Ndio kwanza nimemaliza kusoma kitabu cha mwandishi Sandelin Wundrak; The History Of Economic Thinking. Kisha nimepitia mtandaoni taarifa mbali mbali. Ndio, kwa hapa nyumbani, Jerry Muro ni habari kubwa, ni mshtuko.
Jerry Muro. Sijapata kukutana naye. Nimefuatilia kazi zake tu, kwa kazi zake anaonekana kuwa ni kijana mahiri. Katika lililomfika, nina-sympathy nae. Yuko katika kipindi kigumu sana. Kwa mwanadamu mwenzako, ni kumpa pole tu, hayo mengine ni ya baadae.
Juu hapo mnaona picha ya ukuta. Ndio, bado natafakari ziara yangu ya siku moja pale kijijini Kalenga, ni kwenye ngome ya Chifu Mkwawa wa Wahehe. Nilikwenda huko Jumamosi ya juzi hapa. Mkwawa ni yule shujaa aliyewatoa jasho Wajerumani. Katika kupitapita kwangu mitaa ya kijiji hicho nilikutana na ukuta huo.
Nikakumbuka tungo ya ndugu yangu Mrisho Mpoto; "Ni heri kujenga daraja, kuliko ukuta!" Ningependa nikutane na mwenye nyumba au mwenye ukuta huo unaokaribia kuanguka. Nilitaka tujadili juu ya ukuta wake, kifalsafa zaidi. Hakuwepo nyumbani. Alikuwa shambani akipalilia mahindi yake, anaitwa Baba Gile ( Baba Grace).
Ndugu yangu Mrisho Mpoto, labda si heri kujenga daraja wala ukuta. Labda Baba Gile wa kijijini Kalenga angeniambia kipaumbele chake na cha wenzake ni kujengwa kwa njia mbili za mawasiliano; kati ya kiongozi na mwongozwa.
Naam. Aliye gizani anamwona aliye kwenye mwanga, lakini aliye kwenye mwanga hamwoni aliye gizani. Na ajionaye yuko kwenye mwanga aweza kabisa kuwa yu gizani na asimwone kabisa aliye kwenye giza jingine. Haiyumkini aliye topeni akajaribu kumwinua mwingine aliye topeni, wote watadidimia topeni!
Unajiuliza, yanahusianaje na Jerry Muro? Hii ni tafakari endelevu, haihusiani na Jerry Muro, bali inamhusu kila mmoja wetu akiwamo Jerry Muro. Inahusu maisha.
Maisha ni mapambano, kuna kushinda na kushindwa. Ushindi una gharama. Mwanadamu jiandae na gharama ya ushindi. Ushindi waweza kuwa ghali mno. Unaweza kupambana ukashinda, lakini gharama ya ushindi yaweza kuwa jamaa na marafiki wa wote uliowashinda watageuka kuwa maadui zako, yawezekana watakuwa maadui kwako kwa muda mrefu tu. Watakukasirikia, watafanya yote nawe upate maumivu.
Hivyo, mwanadamu usifikiri tu gharama ya kushindwa, fikiri pia gharama ya ushindi. Na wakati mwingine ni gharama inayostahili kulipwa. Franklin Roosevelt alikuwa Rais wa zamani wa Marekani. Alifahamu faida na hasara za kuwa na maadui. Waliompinga katika sera zake za kiuchumi aliwaita " Watiifu wa Kiuchumi" Na akasema; wamejiunga kwa pamoja kunichukia na nakaribisha chuki zao kwangu!
Kama unapigana vita ya muhimu, kama vita hivyo vyaweza vikawa vya kushinda ( winnable). Na kwamba umejiandaa kulipa gharama ya chuki ya muda mrefu ya utakaowashinda, basi, ingia vitani, na kama la, tafuta suluhu au rudisha majeshi nyuma kimpangilio ( tactical retreat).
Swali ni hili; utafikiaje uamuzi wa ama kuingia vitani au la? Saa yangu inaniambia ni saa saba usiku hapa Iringa. Naweza kuendelea kutafakari usiku kucha, nahitaji kulala. Nawe endelea kutafakari.
