Tatizo la Kukosa Usingizi (Insomnia) na tiba yake

KUKOSA USINGIZI(INSOMNIA/SLEEPLESS NIGHT)
Leo ninapenda tuongelee suala zima la kukosa usingizi.

Kwa kawaida mtumzima anatakiwa kulala masaa7-8 kwa usiku mzima. Lakini kunawatu hushindwa kulala kabisa au hulala kwa masaa machache sana kutokana na sababu mbalimbali.

KUKOSA USINGIZI(INSOMNIA) ni tatizo la kukosa usingizi japokuwa unafursa ya kuweza kulala,tatizo hili linaweza kuwa nilamuda mfupi au nila muda mrefu yani tatizo sugu ambapo mtu hushindwa kulala au kupata usingizi mzuri kw a miezi sita(6)au zaidi. Tatizo hili husababishwa na mambo mbalimbali lakini zaidi nitazungumzia jinsi tatizo hili linayosababisha kwa kuwa na UPUNGUFU WA MELATONIN HORMONE.

Melatonini hormone ni vichocheo vinavyo tengenezwa au kutolewa na pineal gland, homoni hizi husaidia kuucontrol mzunguko wetu wa kawaida wa kulala na kuamka, hurekebisha saa ya mwili(biological clock) hivyo ukiwa na hormone hizi za kutosha utaweza kulala usingizi mzuri wala hautachukua muda mrefu sana kitandani pasipo kupata usingizi kama hauna shughuli maalumu ya kufanya.

Melatonini hormone hupunguzwa uzalishwazi wake kwa asilimia 10%- 15% kila baada mtu akifikia umri wa miaka 35 na kuendelea.

SABABU ZINGINE ZINAZOSABABISHA KUKOSA USINGIZI
sababu ziko nyingi sana zikiwemo;
~Magonjwa hapa nimagonjwa mbalimbali kama Miguu kuwaka moto,pumu,shinikizo la damu,matatizo ya moyo,kipanda uso na kuwashwa au mzio.
~Baadhi ya matibabu hii inahusisha matumizi ya baadhi ya dawa Kali zenye kemikali
~Upungufu wa hormone za kijinsia estrogen
~Msongo wa mawazo

~Ugomvi na kelele

~Mazingira

~Kuishi au kufanya kazi za usiku katika mazingira yenye mwanga kwa muda mrefu hii huathiri sana.

ATHARI ZA KUKOSA USINGIZI
~Uchovu wa mwili au kuhisi mwili hauna nguvu.

~ kuwa na hasira au mkali bila sababu za msingi.

~Maamuzi mabovu

~Kupoteza kumbukumbu au kusahau sahau.

~kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi

~Kupatwa na magonjwa ya shinikizo la damu au kisukari n.k

MATIBABU
~Badili mfumo wako wa maisha hapa ni katika ulaji wa vyakula pendelea kula zaidi vitu asilia kama mboga za majani na matunda na punguza vyakula au vinywaji vyenye caffein.

~Kunywa maji kwa wingi

~Tumia Asali mbichi vijiko viwili usiku

~ weka mazingira mazuri ya mtu kulala

~Tumia dawa zinazo fanya uwe na hormone za melatonini katika kiwango sitahiki

KWA TIBA YA KUKOSA USINGIZI NA MAGONJWA MENGINE KAMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME,MATATIZO YA HORMON,VIDONDA VYA TUMBO,BAWASIRI,MATATIZO YA MIGUU KUWAKA MOTO,PRESSURE NA MENGINE MENGI, PIGA/SMS/WHATSAP +255(0) 717556768

AU
IN BOX FB NELLY BEDAH WAKUSONGWA

Pia unaweza kuniadd facebook kama nelly bedah wakusongwa ili kujifunza zaidi,

Pia usisahau kulike page yangu ya afya nelly health and beauty care products.
 
