Otorong'ong'o
Platinum Member
- Aug 17, 2011
- 39,183
- 28,842
Hahaha hata waumini wake wanapumua maana GOLD zao walau zimetulia vifuani na masikioni mwao, wa kuvaa vilemba kama wadoezi wa ubwabwa nao walau nywele zinaonekana sasa na kushine! shit! mxxxiiiiiii
Ndugu wanaJF,
Nimesikitishwa na kushangazwa na habari iliyochapishwa na kupewa uzito mkubwa sana (lead story) na gazeti la The Citizen toleo la jumapili tarehe 07-04-2013 iliyo na kichwa kifuatacho:[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]"Where on earth is Kakobe? Local church anxious as healer bishop skips town".[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Katika habari hiyo mwandishi wake Bwana Mkinga Mkinga alidai kwamba Askofu Kakobe hajaonekana katika miezi sita iliyopita na kwamba kwa mara ya mwisho kuonekana kanisani Mwenge ilikuwa mwezi Januari mwaka huu. Na kwamba sasa hivi yuko Marekani ndiko alikohamia. Pamoja na madai mengine ya kuzushi mwandishi huyo ambaye kwa kweli ninao ujasiri wa naweza kumwita 'uchwara' anadai kuhudhuria ibada ya Pasaka tar 31-03-2013 na kukuta ikiongozwa na aliyemtaja kama Mchungaji Hezron (jina ambalo sijawahi hata kulisikia). Kwa FGBF Dar es Salaam tunaye mchungaji mmoja tu ambaye ni Mchungaji Zakaria Kabobe.
WanaJF kwa ufupi na watu wengine wapenda ukweli habari hizi ni za uzushi na uongo mtupu, na mimi kama mshirika wa kanisa la FGBF Dar es Salaam nasema hivi tangu Jumapili ya Agosti 15, mwaka 2010 alipokuwa Zambia kwa ajili kazi ya Mungu hatujawahi kumkosa kwenye ibada yoyote ya Jumapili. Kwa mfano, jumapili ya Pasaka tulikuwa na baba yetu Askofu Kakobe kama ilivyokuwa jumapili zote zilizotangulia.
Nilikuwa naliheshimu sana gazeti la The Citizen lakini kwa habari hii naanza kutilia shaka umakini wao. Natoa wito kwa Mtendaji Mkuu wa MCL Mzee Tido Mhando, Mhariri wake Mkuu Bwana Machumu na hata mwandishi wa habari hiyo ya kizushi Bwana Mkinga wawe makini vinginevyo wataliharibu gazeti. Nawasilisha
Kwa habari hiyo ya kizushi fuata link hii: http://Where on earth is Kakobe? Local church anxious as healer bishop skips town
Labda ni wale wabaya wake waliokuwa wakimdai Kakobe Mabilioni ndio wamemwandika vibaya
Au wale waliowahi kudai kuwa Kakobe anatumia nguvu za giza kudanganya watu kuwa anatibuLabda ni wale wabaya wake waliokuwa wakimdai Kakobe Mabilioni ndio wamemwandika vibaya
Hilo nalo swali!!!Nenda mahakamani ama mwandamane kama ni uongo na kwanini kanisa liwe na mchungaji mmoja na akisafiri mnaongozwa na nani kwenye ibada?
Mimi nadhani wakati mwingine siyo vizuri kuwa too emmotional for nothing. Kama gazeti, hakuna kosa kuuliza mahali alipo any public figure, Kakobe akiwa mmoja wapo. Si sahihi pia kuleta emotions zitokanazo na imani binafasi kwa mtu badala ya kuwa na ile imani ya ukweli kwa Mungu. Napata picha kuwa ndugu mleta uzi unamuamini sana Kakobe kuliko hata Mungu wako na ndio maana umejitahidi kuhakikisha kuwa unamponda Bwana Mkinga na huku ukituonyesha waJF kuwa unafahamu The Citizen ni gazeti makini sana likiwa na uongozi thabiti wa Managing Editor Bakari Machumu aliye chini ya Managing Director wa Mwananchi Communications Limited, Tido Mhando. Sidhani kama emotions zako zinaweza kuondoa umakini wa gazeti mbele za wanaJF haswa wale wenye msimamo wa kumwamini Mungu aliyehai kuliko kumwamini mtu.
