Tatizo la Maji na Ukame: Lawama zangu zote ni kwa Waziri Lukuvi na Waziri wa Mazingira

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Kuna muda ni lazima ukweli usemwe maana usiposemwa lazima kumbukumbu zitakuwa za upotoshaji Mkubwa

Kwenye Tatizo linaloikumba Tanzania la ukame na ukosefu wa Maji kwa sasa lawama zangu zote nazipeleka kwa watu wafuatao

1. William Lukuvi

Akiwa Waziri wa Ardhi kuanzia Awamu ya Tano, nchi yetu imeshuhudia urasimishaji mkubwa sana wa Mapori ya akiba pamoja na hifadhi kuwa makazi ya watu!

Jambo hili limepelekea kuongezeka kwa kiasi kikubwa sana uharibifu wa Mazingira hasa ukataji Miti wa kutisha kwenye mapori mengi yaliyokuwa yanategemewa kuleta mvua uliofanywa na Jamii za wafugaji na wakulima hasa kwenye mikoa ya Katavi, Rukwa, Tabora, Morogoro, Pwani na kusini mwa Tanzania.

Mfano wa hili nimejionea kwenye Mikoa ya Katavi, Kigoma na Tabora inayoongoza kwa kuwa na Misitu mingi.

Kwenye mikoa hii kumekuwa na uvamizi sana wa maeneo yenye mapori na misitu ya asili unaofanywa na Jamii za watu wa mikoa ya kanda ya ziwa na nchi jirani za Rwanda na Burundi. Watu hawa wamekuwa wakikata miti kwenye mapori kwa Kiwango cha kutisha na hata sasa takwimu zimeanza kuonesha hivi karibuni mito iliyokuwa ikititirisha maji mwaka mzima kwenye mikoa ya Kigoma na Katavi bila kusahau Rukwa imeanza kukauka kutokana na shughuli hizi za binadamu.

Waziri Lukuvi akiwa waziri wa Ardhi badala ya kushauri Serikali watu hawa waondolewe kwenye maeneo haya na kurudishwa kwenye maeneo yao ya asili yeye amezidi kushauri serikali watu hawa kurasinishwa kwenye maeneo hayo. Hivyo tusilaumu mtu. Tatizo ni Lukuvi

2. Mawaziri wa Mazingira kuanzia Awamu ya 3, 4, 5 na huyu wa Awamu ya 6

Hii ni Kwa sababu Nchi yetu imekuwa na Mawaziri wa Mazingira kwenye Awamu zote. Ila kamwe nchi hii haijawai kuwa na kampeni kubwa ya upandaji Miti.

Kila siku watu wamekuwa wakisema juu ya ukame na ukataji mkubwa wa Miti Ila kusema kweli Mawaziri wa Mazingira hawajawai kuanzisha kampeni ya Kitaifa kubwa inayohusu upandaji miti yenye lengo la kuhakikisha nchi inakuwa na misitu mingi, mapori mengi ivyo kuwa salama dhidi ya majanga ya ukame.

Kwa Waziri wa Sasa wa Mazingira Suleiman Jaffo huyu ndo naona ameshindwa kabisa kazi yake maana hata suala la mifuko ya plastiki naona linaanza kurejea kwa kasi sana. Ukitembea kwa basi kutoka Dar kuelekea mikoani hali unayoikuta barabarani inasikitisha. Kuna mifuko mingi ya plastic na materials nyingine za plastiki zimetupwa kando ya Barabara hadi unafikia kujiuliza Kama kucontrol plastiki au usafi tu inatushinda kwa nini tuwe wa Waziri wa Mazingira au Wakuu wa Mikoa na Wilaya?

Nilikuwa Mkoani Dodoma siku si nyingi nikaona hadi Kuna vibanda vya chips vimeanza kuwafungia wateja wake chips kwenye mifuko ya plastiki. Waziri Jafo lawama zangu haziwezi kukuacha kwenye hili maana unamuangusha Mama Samia. Kama huwezi kazi sema.

Hatari ninayoiona mbeleni
1. Sasa tumeanza ona baadhi ya sehemu zinapata mgao wa maji na umeme kutokana na ukame unaosababishwa na maamuzi mabovu pamoja na usimamizi mbovu ubaofanywa na watu walioaminiwa na kupewa madaraka. Hali ikienda hivi ninaona nchi ya Tanzania ikishindwa kuzalisha umeme wa kutosha na baadae chakula cha kutosha.

