uzito mkubwa sana (lead story) na gazeti la The Citizen toleo la jumapili tarehe 07-04-2013 iliyo na kichwa kifuatacho:
Katika habari hiyo mwandishi wake Bwana Mkinga Mkinga alidai kwamba Askofu Kakobe hajaonekana katika miezi sita iliyopita na kwamba kwa mara ya mwisho kuonekana kanisani Mwenge ilikuwa mwezi Januari mwaka huu. Na kwamba sasa hivi yuko Marekani ndiko alikohamia. Pamoja na madai mengine ya kuzushi mwandishi huyo ambaye kwa kweli ninao ujasiri wa naweza kumwita 'uchwara' anadai kuhudhuria ibada ya Pasaka tar 31-03-2013 na kukuta ikiongozwa na aliyemtaja kama Mchungaji Hezron (jina ambalo sijawahi hata kulisikia). Kwa FGBF Dar es Salaam tunaye mchungaji mmoja tu ambaye ni Mchungaji Zakaria Kabobe.

WanaJF kwa ufupi na watu wengine wapenda ukweli habari hizi ni za uzushi na uongo mtupu, na mimi kama mshirika wa kanisa la FGBF Dar es Salaam nasema hivi tangu Jumapili ya Agosti 15, mwaka 2010 alipokuwa Zambia kwa ajili kazi ya Mungu hatujawahi kumkosa kwenye ibada yoyote ya Jumapili. Kwa mfano, jumapili ya Pasaka tulikuwa na baba yetu Askofu Kakobe kama ilivyokuwa jumapili zote zilizotangulia.

Nilikuwa naliheshimu sana gazeti la The Citizen lakini kwa habari hii naanza kutilia shaka umakini wao. Natoa wito kwa Mtendaji Mkuu wa MCL Mzee Tido Mhando, Mhariri wake Mkuu Bwana Machumu na hata mwandishi wa habari hiyo ya kizushi Bwana Mkinga wawe makini vinginevyo wataliharibu gazeti
 
He he......Kakobe katoroka.
Nini kilipelekea Mwandishi kusema hivyo na si huyo tu nimesikia habari hiyo kipindi cha nyuma

Dada yangu yaani we acha tu, halafu mtu anayesema hivyo yupo hapa Dar na anayo nafasi ya kuja kuthibitisha habari hiyo.
 
Labda ni wale wabaya wake waliokuwa wakimdai Kakobe Mabilioni ndio wamemwandika vibaya
 
Labda ni wale wabaya wake waliokuwa wakimdai Kakobe Mabilioni ndio wamemwandika vibaya

Labda ni kweli lakini kwa gazeti kama the Citizen walitegemewa kufanya uchunguzi wa kutosha kabla ya wao kuingia kwenye mkumbo eti "kahamia Marekani". Lakini pia Mchungaji Kakobe hana DENI lolote kwa mtu yeyote, ila yeye ana deni moja tu; kutenda kazi ya BWANA WA MAJESHI maadamu ni mchana
 
si nasikia asipokuwepo huwa zinawekwa kanda kanda zake akihubiri huwa haruhusiwi kuhubiri mtu mwingine
Sijawahi kusali kwa Kakobe maelezo niliyotoa ni ya kusikia hivyo siwezi kuthibitisha kama ni ukweli au uongo
 
kafulia tu lakini bado yuko town! Biashara ya mazingaombwe imeingia ushindani mwingi! Mzee wa upako, Ndege, Mwingira, Lwakatare, Kingu ......
We kama kazi ya Mungu iliyomtoa Yesu mbinguni na kuja duniani kuokoa watu unaiita mazingaombwe, pole sana. Mimi nakushauri uokoke Bwana Yesu akusamehe dhambi zako nawe utajua ukweli na kuishi maisha ya amani. Lakini ukiendelea kuitukana kazi ya Mungu na watumishi wake, siku usiyodhani yeye ajaye atakukuta hujajiandaa na hapo kwako itakuwa ni kilio na kusaga meno milele.
 
Wapi EngLish Leaner atusaidie maana kithungu ni kithungumkuti lol!
 
Last edited by a moderator:
si nasikia asipokuwepo huwa zinawekwa kanda kanda zake akihubiri huwa haruhusiwi kuhubiri mtu mwingine
Sijawahi kusali kwa Kakobe maelezo niliyotoa ni ya kusikia hivyo siwezi kuthibitisha kama ni ukweli au uongo

Naomba usiridhike na kusikia njoo wewe mwenyewe ujioneee.
 
