ALWATAN KIZIGO
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 541
- 648
Hakika watu wa kale walipata kunena kwamba "Mti mrefu haukosi upepo" - ikiwa na maana kwamba, mtu anayefanya vizuri hukutana na maneno mengi ya ukinzani na nongwa.
Mfano huo naweza kuutumia kwa namna ambavyo baadha ya vikundi maalumu vya watu waliojipanga katika kudogodosha,kuchafua, kudhoofisha neema na mazuri mengi ambayo Mh.Dr.Samia Suluhu Hassan ameyafanya na anayoendelea kuyafanya katika ustawi wa Tanzania.
Hakuna atakayekosa ushahidi wa picha ,namba au idadi ya hatua kubwa alizopiga katika ujenzi wa Taifa letu .
Wale watu maalumu waliojikusanya na kujipanga katika kuharibu taswira hiyo ,ni wanapaswa waulizwe kosa la Rais Samia ni nini??
Je ni kumwaga ajira kama njugu, je kuilowesha Tanzania kwa miradi kemkem ya maji ,Je ni kuipa nuru Tanzania kwa miradi ya umeme vitongonijini,je kuongeza mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, Je ni kupandisha madaraja na mishahara kwa watumishi wa umma, je ni kutoa mikopo kwa wajasiriamali vijana na wanawake,je ni bima ya afya kwa wote, nishati safi, ujenzi wa mashule hopitali, zahanati na vituo vya afya kila kata, ukweli ni kwamba ya kuelezea yapo mengi mwenye macho ajionee.
Ipo siku tutamkumbuka na kusema naam tulipata Rais bora kuwahi kutokea.
Namalizia kwa kusema :
“Bahari haitulii kwa sababu ya mawimbi; mwenye safari huendelea na jahazi lake.”
Mheshimiwa Rais endelea kulisongesha jahazi lako.
Augustino Chiwinga
LINDI
Mfano huo naweza kuutumia kwa namna ambavyo baadha ya vikundi maalumu vya watu waliojipanga katika kudogodosha,kuchafua, kudhoofisha neema na mazuri mengi ambayo Mh.Dr.Samia Suluhu Hassan ameyafanya na anayoendelea kuyafanya katika ustawi wa Tanzania.
Hakuna atakayekosa ushahidi wa picha ,namba au idadi ya hatua kubwa alizopiga katika ujenzi wa Taifa letu .
Wale watu maalumu waliojikusanya na kujipanga katika kuharibu taswira hiyo ,ni wanapaswa waulizwe kosa la Rais Samia ni nini??
Je ni kumwaga ajira kama njugu, je kuilowesha Tanzania kwa miradi kemkem ya maji ,Je ni kuipa nuru Tanzania kwa miradi ya umeme vitongonijini,je kuongeza mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, Je ni kupandisha madaraja na mishahara kwa watumishi wa umma, je ni kutoa mikopo kwa wajasiriamali vijana na wanawake,je ni bima ya afya kwa wote, nishati safi, ujenzi wa mashule hopitali, zahanati na vituo vya afya kila kata, ukweli ni kwamba ya kuelezea yapo mengi mwenye macho ajionee.
Ipo siku tutamkumbuka na kusema naam tulipata Rais bora kuwahi kutokea.
Namalizia kwa kusema :
“Bahari haitulii kwa sababu ya mawimbi; mwenye safari huendelea na jahazi lake.”
Mheshimiwa Rais endelea kulisongesha jahazi lako.
Augustino Chiwinga
LINDI