TBC watangaza rasmi kuonesha Bunge live

TBC watangaza rasmi kuonesha Bunge live

Dikteta katahayari na kugundua alikosea sana kutaka kubaka demokrasi ya bunge live, lakini bado kuna mengi tu ndani ya Serikali hii kuhusu ubakaji wa demokrasi nchini ambayo ni lazima tuendelee kuyamulika kwa nguvu zote.
 
Dikteta katahayari na kugundua alikosea sana kutaka kubaka demokrasi ya bunge live, lakini bado kuna mengi tu ndani ya Serikali hii kuhusu ubakaji wa demokrasi nchini ambayo ni lazima tuendelee kuyamulika kwa nguvu zote.
Kuna dikteta zaidi ya Mwenyekiti wa Chama Wa Maisha?!?!?!?
 
Hoja hapa ni kuruhusu vituo binafsi na TBC1 kuonesha Bunge, hiyo TBC2 wengi hawaioni, kwa hiyo sio sehemu muafaka kuifanya ya pekee kuonesha Bunge.
Kwanza ni channel ya kulipia, pili haipo kwenye visimbuzi vyote. Hapa bado hawajaliachia Bunge kusema kweli ila wamejaribu tu kutuliza mizuka ya wananchi.

Ova
 
Hawa ccm wanafanya mambo wakati mwingine yanakuacha kinywa wazi. Hovyo ksbisa! By the way, mbona Nape ndiye kawa msemaji sana wa bunge kuwa live? Nape ni msemaji wa bunge? Inakuwaje mawaziri wansingilia mambo ya bunge ambalo linatakiwa kuwasimamia? Nani anamsimamia mwenzake? Ndugai, what is this?!!!!
 
Ni kupitia TBC2. Wanadai wataonesha saa 3 asubuhi saa sita mchana, saa kumi na moja jioni na saa 4 usiku (recorded). Chanzo TBC

Naona hatimaye wamebana wee wameachia. Ila nina maswali kadhaa:

Je, TV binafsi zitaruhusiwa kurusha pia?
Je Je huo muda TBC wanarusha live watu watakuwa hawafanyi kazi? Kwa sababu walisema mwanzo lengo la kuzuia ni ili watu wafanye kazi!

Je, kwa nini wameamus kulificha bunge kwenye channel ya kulipia, yaani TBC2? Je kuangalia bunge likijadili mambo yetu wananchi ni luxury?

Je wale wasioweza kulipia hiyo channel hawana haki ya kuwasikia wawakilishi wao wakizungumzia matatizo yao bungeni?

Nina maswali mengi,
Hata hivyo niwapongeze wahusika kwa kukubali kwambs hapa walichemka! Naamini huu utakuwa mwanzo wa kuturudishia wananchi haki yetu ya kufuatilia kikamilifu yanayofanywa na wawakilishi wetu!
Hawa TBC nao vigeugeu
 
Hii kwangu siyo hoja hata kidogo tunamambo mengi sana ya kujali yenye manufaa kwa taifa.
 
Hii kwangu siyo hoja hata kidogo tunamambo mengi sana ya kujali yenye manufaa kwa taifa.
Kuna jambo lenye manufaa kwa taifa zaidi ya sisi wananchi kushiriki bunge live kwa kusikiliza wawakolishi wetu wakihoji serikali kuhusu kodi zetu? Hujui bunge kuoneshwa live linatufanya na sisi wananchi kushiriki moja kwa moja kuchangia na kukosoa pale wawakolishi wetu na serikali wanapofanya mambo yssiyo na maslaha kwetu? Acheni kujichanganya nyie majuha!
 
Mwisho mtasema kila mtu anunuliwe TV ili aone bunge. Kama mtu hana uwezo wa kuona bunge TBC2 basi atapata habari kupitia njia Zingine. Gov can only do so much. Kimsingi bunge inabidi liwe na channel yake inayoendeshwa kwa gharama zake
 
Back
Top Bottom