The Citizen You Can't Be Serious!! Nyie ni Gazeti Makini!!

The Citizen You Can't Be Serious!! Nyie ni Gazeti Makini!!

Kweli ndugu yangu, Mungu amsamehe maana anakejeli kazi ya yule mwenye roho yake mkononi mwake na anaweza kuamua kwamba maisha yako yakomee hapa na ikawa hivyo
Hawa vijana ni wakusamehe maana hawajui walitendalo wala walisemalo, hawajui kama ulimi uanaumba, unaweza kuharibu pia wasamehe!!! Vijana wanatakiwa kumtafuta Mungu ili kuweka maisha yako kwa Bwn Yesu!!

 
Ndugu wanaJF,

Nimesikitishwa na kushangazwa na habari iliyochapishwa na kupewa uzito mkubwa sana (lead story) na gazeti la The Citizen toleo la jumapili tarehe 07-04-2013 iliyo na kichwa kifuatacho:
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]"Where on earth is Kakobe? Local church anxious as ‘healer’ bishop skips town".[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Katika habari hiyo mwandishi wake Bwana Mkinga Mkinga alidai kwamba Askofu Kakobe hajaonekana katika miezi sita iliyopita na kwamba kwa mara ya mwisho kuonekana kanisani Mwenge ilikuwa mwezi Januari mwaka huu. Na kwamba sasa hivi yuko Marekani ndiko alikohamia. Pamoja na madai mengine ya kuzushi mwandishi huyo ambaye kwa kweli ninao ujasiri wa naweza kumwita 'uchwara' anadai kuhudhuria ibada ya Pasaka tar 31-03-2013 na kukuta ikiongozwa na aliyemtaja kama Mchungaji Hezron (jina ambalo sijawahi hata kulisikia). Kwa FGBF Dar es Salaam tunaye mchungaji mmoja tu ambaye ni Mchungaji Zakaria Kabobe.

WanaJF kwa ufupi na watu wengine wapenda ukweli habari hizi ni za uzushi na uongo mtupu, na mimi kama mshirika wa kanisa la FGBF Dar es Salaam nasema hivi tangu Jumapili ya Agosti 15, mwaka 2010 alipokuwa Zambia kwa ajili kazi ya Mungu hatujawahi kumkosa kwenye ibada yoyote ya Jumapili. Kwa mfano, jumapili ya Pasaka tulikuwa na baba yetu Askofu Kakobe kama ilivyokuwa jumapili zote zilizotangulia.

Nilikuwa naliheshimu sana gazeti la The Citizen lakini kwa habari hii naanza kutilia shaka umakini wao. Natoa wito kwa Mtendaji Mkuu wa MCL Mzee Tido Mhando, Mhariri wake Mkuu Bwana Machumu na hata mwandishi wa habari hiyo ya kizushi Bwana Mkinga wawe makini vinginevyo wataliharibu gazeti. Nawasilisha

Kwa habari hiyo ya kizushi fuata link hii: http://Where on earth is Kakobe? Local church anxious as ‘healer’ bishop skips town

Hivi siku Kakobe akiwa anumwa au ana udhuru wowote mnaongozwa na nani?
 
Ukikanusha habari hizo kuwa za uongo,basi tuwekee ukweli? Wewe ni mchungaji Kakobe? Nahisi kama huko updated; habarai zinasema yuko Congo, Marekani ndiko anakofanyia kazi.

Tunaomba utuletee habari sahihi za aliko, kukanusha habari za The Citzen.

Hivi umesoma taarifa yangu vizuri? Hebu soma kipande hiki tena, "na mimi kama mshirika wa kanisa la FGBF Dar es Salaam nasema hivi tangu Jumapili ya Agosti 15, mwaka 2010 alipokuwa Zambia kwa ajili kazi ya Mungu hatujawahi kumkosa kwenye ibada yoyote ya Jumapili."
Sasa hapo ni kipi ambacho hukuelewa!! Yaani ninamaanisha hivi baada ya kumaliza mkutano huko Lusaka Jumapili ya 15 Agosti 2010 na kurejea nchini siku iliyofuata yaani Agosti 16 mwaka huo hajawahi kusafiri nje ya nchi tena, sasa atakuwaje Congo au Marekani!!??
 
