Tatizo la Rais Magufuli ni hili

Tatizo la Rais Magufuli ni hili

Kuna haki za wanyo ge zaid ya huduma za afya?
Kaka nikupe mfano mdogo nilinunua eneo fulani na nilipewa offer lakini wajanja wenye pesa wakanizulumu. Baada ya kuingia hii serikali wengine tuliozurumiwa viwanja vyetu kwa kutumika kwa watumishi wa ardhi tulipewa viwanja vingine. Hilo kwako utalisemaje
 
Sio kwamba ni mtu mbaya au ana nia mbaya ila tatizo lake sina uhakika anajua anachokifanya. Tatizo lake kubwa ni kuharibu mema aliyoyakuta kuwa mapya, haimaniishi waliopita waliyotenda yote ni mabaya ila kuna mazuri.

Tatizo lake ni pale anapoharibu yale mazuri aliyoyakuta kama vile
Mikopo ya elimu
Madawa hospitalini
Demokrasia
Uhuru wa habari
Ajira kila mwaka
Kupanda madaraja na mishahara

Angeweza kuwa bora na kuonekana bora sana kama angefanya anayoyafanya bila kuathiri aliyoyakuta. Sasa unapotafuta watumishi hewa huku hutaki kuajiri na kupandisha watu madaraja hatuwezi kuona umuhimu wa kutoa watumishi hewa.

Sasa unaponunua ndege ilihali watu wanakosa madawa hatuwezi kuona kama kununua ndege kuna umuhimu. Sasa unapopunguza mishara ya wakubwa wakati ya wadogo inakushinda kupandisha hatuwezi kukuelewa.

Rais acha kuharibu mazuri uliyoyakuta bali yaendeleze.
Magufuli ana mchanganyiko wa kuwa na roho mbaya na ushamba.

Mchanganyiko mbaya sana huu.

Bora uwe na roho mbaya halafu sio mshamba utajua kukaa na watu (Mkapa), bora uwe mshamba halafu huna roho mbaya watu watajua kukaa na wewe (Mwinyi).

Ukiwa na roho mbaya halafu mshamba utashindwa kukaa na watu na watu hawatataka kukaa na wewe (Magufuli).
 
Anatetea haki gani ya wanyonge?
Km mnyonge leo hii umezuia ajira zake, umeondoa mkopo, umeondoa fao la kujitoa, hospital hazina dawa, watu hawajalipwa mishahara miezi 7, umeondoa posho na hajapandisha watu madaraja.
Haki gani hiyo anayoipaigania? Angekuwa anapigania hiv vyote vingeenda sambamba .
He is a sadist na ana uwezo mdogo wa kufikiria na kufanya kazi.

Hiv kwa mfano. Ww ni dokta halafu unawaambia wagonjwa warudi nyumbani na huwezi kutibu kwa miezi 3 sbb unafanya ukarabati wa majengo ya hospitali na kununua vifaa. Je, wagonjwa watakuelewa? Ma je, utakuwa mtetezi wa wagonjwa?
Je, kwann usikarabati majengo na kununua vifaa huku unatibu wagonjwa?

HAPO NDIYO HUJUE KUWA UNA UWEZO MDOGO WA KUFIKIRIA NA KUFANYA KAZI
Ana uwezo mdogo wa kufikiri na kufanya maamuzi yenye busara
 
Mkuu kuna official ststement imetolewa inasema hivyo au ni zile threads za Nkanga Chief zilizopelekea apigwe BAN?
Nkanga chief mm namkubali yupo sahihi kbsa alichosema sbb angalia hata ile official statement aliyoitoa madam haijaonesha ajira ni lini zaid ya kukanusha.

Wangekuwa wanaajiri mwaka huu wangesema huu ni mwezi wa 10 na kibaya zaid baada ya kumaliza uhakiki wanahamia kweny mishahara hiv ww unategemea wataajiri lini?
Ni mwakani watapishana mwezi tu na mr hero kinga chief.

Wadogo wakipinga km yule mwalimu aliyekataa timu mag ifanye mahafali shuleni na kuvaa sare kashushwa cheo

lkn mukulu yy alitamka mwezi 1 na nusu haitazidi miwili mpaka leo kimya naye atumbulie, haya madam yupo tu na uhakiki miezi 7 kakomaa tu huku watu wanataabika mtaani naye angetumbuliwa.
Wa diploma kwenda chuo GPA 3.5 mara 3.0 huyu wakutumbuliwa wanakurupuka tu.

Mbona wao hawajitumbui?
 
Tatizo umezoea dili, kwa hiyo aendelee kuzurura, ahachane na wafanyakazi hewa watafune hela zetu, aliyekuambia serikali anaajiri wahitimu wote ni nani??? NAKUULIZA????? Kama tuna wahitimu ambao hawawezi kutumia ujuzi wao kupambana na mazingira wanayoishi wanasubiri ajira ya serikali! Maendeleo yatakuwa mbali sana
Mkuu huu utaratibu wa kuajiri ulikuwepo tangu enzi zz nyerere na kikwete
Najua ww mfia chama lkn kumbuka mwebyekit wenu alisema nn?
Mwezi 1 na nusu haitazidi miwili lkn mpaka leo kimya. Kwann asitoe tamko km alivyosema mwanzo
AJITOKEZE HADHARANI TU ASEME AJIRA HAKUNA, HAMNA MTU ATAKAYE ANDAMANA.
Nyie mbona mnaiba mpaka kura na kutembea na wasanii km fiesta lkn hii yote mpate kulisha matumbo yenu kwann nanyi hamuachi kuiba?
Angalia zenji meshindwa live kbsa kwa vile mna njaa mkaamua mrudie uchaguzi mlishe matumbo yenu.

