MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,223
- 22,301
Wakuu leo naandika nikiwa na mawazo mengi sana. Mara nyingi nimekuwa nikileta nyuzi za masuala ya kitaifa ila leo huu uzi ni wa ishu yangu binafsi. Mimi kada mtiifu wa CCM kwa sasa kuna mambo nimeshindwa kuelewa kabisa kwa huyu mwanamke ambaye nimetangaza nia ya kumuoa. Nataka ushauri wenu.
Baada ya harakati za hapa na pale kutafuta soulmate ndo mwaka 2022 nikabahatika kukutana na msichana mrembo aliyekuwa akimalizia diploma yake ya Nursing. Ingawa hakuwa mwanachama wa CCM nikapiga moyo konde kwamba fresh tu kwasababu ndo sio siasa. Wakati tumeanza mahusiano akanipa sharti la kutomtafuna hadi ndoa. Alisema yeye ni bikra.
Nilishtuka ila nikaona labda kwasababu anataka awe bize na masomo kwa sababu ndo alikuwa akimalizia diploma yake. Hili sharti lake nikasema acha nilivumilie kwasababu kama ni papuchi zipo nyingi nikizidiwa nitajipooza kwingine. Huyu ni wa ndoa.
Siku zikaenda akahitimu masomo yake. Tukakubaliana tuanze taratibu za kuelekea ndoa baada ya graduation yake. Bahati mbaya matokeo yalivyotoka kuna masomo akawa amefeli. Ikabidi arudie mwaka. Nikavumilia tena na kusubiri bila kutuma mshenga wal kufanya lolote hadi alipofanya mitihani yake ya mwisho mwezi May.
Baada ya mitihani nikamwambia inabidi sasa nianze mchakato. Kilichonishtua hadi kuandika uzi huu ni msichana kukataa kabisa hata kutuma mshenga na angalau uchumba kuwa rasmi hadi matokeo yake ya mitihani itoke. Kiukweli hii kwangu mimi naona imenilemea kuliko hata lile sharti la kutofanya mapenzi hadi ndoa. Nimejiuliza inakuwaje matokeo yake ya mitihani yamzuie hata mshenga kupeleka ujumbe wakati nikiwa chuo watu walikuwa wanaoana kabisa wakiwa bado wanafunzi?
JF kwa sasa ni kama familia yangu hivyo nawakaribisha wanafamilia kwa ushauri. Nimeandika nikiwa na ukame mkali sana.
Baada ya harakati za hapa na pale kutafuta soulmate ndo mwaka 2022 nikabahatika kukutana na msichana mrembo aliyekuwa akimalizia diploma yake ya Nursing. Ingawa hakuwa mwanachama wa CCM nikapiga moyo konde kwamba fresh tu kwasababu ndo sio siasa. Wakati tumeanza mahusiano akanipa sharti la kutomtafuna hadi ndoa. Alisema yeye ni bikra.
Nilishtuka ila nikaona labda kwasababu anataka awe bize na masomo kwa sababu ndo alikuwa akimalizia diploma yake. Hili sharti lake nikasema acha nilivumilie kwasababu kama ni papuchi zipo nyingi nikizidiwa nitajipooza kwingine. Huyu ni wa ndoa.
Siku zikaenda akahitimu masomo yake. Tukakubaliana tuanze taratibu za kuelekea ndoa baada ya graduation yake. Bahati mbaya matokeo yalivyotoka kuna masomo akawa amefeli. Ikabidi arudie mwaka. Nikavumilia tena na kusubiri bila kutuma mshenga wal kufanya lolote hadi alipofanya mitihani yake ya mwisho mwezi May.
Baada ya mitihani nikamwambia inabidi sasa nianze mchakato. Kilichonishtua hadi kuandika uzi huu ni msichana kukataa kabisa hata kutuma mshenga na angalau uchumba kuwa rasmi hadi matokeo yake ya mitihani itoke. Kiukweli hii kwangu mimi naona imenilemea kuliko hata lile sharti la kutofanya mapenzi hadi ndoa. Nimejiuliza inakuwaje matokeo yake ya mitihani yamzuie hata mshenga kupeleka ujumbe wakati nikiwa chuo watu walikuwa wanaoana kabisa wakiwa bado wanafunzi?
JF kwa sasa ni kama familia yangu hivyo nawakaribisha wanafamilia kwa ushauri. Nimeandika nikiwa na ukame mkali sana.