Tukishindwa kuzalisha umeme wa kutosha kutokana na ukame Mradi wa Bwawa la Nyerere utaonekana rasmi kuwa mradi ulioliingizia Taifa hasara kutokana na kushindwa kuzalisha umeme uliotarajiwa pamoja na kujengwa kwa gharama kubwa.

2. Naona baadae Taifa litakuwa tegemezi na gharama za maisha kuongezeka maradufu jambo linaloweza kuleta hatari kwa kuongezeka kwa matukio ya uhalifu kutokana na nchi kuanza kuwa tegemezi kwenye nishati na chakula!

Tuchukue hatua sasa
 
Kuna nchi nyingi za Waarabu jangwani hazina mapori, misitu wala mito ila zina maji tele ya kutosha
Kwenye maji wanatumia teknolojia inaitwa desalination. Ni teknolojia ya kusafisha maji chumvi hasa ya Bahari Kwa matumizi ya kunywa. Hii inatumika Israël, Saudia, Qatar, Kuwait na Dubai.

Ni teknolojia aghali sana inayohitaji fedha nyingi sana. Swali ni Je sisi tutaiweza na hali yetu ya kiuchumi?
 
Kwenye maji wanatumia teknolojia inaitwa desalination. Ni teknolojia ya kusafisha maji chumvi hasa ya Bahari Kwa matumizi ya kunywa. Hii inatumika Israël, Saudia, Qatar, Kuwait na Dubai.

Ni teknolojia aghali sana inayohitaji fedha nyingi sana. Swali ni Je sisi tutaiweza na hali yetu ya kiuchumi?
Kama tunaweza kununua ndege za matrilioni kwa cash hatushindiwi kutumia hiyo teknolojia, ni suala la vipaumbele tu.
 
Kwa ujumla nchi hii haina sera wala sheria. Viongozi na watendaji wa Serikali wanafanya mambo kwa unafiki na hulka za kutaka waonekane wazuri kwa kila mtu.

Itawezekana vipi wewe kiongozi au Serikali uonekane mzuri kwa mhalifu na mtu mwema.

Angalia hata suala tu machinga kuzagaa kila sehemu. Mara sijui waondoke, mara sijui wapangwe vizuri, mara sijui watafutiwe maeneo. Kauli zote hizi ni kwa sababu ya unafiki. Badala ya kuangalia sheria, kunakuwa na kauli ambazo hazieleweki ambazo zinawapa shida hata watendaji wa chini.

Sheria kama inasema hairuhusiwi kujenga au kufanya shughuli zozote kwenye vyanzo vya maji na hifadhi ya misitu, inatakiwa iwe hivyo. Kinachofuatia inatakiwa ni usimamizi tu wa sheria, siyo hadithi nyingine.

Sheria kama inasema mifuko ya plastic hairuhusiwi, hairuhusiwi kufanyia biashara au kuweka kitu chochote kwenye barabara au hifadhi ya barabara, inatakiwa iwe hivyo. Kinachofuatia ni taratibu za usimamizi. Hayo mambo sijui watafutiwe maeneo, kuna mtu aliwahi kutafutiwa hata nyumba tu ya kupanga? Si anatafuta mwenyewe?

Unafiki, katiba mbaya inayompa madaraka makubwa kupindukia Rais kiasi cha kila mtendaji kushindwa kufanya kazi mpaka asikie kauli ya Rais ni chanzo cha matatizo mengi. Mkiwa na Rais ambaye maamuzi yake ni ya hovyo, upeo duni au ana hulka ya kujipendekeza, nchi inabakia inayumbayumba tu.
 
Nchi zinazoongoza kuharibu mazingira duniani ni China, Marekani, India, Urusi na Japan ila hazina mgao wa umeme wala maji.
Sisi tuna vyanzo vyote vya maji ila hatujawahi kuacha kuwa na shida ya maji, hili ni tatizo la kiakili zaidi kuliko mazingira.
Kwa iyo tuharibu tu mazingira alafu tutumie hela kwenye teknolojia aghali ili kupata maji? Hii ndo hoja yako?
 
Unafikiri kwa nini watu wanaenda kujenga au kufanya shughuli zao kwenye vyanzo vya maji?
 
