Teuzi Mpya: Rais Samia na falsafa ya kimageuzi kwa Watumishi wa Umma

msuyaeric

JF-Expert Member
Dec 18, 2014
838
1,167
Na Mwl Udadis, Buza kwa Lulenge

Moja ya falsafa ngumu katika uongozi ni uwezo wa kuongoza watu kimageuzi. Rais Samia anaendelea kuiishi falsafa hii kwa weledi na umahiri wa hali ya juu. Nafasi za teuzi siku zote ni dhamana katika kuwatumikia watanzania, dhamana hii inaweza kukabidhiwa kwa mtumishi mwingine kadri itakavyoonekana inafaa na hili tunaliona dhahiri katika mabadiliko ya Mkurugenzi Mkuu wa idara ya usalama wa Taifa.

Kipekee nampongeza Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa anayemaliza muda wake kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa nchi yetu. Utamaduni wa mbio za vijiti ndio lugha ya uongozi wa kimageuzi. Kama ilivyo katika timu bora za soka, sasa anaingia Mkurugenzi mpya kwaajili ya kuendeleza utumishi wake kwa kasi, ari na weledi zaidi.

Baadhi ya sifa za viongozi wengi wanaoteuliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan katika utumishi wa umma;

1. Uzalendo, uchapakazi na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu.

2. Kuhakikisha uzoefu na rekodi ya utumishi iliyotukuka katika kuwatumikia watanzania.

3. Kuzingatia taaluma, ubobezi na stadi za fani mbalimbali zinazoendana na mahitaji ya majukumu.

4. Kuzingatia ujumuishi, haki na usawa katika kupewa dhamana mbalimbali za kiuongozi katika majukumu.

5. Kufuata kanuni, miongozo na taratibu za utumishi wa umma sanjari na sheria za nchi yetu.

Naungana na watanzania wote kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuiishi falsafa ngumu ya kiuongozi kwa vitendo. Kujitoa katika kutekeleza falsafa ya kimageuzi ni matokeo ya uzalendo na mapenzi makubwa kwa nchi yako, Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda na kukubariki Rais wetu mpendwa ili uzidi kuitumikia nchi yetu kwa mapenzi makubwa.
IMG-20230828-WA0521.jpg
 
Ngoja tuone how far this top Agent will reach. Namshauri na yeye akipata fursa ya kutuwekea wazi mikataba mingine kama ule wa DP afanye hivyo bila kusita
 
Kama umeandika hili kwa nia nzuri bila kua na hidden massage na kuunga mkono sana lazima tutafute watu wenye kupanda usawa na haki.
 
Mtu ameamua kuuza nchi anakuwaje mwanamageuzi wakuu? Hatujawahi kupata mtu wa namna hii hakyanani.
 
Siku zote teuzi za sandakalawe huwa hazina tija!!!unapoona mteuaji kila siku anateua na kutengua,mala nyingi ,tatizo liko kwake!!angalia nchi zilizoendelea ambako,teuzi hufanywa kwa makini,tena kwa mifumo iliyowazi,uone!!na hizi mtu ana ibuka tu na teuzi anayoipenda yeye
 
Mtu ameamua kuuza nchi anakuwaje mwanamageuzi wakuu? Hatujawahi kupata mtu wa namna hii hakyanani.
Nchi kauziwa nani? Muache kufuata ptopaganda za watu wasio kua na hoja, hamna mtu wa kuuza hi nchi Tanzania nikubwa kuliko mtu yoyote, mimi ntakua mtu wa mwisho kuamini kama nchi inaweza kuunzwa.
 
Nchi kauziwa nani? Muache kufuata ptopaganda za watu wasio kua na hoja, hamna mtu wa kuuza hi nchi Tanzania nikubwa kuliko mtu yoyote, mimi ntakua mtu wa mwisho kuamini kama nchi inaweza kuunzwa.
Hata waliokuwa wanamuunga mkono Kikwete na Mkapa kwenye mikataba mibovu walikuwa kama wewe.

Hatutaki baada ya 10yrs tusome vitamu vya kuomba radhi kwa kuingizwa chaka na wasaidizi. Huo ni upimbi.
 
Umesahau kuweka namba yako ya sim Mwl Udadis wa Buza kwa Lulenge...😊
 
Nchi kauziwa nani? Muache kufuata ptopaganda za watu wasio kua na hoja, hamna mtu wa kuuza hi nchi Tanzania nikubwa kuliko mtu yoyote, mimi ntakua mtu wa mwisho kuamini kama nchi inaweza kuunzwa.
Dah mkuu, "nchi kuuzwa", ina maana kauli hii wewe unaitafsiri kama vile mtu anavyonunua nguo toka dukani na kwenda nayo kwake?

Kwamba mnunuzi ataikata kipande na kwenda nayo au kumilikishwa akiisha kuinunua?

