Tanzia: Professor Wambali hatunae tena duniani

Tanzia: Professor Wambali hatunae tena duniani

Wana-JF, MMU,

*Prof. Michael Kajela Beatus Wambali, Shule ya Sheria UDSM, ameaga Dunia hii leo akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili

*Maheremu Prof. Wambali atakumbukwa sana kwa umahiri wake katika masomo ya Katiba, Sheria ya Utawala wa Umma ,na procedural laws kwa ujumla hapa Shule ya Sheria, UDSM

source: Maxmilian Tumaini, Mwenyekiti wa Wanafunzi, UDSM School of Law
Pole kwa familia na wanafunzi wote wa UDSM. Mungu amlaze mahali pema.
RIP Prof. Wambali
 
Hakuwa Mwalimu wangu ila alikuwa mtu wa Kwanza kunipa SHULE ya Siasa za Tanzania huko Tanzanet.

RIP Prof. WAMBALI.
 
Safari hii kila mmoja ataipita, ametutoka ila atakumbukwa kwa yale mazuri yake,
Naamini nafsi yake itaendelea kuwa nasi siku zote za maisha yetu hapa duniani.


R.I.P Professor
 
RIP Prof,
Poleni familia,
Poleni wanafunzi
Poleni UDSM
Poleni nyote
 
will be missing you Prof Wambali RIP
 
Cha muhimu tuishi tukijua tuna maisha mafupi sana hapa duniani. Hata kama huamini kuwa kuna Mungu jiulize tu, baada ya maisha haya kuna nini chafuata.

RIP PROF,
Poleni wote mloguswa kwa ukaribu na msiba huu.
 
Cha muhimu tuishi tukijua tuna maisha mafupi sana hapa duniani. Hata kama huamini kuwa kuna Mungu jiulize tu, baada ya maisha haya kuna nini chafuata.

RIP PROF,
Poleni wote mloguswa kwa ukaribu na msiba huu.
 
deep sorrow, unthinkable... rest in peace old friend!
 
Isije ikawa alikuwa katika jopo la wale waliokataliwa kurenew mikataba yao pale UDSM mzee BP juu then akafa.
Hope that is not the case for his death or he is even not in the list of the rejected lecturers
All in all RIP Prof.
 
Nyaga, Mwipopo Judge and now Prof. Wambali, bad week for learned brothers and sisters!
 
Rafiki yangu na mwanadarasa wangu Prof. Michael Kajela Beatus Wambali amefariki dunia leo tarehe 4.4.2013. Kwanza alilazwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo kabla ya juzi kuhamishiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikofariki dunia. Kwanza ilisemwa kuwa Prof. Wambali alikuwa anasumbuliwa na shinikizo la damu. Baadaye,ikasemwa kuwa Prof. Wambali amegundulika kuwa na uvimbe sehemu ya koromeo uliokuwa ukiathiri ulaji wake. UDSM kama mwajiri wake ilishindwa hata kumpatia huduma ya haraka Prof. Wambali. Jibu lililotoka UDSM na kuidhinishwa na Kitivo cha Sheria pale lilisema kuwa 'Chuo Kikuu hakina hela'. Prof. alipaswa kufanyiwa matibabu ya haraka hapa nchini,nchini Afrika Kusini au India. Akaachwa.Akasuswa. Hata Prof. Wambali amefanyiwa hivyo kweli? Chuo kimekosa fedha za matibabu kwa Mhadhiri tegemezi wa Sheria kama huyu? Chuo kina fedha nyingi kulipa safari za Prof. Mukandara na watu wake na si matibabu ya wahadhiri wake? Inauma sana na kutia aibu. Nenda Prof. Wambali. Lakini,UDSM watalaumiwa kwa kukutelekeza pamoja na huduma iliyotukuka uliyowapatia tangu miaka ya 80 hadi leo. Msalimu Comrade mwenzetu,Hayati Prof. Jwan Mwaikusa. Pumzika kwa amani classmate! VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom