Alikuwa na ID ngapi??
RIP
Nimepigiwa simu jioni hii, dakika kadha zilizopita kuwa Mwanajamvi mwenzetu anayekwenda kwa ID ya wasaimon amefariki dunia muda kama dakika 45 zilizopita, katika hospitali ya Selian hapa Arusha, na sasa hivi ndiyo anaingizwa chumba cha ubaridi.
:A S cry::A S cry:
Taarifa hizo zinasema kuwa amenguka akiwa katika harakati za kuonana na Daktari, akiwa amesindikizwa na baba yake mzazi.
Wasaimon alijiunga na jamvi 6.10.2010.
Binafsi nilikuwa nafahamiana sana na wasaimon, alikuwa ni mtu wa kutoa ushauri wa hekima sana kuhusiana na maisha ya miaka hii, na alikuwa mpiganaji asiyechoka, akitumikia kampuni mojawapo ya Tours mjini Arusha. Naelekea msibani, nitawajuza kinachojiri.
wasaimon alivinjari hapa majukwaani hadi juzi 14.01.2013, na naambiwa kuwa hadi jana alikuwa mzima wa afya.
Ameacha Mke na watoto 3.
Mungu Ilaze Roho ya Marehemu wasaimon Mahala Pema Peponi.
Baadhi ya comment za wanajamvi:
1.Janjaweed
he was positive, God fearing, blessed na wa kupeana moyo. Its a loss, hasa kwa wakati huu ambao JF imejawa zaidi na watu type yangu
2.KABOBAkaka hayo hapo juu ndio maneno yako ya mwisho kwangu! Akilini kwangu yatakaa! Na moyoni kwangu nitayaweka ,,nitajitahidi kwa nguvu zangu zote na kwa akili zangu zote na kwa moyo wangu wote nihudhurie mazishi yako! Japo nikuone kwa mara ya kwanza na ya mwisho ndugu yangu! Ulale salama wasaimon!
Irrelevant,Childish, Nincompoopish, sluggish, crookish, absent minded question!Alikuwa na ID ngapi??
RIP