"Kuuzwa" kwa muktadha wa sakata tulilonalo hivi sasa ni uingiwaji wa mikataba mibovu ya wawekezaji.

Impact ya uwekezaji isipoleta matunda ndiyo nchi kuuzwa huko!

Watu wamejifunza kutokana na historia namna mikataba mibovu ya kinyonyaji na kifisadi ilivyoliingiza Taifa kwenye hasara.

Waswahili husema: "mtu aliyekwisha kuumwa na nyoka, hata akiona kamba lazima ashituke".

Sasa kuna kosa gani watu kuhoji uhalali wa uingiwaji wa mikataba ya bandari?

Mfano wa kashifa ya mikataba hiyo nawe utakuwa bado unaikumbuka maana hata miongo miwili haijapita.
 
Dah mkuu, "nchi kuuzwa", ina maana kauli hii wewe unaitafsiri kama vile mtu anavyonunua nguo toka dukani na kwenda nayo kwake?

Kwamba mnunuzi ataikata kipande na kwenda nayo au kumilikishwa akiisha kuinunua?

"Kuuzwa" kwa muktadha wa sakata tulilonalo hivi sasa ni uingiwaji wa mikataba mibovu ya wawekezaji.

Impact ya uwekezaji isipoleta matunda ndiyo nchi kuuzwa huko!

Watu wamejifunza kutokana na historia namna mikataba mibovu ya kinyonyaji na kifisadi ilivyoliingiza Taifa kwenye hasara.

Waswahili husema: "mtu aliyekwisha kuumwa na nyoka, hata akiona kamba lazima ashituke".

Sasa kuna kosa gani watu kuhoji uhalali wa uingiwaji wa mikataba ya bandari?

Mfano wa kashifa ya mikataba hiyo nawe utakuwa bado unaikumbuka maana hata miongo miwili haijapita.
Kama mikataba mibovu ndo uuzaji wa nchi hi nchi ilisha uzwa kitambo na maraisi walio tangulia hatuja wahi kufanya mkataba wenye masilahi kwa raia wetu.
 
Na Mwl Udadis, Buza kwa Lulenge

Moja ya falsafa ngumu katika uongozi ni uwezo wa kuongoza watu kimageuzi. Rais Samia anaendelea kuiishi falsafa hii kwa weledi na umahiri wa hali ya juu. Nafasi za teuzi siku zote ni dhamana katika kuwatumikia watanzania, dhamana hii inaweza kukabidhiwa kwa mtumishi mwingine kadri itakavyoonekana inafaa na hili tunaliona dhahiri katika mabadiliko ya Mkurugenzi Mkuu wa idara ya usalama wa Taifa.

Kipekee nampongeza Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa anayemaliza muda wake kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa nchi yetu. Utamaduni wa mbio za vijiti ndio lugha ya uongozi wa kimageuzi. Kama ilivyo katika timu bora za soka, sasa anaingia Mkurugenzi mpya kwaajili ya kuendeleza utumishi wake kwa kasi, ari na weledi zaidi.

Baadhi ya sifa za viongozi wengi wanaoteuliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan katika utumishi wa umma;

1. Uzalendo, uchapakazi na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu.

2. Kuhakikisha uzoefu na rekodi ya utumishi iliyotukuka katika kuwatumikia watanzania.

3. Kuzingatia taaluma, ubobezi na stadi za fani mbalimbali zinazoendana na mahitaji ya majukumu.

4. Kuzingatia ujumuishi, haki na usawa katika kupewa dhamana mbalimbali za kiuongozi katika majukumu.

5. Kufuata kanuni, miongozo na taratibu za utumishi wa umma sanjari na sheria za nchi yetu.

Naungana na watanzania wote kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuiishi falsafa ngumu ya kiuongozi kwa vitendo. Kujitoa katika kutekeleza falsafa ya kimageuzi ni matokeo ya uzalendo na mapenzi makubwa kwa nchi yako, Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda na kukubariki Rais wetu mpendwa ili uzidi kuitumikia nchi yetu kwa mapenzi makubwa.View attachment 2732203
Hivi huwa TISS wanapatikana vipi?

Polisi, Jwtz ,uhamiaji ajira hutangazwa ,sasa hawa mabwana wao wanapatikanaje?
 
Nchi kauziwa nani? Muache kufuata ptopaganda za watu wasio kua na hoja, hamna mtu wa kuuza hi nchi Tanzania nikubwa kuliko mtu yoyote, mimi ntakua mtu wa mwisho kuamini kama nchi inaweza kuunzwa.
Hata Wamasai hawakuamini Kama kuna siku moja watakuja kutolewa Ngorongoro, leo hii waanalia na Mama kwenye Vyombo vya habari!!
 
Back
Top Bottom