Maryam Malya
Senior Member
- Nov 29, 2021
- 115
- 258
Na Mwl Udadis, Tarime
Utafiti mpya kwa wawekezaji wa kimataifa na wa ndani umetoa takwimu kuwa Tanzania ni nchi ya tatu inayopendelewa zaidi kwa uwekezaji barani Afrika na ya kwanza kwa Afrika Mashariki. Hii ni kwa mujibu wa Kampuni ya wataalam wa kimataifa katika shughuli za mahesabu ya KPMG.
Kwa mara nyingine Tanzania inaendelea kuiacha nyuma nchi ya Kenya katika uwiano ndani ya Afrika mashariki. Sera nzuri na uongozi makini wa Rais Samia Suluhu Hassan hauwezi kutengwa na mafanikio haya makubwa na ya kuvutia.
Nchi 5 bora kwa uwekezaji Kusini mwa Jangwa la Sahara:
1. Afrika Kusini
2. Nigeria
3. Tanzania
4. Ghana
5. Kenya
Asilimia 80 ya wawekezaji walisema wanapendelea kufanya biashara nchini Nigeria (30%) na Afrika Kusini (50%) kwa siku za usoni, ambazo ni nchi kubwa za uchumi barani humo. Tanzania (15%), Ghana (14%), na Kenya (14%) zinashika nafasi ya juu kwenye orodha ya nchi zinazopendelewa kwa uwekezaji.
Kwa mujibu wa TIC katika kipindi cha kuanzia Mwaka 2021 hadi Julai 2023, Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) kilisajili jumla ya miradi 778 yenye thamani ya dola Bilioni 10 na Milioni 532. Usajili huu wa kihistoria ni ushuhuda kwa utafiti huu mpya kuthibitisha mafanikio ya kazi kubwa inayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Utafiti mpya kwa wawekezaji wa kimataifa na wa ndani umetoa takwimu kuwa Tanzania ni nchi ya tatu inayopendelewa zaidi kwa uwekezaji barani Afrika na ya kwanza kwa Afrika Mashariki. Hii ni kwa mujibu wa Kampuni ya wataalam wa kimataifa katika shughuli za mahesabu ya KPMG.
Kwa mara nyingine Tanzania inaendelea kuiacha nyuma nchi ya Kenya katika uwiano ndani ya Afrika mashariki. Sera nzuri na uongozi makini wa Rais Samia Suluhu Hassan hauwezi kutengwa na mafanikio haya makubwa na ya kuvutia.
Nchi 5 bora kwa uwekezaji Kusini mwa Jangwa la Sahara:
1. Afrika Kusini
2. Nigeria
3. Tanzania
4. Ghana
5. Kenya
Asilimia 80 ya wawekezaji walisema wanapendelea kufanya biashara nchini Nigeria (30%) na Afrika Kusini (50%) kwa siku za usoni, ambazo ni nchi kubwa za uchumi barani humo. Tanzania (15%), Ghana (14%), na Kenya (14%) zinashika nafasi ya juu kwenye orodha ya nchi zinazopendelewa kwa uwekezaji.
Kwa mujibu wa TIC katika kipindi cha kuanzia Mwaka 2021 hadi Julai 2023, Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) kilisajili jumla ya miradi 778 yenye thamani ya dola Bilioni 10 na Milioni 532. Usajili huu wa kihistoria ni ushuhuda kwa utafiti huu mpya kuthibitisha mafanikio ya kazi kubwa inayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.