Mkuu hapo kwenye red, watu wanaombewa na kubarikiwa unakejeli ni mazingaombwe? Mungu akusamehe.

Kweli ndugu yangu, Mungu amsamehe maana anakejeli kazi ya yule mwenye roho yake mkononi mwake na anaweza kuamua kwamba maisha yako yakomee hapa na ikawa hivyo
 
kafulia tu lakini bado yuko town! Biashara ya mazingaombwe imeingia ushindani mwingi! Mzee wa upako, Ndege, Mwingira, Lwakatare, Kingu ......

Mhh maneno mazito sana hayo! Biashara ya mazingaombwe?? una uhakika na unachokisema? wewe ni mkristu au huna dini?? Biblia inatuambia siku za mwisho watatokea manabii wa uongo lakini hiyo haitoshi kuwaona hawa watumwa wa Mungu kuwa ni watu wa mazingaombwe!!

Ambao siyo wa mazingaombwe ni akina nani???
 
Ndugu wanaJF,

Nimesikitishwa na kushangazwa na habari iliyochapishwa na kupewa uzito mkubwa sana (lead story) na gazeti la The Citizen toleo la jumapili tarehe 07-04-2013 iliyo na kichwa kifuatacho:
Katika habari hiyo mwandishi wake Bwana Mkinga Mkinga alidai kwamba Askofu Kakobe hajaonekana katika miezi sita iliyopita na kwamba kwa mara ya mwisho kuonekana kanisani Mwenge ilikuwa mwezi Januari mwaka huu. Na kwamba sasa hivi yuko Marekani ndiko alikohamia. Pamoja na madai mengine ya kuzushi mwandishi huyo ambaye kwa kweli ninao ujasiri wa naweza kumwita 'uchwara' anadai kuhudhuria ibada ya Pasaka tar 31-03-2013 na kukuta ikiongozwa na aliyemtaja kama Mchungaji Hezron (jina ambalo sijawahi hata kulisikia). Kwa FGBF Dar es Salaam tunaye mchungaji mmoja tu ambaye ni Mchungaji Zakaria Kabobe.

WanaJF kwa ufupi na watu wengine wapenda ukweli habari hizi ni za uzushi na uongo mtupu, na mimi kama mshirika wa kanisa la FGBF Dar es Salaam nasema hivi tangu Jumapili ya Agosti 15, mwaka 2010 alipokuwa Zambia kwa ajili kazi ya Mungu hatujawahi kumkosa kwenye ibada yoyote ya Jumapili. Kwa mfano, jumapili ya Pasaka tulikuwa na baba yetu Askofu Kakobe kama ilivyokuwa jumapili zote zilizotangulia.

Nilikuwa naliheshimu sana gazeti la The Citizen lakini kwa habari hii naanza kutilia shaka umakini wao. Natoa wito kwa Mtendaji Mkuu wa MCL Mzee Tido Mhando, Mhariri wake Mkuu Bwana Machumu na hata mwandishi wa habari hiyo ya kizushi Bwana Mkinga wawe makini vinginevyo wataliharibu gazeti. Nawasilisha

Kwa habari hiyo ya kizushi fuata link hii: http://Where on earth is Kakobe? Local church anxious as ‘healer' bishop skips town

Ukikanusha habari hizo kuwa za uongo,basi tuwekee ukweli? Wewe ni mchungaji Kakobe? Nahisi kama huko updated; habarai zinasema yuko Congo, Marekani ndiko anakofanyia kazi.

Tunaomba utuletee habari sahihi za aliko, kukanusha habari za The Citzen.
 
Mhh maneno mazito sana hayo! Biashara ya mazingaombwe?? una uhakika na unachokisema? wewe ni mkristu au huna dini?? Biblia inatuambia siku za mwisho watatokea manabii wa uongo lakini hiyo haitoshi kuwaona hawa watumwa wa Mungu kuwa ni watu wa mazingaombwe!!

Ambao siyo wa mazingaombwe ni akina nani???

Kiama kinakuja, wanakula sadaka za wapendwa wakidai kufanya miujiza feki. Mungu huyu huyu tunayemwamini siku moja atatufunulia
 
Back
Top Bottom