Tendwa sasa atishia kukifuta CHADEMA

Tendwa sasa atishia kukifuta CHADEMA

Kila siku hawa ccm na vibaraka wao wanajitahidi wanaongeza hasira zetu. Sijui wanajiamini nini, wana ubavu kuhumili mlipuko wetu?
 
Tendwa kama walivyo maofisa wa polisi ni vibaraka wa CCM, huu ni mwendelezo wa kuwa msemaji na mtetezi wa ccm na kusahau wajibu wake halisi. Tunakumbuka jinsi alivyotete Kikwete kuhutubia mikutano ya kampeni hata baada ya Muda kuisha, halafu akaja kupingwa vikali na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi.

Hawezi kufuta kwa sababu nia na uwezo anao lakini sababu hana, kama anajitafutizia visababu basi ajaribu aone response yake itakuwaje...
 
HILI NI TATIZO LA KATIBA, CCM Msajili wa vyama wao, Tume ya uchaguzi wao, mahakama yao, Speaker wa bunge wao, Jeshi la Polisi wao. Referees wao, Laizimen wao, wachezaji wao, washangiliaji wao, watangazaji wao na Uwanja wao. SISI NI TIMU PINZANI TUU. panakazi kubwa kweli hapo

Wamekosa kitu kimoja tu, nguvu ya umma ambayo ikiamua kuadabisha watawala ni balaa.
 
Siasa za ccm sawa mchezo wa ragby. . . . Kulazimishia kwingiiii, akili kidogo.
 
msajili wa vyama vya siasa nchini john tendwa amesema sasa amechoka kusikia mauaji kwenye mikutano ya kisiasa ya cdm na atatumia rungu lake kufutia usajili chama chochote kitakachoshindwa kutunza amani ya nchi.tendwa amewaambia waandishi wa habari hatishiki na chama chochote kuwa na wabunge kwani sheria inamruhusu kufuta chama hata kama kina wabunge 100.

Katika hali ya kushangaza tendwa ameshauri vyama visubiri nyajati za uchaguzi ndipo vifanye mikutano ya kisiasa.hata hivyo amekiri sheria inaruhusu vyama kufanya mikutano na maandamano wakati wowote.

Source:habari radio tumaini.

nahisi kuna kitu kinaandaliwa hapa ngoja utaona!!!!!
 
Ule vi Mbaya sana huu

Kunywa Gongo
Kuvuta Bangi ( Tena Kuvutia Bangi Chooni)
Kuvuta Bangi iliyochanganywa na Majani ya Chai na Mapapai
Ugoro
Chibuku na Tambaku

Ni Ulevi Mbaya sana

Unajua Job Ndugai angeongezea kidogo ile statement yake kuwa watu wengine wanenda kuongea na waandishi wa habari wakiwa wamevuta sigara mbalimbali na kulamba vitu tofautitofauti.
 
Nakumbuka maneno ya marehemu Nyerere aliwahi kusema "ULEVI WA MADARAKA" ndio huu, yaani ameshajiona anaweza akafikiria lolote likawa atakavyo yeye.
Huwa najiuliza inakuwaje raia mwema katika nchi anabadilika na kuwa gaidi!! ukandamizaji demokrasia kama huu ndio unapelekea mtu kuwa gaidi.

au anaambiwa kitu na mke wake na anakurupuka huko moja kwa moja kukifanya
 
Nilitabiri siku nyingi, huu ni mpango maalumu ulioandaliwa na serikali. Nilitoa comment baada kwamba huyu jamaa atakuja na mkwara wa kuifungia CDM.
 
Walishaambiwa na kapteni wao E.lowasa 'viongozi wengi wa c.c.m ni waoga kutoa na kufanya maamuzi magumu' maneno na vitisho vya nini? Si afanye analoona linampasa?huu ni uoga wa dhahiri
 
Tunajua Tendwa anaharisha....sasa hasitishie kujamba.......najua anatafuta pakufia wakati mda wake bado haujafika..asije akaamsha visukari na presha zilizojificha...oooooohoooo!
 
Msameheni bure kizee cha watu kinatetea ugali wake!

Tumsamehe bure kwani anajua kama akifanya alichotamka ni nini kitatokea na niwangapi watapoteza maisha na kupata vilema vya maisha? Hiyo ya kutetea ugali kwenye maisha ya watu haiwezivumilika
 
Hivi nani alimchagua? bunge au raisi kwani msajili anatakiwa achaguliwe na vyama vyote ili asipendelee chama
nadhani hapa kuna tatizo la kimadaraka kwani mtu mmoja kuwa na mamlaka ya kufuta chama kuna walakini
sheria inayoumruhusu imepitwa na wakati inatakiwa marekebisho mara moja kumuondolea kiburi.
lazima kuwe na tume ya kufuta vyama kama ilivo kwa majaji hawezi kufukuzwa na rais ingawa ndie aliemtea
we have to so something as soon as posible kukitoa hiki kizee na kiburi chake
 
Wamekosa kitu kimoja tu, nguvu ya umma ambayo ikiamua kuadabisha watawala ni balaa.

iko siku litatokea maana hata kama ni panya ukishambana sana akiona anakufa huwa anajaribu kujijitetea hata japo akurukie japo hatoweza kukuu basi walao akutoe ngeu, pia kimya kingi kina kishindo
 
Back
Top Bottom