Tetesi: TCRA Wanaomiliki laini (simkadi) zaidi ya moja katika mtandao mmoja kupokonywa ifikapo June 2020

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,249
21,345
Kusema ukweli kwa hili TCRA mnatuchanganya! Inaonesha hamjajipanga!
Usumbufu umekuwa mwingi mno!
  • Tulisajili kwa majina mara ya kwanza mwaka 2002~2005, mkasema ni batili mkasema zoezi lirudiwe,
  • Tukarudia tukasajili kwa vitambulisho vya kura 2007~2009, napo mkasema ni batili
  • Mkasema tukamilishe usajili kwa kupiga picha mwaka 2012~2014 tukafanya hivyo lakini bado ikawa ni batili tena;
  • Mwaka 2018~19 mkadai tusajili kwa vitambulisho vya NIDA kwa alama za vidole, tumefanya hivyo bado mnaona hiyo haitoshi!
  • Mwaka 2020 wenye laini zaidi ya moja kwenye mtandao mmoja mlitangaza kwamba mtawazimia simu zao walizozisajili
  • Bado baadhivya simu ukipiga zinataka kukamilisha usajili sasa ni USAJILI GANI, yaani UHAKIKI GANI tena mnautaka mtu afanye kama siyo kusumbuana?
Mi naona ni usumbufu mnaofanya wala siyo weledi!

Kuna majibu mepesi eti; kwa wamiliki wanaohitaji laini zaidi ya moja watatakiwa kusaini fom maaalum;
Swali!
  1. Kama electronic data za vidole hamziamini mtu amiliki laini zaidi ya moja, je hizo fomu maalum ndo zitaaminika?
  2. Hizo fomu zinawafikiaje wananchi huko vijijini?
  3. Kuna wafanya biashara ambao wana office zaidi ya moja ambazo zinahitaji namba za simu zaidi ya moja hilo hamjalifikilia?
  4. ufanisi na mazingila ya rushwa katika maombi maalum ya simkad mbili mnayajua?
TCRA mtatukosea sana!

HIZO SIMU ZIMENI TU TUJUE MOJA SIYO KUTISHANA KILA SIKU NA HAMZIMI
 
Haya mambo ya ajabu kabisa.
Tuambieni huu woga wa watu kumiliki namba zaidi ya moja kwa mtandao mmoja unatokana na nini?
Leteni sababu!!

Kama nimesajili namba moja yangu, ya pili nimeacha nyumbani kwa matumizi ya simu ya nyumbani inakuwaje hii?
Kama nimesajili laini tatu zingine za kwenye vibanda vyangu vya biashara ya kawaida sio kampuni inakuwaje hii?
 
Unaandika tetesi wakati kanuni ziko wazi tangia mwezi wa 2 tarehe 7! Na usipoteshe eti watapokonywa ila sema utapaswa kuchagua ni lain hipi uitumie na nyingine uziache na pia unaruhusiwa kuwa na lain zaid ya moja ndani ya mtandao mmoja isipokuwa lazima uireport utaitumia kwa matumizi ya modem tu na si vinginevyo.
 
Unaandika tetesi wakati kanuni ziko wazi tangia mwezi wa 2 tarehe 7! Na usipoteshe eti watapokonywa ila sema utapaswa kuchagua ni lain hipi uitumie na nyingine uziache na pia unaruhusiwa kuwa na lain zaid ya moja ndani ya mtandao mmoja isipokuwa lazima uireport utaitumia kwa matumizi ya modem tu na si vinginevyo.
Mara nyingi watu huwa wanatenganisha laini ya biashara na laini binafsi.

Au Mara nyingine mtu anakuwa na laini moja kwa ajili ya miamala tu na nyingine kwa matumizi ya kawaida.

Kumwambia mtu atumie laini kwa modem tu sio sawa kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaandika tetesi wakati kanuni ziko wazi tangia mwezi wa 2 tarehe 7! Na usipoteshe eti watapokonywa ila sema utapaswa kuchagua ni lain hipi uitumie na nyingine uziache na pia unaruhusiwa kuwa na lain zaid ya moja ndani ya mtandao mmoja isipokuwa lazima uireport utaitumia kwa matumizi ya modem tu na si vinginevyo.
Mkuu bora umemwambie wewe, Watu wamekuwa walalamishi mpaka inakera, anyway wengine wanajitetea kwa uhalifu wao waendeleee na Simu ya Mke na Mchepuko kivyake. Kwa wale Wafanyabiashara Rasmi upo utaratibu wa Simu za Kibiashara unapata mpaaka Laini 50 ktk mtandao mmoja. Sasa kama biashara yako hulipi kodi kazi kwako.
Mwanaume unamiliki laini za Simu kila mtandao kwani wewe Dalaliiii! Hizi dalili mbaya
 
Mkuu bora umemwambie wewe, Watu wamekuwa walalamishi mpaka inakera, anyway wengine wanajitetea kwa uhalifu wao waendeleee na Simu ya Mke na Mchepuko kivyake. Kwa wale Wafanyabiashara Rasmi upo utaratibu wa Simu za Kibiashara unapata mpaaka Laini 50 ktk mtandao mmoja. Sasa kama biashara yako hulipi kodi kazi kwako.
Mwanaume unamiliki laini za Simu kila mtandao kwani wewe Dalaliiii! Hizi dalili mbaya
Hapo kwa hiyo post unajiona booooonge la mjanjaaaa! Kumbe hovyo tu mavi kinuka
 
Hapo kwa hiyo post unajiona booooonge la mjanjaaaa! Kumbe hovyo tu mavi kinuka
Vip nawewe ni Kizazi malalamiko! Tafuta pessa mkuuu malalamiko hayana tijja. Ukiwa na pessa Laini moja tu ya Simu inakutosha huna hajja ya Haloteli umpigie kwa Halo, Voda kwa Voda nk. Ukiwa njema UNATWANGA KOTE KOTE KWA LAINI MOJA hayo mambo ya kuwa na Laini Kibao ni Ishara za Uwoga wa Maisha.
 