Habari ndgu,nimekuwa na tatizo la kukosa usingizi usiku,muda mwingine inanichukua masaa kama matatu kuupata baada ya kulala,nikishutuka usingzn ndo siupat tena had asubuh,nilipitiwa nkacnzia mchana hat kwa dk kdgo uck ndo nakesha kabisa,nipen ushauri make hili jambo laweza kuathiri afya yangu
 
Mimi nilikua na mastress yangu nikawa kawa wewe popo haswaaa.....kwanza tafuta chanzo cha kupoteza usingizi, kama ni mawazo jitahidi upunguze, mchana kuwa busy kupita kiasi mwili uchoke, Wahi kupanda kitandani oga hakikisha umekula umeshiba., zima simu kama kuna tv ama radio vyote fumba macho tafakari ukuu wa Mungu utalala tu.
 
Habari ndgu,nimekuwa na tatizo la kukosa usingizi usiku,muda mwingine inanichukua masaa kama matatu kuupata baada ya kulala,nikishutuka usingzn ndo siupat tena had asubuh,nilipitiwa nkacnzia mchana hat kwa dk kdgo uck ndo nakesha kabisa,nipen ushauri make hili jambo laweza kuathiri afya yangu
kwanza wewe ni tajiri?to sleep is for the rich...bill gate huwa analala lisaa limoja tu linamtosha.utani kidogo mkuu
apo ni kupunguza mawazo tu
 
Na unatakiwa utambue kuna mambo mengi yanafanya mtu akose usingizi,kwa hiyo la muhimu pima sukari kwanza kama hakuna ijue ni stress zinakufanya usilale,
 
KUKOSA USINGIZI(INSOMNIA/SLEEPLESS NIGHT)
Leo ninapenda tuongelee suala zima la kukosa usingizi.

Kwa kawaida mtumzima anatakiwa kulala masaa7-8 kwa usiku mzima. Lakini kunawatu hushindwa kulala kabisa au hulala kwa masaa machache sana kutokana na sababu mbalimbali.

KUKOSA USINGIZI(INSOMNIA) ni tatizo la kukosa usingizi japokuwa unafursa ya kuweza kulala,tatizo hili linaweza kuwa nilamuda mfupi au nila muda mrefu yani tatizo sugu ambapo mtu hushindwa kulala au kupata usingizi mzuri kw a miezi sita(6)au zaidi. Tatizo hili husababishwa na mambo mbalimbali lakini zaidi nitazungumzia jinsi tatizo hili linayosababisha kwa kuwa na UPUNGUFU WA MELATONIN HORMONE.

Melatonini hormone ni vichocheo vinavyo tengenezwa au kutolewa na pineal gland, homoni hizi husaidia kuucontrol mzunguko wetu wa kawaida wa kulala na kuamka, hurekebisha saa ya mwili(biological clock) hivyo ukiwa na hormone hizi za kutosha utaweza kulala usingizi mzuri wala hautachukua muda mrefu sana kitandani pasipo kupata usingizi kama hauna shughuli maalumu ya kufanya.

Melatonini hormone hupunguzwa uzalishwazi wake kwa asilimia 10%- 15% kila baada mtu akifikia umri wa miaka 35 na kuendelea.

SABABU ZINGINE ZINAZOSABABISHA KUKOSA USINGIZI
sababu ziko nyingi sana zikiwemo;
~Magonjwa hapa nimagonjwa mbalimbali kama Miguu kuwaka moto,pumu,shinikizo la damu,matatizo ya moyo,kipanda uso na kuwashwa au mzio.
~Baadhi ya matibabu hii inahusisha matumizi ya baadhi ya dawa Kali zenye kemikali
~Upungufu wa hormone za kijinsia estrogen
~Msongo wa mawazo

~Ugomvi na kelele

~Mazingira

~Kuishi au kufanya kazi za usiku katika mazingira yenye mwanga kwa muda mrefu hii huathiri sana.