Kiama kinakuja, wanakula sadaka za wapendwa wakidai kufanya miujiza feki. Mungu huyu huyu tunayemwamini siku moja atatufunulia

Kitakuja kwako unayemnenea mabaya masihi wa Bwana bila kuwa na uhakika na hayo unayoyasema, Mungu wangu mwema na akusamehe maana hujui ulitendalo. Lakini kumbuka wema wa Mungu wakuvuta ili upate kutubu (Rum 2;4-5)
 
kafulia tu lakini bado yuko town! Biashara ya mazingaombwe imeingia ushindani mwingi! Mzee wa upako, Ndege, Mwingira, Lwakatare, Kingu ......

Naona jamaa wanakushambulia kwa kutumia mgongo wa "Mungu" wakati wewe unamuongelea mwanadamu! Pole bhana!
 
Hivi siku Kakobe akiwa anumwa au ana udhuru wowote mnaongozwa na nani?

Kwa kazi ya Mungu!!! Mungu anao watu wengi sana wa kufanya kazi yake, anaweza kuinua hata mawe yakafanya kazi yake ya kuhubiri habari njema
 
Naona jamaa wanakushambulia kwa kutumia mgongo wa "Mungu" wakati wewe unamuongelea mwanadamu! Pole bhana!

Wewe acha kumuunga mkono katika uovu, yaani ambapo linafundishwa neno la Mungu, watu kuponywa na matatizo yao mengi kutatuliwa mtu aite eti ni mazingaombwe halafu tukae kimya. KUMBUKA Mchungaji Kakobe ni chombo tu maombi yote yanafanyika kwa jina la Yesu na sio kwa jina la Kakobe au kwa jina la mtu mwingine yeyote. MUNGU mwema akusamehe na kukupa neema ya kumjua jinsi alivyo
 
Wewe acha kumuunga mkono katika uovu, yaani ambapo linafundishwa neno la Mungu, watu kuponywa na matatizo yao mengi kutatuliwa mtu aite eti ni mazingaombwe halafu tukae kimya. KUMBUKA Mchungaji Kakobe ni chombo tu maombi yote yanafanyika kwa jina la Yesu na sio kwa jina la Kakobe au kwa jina la mtu mwingine yeyote. MUNGU mwema akusamehe na kukupa neema ya kumjua jinsi alivyo

Bahati mbaya kabisa simwamini Kakobe pia! Namwona msanii tu kama wakina Lusekelo na wengine, hata Waganga wa kienyeji wanaombea na kutoa mapepo. Asante.
 
Free World you are right!

Caroline kama wewe ni mkristu jitahidi kusoma Biblia na tafuta kutengeneza uhusiano wako wewe na Mungu,kama kuna mtu anafanya mazingaombwe muache analo la kujibu mbele za Mungu siku ya mwisho! Usiwe busy na kuangalia nani anafanya mazingaombwe na nani hafanyi maana huo uwezo hauna bali yeye aliyeumba mbingu na nchi na vitu vyote vilivyomo anajua nani ni Mtumishi wake na nani ni mtumishi wa miungu mingine! Kazi yako wewe Caroline si kuhukumu bali mwenye jukumu hilo ni Mungu mwenyewe!! Utajisikiaje mbele za Mungu ukiona huyo uliyefikiri anafanya mazingaombwe kumbe ndiye aliyekuwa mtumwa wa Bwana na alikuwa anafanya yale aliyotumwa kufanya na Mungu mwenyewe???
 
Bahati mbaya kabisa simwamini Kakobe pia! Namwona msanii tu kama wakina Lusekelo na wengine, hata Waganga wa kienyeji wanaombea na kutoa mapepo. Asante.

Wa kumwamini ni nani? Ni Kakobe au Mungu anayemtumia, kumbuka Yesu aliwaambia mafarisayo kwamba hata kama hawamwamini yeye basi waziamini kazi alizokuwa akizifanya, yaani viziwi kusikia, vipofu kuona, wafu kufufuliwa, masikini kuhubiriwa habari njema na nyingine. Ni juu yako kuamua la kufanya sisi watumwa wa Bwana twasema tu yale yanatupasa kuyasema
 
Wa kumwamini ni nani? Ni Kakobe au Mungu anayemtumia, kumbuka Yesu aliwaambia mafarisayo kwamba hata kama hawamwamini yeye basi waziamini kazi alizokuwa akizifanya, yaani viziwi kusikia, vipofu kuona, wafu kufufuliwa, masikini kuhubiriwa habari njema na nyingine. Ni juu yako kuamua la kufanya sisi watumwa wa Bwana twasema tu yale yanatupasa kuyasema

