Mama Maulidah Anna Komu amefariki dunia. Alijiunga na Chadema mwaka 1993 akitokea CCM. Chadema ilimpa fursa mbalimbali za uongozi ikiwemo Ubunge wa viti maalumu, Waziri kivuli wa maendeleo ya Jamii, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini, na baada ya kufariki kwa aliyekua Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini, Sylvester Masinde mama Komu alikaimu nafasi hiyo kwa muda. Hata hivyo, mwaka jana Bi.Maulidah Komu kwa kushirikiana na wajumbe wengine wa Bodi ya Wadhamini ambao ni Ahmed Rashid Khamis na Said Issa Mohamed, walifungua kesi ya mgawanyo wa mali za Chadema katika shauri la madai namba 8960 la mwaka 2025. Katika kesi hiyo waliomba Mahakama izuie Chadema kufanya shughuli zozote za kisiasa na viongozi wake wazuiwe kutumia mali za chama. Mahakama kuu iliweka zuio kwa viongozi wa Chadema kufanya shughuli zozote za kisiasa na wale waliojaribu kufanya japo vikao vya ndani walikamatwa na Polisi. Pia mahakama ilizuia mali za Chadema zisiguswe, hali iliyosababisha ofisi na magari kuharibika kwa kutotumika kwa muda mrefu. Amri hiyo ilidumu kwa takribani mwaka mmoja kabla ya kufutwa na Mahakama ya rufani mwezi April mwaka huu. Kama hiyo haitoshi tarehe 04 Oktoba 2025, Maulidah Komu na wenzake walifungua shauri dogo la kuomba mahakama itoe amri ya kuwakamata na kuwashikilia Viongozi wa CHADEMA, akiwemo Makamu Mwenyekiti John Heche, Katibu Mkuu John Mnyika, na viongozi wengine wakiwemo Godbless Lema, Rose Mayemba, Brenda Rupiah, Hilda Newton, Twaha Mwaipaya na Gervas Lyenda kwa madai ya kukiuka amri ya Mahakama. Maombi hayo yaliwasilishwa mbele ya Jaji Hamidu Mwanga. Baada ya yote hayo, hatimaye Mama Maulidah Anna Valerian Komu amehitimisha safari yake duniani usiku huu, na anatarajiwa kuzikwa kesho. Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un" (إِنَّا لِلَّٰهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ) 🙏🏽