meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,464
- 4,829
- Thread starter
-
- #141
PASCO,Huyo mkurugenzi ni bora angekuwa alisema hivyo.Walichokuwa wanasema na kusisitiza ni wananchi wahakikishe wananunua ving'amuzi ili mitambo ya analogy itakapozimwa waendelee kupata televisheni za nyumbani bure na za ziada za kulipia.Hawakuweka msisitizo unaotakiwa kuelezea utofauti uliopo kati ya hizo leseni ya ving'amuzi mbalimbali.
Wananchi hao wakawa wananunua bora king'amuzi kama walivyoshauriwa na hao TCRA wako.Usiwatetee kwamba wametoa elimu kuhusu utofauti huu unaousema wewe wa ving'amuzi.Wao walikomaa zaidi na kuwapa elimu wananchi wasitupe tv za migongo,jambo ambalo ni rahisi sana kueleweka wakaacha yale tatanishi kama hili la makampuni.
Sasa wale waliofuata maneno ya hilo li TCRA lako wakanunua ving'amuzi walivyovichagua(sio startimes,ting wala hiyo ambayo umesema ya star tv na ITV,ambayo bado haipo sokoni na tayari wana leseni!) wakitegemea kuwa wataona free local channel kumbe hawakuambiwa kuwa hayo makampuni hayana mandate ya kurusha free channel waende wapi sasa?
Ni serikali ipi ilipaswa kutoa elimu hii kuhusu huu utofauti wa makampuni?Kuwalaumu tu kuwa wabongo ni wazito sio kuwatendea haki kwani watu wengi sana wamenunua ving'amuzi vyao kabla hata ya tangazo lenu rasmi TCRA.Wasiliana na huyo ndugu yako Mungi mwambie aje huku kujibu kwanini watu waendelee kulipia local channel kisa hawakununua ving'amuzi tajwa na wao(TCRA) wala hawakuwaambia wasinunue hivyo ving'amuzi.Kwa nini wanasema sasa ambapo watu wameshanunua ving'amuzi hivyo visivyotakiwa.Huoni kama huku ni kuibiana na kunyanyasana?
Mara ya mwisho nimenunua ile ya intelsat kwa 80 na decoder yake.Ningependa kujua satelite dish linauzwa kiasi gani cha pesa za madafu?:confused2:
acha uvivu. inaonyesha hukuwa unafuatilia matangazo ya tcra. changamoto zipo lakini baadhi yetu hatupendi mabadiliko.
nani anayeamua station flani ijiunge na kinga'muzi flani?ni TCRA au Wamiliki wa station husika?
mkunashukuru kwa kuendelea kufafanua swali langu la msingi.naona pasco anahangaika sana kutoa details ambazo hatuhizihitaji kwa sasa.
Naona hakuna mwenye jibu sahihi kwa swali la meningitis...! Shame on TCRA...!
$akubaliano ya wamiliki na Multplex wakishindwana ndio hivyo chali kama clouds na Startimes wameshindwana.
Ukinunua king'amuzi cha kampuni yo yote, free local channels zote unazipata b'cause TCRA wametoa license kwa local providers ikiwa na condition hiyo,nani anayeamua station flani ijiunge na kinga'muzi flani?ni TCRA au Wamiliki wa station husika?
Ukinunua king'amuzi cha kampuni yo yote, free local channels zote unazipata b'cause TCRA wametoa license kwa local providers ikiwa na condition hiyo,
PascoMkuu Jipu, kuhusu pesa kiukweli ninazo, mimi nalipwa elfu 20,000 kila siku, (zile bahasha zetu huwa zinawekwa 20,000), hivyo kwa wiki natengeneza Sh. 100,000 kwa mwezi natengeneza 400,000?= hizi ni pesa nyingi sana kwa mwandishi wa habari, kwa kifupi kwa fedha hizo, mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari matajiri sana, hata nyumba ninayokaa, nimepanga vyumba vitatu!, yaani jiko, chumba na sebule!, usafiri niliokuwa nikiutumia sikuzote ilikuwa ni bodaboda, lakini sasa nimeweza hata kubadili usafiri kutoka boda boda sasa natumia bajaj!.
Huko Sinza tunakokunywa kwenye hizo baa 250, wengi wetu tunakunywa huko kutokana na uwezo, mfano mimi ningependa sana niwe nakunywa Samaki Samaki pale Mlimani City, ila bei yao iko juu, na mimi uwezo wangu ni wa kunywa bia moja kila siku, na siku ya mwisho wa mwezi, huweza hata kuywa bia 3!, hivyo nikijinyima tuu bia 4 kwa mwezi, pesa hiyo inatosha kulipia king'amuzi!.
Siombi msamaha kuwasisitiza kuwa kuna watu wanapenda zaidi kuendekeza starehe kuliko kuzijali familia zao!. Hakuna TV inayouzwa chini ya laki!, kama uliweza kununua TV zaidi ya laki, utashindwaje kununua kingamuzi elfu 30?!.
Kwani wewe "ile starehe" huwa unailipia sh, ngapi?, au unalipwa Sh. ngapi?!. Nunueni vingamuzi, tuko katika ulimwengu wa digitali, lazima na sisi tubadilike tuishi kidigitali!.
P.
Wanatakiwa wajipange upya... Ghafla kupata habari Tanzani kunageuka kuwa ni bidhaa adimu......
Duuuu!!!Hii kali aisee!!!Mimi nadhani tuwape mwez mmoja kama mambo yenyewe ni magumashi hivi tuingie mtaani tudai haki yetu ya kupata habari,nina wiki mbili hata sijui dunia ikoje tena!!!startimes nao wanarusha matangazo ya ki-analojia kwa mtindo wa ki-dijitali.
unaongelea theory au practical experience?