Uko sahihi mkuu, lakini siku hizi hali inakuwa ni ngumu kwa waamini kwa sababu mitume wamekuwa wengi na inachanganya, Yesu mwenyewe alisema watakuja wengi na watatenda miujiza kwa jina la BWANA, sasa ni nani wa uwongo nani wa ukweli wakati kila mmoja anadai yeye ametumwa kufanya kazi ya BWANA! Akili ya kuambiwa unachanganya na ya kwako-JK
 
Uko sahihi mkuu, lakini siku hizi hali inakuwa ni ngumu kwa waamini kwa sababu mitume wamekuwa wengi na inachanganya, Yesu mwenyewe alisema watakuja wengi na watatenda miujiza kwa jina la BWANA, sasa ni nani wa uwongo nani wa ukweli wakati kila mmoja anadai yeye ametumwa kufanya kazi ya BWANA! Akili ya kuambiwa unachanganya na ya kwako-JK

Kwanza Kakobe hajawahi kusema na wala haitwi mtume yeye ni mchungaji wa kanisa la FGBF Dar es Salaam na Askofu Mkuu wa Kanisa la FGBF, Tanzania. Pili Yesu alisema wataotenda miujiza kwa jina lake ni wale wamwaminio (Marko 16:15-18) kuhusu manabii wa uongo alisema watafanya ishara kubwa na kushusha moto kutoka mbinguni (ufunuo 13:12-14)
 
Kwanza Kakobe hajawahi kusema na wala haitwi mtume yeye ni mchungaji wa kanisa la FGBF Dar es Salaam na Askofu Mkuu wa Kanisa la FGBF Dar es Salaam. Pili Yesu alisema wataotenda miujiza kwa jina lake ni wale wamwaminio (Marko 16:15-18) kuhusu manabii wa uongo alisema watafanya ishara kubwa na kushusha moto kutoka mbinguni (ufunuo 13:12-14)

.........Haya!
 
Ndg hii ni mfano tu, tunalishwa habari nyingi za uongo na hisia za mitaani tu, kwenye siasa ndo usiseme.
Kwa kuwa watu wanapenda kusikia wanachotaka kusikia magazeti yanatumia mwanya huo kutengeneza pesa.
 
Kitakuja kwako unayemnenea mabaya masihi wa Bwana bila kuwa na uhakika na hayo unayoyasema, Mungu wangu mwema na akusamehe maana hujui ulitendalo. Lakini kumbuka wema wa Mungu wakuvuta ili upate kutubu (Rum 2;4-5)

Duuh.. Hivi masihi maana yake ci mpakwa mafuta wa Bwana..? so kakobe.. mwingira na mzee wa upako ni wapakwa mafuta wa Bwana..? Wanaishi maisha ya fahari hawa wapakwa mafuta.. wanamiliki magari na majumba ya fahari.. Mh..
Anyway back kwa topic.. kama hicho unachosema ni ukweli unaweza/mnaweza kupeleka malalimiko yenu kwa baraza la habari mkiwa na ushahidi uliojitosheleza.. Najua magazeti wakati mwingine wana tabia ya ku-pre empt habari ili mtokeze na kupinga.. njia ambayo sio nzuri..
 
Uko sahihi mkuu, lakini siku hizi hali inakuwa ni ngumu kwa waamini kwa sababu mitume wamekuwa wengi na inachanganya, Yesu mwenyewe alisema watakuja wengi na watatenda miujiza kwa jina la BWANA, sasa ni nani wa uwongo nani wa ukweli wakati kila mmoja anadai yeye ametumwa kufanya kazi ya BWANA! Akili ya kuambiwa unachanganya na ya kwako-JK

Naamini mkuu CYBERTEQ una uwezo wa kusoma na una uwezo wa kununua BIBLIA! Kama unaamini kama BIBLIA ni Neno la Mungu basi nakushauri usome BIBLIA kwaajili ya kujifunza na zaidi omba Roho Mtakatifu akufundishe na kukufunulia yale unayoyasoma katika Biblia ili uweze kupata ufahamu wa Neno ambalo ni Mungu mwenyewe. Ukipenda na kutamani sana kuongozwa na Roho Mtakatifu yeye ndiye atakayekuongoza wapi mahali sahihi kwa kwenda ambako hakuna mazingaombwa wala usanii ambako Roho wa Mungu ndiye anayetawala na kuongoza kinachofanyika hapo!

Roho Mtakatifu atakusaidia kupambanua uwongo na ukweli maana peke yako huwezi! Ni ngumu kwako kutofautisha Nabii wa Mungu na Nabii wa Uwongo lakini ukiongozwa na Roho wa Mungu atakusaidia ku-discern spirits!!
 
Back
Top Bottom