Alikuwa Nyerere Watanzania mlimuona mbaya mkampa na jina la Musa,,
1: Akaja Mwinyi na sera yake ya Ruksa naye hakutoka salama kwa kulalamikiwa kuwa uchumi wa nchi ulishuka fedha yetu akaiporomosha thamani yke,,
3: Akaingia Mkapa,, akajitahidi kuinua uchumi wetu na kuifanya fedha yetu irudishe heshima yke mipakani mwa jirani zetu,, hata alipo ondoka akasema bila kumung,unya maneno kwamba ameacha Hazina yetu imejaa fedha tele za nje na ndani,, aliye mrithi naye akakili mbele yetu kuwa ni kweli amekuta fedha nyingi ndani ya Hazina ya taifa,,
Lakini Mkapa pia hakutoka salama walimwita ,,Ukapa ,,na lawama nyingi zisizo andikika hapa.
4:Akaja Kikwete ,, huyu sina haja ya kueleza mengi alifanya nchi kuwa ni shamba la bibi,, kila mwenye kucha na meno makali alijikatia apendavyo mali za umma. Huyu Ufisadi wa aina zote ulifanyika ktk utawala wake ,, yeye akatoka na jina la mzee wa Trip na kucheka cheka.
Eti kwamba muda mwingi alikuwa anazurura nje huku watu Waki Escrow,, Epa,na Kurichmond mali za umma.
5: Sasa kaja Msukuma ana uchungu wa ardhi ya kwao ilivyo achwa mashimo baada ya wajanja kuondoka na madini yote waliyoyakuta kule Ardhini,,
Amekuja na machungu ya wizi wa makontena na mafuta pale bandarini,, amekuta nchi imejaa hewa kila kona ya sekta ya umma,, amekuta Hazina haina hata Sumuni ndani yake,,
Amekuta Madeni yamejaa kila kona ya ndani na nje.,
Kwa kifupi amekuta nchi imeoza ngozi yote inatoa harufu,, sasa anaanika juani ngozi ikauke apunguze harufu ndani pado tena Watanzania tunalalamika tu,,
Hivi tunataka tupewe Rais wa namna gani?kama wote Hawakutufaa na huyu naye tunaona hafai tunataka aje malaika kutuongoza?