ATHARI ZA KUKOSA USINGIZI
~Uchovu wa mwili au kuhisi mwili hauna nguvu.

~ kuwa na hasira au mkali bila sababu za msingi.

~Maamuzi mabovu

~Kupoteza kumbukumbu au kusahau sahau.

~kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi

~Kupatwa na magonjwa ya shinikizo la damu au kisukari n.k

MATIBABU
~Badili mfumo wako wa maisha hapa ni katika ulaji wa vyakula pendelea kula zaidi vitu asilia kama mboga za majani na matunda na punguza vyakula au vinywaji vyenye caffein.

~Kunywa maji kwa wingi

~Tumia Asali mbichi vijiko viwili usiku

~ weka mazingira mazuri ya mtu kulala

~Tumia dawa zinazo fanya uwe na hormone za melatonini katika kiwango sitahiki

KWA TIBA YA KUKOSA USINGIZI NA MAGONJWA MENGINE KAMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME,MATATIZO YA HORMON,VIDONDA VYA TUMBO,BAWASIRI,MATATIZO YA MIGUU KUWAKA MOTO,PRESSURE NA MENGINE MENGI, PIGA/SMS/WHATSAP +255(0) 717556768

AU
IN BOX FB NELLY BEDAH WAKUSONGWA

Pia unaweza kuniadd facebook kama nelly bedah wakusongwa ili kujifunza zaidi,

Pia usisahau kulike page yangu ya afya nelly health and beauty care products.
 
Insomnia ni symptoms za tatizo flani ulilonalo na wala si ugonjwa kama ambavo baadhi wamechangia.

Temporary Insomnia huwa muda mfupi na chronic Insomnia huwa ya muda mrefu.

Ipo tofauti kubwa ya mtu kukosa usingizi kisa alfajiri anatakiwa kwenda panda ndege Kwa Mara ya kwanza kwenda masomoni ulaya, huyu anaweza pata temporary Insomnia.
Mwingine aliyefiwa na mtu wake muhimu ktk maisha au mtu kuachishwa kazi na hana kazi Mara huwa na complications na kama majanga yakifuatana ndio kabisaaa balaa.

Lakini umri ukienda Insomnia huwepo, wazee wengi hawalali na inakuwa chronic Kwa sababu ya masahibu aliyoipitia. Unakuta anawajukuu wakulea na uwezo hana.

PM Kwa maelezo zaidi
 
nami nilikuwa nikisikia hivyo nikawa siamini. Mpaka na mimi nilipokuja kupenda,nilipenda kwa kweli usingizi ulikuwa wa tabu,na imagine nae kila sehemu. na nikilala huwa namuota yeye karibu kila siku,na nikishtuka usiku ooh,akili inarudi kwake.nikiongea nae kwenye simu,sitaki simu aikate.kama sijawasiliana nae siku moja tu,basi nakuwa kama sichanganyi vizuri. usiombe ukapenda,bora upende juu juu tu kwani sometimes ni kama mateso fulani hivi.
Kweli kisukari, bidhaa isiyokua na garentii ikunyime usingizi?
 
Wana JF, kuna ndugu yangu yaani yeye asipokunywa chai kabla hajalala basi atakesha akihesabu 'kenchi' na kuna siku alikosa chai akanywa kahawa na matokeo yake 'alikesha', je, hali hiyo ya kutopata usingizi bila kunywa chai ni ugonjwa?

