Bob Fern
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 900
- 131
adhabu aliyopewa haijitoshelezi na kosa kalirudia kwa mara ya pili! hafai kuwa Mchezaji
Mara ya tatu hiyo. Alianza na Amir Maftah,Maguli then Bocco
adhabu aliyopewa haijitoshelezi na kosa kalirudia kwa mara ya pili! hafai kuwa Mchezaji
Kumfungia miaka miwili si kumuua kabisa jamaa.Mi naona angefungiwa miezi kadhaa lakini apewe counselling ya nguvu katika muda huo.Maana jamaa inaonekana ni kawaida kwake kufanya vitendo vya kihuni.Jamaa inaonesha kapata malezi mabovu utotoni
Mara ya tatu hiyo. Alianza na Amir Maftah,Maguli then Bocco
duh! hafai kabisa kuwa mchezaji! sheria ipo vipi kwa kosa kama hilo haswa baada ya adhabu ya TFF maana sioni kama inamtisha wala hajatendewa haki kwa kosa alilofanya halisemeki' watu alio wakosea wana familia wana ndugu wana majamaa na mabosi huoni kuwa ame wafedhehesha wenzake kiasi kisicho ongeleka
Safi sana. Nashauri hiyo faini apewe John Bocco kama kifuta jasho chake cha kudhalalishwa.
Iwe fundisho kwa wengine.
Hiyo faini hailipiki Mkuu. Jamaa kafungiwa miaka miwili kucheza soka, hakuna shaka faini hiyo inatakiwa ilipwe baada ya hiyo miaka miwili kutimia ili arudi uwanjani. Ukimwangalia Nyosso pale alipo baada ya miaka miwili atakuwaje? Huyu hatacheza tena hivyo hana sababu ya kulipa faini ya hiyo milioni mbili. Labda TFF imbane sasa hivi ailipe, lakini najiuliza tayari ameshafungiwa asipolipa atapewa adhabu gani?
Kwa maoni yangu adhabu pekee inayotekelezeka ni kufungiwa kucheza soka miaka 2 hiyo ya fedha haitekelezeki!
Angepelekwa mahakamani iwe somo kwa wavuta bange wengine
Sikubaliani kabisa na vitendo vichafu vya Nyosso lakini tuambiwe kanuni gani imetumika kutoa adhabu ya miaka miwili na faini ya million mbili.
Kama kanuni ni dhaifu zifanyiwe kazi haraka. Kimsingi Nyosso kafungiwa maisha labda kwenye ndondo.
Mimi naona haitoshi,angefungiwa maisha kucheza soka.
Mpuuzi mkubwa huyo.
John Bocco nae alistahili adhabu..Mtt wa kiume unapigwaje kidole halafu unatulia tu..
Huyu Nyoso ni mvuta bange. Wangemfungia hata maisha. Hatuhitaji vichaa kama hawa kwenye mpira wetu.
Naunga mkono hoja yako 100%.
Michezo ni furaha na si kudhalilishana wala uhasama.
Watu wanaoharibu jina la "mchezo" kama huyo mjinga wafungiwe maisha. Anashindwa kuelewa kuwa wanamichezo hususan mpira hapa kwetu wana influence kubwa sana kwa vitendo vyao kwa watoto.
Kuna siku mjukuu wangu alinambia "nataka kunyoa kama Baloteli", nilikuwa simjuwi ndiyo nani, akanambia ntakuonesha akioneshwa kwenye TV, mimi sikusubiri anioneshe nikaenda ku google, nikamuona Baloteli na alivyonyoa, kwanza nilicheka nikamwambia mjukuu wangu hapo utanisamehe sana, sikupeleki ukanyoe kiwazimu namna hiyo. Akanambia "mbona Baloteli kanyoa hivyo kwani yeye mwenda'zimu?". Nikakosa la kumjibu.
Nimeelezea hicho kisa kuonesha ni vipi hawa wachezaji wanaweza kuathiri jamii.
Kitendo alichokifanya si chema kabisa hafai kurudi uwanjani ukichukulia kuwa si mara yake kwanza kufanya hivyo, nimesoma sehemu kuwa alishawahi kufungiwa kwa kitendo kama hicho, hajakoma.
Kumfungia miaka miwili si kumuua kabisa jamaa.Mi naona angefungiwa miezi kadhaa lakini apewe counselling ya nguvu katika muda huo.Maana jamaa inaonekana ni kawaida kwake kufanya vitendo vya kihuni.Jamaa inaonesha kapata malezi mabovu utotoni
KANUNI ZA TFF
Kanuni ya 37 Kifungu cha 24 cha Kanuni za Ligi za TFF toleo la 2015 kinasema: "Mchezaji yeyote atakayepatikana na hatia ya kufanya makosa makubwa ya kimaadili au kinidhamu, au ya kibaguzi au ya kidhalilishaji au yatakayotafsiriwa kuwa ni ukiukaji mkubwa wa taratibu za mchezo na ubinaadamu atatozwa faini kati ya shilingi milioni moja mpaka milioni tatu au/na kusimamishwa kushiriki michezo mitatu mpaka kumi ya klabu yake yoyote atakayoitumikia katika Ligi Kuu na mashindano mengine rasmi ya TFF au kufungiwa kipindi cha kati ya mwaka mmoja na miwili."
hupendezi na uzuri wako kuwa na roho ya kikatili kama hiyo...usisahau nyoso ana mke na watoto wanamtegemea acheze mpira wale wavae wasome...maisha ni adhabu kubwa sana...sawa na kuuwa familia yake.
Jibu lako nimelipenda mkuu. Inakera kuona watu wanaleta utani kwenye tabia za kukemea :angry:Anajua sana kutumia vidole so atanunua kapu na rangi za kucha aanze kusugua wadada miguu na kuwaremba. . . . ..
Au mchukue mpeleke kozi ya kufuma huko wanatumia zaid vidole. . . . .
Acha apotee . . . .
Huyu jamaa apimwe akili, Ni kama vile hicho kitendo kinamburudisha!Mara ya tatu hiyo. Alianza na Amir Maftah,Maguli then Bocco