Nchi zinazoongoza kuharibu mazingira duniani ni China, Marekani, India, Urusi na Japan ila hazina mgao wa umeme wala maji.
Sisi tuna vyanzo vyote vya maji ila hatujawahi kuacha kuwa na shida ya maji, hili ni tatizo la kiakili zaidi kuliko mazingira.
Tatizo ufisadi tu kutengeneza michongo ya hela tu
Mleta mada alichoandika Ni cheap politics
 
Kwenye maji wanatumia teknolojia inaitwa desalination. Ni teknolojia ya kusafisha maji chumvi hasa ya Bahari Kwa matumizi ya kunywa. Hii inatumika Israël, Saudia, Qatar, Kuwait na Dubai.

Ni teknolojia aghali sana inayohitaji fedha nyingi sana. Swali ni Je sisi tutaiweza na hali yetu ya kiuchumi?
Tunanunua ndege kwa Tillions kadhaa na ndege hizo hazina kazi tutashindwa kufanya huo uwekezaji ?
 
Nemc nayo ilaumiwe kwa kushindwa kusimamia Mazingira ya nchi...Lukuvi hamna kitu pale bahati mbaya alifanya usanii akabakia kuwa Waziri ila hamna lolote la maana unaweza kusema kafanya hamna.
 
Kwenye maji wanatumia teknolojia inaitwa desalination. Ni teknolojia ya kusafisha maji chumvi hasa ya Bahari Kwa matumizi ya kunywa. Hii inatumika Israël, Saudia, Qatar, Kuwait na Dubai.

Ni teknolojia aghali sana inayohitaji fedha nyingi sana. Swali ni Je sisi tutaiweza na hali yetu ya kiuchumi?
Serikali ilikuwa imefanya order ya ndege zenye thamani ya $726m wakati huohuo imekopa $936m kujenga madarasa na matundu ya choo!!!!

Hatuna maji halafu tunanunua ndege za kuja kupaki.

Kwa vyanzo vya maji tulivyonavyo hatuhitaji hata hayo maji ya baharini.

Kikubwa ni ccm nchi imewashinda.
 
Nchi zinazoongoza kuharibu mazingira duniani ni China, Marekani, India, Urusi na Japan ila hazina mgao wa umeme wala maji.
Sisi tuna vyanzo vyote vya maji ila hatujawahi kuacha kuwa na shida ya maji, hili ni tatizo la kiakili zaidi kuliko mazingira.
Hujui California Marekani wamekuwa wakipata shida ya Maji? Hujui India napo wanapata shida ya Maji?

Alafu unajua chanzo kikuu cha Umeme kwa izo nchi zote? Kama hujui sio Maji ni Nuclear
 
Nchi zinazoongoza kuharibu mazingira duniani ni China, Marekani, India, Urusi na Japan ila hazina mgao wa umeme wala maji.
Sisi tuna vyanzo vyote vya maji ila hatujawahi kuacha kuwa na shida ya maji, hili ni tatizo la kiakili zaidi kuliko mazingira.
Kwangu mimi naona hii inaweza kuwa ni mipango ya kutuandaa kisaikolojia ili tukubaliane na tutakacholetewa nahisi si ajabu wakatokea wakina aptl wa kutosha lakini swali la msingi hapa ni je hii timu mpya iliyosajiliwa ndio tunaona haya mambo kwa nini sasa tusidhani huu usajili unajambo tusilolijua? Mbona wachezaji wa zamani hatukuona wala kusikia haya? Na je huu ukame wa miezi miwili tu gafla unatia shaka? Kwa kweli mwenda zake sikuwahi kumkubali ila kwa sasa kuna mambo nahisi alikua sahihi ngoja tusubiri dakika tisini
 
Serikali ilikuwa imefanya order ya ndege zenye thamani ya $726m wakati huohuo imekopa $936m kujenga madarasa na matundu ya choo!!!!

Hatuna maji halafu tunanunua ndege za kuja kupaki.

Kwa vyanzo vya maji tulivyonavyo hatuhitaji hata hayo maji ya baharini.

Kikubwa ni ccm nchi imewashinda.
Unadhani vyanzo vya maji vitaendelea kuwepo Kama Mazingira yanaharibiwa?
 
Tatizo ufisadi tu kutengeneza michongo ya hela tu
Mleta mada alichoandika Ni cheap politics
Cheap politics?

Kesho Panda basi kutoka Dar kwenda kanda ya ziwa. Ukikuta mito 5 tu inayotiririsha maji tena mengi nakupa hela. Nitafute inbox
 
Back
Top Bottom