Kuna namna ya kuepukana nayo?
duu, mi najua ukinywa chai au kahawa ndo unakosa usingz, lakin hapo ni tofaut..:)
 
duu, mi najua ukinywa chai au kahawa ndo unakosa usingz, lakin hapo ni tofaut..:)

Mi najua ukinywa coffee unaondoa usingizi! wengine wanasema ukinywa (mtindi) maziwa ya mgando unapata usingizi, lakini ukitaka upate
Usingizi mnono acha mawazo na piga exercise kila siku..kama ndugu yangu alivoeleza (manchoso)
 
Usingizi ni kitu muhimu katika maisha ya mwanadamu.Mtu mzima(adult) anatakiwa alale masaa 6-7 kwa siku.
Tatizo la usingizi limegawanywa katika makundi matatu
1.Tatizo la kuanza kulala
2.Tatizo la kushtuka hovyo(kutokulala usingizi mzito)HIGH RAPID EYE MOVEMENT
3.Kushindwa kulala kabisa
Zipo dawa za usingizi kwenye group linaloitwa BENZODIAZEPINE na BENZODIAZEPINE LIKE DRUGS.mfano ZOPICLONE/ZOLPIDEM,SOBRIL...ila hazitakiwi kutumiwa kwa muda mrefu zaidi ya wiki 2-4 kwasababu unakuwa addicted nazo yaani utakuwa huwezi kulala bila kula hizo dawa.
Jinsi ya kutatua tatizo la usingizi
1.Lala kila siku kwa wakati maalum mfano kila siku saa nne
2.Epuka kulala mchana
3.Epuka kunywa chai/kahawa usiku
4.Weka chumbani katika madhari nzuri kuwe na hewa safi ya kutosha
5.Epuka kutumia computer,ipad,simu kitandani/chumbani
6.Kabla kulala jaribu kuupumzisha mwili ili iwe tayari kiakili kwaajili ya kulala sio uanze kupiga deki robo saa kabla kulala
7.Epuka kulala na njaa au ukiwa na shibe
8.Jaribu kuepuka kufikiria sana ukiwa uko katika harakati ya kulala,andika dairy kama una vitu unahitaji kuvisuluhisha jaribu kuvisuluhisha siku ifuatayo.
9.Jaribu kufanya mazoezi/kuwa na activities ili kuuchosha mwili na ubongo
10.Chumba kitumike kwaajili ya kulala tu sio shughuli nyingine :)
Mmmh!! Tabu ni namba kumi yaani hata tusiburudishane kabisaaa.
 
Na mimi nitajaribu leo maana ucngizi ni shida.
Habari madoctor,
mimi ni mama zaid ya miaka 32 na chini ya 36, naomba kufahamu juu ya hili.
Wakati wa kulala nisipopaka mafuta miguuni mpaka unyayoni na kwenye lips za midomo sipati usingizi kabisa, hata kama nimechoka sana usingizi hauji kabisa ntakaa macho nilipolala mpaka kunakucha, lakin nikipaka mafuta hasa haya mazito ,mfano vaseline,bodyline au vestiline na mengineyo mazito, miguuni mpaka unyayoni ,kwenye lips za midomo halafu ndiyo nalala. Nalala usingizi mzuri saaaana (kama alalavyo mtoto mchanga, kwa wale wenye watoto wachanga watanilewa kuwa ni usingizi wa aina gani),hata nikiamka asubuhi naamka nikiwa na siha njema kabisa.sipaki mafuta mengi napaka kawaida tu.hivyo ni lazima kilasiku nipake mafuta usiku sehemu hizo ili niweze kupata usingizi mzuri na tulivu.mimi nimeligundua hili tangu nilipoanza kujitambua japo wazazi wangu wanasema hili ni tatizo tangu nilipozaliwa.

Halinikeri sana,lakin ninapenda kufahamu kwanini inakuwa hivi, kwa sababu kuna watu wengine mfano wanangu,rafiki zangu,ndugu zangu wao wakioga na kulala pasipo kupaka mafuta wanapata usingizi bila wasiwasi.
Kuna uhusiano gani kati ya mafuta na usingizi kwa baadhi ya watu kama sisi??? .

Nategemea kupata majibu toka kwenu, asanteni.[/QUOTE
 
Sijui wengine, tiba ya kukosa usingizi ni uwe umechokaa oga afu lala
Mfano baada ya kazi siku nzima au mwanaume wako akishakupa mambo mazuri hivi
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom