BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,377
- 8,121
Kwa mujibu wa taarifa za Manunuzi na Mikopo ambayo haijalipwa (OPL) kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), hadi kufikia Desemba 2023, Nchi 8 za Afrika Mashariki zilikuwa na Deni la Tsh. 16,805,982,380,014 kutoka kwa Mkopeshaji huyo (IMF).
Kenya imetajwa kuwa na Deni kubwa zaidi kulinganisha na Nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo hadi Desemba 2023, Deni lilikuwa zaidi ya Tsh. Trilioni 5.1 ikifuatiwa na Nchi za DR-Congo, Uganda, Tanzania, Rwanda, Sudan Kusini, Burundi na Somalia.