TANZIA: Mtambuzi Apata Msiba

TANZIA: Mtambuzi Apata Msiba

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2008
Posts
10,565
Reaction score
7,988
Ndugu wanaJF Salam,

Taarifa zilizonifikia hivi punde ni kwamba mwanaJF mwenzetu ndugu Mtambuzi amefiwa na mama mkwe muda mfupi uliopita.

Mama mkwe wa Mtambuzi amefikwa na mauti akiwa amelazwa katika hospitali ya St. Thomas iliyoko jijini Arusha.

Tutaendelea kufahamishana juu ya taratibu za mazishi. Kwa members wa JF mlioko Arusha support yenu katika kipindi hiki ni muhimu sana.

Natoa pole kwa Mzee Mtambuzi pamoja na familia, ndugu jamaa na marafiki wote waliofikwa na msiba huu. Mungu awaongoze na kuwafariji katika kipindi hiki kigumu na cha majonzi.

UPDATES:
Mipango ya mazishi inafanyika Field Force (FFU) Arusha na maziko yanatarajiwa kufanyika upareni, Mamba Miamba siku ya Ijumaa tarehe 03/05/2013.

MORE UPDATES:
Kwa wale ambao wangependa kuuungana na familia ya mzee Mtambuzi katika msiba huu kwa njia ya rambirambi, tafadhali tumieni namba zifuatazo; Tigo-Pesa 0715 729292 na M-Pesa 0752 729292
 
Last edited by a moderator:
Pole sana kwa familia.

Nakumbuka mama mkwe alilazwa Muhimbili siku si nyingi zilizopita.

R.I.P mama mkwe...
 
Pole sana Mtambuzi kwa kuondokewa na mama mzaa chema.
 
Mtambuzi pole kwa msiba, nawaombea mungu awape faraja ya kweli.
 
Last edited by a moderator:
Pole mtambuzi kwa kumpoteza mama mkwe

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Pole sana baba Ngina......roho ya mama ilale mahali pema peponi.......
 
Kumbe ulikuwa unauguza ndo maana sijaona masomo yako ya ukweli jukwaani?
Pole sana mkuu Mtambuzi.
mwanaume ni kuvumilia, so ni muda wa kujikaza sawasawa na kujipanga ili mama mkwe wako apumzishwe katika usingizi wa kitambo kidogo maana parapanda italia na hao waliokufa hawatawatangulia walio hai kumwona mwana wa Adam arudipo mara ya pili kuwachukua wateule.
 
Pole sana rafiki ndg yetu Mtambuzi

Mama yetu Mwenyenzi MUNGU ampe pumziko la milele shambani mwake Bwana wetu!

Tupo pamoja Mtambuzi
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom