Tatizo la WiFi hotspot na USB teethering kwenye HTC naomba msaada

Tatizo la WiFi hotspot na USB teethering kwenye HTC naomba msaada

Siwezi kufungua mitandao mkuu na kibaya zaidi nilikuwa nimeshapata mteja wa kuinunua na haya majanga ndo yakatokea

Una uhakika umefanya configuration vizuri za APN kwa kila line? ( bila shaka umeweka line 2).
 
Huawei Y518 ni dual SIM ambapo slot moja ni kwa ajili ya GSM network na ya slot ya pili ni kwa ajili ya TD-SCDMA.

TD-SCDMA ni aina ya 3G network ambayo inatumiwa huko China...

Tanzania hatupo katika standard hiyo pamoja na kwamba carriers wetu wana 3G network. Bongo sisi tumekuwa standardized kwa WCDMA kwa traffic zote za 3G...

Hivyo wewe unapata data kwa kupitia slot ya GSM pekee na utakuwa limited kwenye Edge (E) pekee...

Kabla ya kununua simu hizi za Wachina au Wakorea muwe mnafanya review ya matoleo ya simu.

cc Chief-Mkwawa
Asante sana maelezo yako yanafanana na simu ilivyo.
So no option?
 
Wakuu bado nasubiri msaada wenu kwenye teethering naona issue bado ni ngumu
 
Ninakabiliwa na tatizo la kutofanya Tethering kwenye lumia 520.
 
Asee naomba msaada namna ya kuconnect simu yangu na laptop kwa kutumia hotspot and teethering...
 
Hebu tuambie umejaribu ukakwamia wapi na ni simu aina gani.
 
Ndio nimeweka laini mbili mkuu, kwahiyo hiyo configuration inafanywaje?

Utaratibu wa kuconfigure ni ule ule iwe kwa line moja au mbili...

Kitu cha muhimu ni kuwa kila mtandao una parameters zake, mathalani mtandao wa tiGO wao hutumia "tigoweb" kama APN...Usipo-configure APN sahihi hutaweza kupata data.

Pia baada ya kufanya configuration, lazima kwa kila line uactivate data, mathalani kwa simu za Samsung huwa na SIM card manager ambapo hapo utachagua master na slave SIM card kwa ajili ya mojawapo kukupa 3G na nyingine 2G au zote kukupa 2G.
 
Wakuu bado nasubiri msaada wenu kwenye teethering naona issue bado ni ngumu

Mkuu niliomba unipe version ya HTC yako lakini naona kimya...kuna baadhi ya simu zimebaniwa kutumia Foxfi

Anyway kama Foxfi imegoma naomba uitoe halafu rudi ggogleplay na udownload PDANet+ ambayo haina masharti...

Ikigoma tena mkuu nitakuwa sina msaada, labda itahitaji kufanya rooting au kutafuta version nyingine ya OS iliyo international...
 
Back
Top Bottom