Tanzia: Mzee Peter Kisumo afariki Dunia

Tanzia: Mzee Peter Kisumo afariki Dunia

Goodluck Mshana

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2011
Posts
1,272
Reaction score
1,128
Watanzania,

Ni mstuko ndani ya Taifa hili baada ya Mungu kumchukua na kwenda kumhifadhi Mzee wetu Peter Kisumo. Mzee wetu amefariki dakika chache zilizopita.

Tutazidi kuwajuza taratibu zote na baadhi ya Taarifa kadri tutavyobarikiwa kuzipata.

Updates za Taratibu za Mazishi

Ratiba mazishi ya Mzee PK

JUMANNE- August 11
- Heshima za mwisho Dar
- Saa tatu asubuhi
- Karimjee
- safari ya kwenda Moshi

JUMATANO- August 12
- safari Moshi to Usangi

ALHAMISI - August 13
- Misa kanisa kuu Usangi
- Mazishi nyumbani kwa PK

Tunashukuru kwa maombi na faraja katika kipindi hiki kigumu kwa wanafamilia.


Bwana Alitoa na Bwana Ametwa.

Amen!

R.I.P Mzee peter Kisumo
(Huyu mzee alikuwa mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya CCM )

Hapa amzee Peter Kisumo alikuwa hosp
na profesa Mwandosya huko India.

a26508d81dL.jpg
Peter%20Kisumo%281%29.jpg
IMG_0783.JPG
PC24.jpg

RIP Mzee Kisumo.

Mzee Kisumo amefariki akiwa ni mwenyekiti wa barza la wadhamni wa CCM.

Moja ya wosia ambao ameacha lakini ukiwa haukupokwlewa kwa shwari ni kuwaambia wazee wengi walio kwenye chama kwamba hawana budi kuwaachia vijana nafasi.

Mzee Kisumo alipokuwa waziri kwenye serikali ya hayati Mwalimu Nyerere mwaka 1965, Cleopa Msuya alikuwa kamishna katika wizara ya fedha wakti huo, waziri mkuu maehemuRashid Mfaume Kawawa, Michael Kamaliza.

Mzee Kisumo ni miongoni kwa viongozi wane waliojiuzulu mwezi January nwaka 1977 baada ya kashfa ya mauaji huko katika mikoa ya shinyanga na Mwanza. Mzee Alhaji Ali Hassan Mwinyi alijiuzulu nafasi ya uwaziri wa mambo ya ndani, Mzee Siyovelwa nae akiwa waziri wa usalama wa taifa Ikulu nae akajiuzulu, hali kadhalika mzee Peter Kisumo akiwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga na Marco Mabawa akiwa mkuu wa mkoa wa Mwanza.

Baada ya hapo Mwalimu akafanya mabadiliko kwenye baraza lake la mawaziri kama ifuatavyo:

Waziri Mkuu: Edward Sokoine

Mambo ya Nje : Ben Mkapa

Ulinzi: Rashidi Kawawa

Waziri wa Fedha : Edwin Mtei

Waziri wa Ujenzi: Alfred Tandau

Maliasili: Solomon Ole Saibul

Waziri wa Kazi : Crispin Tungaraza

Kilimo: John Malecela

Ardhi: Tabitha Siwale

Elimu: Nicholas Kuhanga

Sheria : Julie Manning

Habari na Utangazaji : Isaac Sepetu

Utamaduni na Michezo: Mirisho Sarakikya

Mawasiliano : Amir Jamal

Biashara : Alphonse Rulegura

Mambo ya ndani : Nassor Moyo

Waziriwa mitaji : Hasnu Makame

Afya : Leader Stirling

Maji : Al-Noor Kassum

Viwanda : Cleopa Msuya

Utumishi : Abel Mwenga

Ilikuwa kazi kazi tu.
 
Tafadhali mleta mada tunaomba source ya taarifa yako, pia tuambie Mzee Kisumo kafia wapi na tatizo gani?
 
Mzee Peter Kisumo alikuwa mmoja wa wajumbe Wa Board ya udhamini ya CCM. Pia kwenye late 2000s alikuwa chairman wa directors Wa Vodacom
 
RIP Mzee Kisumo. Kamwambie Mwalimu kuwa ule upinzani wa kweli hatimae mwaka huu umedhihiri. Punde tu atasikia RIP CCM
 
Kwa haraka haraka atakuwa mpare huyu. Kisumo ni wapare. Ila kama Ritz anamfaham huyu atakuwa alikuwa mtu mkubwa wa CCM huko upareni. Ko tuanzie hapo.
. Mpare
. CCM
. Mwanga upareni
. Mzee

CCM veteran mwenye kuheshimika sana since Nyerere time.
 
Back
Top Bottom