Kusema ukweli kwa hili TCRA mnatuchanganya! Inaonesha hamjajipanga!
Usumbufu umekuwa mwingi mno!
  • Tulisajili kwa majina mara ya kwanza, mkasema ni batili mkasema zoezi lirudiwe,
  • Tukarudia tukasajili kwa vitambulisho vya kura, napo mkasema ni batili
  • Mkasema tukamilishe usajili kwa kupiga picha mwaka juzi tukafanya hivyo lakini bado ikawa ni batili;
  • Mwaka jana mkadai tusajili kwa vitambulisho vya NIDA kwa alama za vidole, tumefanya hivyo bado mnaona hiyo haitoshi!
  • Mnataka mwaka huu wenye laini zaidi ya moja kwenye mtandao mmoja muwazimie simu zao walizozisajili
TCRA kwa hili sasa sio ungwana kabisa! Naona kama ni usumbufu mnaofanya wala siyo weledi!

Kuna majibu mepesi eti; kwa wamiliki wanaohitaji laini zaidi ya moja watatakiwa kusaini fom maaalum;
Swali!
  1. Kama electronic data za vidole hamziamini mtu amiliki laini apendavyo, je hizo fomu maalum ndo zitaaminika?
  2. Hizo fomu zinawafikiaje wananchi huko vijijini?
  3. Kuna wafanya biashara ambao wana office zaidi ya moja ambazo zinahitaji namba za simu zaidi ya moja hilo hamjalifikilia?
TCRA mtatukosea sana
TCRA kimekuwa chombo cha kero na kupokwa uhuru mdogo wa watumia simu. Wasichokijua ni kuwa watanzania wakiacha kutumia hizo simu ni serikali ndio itakayoathirika kwa kukosa mapato. Yaani wao ni kubaba watu, kubana watu, kubana watu tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaandika tetesi wakati kanuni ziko wazi tangia mwezi wa 2 tarehe 7! Na usipoteshe eti watapokonywa ila sema utapaswa kuchagua ni lain hipi uitumie na nyingine uziache na pia unaruhusiwa kuwa na lain zaid ya moja ndani ya mtandao mmoja isipokuwa lazima uireport utaitumia kwa matumizi ya modem tu na si vinginevyo.
Kwanini wawapoke watu uhuru wa kutumia line kwa idadi watakayo? Hivi wamekosa kabisa shuhuli ya maendeleo mpaka kuwanyanyasa watu kwenye simu tu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kwenye namba tatu nimekuelewa sana
Kusema ukweli kwa hili TCRA mnatuchanganya! Inaonesha hamjajipanga!
Usumbufu umekuwa mwingi mno!
  • Tulisajili kwa majina mara ya kwanza, mkasema ni batili mkasema zoezi lirudiwe,
  • Tukarudia tukasajili kwa vitambulisho vya kura, napo mkasema ni batili
  • Mkasema tukamilishe usajili kwa kupiga picha mwaka juzi tukafanya hivyo lakini bado ikawa ni batili;
  • Mwaka jana mkadai tusajili kwa vitambulisho vya NIDA kwa alama za vidole, tumefanya hivyo bado mnaona hiyo haitoshi!
  • Mnataka mwaka huu wenye laini zaidi ya moja kwenye mtandao mmoja muwazimie simu zao walizozisajili
TCRA kwa hili sasa sio ungwana kabisa! Naona kama ni usumbufu mnaofanya wala siyo weledi!

Kuna majibu mepesi eti; kwa wamiliki wanaohitaji laini zaidi ya moja watatakiwa kusaini fom maaalum;
Swali!
  1. Kama electronic data za vidole hamziamini mtu amiliki laini apendavyo, je hizo fomu maalum ndo zitaaminika?
  2. Hizo fomu zinawafikiaje wananchi huko vijijini?
  3. Kuna wafanya biashara ambao wana office zaidi ya moja ambazo zinahitaji namba za simu zaidi ya moja hilo hamjalifikilia?
TCRA mtatukosea sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vip nawewe ni Kizazi malalamiko! Tafuta pessa mkuuu malalamiko hayana tijja. Ukiwa na pessa Laini moja tu ya Simu inakutosha huna hajja ya Haloteli umpigie kwa Halo, Voda kwa Voda nk. Ukiwa njema UNATWANGA KOTE KOTE KWA LAINI MOJA hayo mambo ya kuwa na Laini Kibao ni Ishara za Uwoga wa Maisha.
Mmi nina sim card mbili moja ni ya biashara ipo kwenye social media na vipepereshi hii naizima ikifika saa kumi na mbili jion pia juma pili na sikukuu siiwashi na line nyingine ndio matumiz yangu binafsi hii sheria ni ya ki whack balaa
 
Hawa TCRA wamekua wasanii wasanii tu mimi mpaka leo sijasajili na bado nipo hewani kama kawa (hawajafunga) dogo walimfungia line zake baada ya muda akaziweka hewani zinapiga kazi kama kawaida (kuweka vocha kupiga simu na kujibu msg vyote vinafanyika)

kimsingi naweza kusema ni wazee wa kuzua taharuki tu ili wapate kiki hamna kazi wanafanya kama tu wameshidwa kuwathibiti wale wazee wa "ile hela tuma kwenye namba hii" sasa wataweza nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
38 Reactions
Reply
Back
Top Bottom