Mleta uzi unapaswa kukumbuka kuwa Kakobe ni binadamu kama wewe na kuwa naye yuko kama wengine wote so kumuamini kama yeye ni mtu asiye wakaida kunaweza kuathiri uwezo wako wakufikiri kwa kiasi kikubwa. Wote tunatambua kuwa Kakobe huyu huyu anakesi mahakamani akidaiwa na wale ambao katika kanisa lake mumewapa majina ya 'Wabaya wake' eti kwasababu wamehoji matumizi ya Kanisa mahakamani. Wote twajua kuwa kule mahakamani wale 'Wabaya Wake' wameambiwa kesi hiyo itawasumbuwa kwasababu eti kanisa limesajiriwa kama mali yake huyu Baba Yenu Askofu Kakobe (Kumbuka Yesu alikataa watumishi wake kuitwa Baba - Mathayo 23:1 mpaka mwisho) na hivyo kama ni kweli ametumia vibaya zile TSH14bilini basi ametumia pesa zitokanazo na his own investment. Je, huu ndio utukufu unataka kutuonyesha kuwa yeye hana dhambi? Na hata hiyo habari ya umeme wa Tanesco, ikumbukwe kuwa aliwahi kutuambia Watanzania kuwa ule umeme usingewaka baada ya Tanesco kulazimisha upite mbele ya kanisa lake. Mbona unawaka? Ni ule unabii wa kuwa Mrema angekua Rais wa Tanzania mwaka 1995, mbona haikuwa na sisi tunabaki kujifanya hatutaki kuona, kusikia wala kuambiwa kuwa mwaminini Mungu na siyo binadamu.
Kama unachosema wewe ni kweli, basi mpeleke Bwana Mkinga, Bakari Machumu au Tido Mhando kwa Kakobe. Kama kweli yupo nchini, basi aje kwenye ofisi za Mwananchi ili approve the newspaper wrong. Tuache propaganda ndugu zangu. Kama hayupo ni kweli hayupo. Binafsi nawapa hongera sana The Citizen kwani wangekuwa unprofessional, wangeweza hata kuandika mengine mengi ya mitaani yamhusuyo Kakobe. Wewe mwenyewe jiulize tu: Je, idadi ya wale tuliokuwa tukisali pale bado iko pale pale au wengine wameweza kupata kuokolewa na Mungu sasa amezifungua akili zao mpaka wamepata kuanza kufikri vizuri tena? Angalia idadi na utuletee uzi mwingine kwani ni dhahiri idadi imepungua sana na mumebaki wachache mnaod=subiri Mungu aje awaokoe kutokana na kifungo cha kutokusikia, kuona wala kutaka kuambiwa.
Mimi nimebaki kimya tu.
Lakini kukata mzizi wa Fitna, ingepasa kwa Kakobe kujitokeza hadharani mbele ya waandishi wa habari siku ile ile habari hii ilipotoka(Hata sasa anaweza kujitokeza hadharani) na kukanusha habari hizi kama kweli ni uzushi.
Sidhani kama hili linashindikana Kama kweli Kakobe yupo Tanzania, kwa sababu Kakobe ameshawahi kujitokeza mara kadhaa huko nyuma na kuongea na waandishi wa habari.
Vinginevyo kuna kitu bado kinajifichaficha....
Kinyamana, ukweli unao, ninachokiona kwako ni kujipa moyo. Nilikuwa napindisha sentensi sasa wacha ninyooshe. Kakobe si lolote na mbele ya Mungu ana ya kujibu. Mifano hai ninayo kama hii ligi unaitaka niko tayari. Hakuna aliyemuhukumu, magtendo yake yanaonyesha kwamba siyo.
TANU hakuna uzushi, kakimbia madeni, na kaishaokota sadaka za waumini wake sasa anatanua! God forbide!
Hahaha hata waumini wake wanapumua maana GOLD zao walau zimetulia vifuani na masikioni mwao, wa kuvaa vilemba kama wadoezi wa ubwabwa nao walau nywele zinaonekana sasa na kushine! shit! mxxxiiiiiii
Niliona recently tv fulani ikionyesha akipewa mapokezi makubwa Lubumbashi, kwani ilikua lini?
Au wale waliowahi kudai kuwa Kakobe anatumia nguvu za giza kudanganya watu kuwa anatibu
Nenda mahakamani ama mwandamane kama ni uongo na kwanini kanisa liwe na mchungaji mmoja na akisafiri mnaongozwa na nani kwenye ibada?
Nasikia huwa anawaachia dvd muwe mnamwangalia haruhusiwi mtu kupanda pale kuhubiri
Kama yupo Bongo mbona hatumuoni?