Tetesi: TCRA Wanaomiliki laini (simkadi) zaidi ya moja katika mtandao mmoja kupokonywa ifikapo June 2020

Sasa tukimiliki laini zaidi ya moja kuna madhara gani? labda waje watueleweshe kama kuna sababu yoyote ya msingi. vinginevyo ni kuipunguzia mapato nchi kwa huo muda watakaozima.
wanasema ndiyo chanzo Cha utapeli na wizi eti
 
faini ukikamatwa 5mil au jela 12 month au vyote viwili
 
Kuna kipindi mwaka nafikiri 1985 nilikuwa nasoma gazeti la Mfanyakazi.

Katika sehemu ya "Amini Usiamini" waliandika, jiji la Tokyo Japan lina line za simu nyingi kuliko bara zima la Africa.

Nafikiri tunataka kurudi huko.

Sent from my typewriter using Tapatalk
We kikongwe KUMBE? Mwaka 85!!!!!
 
Na matapeli bado wapo wanatumia simu kutapeli watu TCRA hamlijui hili
ukiwauliza hivyo wanakujibu hawana taarifa za mlalamikaji!
ukiwapelekea wanakujibu Rudi kwa mtoa huduma wako!
ukienda kwa mtoa huduma wanakujibu Rudi polisi ulikotapeliwa, ukifika polisi wanakwambia lete risiti na box la kununulia simu, ukipeleka wanakupa mpelelezi ambaye Hana nauli! hapo ndo utatoboka
 
ukiwauliza hivyo wanakujibu hawana taarifa za mlalamikaji!
ukiwapelekea wanakujibu Rudi kwa mtoa huduma wako!
ukienda kwa mtoa huduma wanakujibu Rudi polisi ulikotapeliwa, ukifika polisi wanakwambia lete risiti na box la kununulia simu, ukipeleka wanakupa mpelelezi ambaye Hana nauli! hapo ndo utatoboka
I see....!!
 
We kikongwe KUMBE? Mwaka 85!!!!!
Kikongwe bibi yako.

Nyie watu wenye life expectancy ndogo kama nzi kila mtu mnamuona kikongwe.

Kumbe tatizo wote mnakufa mapema siku si zenu kwa umasikini, ujinga na magonjwa.

Wakati huku duniani Michael Jackson kafariki na miaka 50, watu wakalalamika "kafariki mdogo sana".

You don't want it with me. I don't do it, I overdo it.

Bloody uharo!
 
Mbona tabu jamani?kwa kazi zangu ninatumia sana internet na kupiga,hivyo nimejiunga chuo na utumishi je ni kosa? Maana siwezi gharama zote kwa pamoja.Ni usumbufu sana TCRA mtuonee huruma.
 
Hii ndio tatizo ya kuwapa wazee waendeshe shirika wana mawazo ya kizamani zamani tu , Mh Raisi tunakuomba hizi taasisi za kiserikali ziongozwe na vijana wa kisasa wenye Elimu na exposure ambayo itakuja kusaidia ubunifu kama nchi za wenzetu (Young Blood)

Hawa Wazee wa TCRA hawana mpya wanataka kuonekana na wao wanafanya kazi kwa kusumbua Sisi wana nchi
 
Hii ndio tatizo ya kuwapa wazee waendeshe shirika wana mawazo ya kizamani zamani tu , Mh Raisi tunakuomba hizi taasisi za kiserikali ziongozwe na vijana wa kisasa wenye Elimu na exposure ambayo itakuja kusaidia ubunifu kama nchi za wenzetu (Young Blood)

Hawa Wazee wa TCRA hawana mpya wanataka kuonekana na wao wanafanya kazi kwa kusumbua Sisi wana nchi
yaani tabu tupu
 
Kusema ukweli kwa hili TCRA mnatuchanganya! Inaonesha hamjajipanga!
Usumbufu umekuwa mwingi mno!
  • Tulisajili kwa majina mara ya kwanza, mkasema ni batili mkasema zoezi lirudiwe,
  • Tukarudia tukasajili kwa vitambulisho vya kura, napo mkasema ni batili
  • Mkasema tukamilishe usajili kwa kupiga picha mwaka juzi tukafanya hivyo lakini bado ikawa ni batili;
  • Mwaka jana mkadai tusajili kwa vitambulisho vya NIDA kwa alama za vidole, tumefanya hivyo bado mnaona hiyo haitoshi!
  • Mnataka mwaka huu wenye laini zaidi ya moja kwenye mtandao mmoja muwazimie simu zao walizozisajili
TCRA kwa hili sasa sio ungwana kabisa! Naona kama ni usumbufu mnaofanya wala siyo weledi!

Kuna majibu mepesi eti; kwa wamiliki wanaohitaji laini zaidi ya moja watatakiwa kusaini fom maaalum;
Swali!
  1. Kama electronic data za vidole hamziamini mtu amiliki laini zaidi ya moja, je hizo fomu maalum ndo zitaaminika?
  2. Hizo fomu zinawafikiaje wananchi huko vijijini?
  3. Kuna wafanya biashara ambao wana office zaidi ya moja ambazo zinahitaji namba za simu zaidi ya moja hilo hamjalifikilia?
  4. ufanisi na mazingila ya rushwa katika maombi maalum ya simkad mbili mnayajua?
TCRA mtatukosea sana
Inawezekana bado hawajambana wanayemtafuta, wakimpata tutatulia.
 
Back
Top Bottom