TAARIFA KUTOKA SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA (TBS)
Ufafanuzi kuhusu bidhaa ya Majani ya Chai ya "SAFARI PRIMIUM TEA"
@TBS_Tanzania
====
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayoonesha utata unaotokana na taarifa iliyopo kwenye kifungashio kuhusu uasili wa bidhaa ya majani ya chai aina ya Safari Premium Tea na matumizi ya alama ya ubora ya TBS kwa chai inayoingizwa kutoka Kenya na kufungashwa hapa nchini.
TBS inapenda kuujulisha umma kuwa bidhaa hiyo inazalishwa na kiwanda cha Afri Tea and Coffee Blenders (1986) Ltd cha jijini Dar es Salaam, Tanzania na kimepewa leseni namba 1595 ya kutumia alama ya ubora ya TBS kwenye bidhaa za Blended Black Tea (Green Label Tea, Kilimanjaro, African Pride, Simba Chai, Simba Chai Tangawizi, Safari Premium Tea) tangu mwaka 2014 na bidhaa zote hizi zinazalishwa Tanzania na kwa kutumia malighafi kutoka ndani ya nchi.
Kutokana na taratibu za utoaji leseni, kiwanda hiki kimekuwa kikikaguliwa kwa vipindi tofauti ambapo ukaguzi wa mwisho ulifanyika tarehe 2022-08-11 ambapo hakukuwa na mabadiliko yoyote kuhusu utaratibu wa uzalishaji na malighafi. Hivyo, kufuatia taarifa hiyo, TBS ilifanya ukaguzi wa dharura kiwandani tarehe 2023-02-20 na kujiridhisha kwamba mzalishaji aliingiza chai kama malighafi kutoka Kenya mwezi Oktoba, 2022 bila kutoa taarifa kwa TBS kama mkataba (Scheme of Inspection and Test) unavyotaka. Hivyo. suala hili linashughulikiwa na hatua stahiki zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria.
TBS inawashukuru wananchi wote ambao wanaendelea kutoa ushirikiano kwani suala la udhibiti wa usalama na ubora wa bidhaa ni mtambuka.
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja kwa namba 0800 110 827.
Ufafanuzi kuhusu bidhaa ya Majani ya Chai ya "SAFARI PRIMIUM TEA"
@TBS_Tanzania
====
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayoonesha utata unaotokana na taarifa iliyopo kwenye kifungashio kuhusu uasili wa bidhaa ya majani ya chai aina ya Safari Premium Tea na matumizi ya alama ya ubora ya TBS kwa chai inayoingizwa kutoka Kenya na kufungashwa hapa nchini.
TBS inapenda kuujulisha umma kuwa bidhaa hiyo inazalishwa na kiwanda cha Afri Tea and Coffee Blenders (1986) Ltd cha jijini Dar es Salaam, Tanzania na kimepewa leseni namba 1595 ya kutumia alama ya ubora ya TBS kwenye bidhaa za Blended Black Tea (Green Label Tea, Kilimanjaro, African Pride, Simba Chai, Simba Chai Tangawizi, Safari Premium Tea) tangu mwaka 2014 na bidhaa zote hizi zinazalishwa Tanzania na kwa kutumia malighafi kutoka ndani ya nchi.
Kutokana na taratibu za utoaji leseni, kiwanda hiki kimekuwa kikikaguliwa kwa vipindi tofauti ambapo ukaguzi wa mwisho ulifanyika tarehe 2022-08-11 ambapo hakukuwa na mabadiliko yoyote kuhusu utaratibu wa uzalishaji na malighafi. Hivyo, kufuatia taarifa hiyo, TBS ilifanya ukaguzi wa dharura kiwandani tarehe 2023-02-20 na kujiridhisha kwamba mzalishaji aliingiza chai kama malighafi kutoka Kenya mwezi Oktoba, 2022 bila kutoa taarifa kwa TBS kama mkataba (Scheme of Inspection and Test) unavyotaka. Hivyo. suala hili linashughulikiwa na hatua stahiki zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria.
TBS inawashukuru wananchi wote ambao wanaendelea kutoa ushirikiano kwani suala la udhibiti wa usalama na ubora wa bidhaa ni mtambuka.
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja kwa namba 0800 110 827.
Imetolewa na:
Gladness H. Kaseka
Gladness H. Kaseka