Tendwa sasa atishia kukifuta CHADEMA

Tendwa sasa atishia kukifuta CHADEMA

atafuta CHAMA lakini wanaojenga Chama wataendelea kuwepo anajisumbua

Nadhani hilo hakulitafakari! (You may kill our bodies but our souls will remain ... forever... to witness the changes we fight for...) Labda afute na wanaojenga chama!!
Kule upande wa pili wanasema ..."msimwogope anayeweza kuua tu mwili .... bali mwogopeni yule ambaye anaweza kuua vyote.... mwili na roho...."
 
''Huyu Tendwa atakuwa mbeya sana'' By Ramadhan Omary Mapuri.
 
Tendwa na CCM yao wanahaha, watu wameshachoka huu mfumo na mambo 2015 yatakuwa mabaya sana kama wakingangania madaraka, mi nawashauri tu wasome alama za nyakati kwani kutumia jeshi la police kuvuruga mikutano ya CDM si njia sahihi ya kufifisha vuguvugu la mabadiliko, watu wameshaamua. kufanya hivyo basi jeshi hilo litakuwa linasafisha njia ya mabosi wao kwenda kwa MR. OKAMPO, watampoza JK bure, wamwache akabidhi nchi na astaafu kwa amani;

Wajibu wa chama chochote cha siasa ni kujinadi kwa wananchi wakati wote, sasa sijui walitaka CDM ijinadi hapo nje ya ofisi ya makao makuu kinondoni? naomba majibu ndugu msajili. Sababu hazina msingi, mara barabara nyembamba, mara sensa, mara msafara utapita, mara watu wanalima eti kilimo kwanza, mara kuna tetesi za al-shabab kuvamia mikutano: yote haya kuzuia CDM isinadi sera zake za kumkomboa mtanzania masikini.

Sasa hizi sababu ndizo zinafanya wananchi wachukie sababu hazina uzito wowote: Sasa hili la mwandishi ndiyo mmeharibu kabisa na mungu kasaidia kutoa ushahidi mweupe pee.


Huyu mzee naye ni gamba lililokomaa.
 
maneno2 hayo hata kwenye kanga yako! Kama yeye kdume afute 2one!....sheeenz*
 
Masaburi

Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa amesema sasa amechoka kusikia mauaji kwenye mikutano ya kisiasa ya CDM na atatumia rungu lake kufutia usajili chama chochote kitakachoshindwa kutunza amani ya nchi.Tendwa amewaambia waandishi wa habari hatishiki na chama chochote kuwa na wabunge kwani sheria inamruhusu kufuta chama hata kama kina wabunge 100.

Katika hali ya kushangaza Tendwa ameshauri vyama visubiri nyajati za uchaguzi ndipo vifanye mikutano ya kisiasa.Hata hivyo amekiri sheria inaruhusu vyama kufanya mikutano na maandamano wakati wowote.

Source:Habari Radio Tumaini.
 
Tendwa kaimarisha imani yangu kuwa hii nchi haina kiongozi hata wa kulea watoto wa chekechekea! Baada ya Nchimbi na Tendwa, atakuja kuimba chorus?
 
Huyo mzee tendwa kweli anatendwa,hajui mageuzi yapo mioyoni mwa watu na si chadema hata akifuta mageuzi yako pale pale.mizee mingine bwana
 
Tendwa amechelewa sana, watanzania wa leo sio wale wakufuata mtu,bendera au jina la chama,

Watanzania wa leo wanajua wanachokipigania, wako tayari hata kuongozwa na mbuzi kwenye kupigania haki zao.

Kwa sasa wanakiunga mkono
CHADEMA kwa sababu kimeonyesha mwelekeo wa kupigania haki zao, sio bendera wala jina la chama!!
 
Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa amesema sasa amechoka kusikia mauaji kwenye mikutano ya kisiasa ya CDM na atatumia rungu lake kufutia usajili chama chochote kitakachoshindwa kutunza amani ya nchi.Tendwa amewaambia waandishi wa habari hatishiki na chama chochote kuwa na wabunge kwani sheria inamruhusu kufuta chama hata kama kina wabunge 100.

Katika hali ya kushangaza Tendwa ameshauri vyama visubiri nyakati za uchaguzi ndipo vifanye mikutano ya kisiasa.Hata hivyo amekiri sheria inaruhusu vyama kufanya mikutano na maandamano wakati wowote.

Source:Habari Radio Tumaini.

TENDWA kesha tendwa na wakuu wake. Hivi ulitegemea atoe tamko gani? Zamani busara ilitambuliwa kwa uwepo wa mvi kichwani, ila kwa leo wasahahu. Matamshi yake leo, yalitosha kuamini kuwa alikua anakikimbia kivuli chake. Ila msimlaumu saaana, kwani yaonekana ni miongoni mwa waliosoma lakini hawakuelimika. Duh!! watu hawa ndo wameifikisha Tanzania hapa ilipo leo. Ni watu wa kujikomba, kujipendekeza na wenye kudai nyeupe kuwa ni nyeusi ilihali ukweli wanaujua
 
Sasa yeye Tendwa analalama nini kama huo uwezo wa kukifuta CHADEMA? Nafikiri anatesti zali. Ajaribu kufuta Mkombozi wa Wanyonge ili aone uhondo na faida ya kutokuwa ethical leader. Kwa msemo wa Mzee Ojwang, akijaribu tu "ataona Kanga aliona" (with jaluo accent).

Kuna umuhimu gani wa kuunda tume wakati Jaji Tendwa ana hukumu mezani tayari? Yaani ukilewa madaraka kishikaji basi akili na busara nazo zinahamia masaburini...sorry but that's the fact.
 
kwa uwazi kabisa nasema na nitaendelea kuamini hivyo; Tendwa kwa sasa hana ubavu wa kuifuta Chadema.
Wino alioutumia kuandika jina la Chadema kwenye makaratasi yake unaweza kufutika lakini ule uliotumika kuiandika Chadema kwenye mioyo ya wananchi huwa haufutiki.
 
Huyu kapata maelekezo maalumu,hili ni jambo muhimu sana katika kuliweka katika tume ya kurekebisha katiba msajili wa vyama hatakiwi kuchaguliwa na chama tawala,inatakiwa uwekwe utaratibu utakaotoa haki kwa vyama vyote,sasa anawekwa msajili wa vyama kutoka CCM si kiama tunatafuta hapa?
 
Tatizo la kuteua ktk nafasi nyeti watu used
 
Viongozi wote wa Serikali, CCM na Dola kweli ni waoga na mbumbumbu kabisa,

Toka harakati za M4C zianze wote matumbo moto, sasa nimeamini mtaji wa watawala wetu ni ujinga na woga wa watanzania.

Asante M4C kwa kutupa uelewa na ujasiri wa ajabu kuhusu haki zetu.

Safii, safi sanaaa!!
 
Back
Top Bottom