KWANN MLIRUDIA UCHAGUZI? Km nyie mlivyorudia uchaguzi ili mlishe matumbl yenu. Na ss tunataka hizo ajira
 
Kweli reforms zinasababisha kelele mingi sana. Mfano chukulia reform ya posho za kuzima mwenge wee!!! Hapo sasa watakapochukuliwa hatua waliosababisha mifumo hewa.

Na washawasha!
 
Mkuu huu utaratibu wa kuajiri ulikuwepo tangu enzi zz nyerere na kikwete
Najua ww mfia chama lkn kumbuka mwebyekit wenu alisema nn?
Mwezi 1 na nusu haitazidi miwili lkn mpaka leo kimya. Kwann asitoe tamko km alivyosema mwanzo
AJITOKEZE HADHARANI TU ASEME AJIRA HAKUNA, HAMNA MTU ATAKAYE ANDAMANA.
Nyie mbona mnaiba mpaka kura na kutembea na wasanii km fiesta lkn hii yote mpate kulisha matumbo yenu kwann nanyi hamuachi kuiba?
Angalia zenji meshindwa live kbsa kwa vile mna njaa mkaamua mrudie uchaguzi mlishe matumbo yenu.

KWANN MLIRUDIA UCHAGUZI? Km nyie mlivyorudia uchaguzi ili mlishe matumbl yenu. Na ss tunataka hizo ajira
Ni akili ndogo kufikiri serikali inafanya kazi kwa mawazo yako. Suala la ajira serikali inajua inachokifanya ni sahihi na kina tija katika kuimarisha mfumo wa utumishi wa umma.
 
Well said Mkuu, tatizo kubwa la Magufuli ni incompetence. He is clueless. Kwa mtu kama Rais kutokujua unachokifanya kunaweza kuwa na garama sawa au hata zaidi ya ufisadi. Vyote ni hasara na tatizo kwa maendeleo ya jamii.
 
Tatizo ninaliliona ni kwamba anaona ni yeye pekee mwenye uwezo wa uongozi
Sidhani anashaurika,wala kujua anaweza kufanya makosa
Mawaziri na viongozi wote serikalini wapo hapo kwa jili ya kutimiza matakwa yake tuu,hakuna. wa kumfunga paka kengele
TATIZO NI KUWA MWL(TEACHER) TEACHERS THEY TREAT EVERYBODY LIKE THEIR STUDENT AND TEST US IF WE MAKE NOISE THEY SIT BACK AND RETHINK (LAZIMA TUPIGE KELELE VINGINEVYO HATUTAFIKA KUMBUKENI HATUNA DIRA YA TAIFA)
 
Huwa mtu wa kawaida akifanya jambo zuri au kuongea point nzuri inaonekana nayo ya kawaida tu,

Hao wanaowaita important figure hata wakiongea au kufanya ujinga inaonekana nacho ni important figure vilevile!!.


Lakin hao important figure hata wakitabasamu kesho yake utakuta vichwa vya habar vimeandika "WAZIRI ATABASAMU" tena kwenye front page...wakati mda huo huo kuna mtu katoa mawazo mazur na kamwe huwez yaskia!!....
 
Mtalalama sana awamu hii lakini ndo kama hivyo JPM harudi nyuma kuinyoosha nchi
Hajalalamika,kaongea point mhim sana,sema kwa sabab kaandika hapa itabaki kuwa ni ya hapa,Magu kuna maeneo anafanya vzr shida kama hashauriki,au anashauriwa vsvyo hasa kwenyebaadhi ya maeneo kama alivyojarbu kuainisha mtoa mada
Kwani mwaka huu imeajiri wangapi unaposema haiwezi kuajiri wote?
Elimu ya Tanzania inaandaje wahitimu kupambana na mazingira kwa kutumia elimu yao?
Tukitaka kuendelea lazima tukubali kukosolewa, sio kusifiwa tu siku zote.
Kumbuka maneno ya Mwinyi (Rais mstaafu awamu ya 2) kuhusu mwenendo wa serikali.
Kauli za watu kama hao lazima zichambuliwe... sio kila kitu mnapinga tu mnapokosolewa.
 
TATIZO NI KUWA MWL(TEACHER) TEACHERS THEY TREAT EVERYBODY LIKE THEIR STUDENT AND TEST US IF WE MAKE NOISE THEY SIT BACK AND RETHINK (LAZIMA TUPIGE KELELE VINGINEVYO HATUTAFIKA KUMBUKENI HATUNA DIRA YA TAIFA)
Hakuna mtu niliyemuona wa hovyohovyo kama wewe usiyejua hata dira ya taifa lako. Hivi kumbe kukosa maarifa na uelewa ni mzigo sana. Kaa na ukasome ujifunze dira ya taifa lako watu watakushangaa sana. Hata ukiwa nje ya inchi utasema inchi haina dira.
 
Hakuna mtu niliyemuona wa hovyohovyo kama wewe usiyejua hata dira ya taifa lako. Hivi kumbe kukosa maarifa na uelewa ni mzigo sana. Kaa na ukasome ujifunze dira ya taifa lako watu watakushangaa sana. Hata ukiwa nje ya inchi utasema inchi haina dira.
Acha kuropoka wewe nchi haina dira inaenda kama gari bovu
 
Back
Top Bottom