Maggid
Iringa
Tembelea: http://mjengwa.blogspot.com
Jerry Muro. Sijapata kukutana naye. Nimefuatilia kazi zake tu, kwa kazi zake anaonekana kuwa ni kijana mahiri. Katika lililomfika, nina-sympathy nae. Yuko katika kipindi kigumu sana. Kwa mwanadamu mwenzako, ni kumpa pole tu, hayo mengine ni ya baadae.
Juu hapo mnaona picha ya ukuta. Ndio, bado natafakari ziara yangu ya siku moja pale kijijini Kalenga, ni kwenye ngome ya Chifu Mkwawa wa Wahehe. Nilikwenda huko Jumamosi ya juzi hapa. Mkwawa ni yule shujaa aliyewatoa jasho Wajerumani. Katika kupitapita kwangu mitaa ya kijiji hicho nilikutana na ukuta huo.
Nikakumbuka tungo ya ndugu yangu Mrisho Mpoto; "Ni heri kujenga daraja, kuliko ukuta!" Ningependa nikutane na mwenye nyumba au mwenye ukuta huo unaokaribia kuanguka. Nilitaka tujadili juu ya ukuta wake, kifalsafa zaidi. Hakuwepo nyumbani. Alikuwa shambani akipalilia mahindi yake, anaitwa Baba Gile ( Baba Grace).
Ndugu yangu Mrisho Mpoto, labda si heri kujenga daraja wala ukuta. Labda Baba Gile wa kijijini Kalenga angeniambia kipaumbele chake na cha wenzake ni kujengwa kwa njia mbili za mawasiliano; kati ya kiongozi na mwongozwa.
Naam. Aliye gizani anamwona aliye kwenye mwanga, lakini aliye kwenye mwanga hamwoni aliye gizani. Na ajionaye yuko kwenye mwanga aweza kabisa kuwa yu gizani na asimwone kabisa aliye kwenye giza jingine. Haiyumkini aliye topeni akajaribu kumwinua mwingine aliye topeni, wote watadidimia topeni!
Unajiuliza, yanahusianaje na Jerry Muro? Hii ni tafakari endelevu, haihusiani na Jerry Muro, bali inamhusu kila mmoja wetu akiwamo Jerry Muro. Inahusu maisha.
Maisha ni mapambano, kuna kushinda na kushindwa. Ushindi una gharama. Mwanadamu jiandae na gharama ya ushindi. Ushindi waweza kuwa ghali mno. Unaweza kupambana ukashinda, lakini gharama ya ushindi yaweza kuwa jamaa na marafiki wa wote uliowashinda watageuka kuwa maadui zako, yawezekana watakuwa maadui kwako kwa muda mrefu tu. Watakukasirikia, watafanya yote nawe upate maumivu.
Hivyo, mwanadamu usifikiri tu gharama ya kushindwa, fikiri pia gharama ya ushindi. Na wakati mwingine ni gharama inayostahili kulipwa. Franklin Roosevelt alikuwa Rais wa zamani wa Marekani. Alifahamu faida na hasara za kuwa na maadui. Waliompinga katika sera zake za kiuchumi aliwaita " Watiifu wa Kiuchumi" Na akasema; wamejiunga kwa pamoja kunichukia na nakaribisha chuki zao kwangu!
Kama unapigana vita ya muhimu, kama vita hivyo vyaweza vikawa vya kushinda ( winnable). Na kwamba umejiandaa kulipa gharama ya chuki ya muda mrefu ya utakaowashinda, basi, ingia vitani, na kama la, tafuta suluhu au rudisha majeshi nyuma kimpangilio ( tactical retreat).
Swali ni hili; utafikiaje uamuzi wa ama kuingia vitani au la? Saa yangu inaniambia ni saa saba usiku hapa Iringa. Naweza kuendelea kutafakari usiku kucha, nahitaji kulala. Nawe endelea kutafakari.
Maggid
Iringa
Tembelea: http://mjengwa.blogspot.com