Tatizo la Rais Magufuli ni hili

Tatizo la Rais Magufuli ni hili

Baba yenu

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2016
Posts
1,053
Reaction score
1,418
Sio kwamba ni mtu mbaya au ana nia mbaya ila tatizo lake sina uhakika anajua anachokifanya. Tatizo lake kubwa ni kuharibu mema aliyoyakuta kuwa mapya, haimaniishi waliopita waliyotenda yote ni mabaya ila kuna mazuri.

Tatizo lake ni pale anapoharibu yale mazuri aliyoyakuta kama vile
Mikopo ya elimu
Madawa hospitalini
Demokrasia
Uhuru wa habari
Ajira kila mwaka
Kupanda madaraja na mishahara

Angeweza kuwa bora na kuonekana bora sana kama angefanya anayoyafanya bila kuathiri aliyoyakuta. Sasa unapotafuta watumishi hewa huku hutaki kuajiri na kupandisha watu madaraja hatuwezi kuona umuhimu wa kutoa watumishi hewa.

Sasa unaponunua ndege ilihali watu wanakosa madawa hatuwezi kuona kama kununua ndege kuna umuhimu. Sasa unapopunguza mishara ya wakubwa wakati ya wadogo inakushinda kupandisha hatuwezi kukuelewa.

Rais acha kuharibu mazuri uliyoyakuta bali yaendeleze.
 
Rais asiyeelewa watu wanataka nini...............

Rais ambaye yupo tayari kukwamisha Marengo nandoto za wengine kwa mawazo yake ya kimasikini ...............

Kama alivyofanya wale wa udom na mikopo chuo kikuu ni janga kwa taifa.......

Kiufupi rais kama huyo inatakiwa tumkemee...........
 
Tatizo ninaliliona ni kwamba anaona ni yeye pekee mwenye uwezo wa uongozi
Sidhani anashaurika,wala kujua anaweza kufanya makosa
Mawaziri na viongozi wote serikalini wapo hapo kwa jili ya kutimiza matakwa yake tuu,hakuna. wa kumfunga paka kengele
 
Sio kwamba ni mtu mbaya au ana nia mbaya ila tatizo lake sina uhakika anajua anachokifanya!!

Tatizo lake kubwa ni kuharibu mema aliyoyakuta! Kuwa mpya haimaniishi waliopita waliyotenda yote ni mabaya ila kuna mazuri

Tatizo lake ni pale anapoharibu yale mazuri aliyoyakuta kama vile

Mikopo ya elimu
Madawa hosp
Demokrasia
Uhuru wa habari
Ajira kila mwaka
Kupanda madaraja na mishahara

Angeweza kuwa bora na kuonekana bora sana kama angefanya anayoyafanya bila kuathiri aliyoyakuta

Sasa unapotfuta watumishi hewa huku hutki kuajiri na kupandisha watu madaraja hatuwez kuona umuhim wa kutoa watumishi hewa

Sasa unaponunua ndege ilihali watu wanakosa madawa hatuwez kuona kama kununua ndege kuna uhim

Sasa unapopunguza mishara ya wakubwa wakati ya wadogo inakushinda kupandisha hatuwez kukwelewa

Jpm acha kuharibu mazuri uliyoyakuta bali yaendeleze
Yeye alishatamka hajaribiwi na anajiona yeye Mungu mtu na analolifanya yeye hataki mtanzania yeyote ahoji..........

Lema ametamka jana kuwa mtu wa aina hiyo Mungu anaweza kukatisha............ Kabla ya mwaka 2020.
 
Well said mkuu, huwa sometimes najiuliza au kuna surprise mkuu anatuandalia? au anataka watanzania tujue umuhimu wa kutumia pesa kwa mambo ya msingi tu?(Japo kwa hili amefanikiwa kwa 80% sasa hivi watu hawapati pesa na wakipata wanatumia kwa mambo ya msingi). Lakini unapotoa hela za deal basi weka njia watu wapate za halali.
 
Tatizo ninaliliona ni kwamba anaona ni yeye pekee mwenye uwezo wa uongozi
Sidhani anashaurika,wala kujua anaweza kufanya makosa
Mawaziri na viongozi wote serikalini wapo hapo kwa jili ya kutimiza matakwa yake tuu,hakuna. wa kumfunga paka kengele
Hivyo ndivyo typical dictators wanavyokuwa...
 
Nakupinga vibaya sana ! Hakuna Mtakatifu yeyote mwenye kasoro bhana .
 
Hali ni mbaya sana kwa Watumishi wa umma, sijui anategemea vipi kufikia matarajio yake huku anawa-frustrate watendaji wake wanaosaidia matarajio hayo yafikiwe.

Mimi hata simuelewi anawaza nini
 
Sio kwamba ni mtu mbaya au ana nia mbaya ila tatizo lake sina uhakika anajua anachokifanya. Tatizo lake kubwa ni kuharibu mema aliyoyakuta kuwa mapya, haimaniishi waliopita waliyotenda yote ni mabaya ila kuna mazuri.

Tatizo lake ni pale anapoharibu yale mazuri aliyoyakuta kama vile
Mikopo ya elimu
Madawa hospitalini
Demokrasia
Uhuru wa habari
Ajira kila mwaka
Kupanda madaraja na mishahara

Angeweza kuwa bora na kuonekana bora sana kama angefanya anayoyafanya bila kuathiri aliyoyakuta. Sasa unapotafuta watumishi hewa huku hutaki kuajiri na kupandisha watu madaraja hatuwezi kuona umuhimu wa kutoa watumishi hewa.

Sasa unaponunua ndege ilihali watu wanakosa madawa hatuwezi kuona kama kununua ndege kuna umuhimu. Sasa unapopunguza mishara ya wakubwa wakati ya wadogo inakushinda kupandisha hatuwezi kukuelewa.

Rais acha kuharibu mazuri uliyoyakuta bali yaendeleze.
Tatizo umezoea dili, kwa hiyo aendelee kuzurura, ahachane na wafanyakazi hewa watafune hela zetu, aliyekuambia serikali anaajiri wahitimu wote ni nani??? NAKUULIZA????? Kama tuna wahitimu ambao hawawezi kutumia ujuzi wao kupambana na mazingira wanayoishi wanasubiri ajira ya serikali! Maendeleo yatakuwa mbali sana
 
Tatizo umezoea dili, kwa hiyo aendelee kuzurura, ahachane na wafanyakazi hewa watafune hela zetu, aliyekuambia serikali anaajiri wahitimu wote ni nani??? NAKUULIZA????? Kama tuna wahitimu ambao hawawezi kutumia ujuzi wao kupambana na mazingira wanayoishi wanasubiri ajira ya serikali! Maendeleo yatakuwa mbali sana
Kwani mwaka huu imeajiri wangapi unaposema haiwezi kuajiri wote?
Elimu ya Tanzania inaandaje wahitimu kupambana na mazingira kwa kutumia elimu yao?
Tukitaka kuendelea lazima tukubali kukosolewa, sio kusifiwa tu siku zote.
Kumbuka maneno ya Mwinyi (Rais mstaafu awamu ya 2) kuhusu mwenendo wa serikali.
Kauli za watu kama hao lazima zichambuliwe... sio kila kitu mnapinga tu mnapokosolewa.
 
Back
Top Bottom